When you are really focused with what you believe and want to achieve then there is a point in life that you have to eliminate some people no matter how close they are you have to free them and it hurts but its healthy as long as they make you loose focus then they should go....come back to them when you are satisfied with your achievements....and they will understand and be happy and proud of you and if NOT then they were never real and true to your life.
ZANZIBAR imefanikiwa kuwa mshindi wa kwanza na kujinyakulia tuzo ya Utalii nchini Russia kwa mwaka 2011, ‘Star Travel.ru 2011’.
Tuzo hiyo hushindaniwa kila mwaka kwa maeneo yalio bora zaidi kwa shughuli za kiutalii barani Afrika, ambapo watalii na waongoza watalii wa nchi hiyo hutembelea.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Mkurugenzi Mkuu wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Ali Khalil Mirza, amesema amepokea taarifa hiyo kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Russia, ikielezea Zanzibar kuchaguliwa kuwa mshindi wa tuzo hiyo, kama eneo lililo bora kwa shughuli za kiutalii barani Afrika.
Alisema kuwa kinyang’anyiro hicho kilihusisha maeneo 23 yalio bora zaidi kwa shughuli za kiutalii, ispokuwa nchi ya Misri haikushirikishwa.
Alisema tayari tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Ubalozi wa Tanzania nchini humo tangu juzi katika hafla maalum ilioambatana na kuanza kwa maonyesho ya Kimataifa ya Utalii nchini.
Mirza alisema ushindi wa tuzo huyo unatokana na msukumo mkubwa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Russia pamoja na hatua ya Kamisheni hiyo kufanya ziara maalum ya kuutangaza utalii wa Zanzibar mnamo 2009.
Alisema makubaliano yaliofikiwa kati ya Kamisheni ya Utalii na Makampuni ya kutembeza watalii yamelifanya soko la Utalii nchini Russsia kuimarika, ambapo wastani wa watalii 300 hufika nchini kila mwaka tangu wakati huo.
Alieleza kuwa hayo ni mafanikio makubwa kwa soko la utalii nchini Russia kwa kuzingatia watalii wanaokuja ni wale wanaotumia zaidi, ambao hufikia katika Hoteli zenye hadhi za juu kama vile Plan Hotel,Lagema,Green of Zanzibar na The Residents.
Aidha alisema Kamisheni yake ina matumaini makubwa kuwa ifikapo 2013 idadi ya wataalii kutoka nchi hiyo itaongezeka, hususan pale Shirika la ndege la Uturuki litakapoanza kufanya safari zake moja kwa moja hadi Zanzibar, ikizingatiwa watalii hao hivi sasa hutumia usafiri wa Shirika la Emirates, na kutembelea kwanza katika Mbuga za wanyama na hatimae kuja Zanzibar.
Mkurugenzi huyo alivitaja baadhi ya vigezo muhimu vinavyozingatiwa katika kumpata mshindi wa tuzo hiyo, kuwa ni pamoja na hali ya usalama, kufikiwa kwa matarajio ya wageni, vivutio vya utalii ikiwemo michezo mbali mbali (pwani na ufukweni), huduma katika mahoteli pamoja na tamaduni za wenyeji.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wanaoshiriki Semina ya Siku Moja inayohusu utekelezaji wa Mkuza wakisikiliza Hotuba ya Ufunguzi iliyotolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hayupo Pichani huko kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika Picha pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar baada ya kuifungua Semina ya Utekelezaji wa Mkuza nje wa ukumbi wa Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani.
Juhudi za kupambana na Umaskini hapa Nchini ni vyema zikajikita zaidi katika kuimarisha Uchumi sambamba na huduma za Kijamii kwa lengo la kustawisha maisha bora ya Wananchi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema hayo wakati akiifungua Semina ya siku mbili ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayohusu utekelezaji wa Mpango wa Kupunguza Umaskini Zanzibar { MKUZA } inayofanyika katika Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani.
Balozi Seif alisema wimbi la umaskini hushamiri iwapo jamii itakosa huduma za Elimu, ongezeko la uzazi katika umri mdogo, ukosefu wa usawa wa kijinsia pamoja na uchumi duni kwa akina mama ambao ndio wengi katika familia.
Balozi Seif alisema Umoja wa Mataifa umepitisha Azimio la utekelezaji wa Malengo la Milenia ili Dunia iondokane na umaskini ifikapo mwaka 2015 na kuzitaka Nchi Wanachama hasa zinazoendelea kujipangia mikakati ya kuuondoa Umaskini kwa kupitia utekelezaji wa Mipango yao ya maendeleo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisisitiza kwamba Serikali imo katika hatua za kupambana na umaskini kupitia utekelezaji wa Mkuza ingawa Wananchi waliowengi bado hawajaelewa Mpango huu.
Alieleza kwamba yapo mafanikio makubwa yamepatikana katika huduma za Kijamii zikiwemo Elimu, Afya na huduma za Maji safi mafanikio yanayoonekana zaidi kwenye kupunguza umaskini usio wa kipato.
Akizungumzia changamoto zilizojichomoza wakati wa utekelezaji wa Mkuza Balozi Seif alisema Mfumko wa bei umekuwa bado tatizo kinyume na lengo la chini ya asilimia 10% ukiathiriwa zaidi na ongezeko la bei ya mafuta na chakula katika soko la Dunia.
Akigusia Ukuaji mdogo wa Sekta ya Kilimo wa asilimia 4.6 Balozi Seif alisema unaonekana kushusha mchango wa Sekta hiyo katika pato la Taifa wakati Sekta ya Kilimo bado ni muajiri Mkuu wa nguvu kazi ya Taifa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alifahamisha kwamba hali hiyo imechangia kuwa na mafanikio madogo katika kuhakikisha kuwepo kwa usalama wa chakula.
Semina hiyo ya siku mbili inahusisha Mada kadhaa ikiwa pamoja na Mipango ya Maendeleo, Mapitio ya Dira
ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020, Matokeo muhimu katika uchagumbuzi wa matumizi ya kaya pamoja na maandalizi ya Bajeti na mahusiano na Mkuza.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
MJANE Specioza Kamala ameendelea kusotea mafao ya mume wake aliyefariki miaka 13 iliyopita, huku mwaka huu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikimwandikia marehemu barua ya kumtaka ajaze fomu ya kulipwa mapunjo ya mshahara baada ya kupanda daraja.
Marehemu Richard Mutakulemberwa aliyekuwa mwalimu katika shule ya sekondari Kahororo iliyopo Manispaa ya Bukoba, alikutwa na mauti August,19 mwaka 1998 wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na T.Kagumisa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ambayo Fikra Pevu ina nakala yake, pamoja na mambo mengine inamtaka marehemu kujaza fomu kutokana na utaratibu mpya wa malipo ya malimbikizo.
Pia barua hiyo ya Januari 4, 2012 iliyotumwa kupitia shule aliyokuwa akifundisha marehemu ya Kahororo inamtaka kufuata maelekezo kwa mujibu wa barua hiyo ili madai yake yaweze kushughulikiwa.
“Tafadhali mara upatapo barua hii jaza na utume kwa Katibu Mkuu fomu halisi na nakala moja (photocopy), pia ambatanisha barua yenye maelezo sahihi ya madai,nakala ya barua ya kupandishwa na kukubali cheo na ‘salary slip’ ya karibuni,” inaeleza sehemu ya barua hiyo kwenda kwa marehemu.
Pia mbali na barua hiyo kumtakia marehemu ushirikiano mwema katika kukamilisha zoezi hilo, inamkumbusha kuwa nyaraka zote lazima zipite kwa mkuu wake wa kituo na kutumwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Naye mjane wa Marehemu, Specioza Kamala mbali na kusikitishwa na hali hiyo, alisema tangu kufariki kwa mume wake mwaka 1998 ameendelea kufuatilia madai ya mume wake bila mafanikio na hata kufika Wizarani huku akipewa kauli za ahadi.
Alisema kuwa mbali na kuwa alishapata barua hiyo aliyoandikiwa marehemu mume wake, anachokumbuka ni kuwa mme wake alifariki kabla hajalipwa mapunjo ya mshahara baada ya kupandishwa daraja ambayo ameendelea kuyafuatilia bila mafanikio na kuwa mirathi ya marehemu ilishatolewa.
“Alipanda daraja mwaka 1996 na kufariki kabla ya kulipwa mapunjo yake ya mshahara,suala hili nilishawaeleza hata watu wa Utumishi wa Umma kutoka Dar es salaam na kunielekeza niende Wizarani na baada ya kwenda walisema faili lake halipo,” alisema mama huyo ambaye pia ni mwalimu katika moja ya shule za msingi Mkoani Kagera.
Alipoulizwa kama suala hilo liliwahi kufika katika Ofisi za Chama cha Walimu Mkoani hapa, Katibu wake wa Mkoa Aaron Masalu alisema halijafika katika ofisi hiyo huku akilihusisha na mfumo mbovu wa utunzaji wa takwimu za watumishi.
Pia alidai vyombo vinavyomshughulikia mwalimu havina utaratibu mzuri wa mawasiliano na kusema kuwa sasa wakati umefika wa mwalimu kushughulikiwa na chombo kimoja tofauti na ilivyo sasa.
Alisema mbali na kuwa utaratibu uliopo unaweza kuchelewesha malipo ya mhusika au kuyakosa kabisa alidai suluhisho ni kuwa namwajiri mmoja ambapo hivi sasa walimu wanashughulikiwa na Tamisemi,Utumishi wa Umma na Wizara yenyewe.
Imeandikwa na Phinias Bashaya-Kagera
[ Read More ]
Marehemu Richard Mutakulemberwa aliyekuwa mwalimu katika shule ya sekondari Kahororo iliyopo Manispaa ya Bukoba, alikutwa na mauti August,19 mwaka 1998 wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na T.Kagumisa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ambayo Fikra Pevu ina nakala yake, pamoja na mambo mengine inamtaka marehemu kujaza fomu kutokana na utaratibu mpya wa malipo ya malimbikizo.
Pia barua hiyo ya Januari 4, 2012 iliyotumwa kupitia shule aliyokuwa akifundisha marehemu ya Kahororo inamtaka kufuata maelekezo kwa mujibu wa barua hiyo ili madai yake yaweze kushughulikiwa.
“Tafadhali mara upatapo barua hii jaza na utume kwa Katibu Mkuu fomu halisi na nakala moja (photocopy), pia ambatanisha barua yenye maelezo sahihi ya madai,nakala ya barua ya kupandishwa na kukubali cheo na ‘salary slip’ ya karibuni,” inaeleza sehemu ya barua hiyo kwenda kwa marehemu.
Pia mbali na barua hiyo kumtakia marehemu ushirikiano mwema katika kukamilisha zoezi hilo, inamkumbusha kuwa nyaraka zote lazima zipite kwa mkuu wake wa kituo na kutumwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Naye mjane wa Marehemu, Specioza Kamala mbali na kusikitishwa na hali hiyo, alisema tangu kufariki kwa mume wake mwaka 1998 ameendelea kufuatilia madai ya mume wake bila mafanikio na hata kufika Wizarani huku akipewa kauli za ahadi.
Alisema kuwa mbali na kuwa alishapata barua hiyo aliyoandikiwa marehemu mume wake, anachokumbuka ni kuwa mme wake alifariki kabla hajalipwa mapunjo ya mshahara baada ya kupandishwa daraja ambayo ameendelea kuyafuatilia bila mafanikio na kuwa mirathi ya marehemu ilishatolewa.
“Alipanda daraja mwaka 1996 na kufariki kabla ya kulipwa mapunjo yake ya mshahara,suala hili nilishawaeleza hata watu wa Utumishi wa Umma kutoka Dar es salaam na kunielekeza niende Wizarani na baada ya kwenda walisema faili lake halipo,” alisema mama huyo ambaye pia ni mwalimu katika moja ya shule za msingi Mkoani Kagera.
Alipoulizwa kama suala hilo liliwahi kufika katika Ofisi za Chama cha Walimu Mkoani hapa, Katibu wake wa Mkoa Aaron Masalu alisema halijafika katika ofisi hiyo huku akilihusisha na mfumo mbovu wa utunzaji wa takwimu za watumishi.
Pia alidai vyombo vinavyomshughulikia mwalimu havina utaratibu mzuri wa mawasiliano na kusema kuwa sasa wakati umefika wa mwalimu kushughulikiwa na chombo kimoja tofauti na ilivyo sasa.
Alisema mbali na kuwa utaratibu uliopo unaweza kuchelewesha malipo ya mhusika au kuyakosa kabisa alidai suluhisho ni kuwa namwajiri mmoja ambapo hivi sasa walimu wanashughulikiwa na Tamisemi,Utumishi wa Umma na Wizara yenyewe.
Imeandikwa na Phinias Bashaya-Kagera
MAMA mmoja anaetambulika kwa jina la Mwantatu Kombo mkaazi wa Miembeni ameelezea kusikitishwa kwake kwa kitendo alichofanyiwa na wauguzi wa hospitali ya Mnazimoja wodi ya wazazi wakati alipokwenda kumpeleka jamaa yake kwa ajili ya kujifungua.
Akisimulia mkasa huo Mwantatu alisema kuwa tukio hilo lilitokea wiki iliyopita majira ya saa 9 usiku, ambapo alifika hospitalini hapo kwa lengo la kumpeleka jamaa yake na hatimaye kujifungua nje ya wodi ya wazazi hospitalini hapo.
Alisema alipofika wodini hapo akiwa amefuatana na mjamzito huyo, anaejulikana kwa jina la Fatma Ali Suleiman ambaye alimuomba ampatie msaada wa kumpeleka hospitali, lakini hakupokelewa kutoka na kutokuwa na vifaa.
Alisema kutokana na kutokuwa na vifaa, aliambiwa na wauguzi hao atoke nje na hawatompokea mjamzito huyo pamoja na kuwaeleza kuwa atavilipia baada ya kujifungua kutokana na hali yake.
Pamoja na Mwantatu kudai kuwafahamisha yote hayo kuhusu mzazi wake lakini madaktari hao hawakumsikiliza kilio chake na kumtaka atoke nje yeye na mjamzito wake huku mzazi huyo akiwa na uchugu na tayari kwa kujifungua.
"Wakati nikiwa natoka nje na mjamzito wangu, alianguka mbele ya wodi ya wazazi na kujifungua hapo hapo chini, mara baada ya kujifungua nilirudi kwa wauguzi kuwambia mgonjwa wangu ameshajifungua nje naomba kuomba msaada lakini pia walikataa.
Kwa upande wake Mzazi huyo Fatma Ali alisema kuwa mwanzo wa kupata ujauzito huo alikwenda kupima na kuambiwa atoe shilingi 10,000 kwa ajili ya kununua gamba na hali yake alikuwa hana hata shilingi na ndipo akaondoka na kwenda zake hadi kujifungua kwake.
Kwa upande wake Msaidizi Katibu hospitali ya Mnazimmoja Mohammed Nadi alithibitisha kutokea tukio hilo kwa madaktari hao na alisema kitendo walichokifanya wauguzi kwa kumuacha mzazi kujifungua nje ya wodi si kitendo cha kiungwana.
Akizungumzia kadhia hiyo Katibu wa Hospitali ya Mnazimmoja, Omar Abdalla Ali, aliwashauri wananchi wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji wawe na utaratibu wa kuripoti kwa ushahidi wa kutosha pamoja na kufika katika vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua za kisheria zaidi.
"Mara baada ya tukio hilo tuliwaandikia barua na kutaka wajieleze lakini hatukuridhika na maelezo yao waliyoyathibitisha kwenye barua yao, hivyo nitawaita kwenye kamati ya maadili wiki ijayo kwa ajili ya kusikiliza pande zote mbili na kulichukulia hatua za kisheria zinazofaa”, alisema Msaidizi huyo.
Aidha aliwataka madaktari kuachana na vitendo vya rushwa ambapo hivi sasa vimeonekana kukithiri kwa kiasi kikubwa na kupelekea kutothamini utu na binadamu.
Barua yenye ripoti kutoka kwa Muuguzi wa Maternity Ward ya Februari 2 mwaka huu, imeeleza kwamba siku ya tarehe saba mwezi huu wauguzi wawili (majina tunayahifadhi) walimpokea mgonjwa vizuri na wamemuweka katika kochi na kabla hawajamchunguza walimtaka atowe vifaa vyake, jamaa zake walijibu hawana na walielekezwa wakanunue hospitali ya Al-Rahma.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa walidai hawana pesa, wakati wanamuelekeza mgonjwa akalale kwenye kitanda, wauguzi hao waliitwa kwenda kumhudumia mgonjwa mwengine mwenye Eclampisia.
Ilieleza taarifa hiyo kuwa walipokuwa wakimshughulikia mgonjwa wa Eclampisia, mama wa jamaa zake walitoka nje na baadae wauguzi walipata taarifa ya mama ameshajifungua walipoulizwa wakunga aliemsaidia mama huyu ni nani, walijibu hawamjui maana wao hawakwenda tena, ilimaliza ripoti hiyo.
[ Read More ]
Akisimulia mkasa huo Mwantatu alisema kuwa tukio hilo lilitokea wiki iliyopita majira ya saa 9 usiku, ambapo alifika hospitalini hapo kwa lengo la kumpeleka jamaa yake na hatimaye kujifungua nje ya wodi ya wazazi hospitalini hapo.
Alisema alipofika wodini hapo akiwa amefuatana na mjamzito huyo, anaejulikana kwa jina la Fatma Ali Suleiman ambaye alimuomba ampatie msaada wa kumpeleka hospitali, lakini hakupokelewa kutoka na kutokuwa na vifaa.
Alisema kutokana na kutokuwa na vifaa, aliambiwa na wauguzi hao atoke nje na hawatompokea mjamzito huyo pamoja na kuwaeleza kuwa atavilipia baada ya kujifungua kutokana na hali yake.
Pamoja na Mwantatu kudai kuwafahamisha yote hayo kuhusu mzazi wake lakini madaktari hao hawakumsikiliza kilio chake na kumtaka atoke nje yeye na mjamzito wake huku mzazi huyo akiwa na uchugu na tayari kwa kujifungua.
"Wakati nikiwa natoka nje na mjamzito wangu, alianguka mbele ya wodi ya wazazi na kujifungua hapo hapo chini, mara baada ya kujifungua nilirudi kwa wauguzi kuwambia mgonjwa wangu ameshajifungua nje naomba kuomba msaada lakini pia walikataa.
Kwa upande wake Mzazi huyo Fatma Ali alisema kuwa mwanzo wa kupata ujauzito huo alikwenda kupima na kuambiwa atoe shilingi 10,000 kwa ajili ya kununua gamba na hali yake alikuwa hana hata shilingi na ndipo akaondoka na kwenda zake hadi kujifungua kwake.
Kwa upande wake Msaidizi Katibu hospitali ya Mnazimmoja Mohammed Nadi alithibitisha kutokea tukio hilo kwa madaktari hao na alisema kitendo walichokifanya wauguzi kwa kumuacha mzazi kujifungua nje ya wodi si kitendo cha kiungwana.
Akizungumzia kadhia hiyo Katibu wa Hospitali ya Mnazimmoja, Omar Abdalla Ali, aliwashauri wananchi wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji wawe na utaratibu wa kuripoti kwa ushahidi wa kutosha pamoja na kufika katika vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua za kisheria zaidi.
"Mara baada ya tukio hilo tuliwaandikia barua na kutaka wajieleze lakini hatukuridhika na maelezo yao waliyoyathibitisha kwenye barua yao, hivyo nitawaita kwenye kamati ya maadili wiki ijayo kwa ajili ya kusikiliza pande zote mbili na kulichukulia hatua za kisheria zinazofaa”, alisema Msaidizi huyo.
Aidha aliwataka madaktari kuachana na vitendo vya rushwa ambapo hivi sasa vimeonekana kukithiri kwa kiasi kikubwa na kupelekea kutothamini utu na binadamu.
Barua yenye ripoti kutoka kwa Muuguzi wa Maternity Ward ya Februari 2 mwaka huu, imeeleza kwamba siku ya tarehe saba mwezi huu wauguzi wawili (majina tunayahifadhi) walimpokea mgonjwa vizuri na wamemuweka katika kochi na kabla hawajamchunguza walimtaka atowe vifaa vyake, jamaa zake walijibu hawana na walielekezwa wakanunue hospitali ya Al-Rahma.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa walidai hawana pesa, wakati wanamuelekeza mgonjwa akalale kwenye kitanda, wauguzi hao waliitwa kwenda kumhudumia mgonjwa mwengine mwenye Eclampisia.
Ilieleza taarifa hiyo kuwa walipokuwa wakimshughulikia mgonjwa wa Eclampisia, mama wa jamaa zake walitoka nje na baadae wauguzi walipata taarifa ya mama ameshajifungua walipoulizwa wakunga aliemsaidia mama huyu ni nani, walijibu hawamjui maana wao hawakwenda tena, ilimaliza ripoti hiyo.
MAMIA ya vijana wa Zanzibar waliofanya mtihani wa kidato cha nne wanakabiliwa na mtihani mwingine, tena ni mkubwa zaidi kuliko ule walioufanya mwaka jana na hawajui waukabili vipi huu mtihani mpya.
Matokeo yao ya mtihani wa kidato cha nne yamefutwa na kuambiwa juhudi zao zote za kujitayarisha kwa miezi kadha zimekwenda na maji, yaani “Ajwar” (pata potea).
Hivi sasa watoto hawa, wengi wao wakiwa wanatokana na familia za kimasikini, wamebaki wakilalama huku wakiwa na huzuni na hivi sasa wanahangaika huku na kule kama kuku anayetaka kutaga na hakuna dalili za kupata mafanikio.
Watoto hawa wa kimasikini wanaona dunia imewapa mgongo na huko wanakokwenda ni kiza kitupu na hakuna mtu wa kuwaashia taa ya kuona kilipo usoni. Ni unyonge mkubwa.
Ama kweli Waswahili hawakukosea waliposema mnyonge hana haki, lakini tukumbuke walipotutahadharisha kwa kusema; ‘Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni”.
Kwa kweli inasikitisha sana, inahuzunisha na inatisha kuona viongozi wetu wengi wanaliona suala la kufutwa matokeo ya mtihani kama vile ni jambo la kawaida na hawataki kukubali madhara yake kwa vijana wetu waliofutiwa matokeo ya mitihani.
Sishangai hata kidogo na mtazamo wao huu kwa sababu watoto wa hawa wakubwa ambao tumekuwa tukidhani na wengi kuamini watatuonea imani na kuwahurumia watoto wa kimasikini wanasoma nje ya nchi. Matatizo ya elimu tuliyonayo nchini, hayawahusu.
Ukifanya utafiti wa haraka utaona kuwa watoto wa karibu viongozi wote wa serikali na matajiri hawawapeleki watoto wao katika shule za serikali kwa sababu wanaelewa vizuri kwamba huko hakuna elimu ila kupoteza wakati.
Kwanza kuna msongamanao ndani ya madarasa, walimu ni wa kuokoteza na wanafunzi wanatumia muda mwingi kupokea wageni au kutakiwa kwenda kwenye sherehe za kitaifa zisizokwisha.
Baaadhi ya viongozi wa serikali na matajiri, bila ya aibu, wamewapeleka watoto wao katika shule zilizodhaminiwa na washirika wa maendeleo wa nchi za nje kusaidia watoto yatima.
Hii leo ukienda shule ya yatima ya OSS ya Zanzibar utashangaa na kushitushwa kuona zaidi ya asilimia 60 ya wanafunzi si yatima bali ni watoto wa viongozi na wafanyabiashara wakubwa wa nchi hii.
Hii ni aibu na ni dhambi, lakini wenye fedha na vyeo mara nyingi huwa hawajali kwa vile wanaongozwa na jeuri na kibri na si utu na ubinaadamu, imani wema au hisani. Watu hawa hawaoni kuwa wanavyofanya ni vibaya.
Wakati sasa umefika kwa serikali kulitupia macho suala hili kwa kuonyesha imani na huruma kwa watoto wa kimasikini.
Huu mchezo wa kuchezea mitihani na hatimaaye kuathiri zaidi watoto wa kimaskini ni wa hatari na hauna mwisho mwema.
Hivi sasa katika kila pembe ya Unguja na Pemba wazazi na watoto wao wanasikitika na wengine kulia kutokana na kufutwa kwa matokeo ya mithani wa kidato cha nne kwa mamia ya watoto wa kimaskini.
Ukweli ni kwamba Baraza la Mitihani Tanzania limeshindwa kazi yake na wizara zetu za elimu, Bara na visiwani zimeshindwa kuwajibika katika kuhakikisha mitihani haivuji.
Matokeo yake ni kwamba watoto wa kimasikini na wazee wao walioweka matumaini kwamba elimu ingewasaidia kutokana na umaskini (ukweli ni ufukara) na unyonge wa maisha ndio wanaoumia na kuteseka.
Hapa tujiulize ni nani wa kulaumiwa kwa kuvuja mitihani? Ni hawa wanafunzi au kutokuwepo uadilifu na ulinzi wa kutosha hata mitihani ikavuja?
Kilichojitokeza hapa ni kwamba wanaostahiki kulaumiwa na kubeba dhamana ni Baraza la Mitihani kwani ni dhahiri kuwa kazi imewashinda na kwa vile imedhihirika wazi kuwa hawawezi kusimamia mitihani kinachotakiwa ni kujiuzulu.
Lakini lililo muhimu zaidi ni kwa wahusika kuwajibishwa kikazi na kisheria na si kuwaadhibu watoto wa kimaskini.
Hapa nataka nikumbushe kwamba zama za ukoloni nilipokuwa ninafanya mitihani ya darasa la nane na baadaye kidato cha nne hizi habari za kuvuja mitihani na udanganyifu zilikuwa hazisikiki.
Kama wakoloni waliweza kudhibiti mitihani isivuje miaka ile nini kinachopelekea leo kuvuja kwa mitihani iwe jambo la kawaida kama si kutokuwapo uadilifu na kushamiri kwa uhuni?
Tujiulize kulikoni hii leo? Jawabu unayoipata na ambayo ni sahihi kwa mapana na marefu ni kutokuwepo uongozi mzuri katika kusimamia mitihani na uhuni kutawala mwenendo mzima wa kuendesha shughuli za serikali.
Hii ni aibu na fedheha, tena kubwa na wahusika hawastahili kuvumiliwa wala kuonewa huruma. Kama wao hawahurumii watoto wa kimasikini hapana sababu kwa jamii kuwaonea huruma.
Lakini ukichunguza utaona waliohusika na uvujaji wa mitihani wamepoa na hawana wasiwasi kwa vile wana uhakika wa kulindwa kwa sababu za kisiasa.
Si ajabu hivi sasa waliohusika na kuvujisha mitihani wakawa wanapanga namna bora ya kuvujisha mitihani ya mwaka huu ili kujipatia fedha za bure kwa kuwa wanaelewa na kujiamini kuwa hawatawajibishwa kikazi wala kisheria. Kwa watu hawa kuvujisha mitihani ni sehemu ya kazi yao.
Hali hii ni ya hatari na inatisha. Serikali inapaswa kuelewa kwamba uhuni wa kuvujisha mitihani na baadaye kufuta matokeo ya shule kadhaa unawaumiza na kuwadhulumu watoto wa kimasikini ambao walitegemea elimu hapo baadaye ingewakomboa na maisha duni wanayokabiliana nayo hivi sasa.
Katika nchi nyingi zinazoheshimu utawala bora na demokrasia (tofauti na ilivyo Tanzania) panapotokea aibu kama hii ya kuvuja mitihani hatua ya kwanza inayofuata ni kwa viongozi wa juu wa Wizara ya Elimu (Bara na Visiwani) na wale wa Baraza la Mitihani kuachia ngazi kwa vile kazi waliopewa imewashinda.
Lakini huu utamaduni mchafu na unaonuka tulionao wa kulindana kwa maovu tunayoyatenda au kuruhusu wasaidizi wetu kufanya uhuni na wasiwajibishwe utaendelea kutuponza na gharama zake ni kubwa.
Mpaka pale tutapoanza kutoa umuhimu kwa uwajibikaji hizi hadithi za kuvuja mitihani kila mwaka zitaendelea na matokeo yake ni kuendelea kuwaumiza watoto wa kimasikini zitaendea tena kwa kasi zaidi.
Wahusika na uvujaji wa mitihani watasema Tumethubutu na tunaweza na tutaendelea”.
Ni vizuri kama hatuwezi kuwasaidia watoto wa kimaskini tuache kufanya maovu yanayosababisha kuwakandamiza.
Leo mambo haya yananyamaziwa na hapa na pale ndiyo hupigiwa kelele, lakini tukumbuke kama leo suala hili halitazusha balaa historia hapo baadaye itatuhukumu kwa kuwadhulumu watoto wa kimaskini.
Suala la mitihani ni mtihani, lakini maisha ni kupambana na mitihani. Ni vema tukapambana na mtihani huu bila ya woga au kulindana bila ya sababu za msingi
Chanzo: Tanzania Daima
Aziza Mohammed mwanafunzi aliyeathirika kufutiwa matokeo yake ya mtihani wa kidatu cha nne aliacha simanzi kubwa ukumbini baada ya kueleza masikitoko yake ya kufutiwa mitihani na kuelezea jeshi la polisi lilivyowanyanyasa wakati wlaipopanga kuandamana kupinga matokeo hayo ambapo licha ya kupata kibali cha maandamano lakini jeshi la polisi liliingilia kati na kuwatawanya kwa kuwarushia mabomu ya machozi na kuwanyanyasa huku wengine wakipigwa na kutupwa katika gari la polisi hivi karibuni, lakini Aziza aliwalaumu wazazi wa wanafunzi hao ambao walishindwa kuwaunga mkono watoto wao katika hilo pamoja na kuwalaumu waandishi wa habari kwa kushinda kuwapa coverage katika tukio hilo
BAADHI ya wazazi ambao watoto wao wamefutiwa matokeo ya mitihani ya kidato cha nne visiwani Zanzibar wanakusudia kulifikisha mahakamni Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) kwa kutoa adhabu hiyo kinyume cha sheria.
Wazazi hao walitoa kusudia hilo mjini hapa jana katika wakati wa mjadala uliowashirikisha wadau mbali mbali wa sekta ya elimu na wanaharakati kujadili uamuzi wa Necta wa kuwafutia matokeo wanafunzi 3,303 kutoka Tanzania bara na Zanzibar na kuwazuia kufanya mitihani kwa muda wa miaka mitatu.
Ameir Hassan Ameir alisema pamoja na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya baraza hilo , kuna haja kwa wananchi visiwani humo kuitisha maandamano makubwa kupinga kufutwa kwa matokeo hayo na kushinikiza kuondolewa kwa dhabu dhidi ya wanafunzi.
Akipinga taarifa ya Necta kwamba mitihani hiyo imefutwa kwa sababu ya udanganyifu uliofanywa na wanafunzi, Ameir alisema baraza limeshindwa kuthibitisha udanganyifu huo na hivyo haliwezi kujiondoa katika kashfa ya kuvuja mtihani.
Alisema kushindwa kwa Katibu Mtendaji wa Necta, Joyce Ndalichako kutoa maelezo juu ya idadi na majina ya wananfunzi waliofutiwa mitihani kutoka kila upande wa Muungano, kumeibua hisia kwamba Tanzania bara imeandaa njama za kuua elimu elimu Zanzibar .
“Necta wanayo majina ya shule na namba za shule zote za Zanzibar , hivyo si kweli kwamba hawajui majina ya wanafunzi waliofutiwa mitihani,” alisema Ameir huku akihoji uwepo finyu wa ushiriki wa Zanzibar katika muundo wa Bodi ya Wakurugenzi wa Necta.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana wakati wa mjadala huo, bodi ya Necta ina wajumbe 14 na kati ya hao sita wanatoka upande wa Zanzibar .
“Sisi tuna uchungu na Zanzibar yetu, kuvuja kwa mitihani na watoto kufutiwa mitihani ni matokeo ya kero za Muungano. Adhabu ya miaka mitatu itawapotezea watoto wetu muda wa kusoma, Wazanzibari tuungane tulishtaki Necta,” alisema.
Ali Hassan, Mkuu wa zamani wa Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja alisema ingawa Necta imeshindwa kutoa idadi ya wanafunzi waliathirika na uamuzi wa kufutwa matokeo, anaamini asilimia kubwa wanatoka upande wa visiwani wa Muungano.
Alisema maelezo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Necta mbele ya mkutano na waandishi wa habari Februari 14 mjini hapa yanapaswa kusikilizwa tu na mtu asiyejua chochote na kuongeza kuwa kwa hatua hiyo: “ Mama Ndalinacho amefeli astep down.” Akiwa na maana aachie ngazi.
Faisal Mohamed, ambaye pamoja na Ali walisema ni miongoni mwa waathirika wa watoto wao kufutiwa mtihani alisema alivishambulia vyombo vya habari na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa alichoeleza kuwa kushindwa kuandika kwa kina habari za kashfa ya mitihani na kupokea kutoka Necta na kusaini taarifa bila kudadisi maelezo ya baraza hilo juu ya utata wa matokeo na hatua zilizochukuliwa dhidi ya wanafunzi.
Hata hivyo walalamikaji wote hawakueleza kusudio la kulishtaki baraza litatekelzwa kwa sheria, lakini walisema chini ya makosa ya jinai ni kinyume cha sheria kutoa hukumu ya jumla kwa kosa ambalo ni la mtu mmoja mmoja. Kwa kufuatilia taarifa hii tafadhali nenda katika wall yangu ya facebook ya salma said.
Dressed in black: Two women pause to look at the memorial display before they go into the church to pay their last respects to Whitney Houston
Escort: A procession of cars with flowers - one of which is the golden hearse carrying her casket - drive down the Newark street after the service escorted by a police car
The golden hearse carrying the body of singer Whitney Houston bears a photo of her in the window as her family and friends prepare to say goodbye to the star
Death of a star: Pall-bearers carry the casket of pop singer Whitney Houston to a hearse following her funeral service at the New Hope Baptist Church in Newark, earlier today


Denied: Brown is believed to have got into an argument with Whitney's family over whether or not he could bring nine people into the church with him. He was invited and told he could bring two people but instead showed up with an entourage of nine and stormed out when he was told they could not be seated

Final journey: Whitney Houston's silver casket was carried out as her greatest hit I Will Always Love You was played
Emotional time: Whitney Houston's mother Cissy Houston, 78, was seen arriving at the funeral home for a special private viewing with close friends and family on Friday afternoon
Sad day: Whitney's daughter Bobbi Kristina was also seen arriving at Whigham Funeral Home in New Jersey yesterday
Kim Burrell sings one of Whitney's favourite songs, changing the lyrics to make it more personal to the singer
Not singing: Aretha Franklin, who performed at Radio City Music Hall in New York last night, pulled out of singing at her god daughter Whitney's funeral at the last minute, saying she was 'too ill'
Stevie Wonder said in his fantasy world he had a crush on Whitney before serenading the audience with Ribbons In The Sky
Singer Alicia Keys was tearful as she walked to the piano and spoke about her friendship with the singer
The Bodyguard co-star: Kevin Costner paid tribute to Whitney Houston today and shared fond memories of his time with the singer with the rest of the congregation
First mourner: The Rev Jesse Jackson leaves Whigham Funeral Home after visiting with the family of Whitney Houston before going to the New Hope Baptist Church to prepare for the service

A year later: Whitney Houston and her daughter Bobbi Kristina Brown were pictured together at the 2011 Pre-GRAMMY Gala. She died on the day of the same event this year
Last moments: Whitney Houston's last ever public performance on Thursday February 9 with her close friend Kelly Price. She was found dead two days later























