Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Shambulio la bomu hotelini Pakistan


Takriban watu kumi na mmoja wameuawa na wengine zaidi ya sitini kujeruhiwa katika shambuli la bomu la kujitoa mhanga katika hoteli moja nchini Pakistan.

Kwa mujibu wa maafisa waandamizi nchini humo, shambulio hilo lilitokea katika mji wa Peshawar kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.

Ripoti za vyombo vya habari nchini humo, zimeeleza watu waliokuwa wamejihami waliwashambulia walinzi karibu na hoteli ya kifahari ya Pearl Continental kabla ya kulipua gari liliokuwa limebeba shehena ya mabomu eneo la kuegeshea magari.

Walioshuhudia tukio hilo waliiambia BBC, mlipuko huo ulionekana hadi umbali wa kilomita tano. Sehemu moja ya hoteli hiyo imeporomoka kabisa.

Mwandishi wa BBC nchini Pakistan amesema hoteli hiyo ndiyo maarufu zaidi katika mji wa Peshawar na ni mojawapo ya majengo yanayotambuliwa zaidi ya mji huo.

Miji kadhaa nchini Pakistan ukiwemo ule wa Peshawar imekumbwa na mashambulio ya mabomu tangu jeshi la nchi hiyo lilipoanza harakati za kupambana na wanamgambo wa Taliban.

Hata hivyo hakuna aliyekiri kuhusika na mashambulio hayo.

[ Read More ]

Ghailani lands in New York


UNITED States authorities have announced that Ahmed Khalfan Ghailani, a Tanzanian national accused of involvement in the 1998 US embassy bombing in Dar es Salaam arrived early yesterday morning in New York to face criminal charges. Ghailani had been held at the notorious Guantanamo Bay detention facility in Cuba since September 2006. After a thorough review of his case, the Tanzanian was recently referred for criminal prosecution in the Southern District of New York pursuant to a March 12, 2001 indictment against him. Ghailani was transferred from the custody of the US Department of Defence to the Southern District of New York by America’s Marshals Service. He is currently in custody at the Metropolitan Correctional Centre in New York, which has housed numerous terror suspects over the years during their prosecutions in the city’s Southern District. The Tanzanian was later yesterday expected to make his initial appearance in Manhattan federal court. Ghailani faces 286 separate counts in the indictment. Among other violations, the superseding indictment charges him with conspiring with Osama bin Laden and other members of al-Qaeda to kill Americans anywhere in the world, as well as separate charges of murder for the deaths of each of the 224 people killed in the simultaneous US embassy bombings in Tanzania and Kenya and various other offences related to the bombings. ’’With his appearance in federal court today, Ahmed Ghailani is being held accountable for his alleged role in the bombing of US embassies in Tanzania and Kenya and the murder of 224 people,’’ said US Attorney General Eric Holder. ’’The Justice Department has a long history of securely detaining and successfully prosecuting terror suspects through the criminal justice system, and we will bring that experience to bear in seeking justice in this case.’’ Ghaliani has already admitted having once met bin Laden, but apologized for his role in the bomb explosion. He insisted that he had been kept in the dark about the purpose of the attack on the US embassy in Tanzania. ’’It was without my knowledge what they were doing, although I helped them,’’ said Ghailani, according to official court transcripts. He added: ’’I’m sorry for what happened to those families who lost...who lost their friends and their beloved ones.’’ Ghailani also said he once met Osama bin Laden. More than a decade ago, a federal grand jury in New York indicted Ghailani on charges that he helped plan the bombing of the US embassy in Dar es Salaam on August 7, 1998. At the time, he was still a fugitive. He was finally captured in Pakistan in 2004, held in secret prisons run by the Central Intelligence Agency (CIA), and transferred in 2006 to the naval base at Guantanamo Bay. Last year, US military prosecutors filed war crimes charges against him in connection with the embassy bombing episode. Ghailani thus became a rare detainee facing similar charges in both military and civilian courts, for the same act. The baby-faced and diminutive Tanzanian -- known as ’’Fupi’’ -- faced a bounty of $25m when he was nabbed after a 12-hour shoot-out at an Al Qaeda safe house in Pakistan. Ghailani rose from an Al Qaeda ’’rank-and-file soldier’’ in Afghanistan before the September 11, 2001 (9/11) attacks in the US to become Bin Laden’s cook and his most prolific passport forger and travel agent, according to official records. He was among the original 22 ’’most wanted’’ terrorists designated by ex-President George W. Bush’s Federal Bureau of Investigations (FBI) after 9/11, even though the US government admits he ’’was not directly involved in operational planning’’ by Al Qaeda. US President Barack Obama has come under sharp criticism from Congress for allowing Ghailani to be transferred to America to face criminal charges.
[ Read More ]

Shahidi aeleza maiti ya albino alivyookotwa

KESI inayowakabili washitakiwa wa mauaji ya albino mkoani Shinyanga iliendelea kusikilizwa jana ambapo shahidi wa kwanza alianza kutoa ushahidi wake mbele ya Jaji Gadi Mjemas wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Akitoa ushahidi huo huku akiongozwa na wakili wa Serikali Bi. Veritas Mlay shahidi huyo Bw. Mayenga Matongo ambaye alikuwa Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Harawa alidai kuwa Desemba 4 mwaka juzi akiwa ofisini kwake alipokea taarifa kutoka kwa Yusuph Ramadhani kuwa kuna maiti imeonekana imetupwa katika mto Kidamlida.

Bw. Matongo alidai baada ya kupokea taarifa hizo aliandika barua kwa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Isanga Bw.Sayi Gamanya kumtaka aende kuangalia sehemu ya tukio ili kuthibitisha tukio hilo.

Aidha Shahidi aliongezea kuwa Bw. Gamanya hakutii agizo hilo ndipo shahidi alikwenda na baadhi ya watu katika mto wa kidamlida na kuanza kuusaka mwili ambapo saa 12:00 jioni Mei 4 mwaka jana walifanikiwa kuuona ukiwa kwenye kisima cha kunyweshea mifugo.

Bw.Matongo aliendelea kudai kuwa alitoa taarifa polisi wa Wilaya ya Bariadi Aprili 5 saa 7 mchana polisi walifika eneo hilo na zoezi la kuutoa mwili huo lilianza ambapo ilikutwa imekatwa kichwa na miguu yote miwili na kuhifadhiwa kwenye mfuko wa ambao ulikuwa umeanza kuoza.

Matongo alidai kuwa Diwani wa kata hiyo Bw. Juma Mapilipili kwa kushirikiana na wananchi wengine waliweza kuutambua mwili huo kuwa ni wa marehemu Lyaku Willy ambapo polisi walianza upelelezi wao ambapo iligundulika Mboje Mawe na Masahi Magumba waliokuwa wakiishi kijijini hapo walikuwa hawaonekani.


Alidai kuwa Desemba 6 mwaka jana alipata taarifa kuwa watuhumiwa hao walikuwa wamejificha katika milima ya kijiji cha Harawa na aliwachukua wanamgambo wawili wa vijiji vya Nkwindabuye na Harawa ili kumsaidia kazi ya kuwatafuta watuhumiwa hao.

Alidai tarehe hiyo hiyo majira ya jioni wanamgambo ho waliweza kumkamata Mboje kwenye milima ya kijiji cha Harawa ambapo
inadaiwa aliwataja watu wengine alioshirikiana nao katika mauaji hayo kuwa ni Sayi Mafizi,Chenyenye Maganyale,Sayi Gamanya,Gumbo Nzige na Masihi Magumba.


Kesi hiyo iko Mbele ya Jaji wamahakama Kuu ya Tanzania Bw. Gadi
Mjema ambapo mashahidi wanaendelea kutoa ushahidi wao. Hukumu ya kesi hiyo inatarajiwa kutolewa mwezi ujao.
[ Read More ]

Mama ajinyonga kwa wivu

MKAZI wa Kijiji cha Ukata katika kata ya Ukata wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, Bi. Rehema Ndunguru (40) amejinyonga na kufa kwa kinachosadikiwa ni kutokana na mgogoro wa mapenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Bw. Michael Kamuhanda amesema tukio hili lilitokea Juni 8, mwaka huu saa 3 asubuhi kijijini humo.

Alisema, Bi. Ndunguru alikutwa akiwa amejinyonga chumbani kwakwe kwa kutumia kanga na chanzo kimetokana na wivu wa kimapenzi ambapo imedaiwa mara nyingi alikuwa akimtuhumu mumewe kuwa si mwaminifu katika ndoa yao.

Alifafanua kuwa wakati mama huyo anajinyonga mume wake hakuwepo na kwamba watoto wake waliokuwa wakicheza nje walipoingia ndani walimwona mama yao akiwa ananing'inia chumbani na kutoa taarifa kwa majirani waliotoa taarifa Polisi.

Bw. Kamuhanda ameongeza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.
[ Read More ]

Mv Fatih yaundiwa tume

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeunda tume ya watu 8 kuchunguza chanzo cha ajali ya Mv. Fatih ambayo ilisababisha vifo vya watu 6 pamoja na hasara ya mali.

Akitangaza kuundwa kwa tume hiyo, Waziri wa Nchi, Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, Bw. Machano Othman Said alisema tume hiyo imepewa kazi ya kujua chanzo cha ajali ya Mv Fatih

Bw. Machano alisema tume hiyo imepewa muda wa mwezi mmoja kukamilisha kazi yake na kuwasilisha ripoti kwa wizara husika ambapo Mwenyekiti wa tume hiyo ni Jaji Omar Makungu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar akisaidiwa na nahodha mkongwe ambaye, Meneja Mkuu wa Shirika la Meli la Zanzibar Alhaji
Masoud Sururu.

Wajumbe wengine katika tume hiyo ni Bw. Abdalla Kombo, Bw. Mohamed Mahmoud Juma, Bw. Nahodha Hatib
Katundula kutoka katika kikosi cha jeshi la majini la KMKM, Meneja wa Ufundi wa Shirika la Bandari Zanzibar, Bw. Abdi Maalim.

Meli ya Mv Fatih ilipata ajali wakati ikikaribia eneo la Bandari ya Malindi mjini Zanzibar ambapo watu 34 walifanikiwa kutoka katika chombo hicho na wengine kuokolewa baada ya kuzama baharini.
[ Read More ]

Mahabusu wa Guantanamo awasili New York


Maafisa wa Marekani wameeleza mahabusu wa kwanza wa gereza la Guantanamo, atakayeshitakiwa katika mahakama ya kiraia ya Marekani amewasili New York.

Ahmed Ghailani amepelekwa kukabiliana na mashtaka katika mahakama ya New York akihusishwa na uripuaji wa mabomu wa balozi za Marekani katika Afrika Mashariki.

Bwana Ghailani, Mtanzania, alikamatwa nchini Pakistan mwaka 2004. Anatazamiwa kufikishwa kwa mara ya kwanza katika mahakama ya Manhattan baadae siku ya Jumanne.

Alipelekwa Guantanamo akiwa pamoja na mahabusu wengine wanaoitwa "muhimu sana" mwishoni mwa mwaka 2006.

Kuhamishwa kwake kumekuja huku Rais Obama akiwa katika hekaheka za kutafuta utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa wakati wa uchaguzi ya kufunga gereza la Guantanamo Bay katika kipindi cha mwaka mmoja akiwa madarakani.

Waandishi wa habari wanasema kesi ya Bwana Ghailani litakuwa jaribio muhimu katika mipango ya utawala wa Obama kufunga gereza hilo na hatimaye kuwafikisha mbele ya sheria watuhumiwa.

Serikali ya Marekani ina matumaini ya kuwasafirisha baadhi ya watuhumiwa wengine katika baadhi ya nchi, lakini hadi sasa mashauriano juu ya hilo yamekwama hasa iwapo Marekani nayo ipo tayari kupokea mahabusu.

Baraza la Congress lilikataa maombi ya serikali ya kugharamia kufungwa gereza la Gauantanamo, kukiwa na upinzani mkali wa kuwapeleka watuhumiwa Marekani.

[ Read More ]

Mahabusu Keko wagoma kula

KESI za mahabusu wa gereza la Keko, jijini Dar es Salaam, waliogoma kula kushinikiza kesi zao kusikilizwa, zitaanza kuunguruma Mahakama Kuu ya Tanzania, mwezi huu.

Habari za kuaminika ambazo gazeti hili imezipata kutoka kwa maofisa wa Gereza hilo mwishoni mwa wiki, zilieleza kuwa tayari kesi hizo zimewekwa kwenye kalenda ya mahakama.

Ufafanuzi huo ulitolewa na mmoja wa maofisa wa gereza hilo, aliyezungumza na gazeti hili kwa sharti la jina lake kutochapishwa gazetini, kufuatia kuwepo taarifa za mahabusu kuanza mgomo.

"Hapa hakuna mgomo wa mahabusu kwa sababu wote wameishaelezwa kuwa kesi zao zinasikilizwa mwezi huu," kilisema chanzo chetu kutoka ndani ya gereza hilo.

Alisema ndani ya gereza hilo wapo mahabusu wanaotaka kuishinikiza Serikali iwe inafanya kila kitu wanachotaka,jambo ambalo halikubaliki.

Chanzo hicho kilifafanua kuwa ndani ya gereza hilo wapo wafungwa wanaoshinikiza migomo. "Mahabusu hao ni miongoni mwa wanaoanzisha migomo wakati wanajua wazi kuwa kesi zao zipo mbioni kuanza kusikilizwa," alisema.

Wiki iliyopita baadhi wa mahabusu katika gereza hilo walipenyeza ujumbe kwa njia ya simu kwenye vyombo vya habari juu ya kuwepo kwa mgomo wa kugomea chakula ili kushinikiza kesi zao zianze kusikilizwa.

Baadhi ya mahabusu hao, walidaiwa hali zao ni mbaya, madai ambayo yalikanushwa na mmoja wa maofisa wa gereza hilo.

Ofisa huyo alidai kuwa awali mgomo wa mahabusu hao ulikuwa ni wakutaka kesi zao zisikilizwe. "Kama tayari mahakama imewapangia tarehe ya kusikilizwa kwa kesi zao ni kitu gani wanataka?"alihoji ofisa huyo.

Mwaka jana mahabusu wa gereza hilo waligoma kula wakipinga kesi zao kutopangiwa tarehe za kusikilizwa.

Mahabusu hao walikuwa wakihoji sababu za kesi inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Bw.Abdallah Zombe, na wenzake ya mauaji ya wafanyabiashara wa madini kusikilizwa haraka wakati wao wamekaa muda mrefu gerezani bila kesi zao kupangiwa tarehe ya kusikilizwa.

Mgomo huo ulimlazimu maofisa waandamizi wa Idara ya Mahakama na Wizara ya Sheria na Katiba kuwatembelea gerezani na kuzungumza nao.
Mwisho
[ Read More ]

Mtoto aunguzwa Dar kisa chakula!

Hali ya afya ya mtoto Comfort Kimaro, 7 wa Mbezi Saranga Jijini Dar bado haijatengemaa na anaendelea kuuguzwa katika Hospitali ya Tumbi wilayani Kibaha kutokana na majeraha mabaya ya moto yaliyotokana na kile kinachodaiwa kuwa ni kuunguzwa moto na mke wa baba yake mdogo.

Taarifa zinadai kuwa mtoto huyo, aliunguzwa mwilini kwa mkasi wa moto na mke wa baba yake mdogo anayetajwa kwa jina la Domina Kimaro, kutokana na kosa la kula chakula kilichokuwa kimehifadhiwa kwa ajili ya msichana wa kazi almaarufu kama hausigeli.

Inaelezwa kuwa Comfort ameunguzwa kwa kutumia mkasi uliokuwa ukiwekwa kwenye mafuta ya moto na mke huyo wa baba yake mdogo (Domina) na kisha kupitishiwa mwilini mwake mara kadhaa kwa ni ya kumuadhibu.

Taarifa zinadai kuwa tukio hilo limejiri hivi karibuni, mishale ya saa 4:00 usiku baada ya kubainika kuwa mtoto huyo alikula chakula cha msichana wa kazi.

Imeelezwa kuwa siku ya tukio, mama huyo (Domina) alipandwa na hasira aliposikia kuwa Comfort amekula chakula cha msichana wa kazi na kuamua kuchukua hatua hiyo ya kumuunguza mwilini kwa mkasi uliokuwa ukichemshwa kwenye mafuta ya moto na kumbabua mwilini tena na tena.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amesema polisi wanamshikilia mtuhumiwa Domina na kesho wanatarajia kumpandisha kizimbani.

Aidha, akizungumza na waandishi wa habari, Afisa Habari wa Shirika la Elimu Kibaha, ambaye pia ni Afisa uhusiano wa Hospitali ya Tumbi Bw. Gerald Chami, amesema hali ya Comfort bado haijawa nzuri na hivyo anaendelea kulazwa ili apate matibabu zaidi.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa majirani ndio waliomfikisha mtoto huyo hospitalini baada ya kumtwaa toka kwa Bi. Domina aliyekuwa ameshamuunguza mwilini bila huruma na kumuacha ndani pasi na kumpeleka jospitalini.

Mjumbe mmojawapo wa eneo hilo la Mbezi Saranga, Bw. Christopher Francis, amesema kuwa siku ya tukio, mtoto huyo alikuwa akipiga kelele nyingi za kuomba msaada.

Akasema majirani walipojaribu kwenda kumsaidia, wakashindwa kwa vile Domina alikuwa ameufunga mlango wa nyumba na kuendelea kumuadhibu akiwa ndani.

Hata hivyo, akasema yeye na majirani wengine wakaenda tena siku nyingine na kufanikiwa kumpata mama aliyefanya ukatili huo ambaye kazi yake ni kupika na kuuza chakula katika eneo la Saranga Temboni.

Akasema baada ya kumpata walimuhoji kuhusina na adhabu hiyo, lakini mama huyo akakana kuwa hakumuunguza.

Akasema baada ya kuona mama huyo anakwepa tuhuma, walimua kumuhoji msichana wa kazi wa mama huyo ambaye ndiye aliyetakiwa kula chakula kile kinachodawa kuliwa na mtoto Comfort.

Mjumbe huyo wa shina akasema msichana huyo wa kazi ndiye aliyefichua kuwa mtoto huyo alichomwa na mama yake mdogo kwa kutumia mkasi uliokuwa ukilowekwa kwenye mafuta ya moto.

Bw. Fransis akasema kwa kushirikiana na wananchi, waliamua kutoa taarifa Polisi na mama huyo akapelekwa kituoni kwa ajili ya kutoa maelezo zaidi.

Akasema baadaye majirani waliamua kuchangishana fedha na kupata zaidi ya shilingi 60,000 walizozitumia kumpeleka mtoto Comfort katika hospitali ya Tumbi, ambako hadi sasa anaendelea kutibiwa.

Aidha, alipohojiwa, Comfort amesema mama yake mdogo alikuwa na tabia ya kumpiga mara kwa mara, hasa baba yake mdogo aitwaye Geofrey Kimaro anapokuwa safarini.

Akasema siku ya tukio baba yake mdogo alikua safarini na hakupewa chakula tangu asubuhi hadi jioni na ilipofika mishale ya saa 10:00 jioni, mama yake mdogo alimpa chakula ili akipeleke nyumbani kwa msichana wao wa kazi.

Akasema kwa vile yeye (mtoto) alikuwa na njaa kutokana na kuwa alikuwa hajala chochote, aliamua kukila na ndio maana akajikuta akiunguzwa moto kwa kosa hilo.

Akasema mama huyo alimuunguza kwa kutumia mkasi alioukuwa akiuloweka kwenye mafuta ya moto.

Hata hivyo, akasema baada ya kuunguzwa huko, mama yake mdogo (Domina) hakumpeleka hospitali na badala yake akawa anampaka yai, hali iliyomfanya awe akipata maumivu makali zaidi.

Kwa upande wa mama mzazi wa mtoto huyo Elinani Lalashowi, 36, mkazi wa Moshi ambaye alifika juzi kumuuguza mwanawe baada ya kupata taarifa kutoka kwa shemeji yake aitwae Vicent, amesema hana la kuongea kwa sasa kwani hakuwahi kuwa na ugomvi wowote na mke huyo wa shemeji yake.

[ Read More ]

mbunge wa busanda akaribishwa bungeni


Mbunge wa Busanda, Lolesia Bukwimba (mbele kulia), akisindikizwa na wabunge wanawake wa Chama Cha Mapinduzi kuingia bungeni ili kula kiapo jana baada kushinda uchaguzi mdogo wa jimbo hilo uliofanyika Mei 24, mwaka huu.
[ Read More ]

Basi laua watano Dodoma

WATU watano wamekufa baada ya basi la abiria kupinduka leo saa tano asubuhi wakati likitoka Dar es Salaam kwenda mkoani Singida.

Basi hilo liitwalo, Hajjiz, aina ya Scania lilipinduka baada ya tairi ya mbele kupasuka.

Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dodoma, Salum Msangi amesema, basi hilo lenye namba za usajili T 441 AYN lilipinduka saa 5.40 katika kijiji cha Mtumba, takribani kilomita 17 kutoka mjini Dodoma.

Inadaiwa kuwa watu wanne walikufa papo hapo, mwingine alifariki dunia wakati akikimbikizwa hospitali.

Kwa mujibu wa Msangi, walioshuhudia ajali hiyo wamedai kuwa basi hilo lilikuwa kwenye mwendo mkali, na baada ya ajali dereva alikimbia polisi wanamtafuta.
[ Read More ]