Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

ZAIDI YA WAGONJWA 263 WA FESTULA NA MDOMO WA SUNGURA WAMENUFAIKA NA HUDUMA YA M PESA


Mkurugenzi msaidizi wa hospitali ya CCBRT Haika Mawala akimkaribisha Mkurugenzi wa mahusiano na Vodacom Foundation Mwamvita Makamba wa pili toka kushoto akiambatana na Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo walipotembelea hospitali ya CCBRT kwa lengo la kujionea jinsi gani huduma ya Vodafone M pesa inavyosaidia wagonjwa wa fistula na mdomo wa sungura kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.
Mkurugenzi msaidizi wa hospitali ya CCBRT Haika Mawala akimkaribisha
Mkurugenzi wa mahusiano na Vodacom Foundation Mwamvita Makamba
Mkurugenzi wa Vodafone Foundation wa Egypt Noha Saad kushoto akisaini kitabu cha wageni katika hospitali ya CCBRT mara baada ya kutembelea hospitalini hapo na wakurugenzi wenzake Mwamvita Makamba,Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo wakiwa na lengo la kujionea jinsi gani huduma ya Vodafone M pesa inavyosaidia wagonjwa wa mdomo wa sungura na fistula kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.
Mkuu wa kitengo cha Safaricom Foundation-Kenya Sanda Ojiambo(kushoto)akizungumza na waandishi wa habari katika hospitali ya CCBRT walipotembelea hospitalini hapo kwa lengo la kujionea ni jinsi gani huduma ya M pesa inavyosaidia wagonjwa wa fetula na wa mdomo wa sungura kwa kutumiwa fedha za nauli na matumizi ya njiani kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo,katikati Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Uingereza Andrew Dunnet,Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Tanzania Mwamvita Makamba.
Mkurugenzi wa hospitali ya CCBRT Tom Vanneste akifafanua jambo kuhusu ugonjwa wa mdomo kisungura na fistula kwa maafisa wa Vodafone M pesa Afrika walipotembelea hospitalini hapo hawapo pichani kujionea jinsi gani huduma ya M pesa inavyosaidia wagonjwa kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini na kuja kutibiwa hospitalini hapo zaidi ya wagonjwa 263 wamenufaika na huduma hiyo.

[ Read More ]

NIZAR KHALFANI AENDELEA KUNG'ARA NYUMBANI NA CANADA


Mchezaji nyota wa Vancouver Whitecaps ya jijini Vancouver huko British Columbia, Canada, akiwa anafundisha watoto kuliskata kabumbu maeneo ya Tabata jijini Dar alipokuja kuchezea Taifa Stars. Nizar amekuwa lulu kwa timu hiyo ya kulipwa na Taifa Stars, yote hii ikitokana na kujituma, nidhamu na kupenda kazi yake. Ni mfano wa kuigwa
Nizar ana mashabiki wengi watoto kwa wakubwa 
na anapeperusha vilivyo bendera yetu
Nizar akinyanyasa ngome ya adui
Nizar akiwakilisha wakati Taifa Stars ilipocheza na Brazil Dar
Nizar huwa haachwi peke yake. akiachwa tu nyavu hizi...
Nizar na kikosi cha kwanza cha Vancouver Whitecaps. 
Kwa habari kamili ya timu hiyo
BOFYA HAPA
[ Read More ]

Nelson Mandela discharged from hospital in South Africa

Nelson Mandela (file image) 

South African former President Nelson Mandela has been discharged from a hospital where he spent two nights.
Surgeon General Vejaynand Ramlakan said Mr Mandela, 92, was suffering from ailments that are common in people his age but was in good spirits.
Deputy President Kgalema Motlanthe - using Mr Mandela's clan name - said: "Madiba is well."
South Africa's liberation hero flew from Cape Town to Johannesburg on Wednesday for a check-up.
Friends and family visited him amid tight security at Milpark hospital on Thursday.
On Friday Mr Ramlakan said Mr Mandela had suffered a respiratory infection, but was responding well to treatment and would be receiving home-based care.
"To us he is stable, but will be subject to intense monitoring," he told reporters.
A convoy is now believed to be taking Mr Mandela to his home in the Johannesburg suburb of Houghton.
Correspondents say he has seemed increasingly frail since retiring from public life in 2004.
His last public appearance was at the football World Cup closing ceremony last July.
[ Read More ]

Mandela 'very sick,' But Not in Danger


South Africa's revered former president Nelson Mandela was Thursday described as "very sick" but his condition was "not life-threatening."
The news that Madiba -- the clan name by which the 92-year-old Nobel Peace Prize winner and country's first elected black leader is affectionately known -- was to spend a second night in hospital has gripped the nation.
The public has grown increasingly concerned for Mandela's health but he could be released as early as today, a source close to Mandela said on condition of anonymity.
"The old man is very sick but his condition is not life threatening," the source said.
"He came in for a checkup but the doctor decided to keep him in for observation.
"He is still not well but we expect him to be released tomorrow."
President Jacob Zuma
described the hospital visit as a checkup and called for calm, but a report said Mandela had been treated for a lung problem.
Mandela spent 27 years in prison for his role in the fight against apartheid in South Africa, emerging in 1990 to lead the transition to democracy.
[ Read More ]

MTANZANIA AFUNGWA MAISHA MAREKANI!!!!


Mfungwa wa kwanza katika jela ya Guantanamo kushtakiwa kwenye mahakama ya kiraia, Ahmed Ghailani kutoka Tanzania amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani.

Hukumu hiyo ilitolewa na mahakama ya jimbo la Manhattan.

Ghailani alipatikana bila hatia mwaka jana, katika kesi ambayo alishtakiwa kwa mauaji pamoja na mashtaka mengine kuhusiana na mashambulizi ya kigaidi ya mwaka 1998 katika balozi za Marekani mjini Nairobi, Kenya na Dar es Salaam, Tanzania


Mchoro ukionyesha Mtanzania Ahmed Ghailani

Jopo la majaji hata hivyo limempata na hatia ya kufanya njama ya kuharibu majengo ya serikali.

Upande wa mashtaka ulijaribu kumshawishi jaji kwamba Ghailani alipaswa kuonewa huruma kwa sababu hakujua kuhusu njama hiyo.

Vile vile walisema kuwa Ghailani aliteswa na CIA baada ya kukamatwa.

Hata hivyo waendesha mashtaka walitaka apewe kifungo cha maisha gerezani huku wakisisitiza kuwa alijua kuhusu njama hiyo.

Akijiandaa kutoa hukumu yake, Lewis A. Kaplan alisema ilikuwa siku ya haki kwa jamii za watu 224 waliofariki kwenye mashambulizi ya bomu ya mwaka wa 1998 pamoja na wale wote waliojeruhiwa.

Kaplan alisema aliridhishwa na ushahidi aliopata kwamba Ghailani alijua kwamba watu wangekufa kutokana na vitendo vyake.

Ghailani alikamatwa nchini Pakistan mwaka 2004.

Alipelekwa kwenye kambi ya siri inayosimamiwa na shirika la Ujasusi la Marekani, CIA, kabla ya kupelekwa Guantanamo Bay, Cuba, mwaka 2006.

Baadaye alihamishwa hadi New York alikoshtakiwa.
Credit to BBC.
[ Read More ]

KESI YA JERRY MURO ILIVYOUNGURAMA LEO

MAHAKAMA ya Hakimu mkazi Kisutu imepokea pingu, miwani na hati ya upekuzi katika kesi ya kuomba rushwa ya sh milioni 10 inayomkabili aliyekuwa mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC1) Jerry Muro kama kielelezo cha ushahidi katika kesi hiyo.
Vielelezo hivyo viliwasilishwa jana mahakamani hapo na Ofisa wa Polisi dwani Nyanda ambaye ni shahidi wa sita katika kesi hiyo, mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Gabriel Mirumbe.
Shahidi huyo aliieleza Mahakama kuwa Januari 29, mwaka 2010 akiwa ofisini kwake alipokea maagizo kutoka kwa mkuu wake wa kazi Kamishina wa Upelelezi Charles Mkumbo akimtaka kufanya upekuzi katika gari yenye namba za usajili T 545 BEH mali ya Jerry Muro.
Alidai alishuka kwenda kulifuata gari hilo lililokuwa limepaki kwenye maegesho ya magari ya kituo kikuu cha polisi kati akiwa na mlalamikaji Michael Wage pamoja na mashahidi wengine ili kushuhudia zoezi la upekuzi huo.
“Wage aliyekuwa analalamika kutishiwa kuuawa na Muro alikuwepo makusudi ili kuitambua miwani yake aliyodai kuisahau katika gari ya Muro siku aliyokamatwa na pingu aliyodai kutishiwa kufungwa nayo.
“Baada ya upekuzi huo vitu vyote vilirekodiwa na kusainiwa na mimi na Muro mwenyewe kama uthibitisho kwamba kweli vitu hivyo vilikutwa garini kwake,” alidai shahidi huyo.
Katika kesi hiyo Muro na wenzake Edmund Kapama na Deogratius Mgasa wanadaiwa kuomba rushwa ya Sh milioni 10, kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Michael Wage, Januari 29 mwaka jana.
Mwendesha mashitaka wakili Mkuu wa Serikali Boniface Stanslaus alidai kwa jana upande wa mashitaka ulikuwa na shahidi mmoja ambapo wengine watatu waliobaki watatoa ushahidi wao pindi kesi hiyo itakapopangiwa tarehe nyingine. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 7 na 8, mwaka huu itakaposikilizwa tena.
[ Read More ]

OPRAH REVEALS HER FAMILY SECRET ON HER SHOW.


Meet Oprah Winfrey's Half-Sister Patricia
Oprah Winfrey and sister Patricia
Reunion: Winfrey sits down and chats to her half-sister in front of fans on her TV talk show
She was the family secret that Oprah Winfrey called "one of the greatest surprises" of her life. 

But on Monday's 
Oprah Winfrey Show, Patricia, the media mogul's half-sister, stepped forward in a very public way. 

During the show, Winfrey revealed that she learned she had a sister last October, saying the discovery "left me speechless." 

She was 9-years-old and living with her father in Tennessee when her mother, Vernita Lee, became pregnant with a daughter, Patricia, who was given up for adoption. Born in 1963 in Milwaukee, Patricia would later live in a series of foster homes until the age of 7. She was then adopted, but said her childhood was "difficult." 

Tracing her roots took years of perseverance but Patricia finally discovered her mother – and her half-sister. 

"I received this big old package of information in the mail," Patricia said during Monday's interview. "And it has all of my birth information in it. I was like, 'Oh my God. I have a family.' " 
**************************************



OPRAH'S FAMILY HISTORY

Oprah
Oprah was born to unmarried teenagers, Vernita Lee, a housemaid, Vernon Winfrey, who was in the Armed Forces.
During her childhood was raised at various times by her grandmother Hattie Mae Lee in Mississippi, her mother in Milwaukee, and her father in Nashville.
She was raped and abused by family friends, who have not been publicly  identified, while in Milwaukee.
She moved to Nashville permanently in 1968 to live with her father while she was secretly pregnant at 14. She gave birth to a son, who died when he was just a week old.
Oprah had two half-siblings on her mother's side - Jeffrey, who died in 1989, and Patricia, who passed away in 2003.
She met her secret half-sister - who, by coincidence, is also named Patricia - in November last year.
[ Read More ]

KESI YA JERRY MURO YAZIDI ILIVYOUNGURAMA LEO

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imepokea risiti ya pingu kama kielezo cha ushahidi katika kesi ya kuomba rushwa ya sh. milioni 10 inayomkabili aliyekuwa mtangazaji wa TBC 1 Jerry Muro na wenzake Edmund Kapama na Deogratius Mgasa.

Risiti ya Pingu hiyo iliwasilishwa na shahidi wa tano katika kesi hiyo ofisa mpelelezi Anthony Mwita (45), ambaye aliieleza Mahakama kuwa risiti hiyo yenye namba 341573B, aliipata katika duka la silaha la Mzinga lililoko Upanga jeshini jijini Dar es Salaam.

Alisema alifika katika duka hilo kupata uthibitisho kama pingu aliyokutwa nayo Jerry ilinunuliwa kwao ambapo nao walithibitisha kumuuzia pingu hiyo yenye thamani ya sh.25000 Mei 26, mwaka 2009 .

Mbali na kuwasilisha risiti hiyo pia shahidi huyo alidai katika upelelezi wake alienda katika Hoteli ya Seacliff ili kuthibitisha kama Jerry alifika hotelini hapo Januari 29, mwaka 2010.

Alidai alifika hotelini hapo Januari 31, mwaka jana na kumuona mlinzi wa KK Security aliyemtaja kwa jina la Brightone Babamika na kumuomba daftari la kuandikisha magari yaliyoingia hotelini hapo Januari 29 ambapo aliwapatia na kuona gari ya Jerry yenye namba za usajili T 545
TEH aina ya Cresta ambayo iliingia saa 7:33 mchana na kukabidhiwa kadi namba 673 na kuondoka saa 8:44 mchana.

Mwita alidai aliingia hotelini na kuuomba uongozi kuwaonyesha picha katika kamera ya CCTV ya matukio ya Januari 29 ambayo walionyeshwa na kupatiwa nakala ya picha hizo, lengo likiwa ni kuthibitisha kama kweli Jerry alifika hapo siku hiyo.

Naye shahidi wa nne alidai mahakamani hapo kuwa malalamikaji Michael Wage alikuja na fedha kiasi cha Sh milioni 10 kwenye ‘briefcase’ lakini hakuzihesabu.

Kesi hiyo itaendelea tena kesho mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Gabriel Mirumbe.
[ Read More ]

KESI YA JERRY MURO ILIVYOUNGURAMA LEO

MHASIBU wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo aliyesimamishwa kazi na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa ubadhirifu wa fedha za Umma Michael Wage, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa alikubali kutoa Sh milioni 10 alizoombwa na aliyekuwa mtangazaji wa shirika la Habari Tanzania (TBC1) Jerry Muro kwa kuogopa kubambikiziwa kesi kama Liyumba.

Wage, ni shahidi wa tatu katika kesi ya kuomba rushwa ya Sh milioni 10, inayomkabili Muro na wenzake Edmund Kapama na Deogratius Mgassa, walidai mahakamani hapo kuwa alitishiwa maisha na washitakiwa hao na alikiri kutoa Sh milioni moja kwa ahadi ya kumalizia nyingine tisa
kesho yake.

Akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Gabriel Mirumbe, alidai kuwa mfululizo wa matukio hayo ulianza Januari 28, mwaka 2010 jioni, akiwa nyumbani kwake Bagamoyo ambapo alipokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa jina la Jerry Muro na mtangazaji
wa TBC1.

Alidai Muro alimtaka kufika Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya naye mahojiano kwamba kuna taarifa za tuhuma zinazomkabili zilizoanza kusambaa ambazo alitaka kuweka sawa ambapo alikuja na kukutana na Muro katika mgahawa wa Carlifonia kama walivyoahidiana ambapo baada ya kukutana Muro alimwambia alikua akiandaa kipindi kuhusiana na tuhuma zake ambapo alimtaka waende katika Hoteli ya Seacliff ambako mahojiano hayo yangefanyika.

Alidai wakiwa njiani kwenye gari ya Muro kuelekea Seacliff Muro alimpigia mtu simu na katika maongezi yake alimtaja yeye (Wage) na alipokata simu alimuuliza alikuwa akiongea na nani, Muro akamjibu kuwa huyo ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambaye pia alikuwa na maongezi na yeye.

Wakiwa bado njiani Wage alidai kuwa Muro alimwambia kuwa yeye ni Ofisa wa jeshi, ana nyota tatu na amesomea Marekani, ambapo alifungua ‘dashboard’ ya gari akatoa pingu na kumwambia kama akifanya vurugu au fujo ya aina yoyote angemfunga pingu na kisha alitoa bastola yenye
kitako cha rangi ya damu ya mzee na kumwambia kama yote yangeshindikana basi angempiga risasi na kumuua.

Alidai walipofika Seacliff walipokelewa na mtu mmoja mrefu, mweupe na mnene aliyejitambulisha kuwa yeye ni Kaimu mkurugenzi wa TAKUKURU anaitwa Mussa na baada ya muda akaja mwingine aliyejitambulisha kuwa ni msaidizi wa Kaimu Mkurugenzi wa TAKUKURU.

Wakiwa wamekaa meza moja Kaimu Mkurugenzi akamwambia kuwa ana tuhuma za ufisadi na kwamba hajafikishwa mahakamani aseme kama atahitaji msaada wao ambapo aliwajibu kuwa yeye sio fisadi.

Wage alidai Kaimu Mkurugenzi alimwambia kuwa hata Liyumba hakufanya kosa bali alimuambukiza Ukimwi bibi wa jamaa yake ambaye wanafanya naye kazi.

Alidai baada ya maelezo hayo alimuomba Muro amsaidie ambapo alimuomba atoe Sh milioni 10, naye akawajibu hakuwa nayo pale alikuwa na Sh. milioni moja tu, na hizo nyingine angekwenda kuwatafutia na kuziwasilisha kesho yake.

Alieleza akiwa na watu hao aliamua kumpigia mke wake aliyekuwa Morogoro simu na kuweka kipaza sauti ambapo alimtaka kumletea Sh. milioni tisa kesho, mkewe huyo alidai asingeweza kupata milioni tisa kwa kesho badala yake angeleta milioni nne tu.

Alidai kutokana na matukio ya siku hiyo aliwapigia simu ndugu zake ambao walimshauri kuripoti polisi ambapo kesho yake alienda kuripoti katika kituo cha polisi kati jijini Dar es Salaam, ambapo walimwambia ampigie simu Muro amwambie wakutane katika mgahawa wa City Garden maeneo ya Posta mpya mkabala na klabu ya Billicanas.

Wage alidai alimpigia simu Muro na kukubaliana kukutana hapo ambapo alifika saa 4:30 asubuhi na kumpigia simu kumfahamisha kama ameshafika na ndipo akajitokeza akiwa na polisi waliovalia kiraia ambapo Muro alipowatambua akataka kukimbia lakini polisi wakalizuia gari lake.

Shahidi huyo aliwatambua washitakiwa hao mahakamani na pingu, bastola na miwani ambavyo viliwasilishwa na upande wa mashitaka kama utambulisho katika kesi hiyo. Shauri litaendelea kusikilizwa tena leo kwa mashahidi upande wa mashitaka kuendelea kutoa ushahidi wao.
[ Read More ]

MFUNGWA KUTOKA URUSI AFARIKI ZANZIBAR CHUO CHA MAFUNZO


RAIA mmoja wa Russia, aliyekuwa akitumikia kifungo cha maisha katika Chuo cha Mafunzo Zanzibar amefariki dunia.

Inarserger Othirov, amefariki dunia Januari 9, mwaka huu katika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja ambapo alikuwa amelazwa katika hospitali hiyo akipatiwa matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa za Daktari kutoka Hospitali hiyo ya Mnazimmoja, marehemu alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya homa, kifua kikuu (TB), pamoja na uvimbe uliojaa maji katika pafu lake la upande wa kulia.

Staff Ofisa wa Vyuo vya Mafunzo, Makao Makuu Kilimani wilaya ya Mjini Unguja, Makame Kombo Ame, alithibitisha kutokea kifo cha mwanafunzi huyo wa Chuo cha Mafunzo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko ofisini kwake, Staff Ofisa huyo, huyo alisema kuwa, marehemu amefariki siku tisa mara baada ya kufikishwa hospitalini hapo kwa matibabu.

Alisema kuwa, kabla ya kifo chake Ivan Ochirov kama jina lake la umaarufu alilokuwa akijulikana nalo Chuoni humo, alikuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Chuoni humo, lakini baadae alilazimika kupelekwa Hospitali Kuu ya Mnazimmoja baada ya hali yake kuwa mbaya.

Akiwa hospitalini hapo kwa matibabu, Januari 9 mwaka huu majira ya saa 12:15 za asubuhi Ivan alifariki dunia, kwa mujibu wa Staff Ofisa huyo.

Alifahamisha kuwa, mara baada ya kifo hicho mwili wake ulikabidhiwa wazee wake wote wawili waliokuwepo hapa nchini, chini ya usimamizi wa Balozi wa Russia nchini Tanzania kwa taratibu za mazishi.

Kwa mujibu wa Staff Ofisa huyo, mazishi ya marehemu huyo yalifanyika Zanzibar saa nane mchana, katika ufukwe wa pwani ya Migombani ngazi mia, kwa kuuchoma moto mwili wa marehemu huyo.

Ivan alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi wawili wanaotumikia kifungo cha maisha Chuo hicho cha Mafunzo, baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi kijana mwenzao raia wa Russia kwa kumchoma moto, tukio ambalo lilitokea Zanzibar mwaka 1998.

Kabla ya adhabu hiyo, Ivan na mwenzake huyo (jina halikupatikana), ambaye naye pia ni raia wa Russia, Mei 31, 2001 walihukumiwa kutumikia Chuo hicho kwa muda wa miaka 15, baada ya kupatikana na hatia ya kuua bila ya kukusudia katika kesi ya jinai namba 14/1998 iliyokuwa ikiwakabili Mahakama Kuu ya Zanzibar.

Lakini hata hivyo, Aprili 23, 2004 jopo la Majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, ilitengua adhabu hiyo na kuwahukumu kunyongwa hadi kufa, baada ya kuonekana kuwa wameua kwa makusudi.

Adhabu hiyo imetolewa baada ya kushindwa kwa rufaa yao waliyoiwasilisha mahakamani hapo, kwa kupinga adhabu hiyo ya miaka 15 Chuo cha Mafunzo iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Zanzibar.

Hata hivyo, aliyekuwa Rais wa Zanzibar kwa wakati huo Dk. Amani Abeid Karume, Novemba 12, 2002 aliwapatia msamaha kutoka adhabu hiyo ya kunyongwa hadi kifungo cha maisha.

Kwa mujibu wa Staff Ofisa huyo, pamoja na kutumikia kifungo cha maisha Chuoni hapo, hali ya mwanafunzi mwenzake bado inaendelea vizuri.
[ Read More ]