Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

KESI ZA ALBINO KUANZA J'TATU


Mahakama Kuu ya Tanzania inatarajia kuanza kusikiliza kesi tano za mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi ‘albino’ katika miji ya Wilaya za Kahama na Shinyanga mkoani Shinyanga kuanzia Jumatatu. Kwa mujibu wa Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu, John Utamwa, kesi tatu zitasikilizwa mjini Kahama na Jaji Gabriel Rwakibarila kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza na zimepangwa kusikilizwa kwa muda wa siku 35.

Utamwa alisema Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Kanda ya Dodoma, Gadi Mjemas anatarajiwa kusikiliza kesi nyingine mbili katika Mahakama Kuu mjini Shinyanga zilizopangwa kusikilizwa kwa muda wa siku 21. “Taratibu zote kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hizo zimekamilika,” alisema Utamwa.

Akizungumza jana Dar es Salaam, Msemaji wa Wizara ya Katiba na Sheria, Omega Ngole alisema tayari Mawakili wa Serikali wameshawasili katika miji ya Kahama na Shinyanga kwa ajili ya kuendesha kesi hizo ambazo upelelezi wake umekamilika. Kuanza kusikilizwa kwa kesi hizo, kunaifanya Tanzania kuungana na nchi za Rwanda na Burundi ambazo zimeanza kusikiliza kesi za aina hiyo hivi karibuni.

Katika siku za hivi karibuni kumekuwapo na malalamiko ya kuchelewa kusikilizwa kwa kesi za mauaji ya albino nchini. Pia Mbunge kutoka Canada ambaye ni albino aliishinikiza nchi yake kuinyima misaada Tanzania kwa kile alichodai tatizo la mauaji hayo kutomalizika nchini. Licha ya malalamiko hayo, tayari serikali ilishafanya kura za maoni nchi nzima kwa watu kuwataja wanaohusika na biashara ya viungo vya albino.
[ Read More ]

Nahodha meli iliyozama atahadharisha kuhusu uopoaji


NAHODHA wa meli ya MV Fatih iliyozama katika Bandari ya Malindi mjini Zanzibar wiki iliyopita, ameonya kuwa jitihada za kuopoa meli hiyo zisipofanywa kwa umakini, zinawesababisha uharibifu utakaosabaisha uchunguzi wa ajali hiyo kutokwenda sawa.

Akizungumza na Mwananchi jana ikiwa ni mara yake ya kwanza kuzungumza tangu kutokea kwa ajali hiyo, Nahodha Usi Ali Ussi, alisema taarifa kuwa meli hiyo inamomonyoka kutokana na kuchakaa wakati wa kuvutwa si za kweli.

Alisema tatizo ni watu kutofunga minyororo, katika sehemu ngumu za meli zilizowekwa maalum kwa kazi hiyo.

“Ikiharibiwa zaidi itasababisha uchunguzi uwe mgumu kwani chanzo cha ajali hiyo kitakuwa kigumu kugundulika…kinachotakiwa ni kujua kitu kilichosababisha meli kuzama ghafla” alisema.

Alisema wao wako tayari kutoa ushirikiano kwa mamlaka zinazohusika ili kuharakisha kazi ya kuopoa meli hiyo.

Nahoodha huyo ambaye ni Luteni kanali mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, pia alikanusha madai kuwa alipata matatizo kabla ya kutia nanga katika bandari hiyo, baada ya kukosa ushirikiano na watu wa bandari.

Alisema aliweza kuifikisha meli hiyo katika Bandari ya Malindi ikiwa salama na kufunga kamba gatini.

“Kama kungekuwa na tatizo muda mrefu ningeweza kuamuru wafanyakazi wawaandae abiria kwa tahadhari kwa kuwapa Life jackets, lakini tatizo lilitokea baada yakufika salama na baadhi ya abiria walikuwa wakiteremka.

Hata hivyo nahodha huyo alilalamikia kukosekana kwa taa katika bandari hiyo ambako kulisababisha juhudi za uokoaji kukwama.

Kwa mujibu wa nahodha huyo, wakati meli ilipoanza kulalia upande wa kushoto alikuwa katika chumba cha kuongozea meli na Mhandisi wa meli hiyo.

Alisema pia walikuwa na Afisa Mkuu wa meli na kwamba ghafla waliona chombo hicho kikiinama kwa kasi kubwa.

“Mimi niliruka kwenye mizigo nikatembea hadi nilipofika mwisho wa meli nikaruka katika kuta za gati ili kujiokoa.Kama tungejua kuwa hatari inayokuja tusingeliacha mizigo ndani ya vyumba na mpaka sasa vifaa vyetu bado havijatolewa.

Nahodha huyo ambaye aliendesha meli hiyo kwa takribani mwezi mmoja tangu ajiunge na kampuni hiyo, alisema hii ni ajali yake ya kwanza lakini amekuwa akipata matatizo madogo madogo tangu mwaka 1972 alipoanza kazi katika vyombo vya maji vinavyomilikiwa na jeshi.

[ Read More ]

Wabunge waipania bajeti ya Waziri Mkulo waonya inaweza kuvunja bunge


BAJETI ya serikali kwa mwaka 2009/2010, imekaa vibaya na inaonyesha kuwa Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo, atakuwa na wakati mgumu wakati atakapoisoma bungeni Juni 11 kutokana na baadhi ya wabunge kutangaza dhahiri kutoa shilingi huku wakionya kuwa huenda hata bunge likavunjwa.

Onyo la wabunge hao ambao wengi ni kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kusini, limekuja baada ya Mkulo kuwasilisha Sura au Mwelekeo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2009/2010, mbele ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, ambayo inatarajiwa kuwa ya Sh9.5trilioni ikilinganishwa na Sh7.3 trilioni za mwaka 2008/09.

Mwelekeo huo wa bajeti ya 2009/2010, unaonyesha serikali inatarajia kukusanya Sh9.5 trilioni ambazo kati ya hizo, Sh5.1 trilioni ni mapato ya ndani, Sh3.2 trilioni ni misaada na mikopo kutoka kwa wahisani na Sh1.2 trilioni, ni mapato mengine, huku matumizi ya kawaida yakitarajiwa kuwa Sh6.7 trilioni na maendeleo Sh2.8 trilioni.

Wabunge kutoka kamati mbalimbali nje ya Fedha na Uchumi, pamoja na baadhi ambao ni wajumbe wa kamati hiyo, walianza kuchambua mwelekeo huo wa bajeti kwa kumlipua Mkulo mbele ya jopo la wataalamu kutoka wizara hiyo na idara zake, hasa katika kipengele cha ujenzi wa barabara.

Walienda mbali zaidi kwa kusema kila waziri anajipendelea kwake, akiwemo waziri huyo wa fedha.

Mbunge Anthony Diallo (CCM-Ilemela), ndiye aliyeweka msimamo akimtahadharisha Waziri Mkulo kwamba bajeti hiyo kama ilivyo katika mwelekeo, haitaweza kupita bungeni na kuonya kuwa inaweza kuandika historia kwa bunge kuvunjwa.

"Nakwambia kama ndugu yangu, bajeti hii ikija kama ilivyo haitapita bungeni, Iam telling you my brother (nakwambia kaka yangu)... sikufichi, haipiti hii bajeti," alizungumza Diallo kwa msisitizo.

Diallo alisema karibu Sh100 bilioni zimetengwa katika barabara zile zile, huku maeneo mengine ya nchi yakiwa hayana barabara za lami.

Alisema haingii akilini kuona sehemu ya barabara ya lami kutoka Same hadi Korogwe inatengewa fungu la Sh44 bilioni.

"Ukiangalia, karibu Sh100 bilioni ni barabara zile. Utakuta ni Morogoro, Dares Salaam na Iringa. Nasema kwa mara ya kwanza bunge linaweza kuvunjwa," alionya Diallo kabla ya kubeba mkoba wake na kuondoka.

Naye mbunge wa Busega (CCM), Dk Raphael Chegeni alionya bajeti hiyo inaweza kuigawa nchi kutokana na kuruhusu maendeleo makubwa katika baadhi ya maeneo huku mengine yakiwa na umasikini wa kutisha.

Dk Chegeni alifafanua kwamba, kitendo cha kukarabati barabara ya lami kati ya Chalinze-Segera-Tanga, haina mantiki wakati kuna maeneo hayana kabisa miundombinu ya lami.

Mbunge huyo wa moja ya majimbo ya kanda ya ziwa, alidiriki kusema: "Hata barabara ya Msata Bagamoyo haikupaswa kupewa kipaumbele zaidi kama kuna nyingine hazina lami. Labda kwa sababu anatoka Waziri wa Miundombinu (Dk Shukuru Kawambwa)."

Dk Chegeni alihoji barabara hiyo kuzidi kutengewa fedha wakati tayari nyingi zilichukuliwa kutoka Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA).

Akitoa mfano kuhusu hoja yake ya mawaziri 'kujimegea bajeti', Dk Chegeni alidai kuwa hata Basil Mramba akiwa Waziri wa Miundombinu alihamisha mabilioni ya fedha ya ujenzi wa barabara ya Usagara- Geita na kuzipeleka Rombo, ambako aliweka viwango ya Sh900 milioni kwa kilomita moja, kitu alichosema: "Kwa wakati ule haikuwezekana ni fedha nyingi."

Alisema pia haingii akilini kuona uwanja wa ndege wa Songwe Mbeya, ukitengewa tena Sh15 bilioni wakati uliwahi kutengewa Sh 30 bilioni, kitu alichosema si sahihi kwani kuna uwanja wa ndege wa Mwanza unahitaji kukarabatiwa au kujengewa eneo jingine (Terminal).

Mbunge wa Mvomero, Suleiman Saddiq (Mvomero-CCM), alitishia kwenda Ikulu kuonana na Rais Jakaya Kikwete kama barabara alizoahidiwa hazitakuwemo katika bajeti hiyo.

Hata hivyo, hoja hizo zilipingwa na wabunge wawili ambao ni Dk Omari Mzeru (Morogoro Mjini-CCM) na Dk Abdallah Kigoda (Handeni-CCM), ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo ya fedha na uchumi.

Dk Mzeru alifafanua kwamba hakuna mantiki watu kuhoji ujenzi wa barabara ya Msata-Bagamoyo wakati ndiko anatoka Rais Kikwete, ambaye anapaswa kupita katika barabara salama yenye lami.

Kwa mujibu wa Dk Mzeru, hajaona duniani sehemu ambako wananchi hawathamini heshima ya rais wao na kuongeza kuwa eneo hilo ni la kiuchumi kwani litafungua utalii.

Dk Kigoda alihoji mantiki ya wabunge wenzake kushambulia ujenzi wa barabara ya Chalinze- Segera- Tanga, wakati ujenzi wa barabara ya Mwanza ni wa muda mrefu.

Hoja ya Dk Mzeru kuhusu heshima ya Dk Kikwete, ilipingwa na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed (Wawi-CUF), ambaye alisema jambo la msingi si kuangalia nani anatoka wapi, bali barabara zinapaswa kujengwa kwa kuangalia matokeo na faida kiuchumi.

"Napenda kupingana na hoja ya Dk Mzeru kuhusu ujenzi wa barabara ya Msata-Bagamoyo. Asiseme kwa sababu anatoka Rais basi ijengwe, tuangalie Economic impact (umuhimu wake kiuchumi), sasa ikiwa hivi kwingine ambako Rais hatoki itakuaje," alihoji Rashid.

Akifanya majumuisho ya hoja ya bajeti hiyo, ambayo inaonekana kurejesha kero zile zile za kodi, Mkulo alisema suala la ujenzi wa barabara hizo mbili unaweza kukwamishwa kwa chuki dhidi ya Dk Kawambwa.

Alisema barabara ya Chalinze-Segerea inajengwa na Denmark ambayo ndiyo imetoa fedha na kuchagua miradi yao hivyo, si rahisi kwa serikali kuipanga vinginevyo wangekataa na kuondoa fedha zao.

Akizungumzia bajeti yenyewe, Mkulo alisema mwaka 2009/2010, sera za mapato zinalenga kukusanya mapato ya ndani yasiyopungua Sh5.1trilioni sawa na asilimia 16.4 ya Pato la Taifa (GDP), ikilinganishwa na mapato ya asilimia 15.9 kwa mwaka 2008/09.

Mkulo aliongeza kwamba pamoja na msukosuko wa kiuchumi wa dunia, serikali imeongeza nguvu katika kukusanya mapato ya ndani ya nchi.

Mchanganuo huo unaonyesha, mapato ya mikopo na misaada ya nje (MDRI/MCA -T) ni Sh3.2 trilioni, mapato ya halmashauri (Sh132 b), mapato yatokanayo na mauzo ya hisa (Sh 15 b) na mikopo ya ndani (Sh1.2 trilioni).

Akitaja mchanganuo wa bajeti hiyo kisekta kwa kujumuisha mishahara kwa mwaka 2009/2010, ambayo inaonyesha kupungua maeneo ya vipaumbele na kurejesha kodi, Mkulo alisema elimu itatengewa Sh1743.9 bilioni ikilinganishwa na Sh1,430.4 bilioni kwa mwaka 2008/09.

Kuhusu upatikanaji wa pembejeo za kilimo kwa wakulima na wafugaji, sekta ya kilimo kwa ujumla imetengewa Sh666.9 bilioni ikilinganishwa na Sh513.0 bilioni za mwaka 2008/09, sawa na ongezeko la asilimia 30.

Kwa upande wa miundombinu, Mkulo alisema kipaumbele kitakuwa ni kukamilisha miradi ya barabara inayoendelea, hivyo kwa ujumla imetengewa Sh1,096.6 bilioni ikilinganishwa na sh 973.3 bilioni za mwaka 2008/09, sawa na ongezeko la asilimia 12.7.

Sekta ya Afya, alisema kipaumbele ni kuendelea kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM), kuimarisha ubora na upatikanaji wa huduma za uzazi na mtoto na kuimarisha uwezo wa rasilimali watu katika ngazi zote.

Kwa ujumla, Mkulo alisema sekta ya afya imetengewa Sh963.0 bilioni ikilinganishwa na Sh910.8 bilioni mwaka 2008/09, sawa na ongezeko la asilimia 5.7, huku huduma za maji umuhimu utawekwa katika kuboresha umwagiliaji na matumizi ya kawaida, ambayo mwelekeo unaonyesha itatengewa Sh347.3 bilioni ikilinganishwa na Sh231.6 bilioni za mwaka 2008/09.

Katika nishati na madini, Mkulo alisema kwa ujumla sekta hiyo imetengewa Sh285.5 bilioni ikilinganishwa na Sh378.8, sawa na upungufu wa asilimia 24.6.



[ Read More ]

Aliyetoka gerezani kwa msamaha, auawa

Mkazi wa Kijiji cha Hombolo, mkoani hapa, Chibenene Fwaru (50) aliyekuwa ametoka gerezani hivi karibuni kwa msamaha wa Rais ameuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Omar Mganga alisema Polisi inaendelea na msako wa waliohusika katika tukio hilo lilitokea juzi kijijini hapo.

Kamanda alisema Chibenene alikatwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake. Kwa mujibu wa Kamanda, awali mkazi huyo aliwahi kupigwa mshale mguuni na watu wasiojulikana.

Inadaiwa kuwa kijana huyo alikuwa akituhumiwa kwa mauaji ya watu wawili kijijini hapo lakini alitoka gerezani kwa msamaha wa Rais kitendo ambacho kinadaiwa kuwa kiliwaudhi wananchi hao na kuamua kumuua kijana huyo. Kamanda Mganga alisema watu waliohusika kwa mauaji hayo, walikimbia. Alisema Polisi inawasaka kwa lengo la kuwafikisha mahakamani watakaobainika kuhusika.
[ Read More ]

Zuma promises half a million jobs


New South African President Jacob Zuma has promised to create half a million jobs this year in his first state of the nation address.

He said fighting poverty was his priority, a week after South Africa officially announced it was facing its worst recession in 17 years.

"We must act now to minimise the impact of this downturn on those most vulnerable," he said in Cape Town.

But he also told parliament the government had to spend wisely.

Mandela cheers

The BBC's Karen Allen in Cape Town says Mr Zuma, in power for less than a month, has had to perform a delicate balancing act to appease his unions allies, currently staging strike action, and avoid scaring off investors.


"Between now and December 2009, we plan to create about 500,000 job opportunities," he told MPs.

He promised his government would create a further four million jobs by 2014, but did not explain how.

Mr Zuma also:

• announced an annual national holiday, Mandela Day, on 18 July, prompting cheers from the audience and a wave from the watching anti-apartheid icon himself

• promised to deliver "the best World Cup ever" when South Africa hosts the football tournament in June 2010

• promised to provide anti-retroviral HIV drugs for 80% of those in need by 2011, as part of efforts to halve the rate of new HIV infections within that period

• stuck by pledges to cut violent crime by between 7%-10% a year (in a country where 50 people are killed every day)

Mr Zuma, whose African National Congress Party (ANC) swept into power in April elections on the back of strong support from unions and the poor, cautioned against expectations of a quick fix to the financial slump.

"The economic downturn will affect the pace at which our country is able to address the social and economic challenges it faces. But it will not alter the direction of our development," he said.

Ex-South African President Nelson Mandela listens to the state of the nation address by President Jacob Zuma in parliament, Cape Town, on 3 June 2009
Ninety-year-old Nobel laureate Nelson Mandela was in the audience

Fifteen years after the end of apartheid, about 40% of South Africans live in poverty - more than half of that number surviving on less than one dollar a day, according to government data.

Its economy shrunk by 6.4% during the first quarter of this year and almost one in four South Africans is unemployed.

Mr Zuma said a three-year 787bn rand ($98bn; £60bn) spending programme announced in this year's budget - and including funds for schools, transport, housing and sanitation - must be properly planned.

"In the face of the economic downturn, we will have to act prudently - no wastage, no rollovers of funds - every cent must be spent wisely and fruitfully," he said.

[ Read More ]

Kinakili safari huenda kisipatikane


Maafisa wa safari za ndege wa Ufaransa wamesema vifaa vya kunakili safari ya ndege iliyotoweka katika bahari ya Atlantic huenda visipatikane.

Maafisa hao walisema watafanya uchunguzi kwa makini mno, lakini walisema kazi yao wanaitekeleza katika mazingira ya hali ngumu mno.

Ndege hiyo, nambari AF 447, ilitoweka siku ya Jumatatu ilipokuwa safarini kutoka Rio nchini Brazil, ikielekea Paris, nchini Ufaransa, na ikiwa na abiria 228.

Mabaki ya ndege hiyo yameonekana kilomita 650 (maili 400) kutoka pwani ya Brazil, na wanamaji wa nchi hiyo wamekuwa wakifanya uchunguzi zaidi katika eneo hilo.

Maafisa wa Brazil na Ufaransa wamesema hakuna shaka mabaki yaliyopatikana ni ya ndege iliyotoweka.

Baadhi ya vitu vya kwanza kabisa kuonekana ni mafuta yaliyomwagika, kiti cha abiria na vinginevyo.

[ Read More ]

Obama aanza ziara mashariki ya kati


Rais wa Marekani Barack Obama amewasili nchini Saudi Arabia katika mwanzo wa ziara yake mashariki ya kati, inayolenga kuimarisha uhusiano baina ya Marekani na nchi za Kiislamu.

Bwana Obama alitarajiwa kuwa mjini Riyadh kwa muda wa saa nne kabla ya kuelekea nchini Misri, ambako atatoa hotuba muhimu mjini Cairo.

Anasema anataka kuanzisha mdahalo na waislamu , kuondosha hali ya kutoelewana na kufufua mashauriano ya amani ya mashariki ya kati.

Hii ni ziara ya kwanza ya rais Obama katika eneo hilo, mbali na kupitia Iraq muda mfupi mwezi Aprili.

Saudi Arabia ndiyo inayodhamini mpango wa kipekee wa amani kwa uhusiano kati ya nchi za kiarabu na Israel, ingawa kwa sasa hivi mazungumzo yamekwama.

Misri inahusika sana katika matatizo ya WaPalestina , kwa kuwa msuluhishi kati ya Israel na kundi la Hamas kwenye ukanda wa Gaza.

Bwana Obama alipata mapokezi ya taadhima mjini Riyadh kabla ya kufanya mazungumzo na mfalme Abdulla.

Bwana Obama hakutarajiwa kutoa taarifa yoyote mjini Riyadh, lakini lakini siku ya Alhamisi anatarajiwa kutoa hotuba katika chuo kikuu cha Cairo nchini Misri, ambayo mwandishi wa BBC anasema ni mojawapo ya hotuba muhimu sna za rais Obama kama rais wa Marekani.

Safari ya rais Obama mashariki ya kati haijumuishi Israel, lakini muda mfupi kabla ya kuondoka kuelekea Saudi Arabia alikutana na waziri wa ulinzi wa Israel Ehud Barak mjini Washington.

Akizungumza na BBC kabla ya ziara hiyo, rais Obama alisema anaamini Marekani '' itaweza kufufua tena mashauriano ya kufana'' kati ya Israel na Palestina.

Alisema ziara hiyo inakusudiwa kutoa fursa kwa Marekani na nchi za kiislamu kusikilizana zaidi.

Ziara hiyo ya mashariki ya kati imekuja huku kukiwa na taarifa zilizodaiwa kutoka kwa viongozi wa Al Qaeda, ukiwemo ujumbe ulionakiliwa kutoka kiongozi mkuu wa kundi hilo Osama Bin Laden.

Kwenye kanda hiyo iliyoonyeshwa na Televisheni ya Ki-Arabu ya al-Jazeera , Bin Laden anamlamu rais Obama na mtangulizi wake George W Bush kwa kukuza chuki dhidi ya Marekani.

[ Read More ]

Mwanajeshi Dar afa ajalini


Askari mmoja wa Jeshi la Wananchi Tanzania, JWTZ, mwenye cheo cha Kapteni, aliyetambuliwa kwa jina la Robert Makongoro, 31, amefariki dunia papo hapo baada ya gari alilokuwa anaendesha kugongwa na gari lingine katika barabara ya Sam Nujoma Jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye amesema ajali hiyo ilitokea jana mishale ya saa 10:30 jioni eneo la Super Star kwenye makutano ya barabara inayotokea Sinza Makaburini.

Amesema mwanajeshi huyo aligongwa na gari lenye namba za usajili T 792 ARX aina ya Suzuki, iliyokuwa ikiendeshwa na Joanes Kacheche, 41, akitokea Mwenge kuelekea maeneo ya Ubungo.

Kamanda Kalunguyeye amesema gari la Joanes lilipofika maeneo hayo, lilivaana na la mwanajeshi lenye namba za usajili T 715 AZX aina ya Toyota Carina lililokuwa likitokea Sinza Makaburini.

Amesema gari la mwanajeshi liligongwa upande wa dereva.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Lugalo.

Kamanda amesema Polisi wanamshikilia dereva Joanes kwa uchunguzi zaidi na endapo atabainika ana makosa hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa.

[ Read More ]

SMZ yaunda tume kuchunguza meli iliyozama


Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamua kuunda Tume kuchunguza chanzo cha kuzama kwa meli ya MV Fatih ikiwa na abiria na mizigo katika Bandari ya Malindi ya Zanzibar.

Meli hiyo iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuja Zanzibar ilizama Ijumaa iliyopita baada ya kukumbwa na tatizo la kuingiza maji ikiwa katika mkondo wa bahari, hatua iliyosababisha mabaharia kutumia mashine kumwaga maji.

Waziri wa Nchi Afisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma, aliiambia Nipashe kwamba tume hiyo itaangalia sura nzima ya tukio, hasa ubora wa chombo hicho pamoja na kupitia ripoti mbali mbali za ukaguzi wa meli hiyo.

Alisema iwapo kutabainika kwamba kuna uzembe ulikuwepo, hatua zitachukuliwa kwa wahusika kulingana na sheria.

Alisema kumejitokeza matapeli wanaodai wao ni waathirika wa ajali hiyo tangu serikali ilipotangaza itawasaidia watu walioaathirika.

Nae Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, Dk. Vuai Iddi Lila, alisema idadi ya abiria bado inaleta utata kwa vile watu waliosalimika idadi yao sasa imefikia 33 na waliokufa ni sita. Orodha ya awali ilidai kuwa abiria walikuwa 25 na mabaharia 13.

Wakati huo huo Kazi ya kuiopoa meli hiyo katika bandari ya Malindi iliendelea jana lakini hadi alasiri chombo hicho kilikuwa bado hakijaopolewa.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirika la Bandari, Abdi Omar, alisema chombo cha kunyanyua vitu vizito maarufu kama ndovu, kiliharibika ghafla katika sehemu ya jenereta na kukwamisha zoezi hilo. Alisema mafundi walikuwa wanaendelea kutengeneza.

Awali Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Generali Davis Mwamnaynge na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Said Mwema walitembelea eneo la tukio na kuwataka askari wa uokozi kuzidisha ushirikiano ili kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa.

[ Read More ]

Kiti cha ndege chakutwa kikielea

Kiti, koti okozi, vipande vya chuma na dalili za mafuta vimeonwa katikati ya Bahari ya Atlantic na rubani wa Jeshi la Brazil ambaye ni mmoja wa wataalamu wanaoitafuta ndege ya Shirika la Ndege la Ufaransa, Air France, iliyopotea tangu juzi. Mabaki hayo yalionekana jana kutoka angani umbali wa kilometa 650 Kaskazini mwa kisiwa cha Brazil cha Fernando de Noronha, karibu na njia ambayo ndege hiyo ilipitia kabla ya kupotea ikiwa na watu 228, msemaji wa Jeshi la Anga, Jorge Amaral alisema jana. Licha ya kuonekana mabaki hayo, bado hakukuwa na dalili zozote za uhai katika maeneo mawili tofauti yaliyokutwa na mabaki hayo yaliyoachana umbali wa kilometa 60.

"Maeneo yalikopatikana mabaki hayo ni kuelekea pale ambapo ishara ya mwisho kutoka ndege hiyo ilipoonekana kwa waongoza ndege na kisha ikashindwa kuonekana tena," Amaral alisema. "Hiyo inamaanisha kuwa ilijaribu kukata kona, pengine ikitaka irudi Fernando de Noronha, lakini hizo ni hisia tu." Amaral alisema Serikali isingeweza kuthibitisha kuwa mabaki hayo yanatokana na ndege hiyo hadi hapo itakapokuwa imeopolewa kutoka ndani ya maji na kuitambua. Meli za kivita za Brazil zinatarajiwa kufika eneo la tukio leo.

Ugunduzi huu umekuja muda wa zaidi ya saa 24 baada ya ndege hiyo kuripotiwa kutoweka na kusababisha hofu ya watu wote waliokuwamo kupoteza maisha. Waokoaji bado wanaendelea na msako katika eneo pana la bahari hiyo kuanzia Kaskazini Mashariki mwa Brazil hadi pwani ya Afrika Magharibi. Ndege hiyo aina ya Airbus A330 yenye umri wa miaka minne, ilipoteza mawasiliano Jumapili saa 4.14 usiku. Ujumbe uliotoka katika ndege hiyo muda mfupi kabla ya kutoweka, ulisema ilikuwa imepoteza msukumo wa hewa na kukabiliwa na matatizo ya umeme.
[ Read More ]