Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

MUUNGANO WA MAKAMPUNI YA OMAN KUWEKEZA SHIRIKA LA NDEGE ATCL SHS. BILIONI 160

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Oman Oktoba mwaka 2012 baada ya kualikwa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said ambapo aliambatana na ujumbe wa mawaziri na viongozi waandamizi wa biashara.
Katika ziara hiyo Rais Kikwete alibadilishana uzoefu wa uhusiano na kuangalia namna ya kudumisha
ushirikiano wa nchi hizo mbili kuhusiana na biashara, elimu, utamaduni na mambo mengine.
Hiyo ilikuwa ni ziara ya pili muhimu ya kiongozi wa Tanzania kutembelea nchi hiyo tangu mwaka 1985 wakati Rais wa kwanza, hayati Julius Nyerere akiwa madarakani.
Ziara hiyo ya Rais Kikwete inaonyesha umuhimu wa namna nchi hizo mbili zinavyojenga mahusiano makubwa na undugu baina yao.
Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na Oman lililofanyika Oktoba 16 katika Hoteli ya Al Bustan Palace wakati Rais Kikwete akitoa hotuba yake.
Kongamano hilo liliangalia fursa za kibiashara katika rasilimali zilizopo katika nchi hiyo iliyopo Ukanda wa
Afrika Mashariki zikiwemo kilimo, viwanda, utalii, usafirishaji, mafuta na gesi.

Kituo cha Uwekezaji (TIC)Tanzania kiliwasilisha namna uwekezaji katika kiuchumi na nafasi za uwekezaji nchini Tanzania.
Mwishoni mwa tukio hili muhimu, malaka za nchi hizi mbili zilisaini na kukubaliana kuanzisha Baraza la Biashara kati ya Oman na Tanzania ambalo litakuwa ni hatua muhimu katika kuanzisha uhusiano wa mataifa hayo mawili katika ngazi ya juu.
Madhumuni mengine muhimu ya ziara hiyo yalikuwa ni pande hizo mbili kusaini makubaliano ya kukuza na kuulinda uwekezaji jambo ambalo ni kichochezi katika Baraza hilo la Biashara la Oman na Tanzania, itarahisisha kutoa fursa za kibiashara na uwekezaji kati yao.
Pia makubaliano ya kupeana ushauri katika masuala ya siasa yamesainiwa hivyo itakuwa ni njia nzuri ya uzileta nchi hizo mbili zenye undugu karibu katika jambo hilo
muhimu.
Walisaini makubaliano kuhusu Utunzaji kumbukumbu na Nyaraka ambazo zinatunza kumbukumbu za historia muhimu kwa vile nchi hizo mbili zina historia inazofanana kiasi fulani.
Kubadilishana huko kwa nyaraka na kumbukumbu za historia kunaweza kusaidia kuchimbua matukio
ya kihistoria yaliyotokea zama hizo. Walisaini makubaliano ya kushirikiana katika elimu ya juu.
Oman na Tanzania zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu hivyo ziara hiyo ya Rais Kikwete inalenga
kufungua fursa nyingi na hatimaye kufikia ngazi wanazostahili wananchi.
Nchi hizo zinafaidika na upendo baina ya watu wake kwa sababu Oman ni nchi pekee nje ya Afrika ambako wananchi wengi wanazungumza Kiswahili na Wa-Oman wamezaliana na Watanzania pamoja
na kuwa na utamaduni wa aina moja.
Kuna uwezekano mkubwa wa kufungua fursa za usafiri wa ndege ndani na nje ya Afrika katika uwekezaji na biashara katika juhudi za kibinadamu.
Tanzania ina fursa kubwa za uwekezaji katika sekta za
mifugo, uvuvi na kilimo.
Ikiwa imebarikiwa kuwa na eka za ardhi yenye rutuba, maji na hali nzuri ya hewa, Tanzania ni mahali
pazuri kwa Oman kuwekeza na kukuza shughuli za kilimo ili kufanikisha mahitaji yake.
Hii ni namna Oman inavyoweza kujibadilisha yenyewe kutoka kuwa muingizaji wa bidhaa nchini na kuwa muuzaji wa bidhaa za matunda na mboga mboga nje ya
nchi hivyo kujihakikishia kutokuwa tegemezi wa chakula.
Kwa vile Tanzania imegundua visima kadhaa vya Mafuta na gesi, na nchi hizo mbili zinaweza kuanzisha
ushirikiano katika suala hili ambalo litawanufaisha wote kwa pamoja.
Oman inaweza kuwekeza katika miundombinu iliyokua nchini Tanzania kama barabara, madaraja, hoteli,
resort na pia katika usafirishaji, na sekta ya usafiri wa njia ya meli.
Pia sekta ya viwanda itatoa fursa za uwekezaji kwa Serikali ya Oman na jamii ya biashara.
Cha muhimu ni kwamba nchi ya Tanzania yenye ananchi 44,929,002 inahudumia soko la watu milioni 150 katika nchi zake za jirani kupitia Bandari ya Dar es
Salaam.
Tanzania ni nyumbani kwa baadhi ya maeneo muhimu duniani kwa shughuli za utalii na miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la wageni kutoka Oman wakienda nchini Tanzania jambo ambalo limefanya safari za ndege za Ndege ya Oman ziwe nyingi.
Tanzania ni nchi kubwa zaidi Afrika Mashariki ikiwa na jiografia inayoruhusu uwekezaji katika sekta ya utalii ambapo pia inasifika kuwa na hali nzuri ya hewa, ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha na rasilimali
ambayo inavutia uwekezaji.
Baada ya ziara Rais Mheshimiwa Dk.Jakaya Kikwete, Umoja wa wadau wa biashara nchini Oman umeamua kuwekeza fedha kiasi cha sh.bilioni 160 ili kuendeleza Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).
Hatua hiyo ilikuja baada ya mkutano kati ya Kikwete na ujumbe wa wafanyabiashara hao.
Akizungumza wiki hii, Mwenyekiti wa Al Hayat Development na kampuni yake ya uwekezaji, Sheikh
Salim Al Harthy alisema wanashukuru kwa msaada huo uliotolewa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said Sultan wa Oman.
Alisema wanashukuru kwa vile msaada huo utasaidia na kuimarisha ushirikiano wa kibiashara kati ya mataifa hayo mawili hasa baada ya makubaliano kufikiwa kati ya viongozi wa nchi hizo.
Na kama sehemu ya kujitolea kwao huko wanadhamiria kusaini makubaliano na Air Tanzania na kuwekeza
dola milioni 100 na kuongoza wawekezaji ambao tumekuwa na uhusiano nao wa karibu.
Alisema uekezaji huo utatumika katika kukodisha na kununua ndege ambazo zitatumika katika safari za
ndani na nje ya Afrika kukuza biashara ndani ya Tanzania na nchi
nyingine.
Sheikh Salim Al Harthy aliongeza kuwa fursa hiyo ilikuja kwa ukarimu na matarajio mazuri ya Rais Kikwete na Serikali ya Tanzania kwa kutuamini kuja kuwekeza
katika kushughuli za kiuchumi nchini Tanzania.
“Tunamshukuru Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said wa Oman na Rais Kikwete wa Tanzania kutupa nafasi
hiyo hasa ukizingatia kipindi hiki tuna mpango wa kujenga kituo cha mafunzo ya masuala ya ndege, ofisi
nzuri kwa ajili ya ATCL, kununua ndege na kufanya shughuli nyingine za maendeleo tunazotarajia kuanza
ndani ya miezi sita hadi kumi” alisema.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akiwa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said wakati wa
ziara yake nchini Oman.
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Al Hayat, Shaikh Salim Al Harthy, wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mkuu wa ATCL, Kapteni Milton Lazaro. Wa kwanza kushoto ni Al Sayyid Fahar Bin Taimur Al Said na kulia ni Bwana Saeed S. Bawazir kama wa wakilishi wa Al Hayat inchini Tanzania.
[ Read More ]

SMZ UIMARIKAJI WA SECTA YA UTALII UMEANZA KUSHAMIRI ZANZIBAR


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akishusha Nanga kuashiria kuweka jiwe na nanga la ujenzi wa chumba cha chini ya bahari katika Hotelai ya Manta Resort iliyoko Makangale Kaskazini mwa Kisiwa cha Pemba.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akishusha Nanga kuashiria kuweka jiwe na nanga la ujenzi wa chumba cha chini ya bahari katika Hotelai ya Manta Resort iliyoko Makangale Kaskazini mwa Kisiwa cha Pemba.
Harakati za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha Sekta ya Utalii zimeanza kuonyesha dalili za mafanikio kufuatia uwekezaji wa daraja la juu katika sekta hiyo kuanza kushamiri kidogo kidogo hapa Nchini.
Ujenzi wa chumba cha chini ya bahari { under water room} ulioanzishwa kama mradi maalum wa kuvutia watalii wa daraja la kwanza unaofanywa na Uongozi wa Hoteli ya Manta Resort iliyopo Makangale Mkoa wa Kaskazini Pemba ni miongoni mwa dalili hizo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikuwa mgeni rasmi katika uwekaji wa jiwe la nanga la ujenzi wa chumba hicho kitakachokuwa chini ya Bahari ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya kutimia miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Balozi Seif akiambatana na Viongozi mbali mbali wa Serikali, Wizaraya ya Habari wakiwemo maafisa wa sekta ya Utalii na wanasiasa alionekana kufarajika na mradi huo mpya ndani ya Bara la Afrika na ni wa pili kufanywa Duniani ukitanguliwa na ule wa Sweden ulioko katika maji ya ziwa.
Chumba cha chini ya Bahari kikionekana kwa mbali kikiendelea na matengenezo kwenye Hoteli ya Manta Resort Makangale iliyoko Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Chumba cha chini ya Bahari kikionekana kwa mbali kikiendelea na matengenezo kwenye Hoteli ya Manta Resort Makangale iliyoko Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Akizungumza katika hafla hiyo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema ni jambo la kutia moyo kuona Kisiwa cha Pemba hivi sasa kinanza kupanuka Kiutalii kufuatia kuimarika kwa miundombinu iliyowekwa.
Aliwataka wananchi wa Kisiwa cha Pemba kuchangamkia sera ya Utalii kwa wote kwa lengo la kuitumia fursa hiyo adhimu kabla haijavamiwa na wafanyakazi wa nje ya Visiwa hivi.
‘’ Pemba sasa ni eneo ambalo Serikali inaliangalia katika kufunguka kiutalii hasa kutokana na kukamilika kwa miundombinu ya umeme na Bara bara’’. Alifafanua Balozi Seif.
Alikumbusha kwamba Zanzibar bado haijatangazwa kiutalii nje ya Nchi na watu wanaofikia hatua za kufanya hivyo huitangazia kwa
maslahi yao binafsi.
Balozi Seif ameiagiza Taasisi inayosimamia uwekezaji vitega uchumi Zanzibar { ZIPA } kuziangalia upya sheria zilizopo za uwekezaji ili kuwepuka kurejea makosa yaliyojitokeza tokea kuimarishwa kwa sekta ya Utalii Nchini.
Alisema ipo miradi ya uwekezaji ambayo imekuwa mtihani kwa serikali kwa vile imeshindwa kutoa huduma zilizokusudiwa akiutolea mfano mradi wa Hoteli ya Mawimbini ambao kmwa sasa umeshindwa kufanya kazi.
Akimkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Mh. Said Ali Mbarouk alisema mradi huo wa chumba cha chini ya Bahari masafa ya Mita 100 ni wa majaribio.
Mh. Said alieleza kuwa mradi huo wa chumba kimoja  utakapofaulu Uongozi wa Hoteli ya Manta Resort umekusudia kujenga vyumba vingi zaidi ili kufanikisha utali wa daraja la juu.
Mapema Meneja wa Hoteli ya Manta Resort Makangale Bwana Metthew Saus Maarufu kwa jina la Babu kwa nini alisema wazo la ujenzi wa mradi huu lilichukuwa takriban miaka saba kwa kufanywa utafiti chini ya bahari.
Babu kwani alisema Kisiwa cha Pemba kina mazingira mazuri ya kuendeleza mradi huo ikilinganishwa na mradi wa mwanzo Duniani kama huo ulioanzishwa Nchini Sweden.
Amewapongeza wananchi wa Zanzibar kwa kusherehekea miaka 49 ya mapinduzi Matukufu ya mwaka 1964 yaliyowatoa katika makucha ya wakoloni.
 Meneja wa Hoteli ya Manta Resort Makangale mkoa wa kaskazini Pemba Bwana Metthew Saus { Maarufu Babu kwanini na msaidizi wake  wakiwa tayari kumsubiri mgeni rasmi Balozi Seif Ali Iddi kuweka jiwe la nanga katika ujenzi wa chumba cha chini ya bahari.
Meneja wa Hoteli ya Manta Resort Makangale mkoa wa kaskazini Pemba Bwana Metthew Saus { Maarufu Babu kwanini na msaidizi wake wakiwa tayari kumsubiri mgeni rasmi Balozi Seif Ali Iddi kuweka jiwe la nanga katika ujenzi wa chumba cha chini ya bahari.
[ Read More ]

UTATA WAGUBIKA KIFO CHA MWANAFUNZI ALIYEFIA HOTELINI


UTATA mkubwa umegubika kifo cha mwanafunzi Jackline Musa Matiko (15) aliyekuwa akisoma katika Shule ya Sekondari Juhudi iliyopo Gongo la Mboto Wilaya ya Ilala aliyekutwa amekufa katika Hoteli ya Southern Resort, Kigamboni Dar es Salaam baada ya wazazi wake kudai kuwa hakufa maji bali alinyongwa.
Ndugu na jamaa wa marehemu Jackline Musa Matiko, wakitoa mwili wa ndugu yao katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, baba wa marehemu, Mussa Matiku alisema baada ya kuikuta maiti ya mtoto wake kando ya bwawa katika hoteli hiyo na kuichunguza shingo yake aliiona imelegea na tumbo lake halikujaa maji kama watu wanaokufa kwa maji wanavyokuwa.
Alisema kwa vigezo hivyo ni wazi kwamba mwanaye hakufa maji na amelitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini waliomuua kikatili binti yake.
 Naye mjomba wa marehemu ambaye alikuwa na Jackline kabla ya kifo chake aliyejitambulisha kwa jina moja la Abdul, alisema  binti huyo alitoka nyumbani kwa wazazi wake maeneo ya Mazizini Ukonga kwenda Gongo la Mboto kwa bibi yake kusherehekea Sikukuu ya  Mwaka  Mpya.
Jackline Musa Matiko (15) enzi za uahi wake.
“Baada ya kufika pale na kupata chakula cha mchana pamoja  na ndugu zake, Ilipangwa kwenda  kutembea kokote walikohitaji ambapo walichagua  kwenda Quality Centre.
Aliongeza kuwa walipofika huko waliamua kwenda Southern Beach Resort Kigamboni ambako ndiko waliposherehekea siku hiyo ya mwaka mpya.
 Akadai kuwa wakati wakiwa huko walikuwa wakinywa vinywaji laini, kucheza muziki pamoja na kuogelea lakini akawapa  tahadhari kuwa kila anayetoka kwenda sehemu yoyote ahakikishe anarejea walipokuwepo wenzake.
Akaongeza: “Ilipofika saa moja usiku Jackline hakuonekana ndipo nikawa na hofu na kuanza kumtafuta huku nikiwa nimewaambia wenzake wasitoke eneo nililowaacha.
“Kutafuta kwangu hakukuzaa matunda nikaenda kwa uongozi wa bichi kueleza kuhusiana na tukio hilo nao pia wakatangaza  kwa kutumia kipaza sauti kuwa mtoto amepotea huku akiwa  anatajwa  jina lake pia hapakuwa na mafanikio.”
Baada ya kuona jitihada za kumpata Jack hazikuzaa matunda walikwenda kutoa taarifa Kituo Kidogo cha Polisi Vijibweni kisha wakarudi nyumbani.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Jackline Musa.
Abdul aliongeza kuwa anachohisi uongozi ulishajua kuwa tukio  hilo lilitokea lakini waliamua  kumficha kwa kuhofia  kama wangesema ukumbi ungefungwa na biashara  ingekuwa ndiyo mwisho kwa siku hiyo.
Aliongeza kuwa asubuhi walipigiwa simu na polisi wakielezwa kuwa kuna mtoto aliokotwa akiwa amekufa na walipokwenda kuhakikisha wakakuta ni Jackline.
Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Kipolisi Temeke, ACP Engelbert Kiondo alipohojiwa na gazeti hili alisema upelelezi wa tukio hilo ulisubiri ripoti ya madaktari ili kujua kama mtoto huyo alikufa maji au aliuawa kisha kutupwa karibu na bwawa la hoteli hiyo.
Marehemu Jackline alizikwa Januari 3, mwaka huu eneo la Moshi Bar Ukonga.

Habari na global.
[ Read More ]

Disappointment Misses No One.



Each of us experiences disappointments in our life,Disappointment springs up regularly in the workplace because many of us have limited control over our work surroundings.
You get passed over for leading a task force, even though you have all the requisite skills and experience. Someone else gets the raise that you thought you deserved. Your co-worker says she is going to support you on a task and she ducks out. That manuscript you submitted was rejected by a third journal. One of your clients pulled the plug – he doesn’t want to work with you anymore .
None of this feels good.
Ever notice how you don’t like the feeling of disappointment? How incredibly discomforting it is? What you will do to avoid it? Me too.
As humans, we squirm away from disappointment. Oftentimes we get disheartened and start obsessing about the story line that led to our disappointment instead of connecting with the actual feeling. We blame – others, the economy, our childhood, traffic — even the dog. We think of ourselves as failures. We push disappointment away turning it into anger. Or we push it down turning it into depression. Just having it near us can be so scary.

Life is a constant changing wave – with the high tide of joys and the low tides of disappointment and everything else in between. When we keep pushing disappointment away from us at work, we also give our human wholeness  a shove. That part of us that contains our essential goodness.
I don’t want to get carried away with the eye story, but last year I had a lot of disappointments. separated from my family, hospitalized more than six time,  Diagnosed With Keratoconus , undergo c3r surgery, good-bye chocolate, ice-cream and all delicious food .
In my reflection time during treatment, I realized that the more pushed the feelings of disappointment away, the more miserable I became. And when I tried to hide from them, they started to creep toward me like King Kong. When I shunned them, they were so persistent – tapping me on the shoulder.
And so I started snuggling up with them, just like a good book. I leaned in, got comfortable, and remained still. No pushing. No blaming. Some moments, disappointment would be stuck in my body – not budging. I’d need to breathe into it and invite it in a bit closer. Holding my vulnerability, being with the tenderness. Soothing, without a story. Tuning into the sensation. Naming the feeling, “Aah, that was disappointment.” And off it would go.
What I experienced over and over again is that disappointment doesn’t want to stick around. It wants to get its running shoes on and trek out away from us. But sometimes it’s us that keep dragging our disappointments through our muddy storylines. We won’t let go of it. We are tethered to its pay-off. More suffering.
It’s truly our choice.

I’ve had enough disappointments professionally and personally to know they are transitory. What is a disappointment one day may turn out to be an opportunity the next. Think about when you thought a window was closing and then all of a sudden a big door of opportunity swung open. Perhaps your job was getting grueling and laborious but it was just the spark plug for you to seek a better one. Sometimes a disheartening event gets us ready to take the next big leap – the next big jump toward bigger joy, more appreciation, and greater kindness.
I can’t imagine a more perfect this day – with my  friend and a heart full of gratitude for each step of the way. All year’s disappointment transformed into this year’s magnificent joy.

May your disappointments circle back as blessings. And this day, as always, may you be wise at work.

Remember Inspire Me Daily.One Person Can Make a Difference

[ Read More ]

RAIS DK. SHEIN AZINDUA BOHARI KUU YA DAWA ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kama ishara ya uzinduzi
wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa,Maruhubi Nje ya Mji wa Zanzibar jana
ikiwa ni shamra shamra za kilele  cha miaka 49 ya Mapinduzi Matukufu
ya zanzibar,(kulia)  Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Alfonso
Lenhardt.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akikata utepe kama ishara ya uzinduzi
wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa,huko Maruhubi Nje ya Mji wa Zanzibar
jana ikiwa ni shamra shamra za kilele  cha miaka 49 ya Mapinduzi
Matukufu ya zanzibar,(kulia) ni Naibu waziri wa Afya Sira Ubwa Mamboya
na  Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Alfonso Lenhardt.[Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa
Bohari Kuu,Said Mohamed,(kulia) alipotembela sehemu ya kuhifadhia
Dawa,baada ua uzinduzi wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa huko Maruhubi
Nje ya Mji wa Zanzibar,ikiwa ni shamra shamra za kilele  cha miaka 49
ya Mapinduzi Matukufu ya zanzibar,(wa tatu kushoto)  Balozi wa
Marekani Nchini Tanzania Alfonso Lenhardt.[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa tatu Kulia)pamoja na Viongozi
wengine akiwemo Balozi wa Marekani Nchini  Alfonso
Lenhardt.wakiangalia namna ya uchukuwaji dawa kwa kutumia mashine
maalum na kutoa nje ya Bohari kuu ya Dawa,baada ya ufunguzi rasmi jana
huko Maruhubi Nje ya mji wa Zanzibar,ikiwa ni shamra shamra za kilele
cha miaka 49 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzíbar  
………………………………………………
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema uzinduzi wa Bohari kuu ya Dawa utaiwezesha Serikali ya Mapinduzi Zanzíbar kupanga bajeti yake vyema ya dawa na kusaidia utoaji wa huduma za afya kwa ubora wa hali ya juu.
 Rais Shein ameyasema hayo katika hafla ya uzinduzi wa Bohari Kuu ya Dawa iliyopo Maruhubi mjini Zanzibar ikiwa ni mwendelezo wa shamra shamra za kutimiza miaka 49 ya Mapinduzi Zanzibar.
 Amesema Bohari hiyo ya kisasa ni matunda ya kujivunia ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo kwa hakika italeta tija katika upatikanaji wa dawa na uimarisha wa afya za wananchi.
 Dkt. Shein ameelezea matumaini yake kwa sekta ya afya kupitia Bohari hiyo na kwamba anaamini baada ya miaka mitatu Zanzibar itakuwa haipeleki tena Wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu.
 Aidha Dkt. Shein amewataka watumishi wa Serikali kubadilika kiutendaji kulingana na kasi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wa Bohari hiyo kuitunza vyema ili iendelee kutoa huduma kama inavyotakiwa.
 Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya Sira Ubwa amesema Bohari hiyo itaboresha utoaji wa huduma kwa uhakika kutokana na ubora wa vifaa na mitambo ya kisasa ambapo wataalamu wataweza kubaini mahitaji ya Dawa zinazohitajika katika kila Hospitali za Unguja na Pemba.
 Kwa upende wao Mabalozi wa Marekani na Denmark wameelezea kufurahishwa kwao na juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha afya ya Wananchi hasa katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Malaria na Ukimwi.
 Aidha wameahidi kuendelea kutoa mashirikiano kwa Serikali hasa katika huduma za Afya kwa Mama na Watoto, Elimu,Mapambano dhidi ya magonjwa ya maambukizi pamoja na uzazi wa mpango.
 Bohari hiyo iliyojengwa na Serikali ya Mapinduzi kwa msaada wa Shirika la USAID na NIDA inaelezewa kuwa ya tatu duniani katika viwango vya ubora ambapo jumla ya Dolla za Kimarekani Milion 1.2 zimetumika kukamilisha ujenzi wake.
[ Read More ]

YUSUF OMAR CHUNDA AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUWA NA VITAMBULISHO (PRESSCARD)


 
.                                     Mkurugenzi Idara ya Habari,Maelezo Zanzibar Yusuf  Omar Chunda amewataka waandishi wa Habari Nchini kuhakikisha kwamba wanafanya kazi zao wakiwa na leseni za uwandishi wa habari (PRESSCARD) ilikuhakikisha kwamba wanafanya kazi zao hizo    kwa mujibu wa sheriaNo5 ya mwaka 1988 ya magazeti .
 Hayo ameyaeleza leo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali huko katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Chake chake Pemba.juu ya utendaji wa kazi za Idara hiyo kwa mwaka 2012na kuomba mawazo yao kwa utendaji wa kazi kwa mwaka 2013.
 Amesema kuwa na kitambulisho   kitamrahishia mwandishi huyo kufanya kazi kwa mujibu wa sheri  na kupata habari anazozihitaji kwa wahusika bila ya matatizo ambazo  zitachapishwa na kutangazwa katika vyombo mbalimbali vya habari.
 Mkurugenzi huyo amewataka waandishi hao kutopuuza agizo hilo la kuwa na kitambulisho kwani ni kwa faida yao wenyewe kutokana na kazi zao wanazo zifanya kila siku.
 Chunda amesema kuwa viongozi wasionekane wagumu pale wanapotaka kutoa habari kwanza kwa kuuliza waandishi vitambulisho vyao kwani wao wanahitaji kupata uhakika wa mwandishi huyo kama amepata kibali cha kuandika habari nchini kama sheria inavyotaka .
 Amesema kuwa ni vyema kwa waandishi kuelewa kazi zote zinakwenda kwa mujibu wa sheria kwa hivyo waandishi kama kioo cha jamii na wao wanastahiki kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria na wawe mfano.
 Mkurugenzi huyo amewashukuru waandishi wa habari wote kisiwani Pemba kwa mashirikiano mazuri walioipa idara yake katika utendaji wa kazi kwa mwaka 2012 na amewataka mashirikiano hayo yawe endelevu ili kufanikisha shughuli za idara hiyo na Taifa kwa Ujumla .
 Aidha amewashukuru pia waandishi wa habari, viongozi wa dini pamoja na NGOs za habari kwa mashirikiano walioyatoa wakati wakutoa mawazo yao juu ya mabadiliko ya sheria No5 ya mwaka 1988 ya magazeti na Majarida Zanzibar

[ Read More ]

Eti wanawake wenye kipato kisichopungua Milioni 3 kwa mwezi hawaoleki




Inadaiwa kwamba mwanaume anapooa mwanamke ambaye ana mafanikio na ambaye ni msomi au mwenye taaluma, ajue kwamba, ndoa yake imeegeshwa kwenye mawe.

Tafiti za hivi karibuni kabisa zinaonyesha kwamba wanawake wenye mafanikio ya kimasomo pamoja na kipato wako kwenye hatari kubwa zaidi ya kupambana na talaka ukilinganisha na wanawake wa kawaida. Siyo hivyo tu, pia wanaonekana kuwa wako kwenye nafasi ya kutoka nje ya ndoa kirahisi na kutojali sana kuhusu watoto.
Utafiti ulioripotiwa kwenye jarida la Social Forbes kwa mfano, unaonesha kwamba, wanawake wenye mafanikio ya kitaaluma pamoja na kipato hata wanapopata watoto, furaha yao haiwi kubwa kama ya wanawake wengine.
Wanawake hawa hupenda kuona waume zao wanakuwa chini yao kimapato. Hapa kuna utata mkubwa kwa kuzingatia kwamba, wanaume wenye mafanikio hupendelea wanawake wa kaliba yao. Hivyo wanapooana nao ndoa ni lazima iyumbe sana kwa sababu hawa wanawake nao wanataka kutokeza pembe zao.
Kwa kadiri mwanamke anavyostawi kimapato na kupanda juu kitaaluma au hata kicheo, ndivyo ambavyo hamu yake kwa mumewe ambaye naye ana mafanikio inavyopotea.

Kuna mambo mengi yanachangia kufanya ndoa kuwa imara au kuyumba na pengine kuvunjika. Kwa mfano mtu ambaye ametoka familia iliyovunjika kwa talaka, anaweza kuingia kwenye talaka kirahisi, umri wa kuolewa, imani na sababu nyingine zinachangia. Lakini mafanikio ya kipato ni jambo lingine kubwa.
Nikisema mafanikio, nina maana wanawake ambao wamemaliza elimu ya chuo kikuu na ambao pato lao kwa mwenzi haliwezi kuwa chini ya shilingi milioni 3. Je mmeelewa sasa wanawake ninaowazungumzia…?

Kama inabidi tuamini tafiti zote ambazo zimefanywa kuhusu wanawake hawa, ina maana kwamba, kuoa wanawake wa aina hii ni hatari sana. Nasema ni hivyo kwa sababu tafiti nyingi zinaonyesha kuwa wanawake wenye mafanikio kitaaluma pamoja na kipato, huteleza sana kwenye ndoa


source-jamii forum.
[ Read More ]

[ Read More ]

Cyber thieves pose as Google+ social network



..
Web browser makers have rushed to fix a security lapse that cyber thieves abused to impersonate Google+
The loophole exploited ID credentials that browsers use to ensure a website is who it claims to be.
By using the fake credentials, criminals created a website that purported to be part of the Google+ social media network.
The fake ID credentials have been traced back to Turkish security firm TurkTrust which mistakenly issued them.
Screengrab of Google Plus social network
The lapse let cyber thieves trick people into thinking they were on Google+



Secure code
An investigation by TurkTrust revealed that in August 2011 it twice accidentally issued the wrong type of security credential, a form of identification known as an intermediate certificate. Instead of issuing low level certificates it mistakenly gave out two "master keys" that are typically only given to owners of websites. This master key is a guarantee of a site's identity.
"These certificates could be used to impersonate any website to any browser without the end user being alerted that anything is wrong," wrote security analyst Chester Wisniewski from Sophos in a blogpost about the security lapse.
The certificates are important, he said, because secure use of web shops and other services revolve around interaction between the master keys and the lower level security credentials.
The lapse was spotted when automatic checks built in to Google's Chrome browser noticed the fake credentials.
GoogleMicrosoft and Firefox developer Mozilla have all issued updates which revoke the two wrongly issued master security certificates. In addition, Mozilla has updated Firefox to reject any certificate issued by TurkTrust while the browser maker investigates the security lapse.
This is not the first time that websites and browser makers have had a problem with security certificates. Fake certificates have been issued before now by several other firms and exposed confidential data including login names and passwords.
"It is really time we move on from this 20-year-old, poorly implemented system," wrote Mr Wisniewski. "It doesn't need to be perfect to beat what we have."
source bbc
[ Read More ]

MAREHEMU SAJUKI AZIKWA LEO HII KATIKA MAKABURI YA KISUTU! INNA LILLAHI WA INNA ILAYHI RAJ'UN...!!!




 Waombolezaji wa Msiba wa Msanii wa Filamu hapa nchini Marehemu  Sadick Juma Kilowoko wakibeba jeneza lenye mwili wake tayari kwa taratibu za kwenda Mazikoni, wakitokea Nyumbani kwa Marehemu Tabata Bima.
Mwili wa Marehemu Sajuki ukipakiwa kwenye gari
Dua ikisomwa kabla ya kuondoka kwa Mwili wa Marehemu kwenda mazikoni.

Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania,Saimon Mwakifwamba akimpokea Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe alipokuwa akiwasili msibani hapo

Pamoja na mvua kubwa kunyesha haikuzuia watu kufika kwa aajili ya kuomboleza kifo cha Marehemu sajuki
Waombolezaji wakiwa wanajifunika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar


This is it! Hapa ndipo sajuki amelala! May his soul R.I.P

Inna Lillahi Wa Inna Ilayhi Raj'un
[ Read More ]