Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solutions, Peter Mwendapole akiwa na watoto wa wenye ulemavu wa ngozi wanaosoma na kulelewa katika shule ya Buhangija mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solutions Bw. Peter Mwendapole na Miss Progress International Julieth William Lugemba na wenyeji wao wenye ulemavu wa ngozi wanaosoma na kulelewa katika shule ya Buhangija mkoani Shinyanga.
Miss Progress International, Julieth William Lugembe akiwa na watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Buhangija kilichopo mkoani Shinyanga wakati alipofanya ziara mkoani humu kuangalia matatizo mbalimbali yanayowakabili albino.
MSHINDI wa dunia taji la Miss Progress International Julieth William, leo ametembelea watu wenye ulemavu wa ngozi Mkoani Shinyanga.Julieth alitembelea watu hao na watoto wenye ulemavu huo wa ngozi kwa lengo la kutaka kufahamu mahitaji yao kabla ya kuweza kuwasaidia.Ziara hiyo iliyoandaliwa na kampuni ya One Touch Solutions inayoandaa shindano la Miss Progress Tanzania ilimedhaminiwa na Precision Air na kampuni ya simu za mkononi ya AirtelMlimbwende huyo aliyetwaa taji hilo mwaka jana nchini Italia alianza kwa kutembelea shule ya Buhangija, ambayo inatunza watoto wenye ulemavu huo.Akiwa katika shule hiyo alipata fursa ya kutanzama mazingira ya shule hiyo pamoja na kuzungumza na watoto hao kwa muda wa dakika 30.Katika moja ya mahitaji waliyotaka watoto hao ni kumaliziwa kwa moja ya bweni lao ambalo halijamalizika ili kuweza kupata nafasi nzuri ya kulala kutokana na lile wanalotumia kuwa dogo, jambo linalowafanya walale kitanda kimoja watu watatu.Baadaye alitembelea ofisi za mkoa za Chama cha Maalbino (TAS) na kuweza kuzungumza na watu wazima ili nao kutaja mahitaji yao.Katika kikao hicho watu hao wenye ulemavu walitaja mahitaji yao ikiwaa ni pamoja na kutaka kupewa elimu ya ujasiliamali ili waweze kuendesha maisha yao na kuondokana na utegemezi.Pia alikutana na Ofisa Elimu wa mkoa wa Shinyanga, Eva Lopa, Ofisa Ustawi wa Jamii, Jesca Kagunila. Leo Julieth atakuwa mkoani Mwanza kabla kuelekea Arusha.
MSHINDI wa dunia taji la Miss Progress International Julieth William, leo ametembelea watu wenye ulemavu wa ngozi Mkoani Shinyanga.
Julieth alitembelea watu hao na watoto wenye ulemavu huo wa ngozi kwa lengo la kutaka kufahamu mahitaji yao kabla ya kuweza kuwasaidia.
Ziara hiyo iliyoandaliwa na kampuni ya One Touch Solutions inayoandaa shindano la Miss Progress Tanzania ilimedhaminiwa na Precision Air na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel
Mlimbwende huyo aliyetwaa taji hilo mwaka jana nchini Italia alianza kwa kutembelea shule ya Buhangija, ambayo inatunza watoto wenye ulemavu huo.
Akiwa katika shule hiyo alipata fursa ya kutanzama mazingira ya shule hiyo pamoja na kuzungumza na watoto hao kwa muda wa dakika 30.
Katika moja ya mahitaji waliyotaka watoto hao ni kumaliziwa kwa moja ya bweni lao ambalo halijamalizika ili kuweza kupata nafasi nzuri ya kulala kutokana na lile wanalotumia kuwa dogo, jambo linalowafanya walale kitanda kimoja watu watatu.
Baadaye alitembelea ofisi za mkoa za Chama cha Maalbino (TAS) na kuweza kuzungumza na watu wazima ili nao kutaja mahitaji yao.
Katika kikao hicho watu hao wenye ulemavu walitaja mahitaji yao ikiwaa ni pamoja na kutaka kupewa elimu ya ujasiliamali ili waweze kuendesha maisha yao na kuondokana na utegemezi.
Pia alikutana na Ofisa Elimu wa mkoa wa Shinyanga, Eva Lopa, Ofisa Ustawi wa Jamii, Jesca Kagunila. Leo Julieth atakuwa mkoani Mwanza kabla kuelekea Arusha.
Today our First Lady Michelle Obama celebrates her 47th birthday. We've loved watching this Chicago native ever since she hit the world's stage alongside her husband, President Barack Obama. Since then she has awakened within all of us a sense of pride in being Black women.There's no question that Michelle Obama is a First Lady with style.Ilove her sense of fashion age apropriate.She and her family marked the occasion by paying tribute to MLK with a painting project at a school on Capitol Hill.
Ngozi Nyororo inayowaka muda mfupi baada ya kupaka My Lotuion ya Teddy Kalonga
Sample za Lotuon za Teddy Kalonga
Supamodo wa Kimataifa Teddy Kalonga akiwa katika pozi
Supamodo wa Kimataifa Teddy Kalonga akiwa katika picha ya pamoja na Mume wake.....
--------------
A few months ago, fellow blogger Teddy Kalonga aka TK of Total Knockout Blog launched a body lotion called My Lotion. According to the site, My Lotion is full of natural ingredients and comes in two scents; Lime and Vanilla. The lotion is incredibly moisturizing and guarantees you a healthy, radiant complexion, and will make your skin feel luxurious all the time.
Kununua Teddy Kalonga 'My Lotion' Online Nenda
www.mylotionbytk.blogspot.com
Kununua Teddy Kalonga 'My Lotion' Online Nenda
www.mylotionbytk.blogspot.com
Tumpongeze Bi.Shija Maige (33)mkazi wa Kahama Mkoani Shinyanga kwa kujifungua salama watoto watano.Yeye na wanawe wako na afya tele.
Mke wa Rais Jakaya Kikwete, Mama Salama Kikwete (kushoto) akibusiana na Mke wa Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamini Mkapa, Mama Anna Mkapa wakati wa hafla ya Wenza wa mabalozi na wawakilishi wa Taasisi za Kimataifa ya kuukaribisha Mwaka Mpya wa 2011 Ikulu, Dar es Salaam jana jioni.
Mama Salma akifurahia jambo na Mke wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mama Tunu Pinda (wa pili kulia) pamoja na wake wa Makamu wa Rais Dk Bilali, Zakia (kulia) na Asha.
Mama Salma akiagana na wenza wa mabalozi baada hafla hiyo kumalizika kwmeye viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam Jana
Mama Salma akijadiliana jambo na Mwakilishi wa UNFPA nchini, Dk. Julitta Onabanjo wakati wa hafla hiyo.
Mama Salma Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Vodacom Foundation, Mwanvita Makamba ambaye alikuwa miongoni mwa wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wenza wa mabalozi wakati wa sherehe ya mwaka mpya(Sherry Party) iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana jioni
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein(kulia) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) wakibadilishana mawazo jana wakati sherehe za maadhimisho ya miaka 47 ya Mapinduzi ya Zanzibar uwanja wa Amaan Stadium mjini Unguja leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein(kulia) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) wakiwa wamesimama kupokea maandamano ya wawakilishi wa wananchi kutoka mikoa mbalimbali za Zanzibar kwa ajili ya kusherekea ya miaka 47 ya Mapinduzi
Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba wakato wa sherehe za maadhimisho ya miaka 47 ya Mapinduzi ya Zanzibar
Makamba-Katibu wa CCM Yusuph Makamba (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba(kulia)jana mjini Zanzibar wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 47 ya Mapinduzi ya Zanznibar
Waziri wakuu wastaafu Dkt Salim Ahmed Salim (kushoto) na Fredrick Sumaye (katikati) wakibadilishana mawazo na Waziri Kiongozi Mstaafu Vuai Nahodha jana wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 47 ya mapinduzi ya Zanzibar.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange akiwa ameshikilia mfano wa funguo baada ya kukabidhiwa na Meja Jenerali Qian Lihua kutoka nchini China ikiwa ni ishara ya kumkabidhi chuo hicho.
Waziri wa Ulinzi na JKT Dk. Hussein Mwinyi akikagua darasa la Computer la Chuo Kikuu cha Kitaifa cha kijeshi
Waziri wa Ulinzi na JKT Dk. Hussein Mwinyi akikagua darasa la Computer la Chuo Kikuu cha Kitaifa cha kijeshi
Waziri wa Ulinzi na JKT Dk. Hussein Mwinyi na Meja Jenerali Qian Lihua kutoka nchini China wakikata utepe wakati wa makabidhiano ya Chuo Kikuu cha Kitaifa cha kijeshi (NDC) kilichojengwa Kunduchi Dar es Salaam.
















