Gari ya mizigo ikiwa imeingia ufukweni mwa bahari ya funguni ikipakia mbao zinazotoka katika jahazi wakati maji yakiwa yametoka, bandari hii hutumika kwa kushushia mizigo aina ya miti na mkaa kutoka Dar-es-Salaam, awali ushushaji wa mizigo ulikuwa ukitolewa juu baada ya ukuta wa bandari hii kuharibika kwa maji ya bahari inakuwa usumbufu wakati wa maji yakiwa yamejaa inakuwa shida uchukuzi wake.
A cross section of international participants at the Star Travel.ru award ceremony in Moscow
Mr. Mbarouk N. Mbarouk, HOC Embassy of Tanzania Moscow, after receiving the Star Travel.ru award for Zanzibar
Star Travel.ru Diploma for Zanzibar - the best resort in Africa
Tanzania stand at the Moscow International Travel and Tourism Exhibition 2012, Moscow, Russia
Team Tanzania at the MITT 2012 Tanzania Stand with Star Travel.ru award of Zanzibar
Zanzibar became the winner of the annual Russian tourism consumer award "Star Travel.ru"-2011. The islands won the award for "Best Resort in Africa (excluding Egypt)”. Among the 23 resorts nominated by tourists and travelers for the award, Zanzibar gained the most votes.
The official Star Travel award ceremony was carried on 22 March 2012 within the framework of the Moscow International Travel and Tourism Exhibition (MITT 2012). Mr. Mbarouk N. Mbarouk, Head of Chancery of the Tanzanian Embassy in Moscow, received the award on behalf of the Embassy.
“Star Travel.ru "- is the first consumer award in tourism and the only one of its kind in Russia. The prize was conceived in 2003 and is awarded on the results of online voting by tourists and travelers. In 2010 the Star Travel Award for the best resort in Africa (excluding Egypt) was won by Agadir (Morocco)
This year mark the 10th anniversary since Tanzania started regular promotions of its tourism attractions in the Russian Federation by participating in tourism exhibitions, organizing roadshows, seminars, press tours, distribution of brochures etc. The Star Travel award, therefore, is partly recognition of these promotion efforts carried out by tourism stakeholders, namely Tanzania Tourism Board, Zanzibar Tourism Commission, Tanzania National Parks, the Embassy of Tanzania in Moscow and others, over the last 10 years.
Wasanii wa maigizo wa kikundi cha Valentine Arts Group cha mtaa wa Jang'ombe, juzi walinusurika kupata kipigo baada ya watu waliohudhuria onesho lao kuzusha vurugu, na wasanii hao kuokolewa na polisi.
Onesho la kikundi hicho lilifanyika katika skuli ya Chumbuni kwa kutunia umeme wa jenereta kutokana na juzi Jumapili nishati hiyo kuzimwa nchi nzima kwa ajili ya matengenezo katika kituo cha Ubungo mjini Dar es Salaam.
Vurugu hizo zilianza mara baada ya kuharibika kwa jenereta hali iliyosababisha kuvunjika kwa onesho hilo.
Hali hiyo iliwafanya baadhi ya watu waliohudhuria kuanza kurusha mawe dhidi ya wasanii hao akiwemo mwanamama aliyejipatia umaarufu kwa jina la Bi Tele anayeigiza uchawi katika igizo la ‘Husdaa’ linalorushwa kila siku ya Jumatano katika kituo cha ZBC Televisheni.
Akizungumza na gazeti hili mara baada ya polisi kudhibiti ghasia hizo, Mwalimu msaidizi wa kikundi hicho Samuel Said Makunga, alisema vitendo hivyo si uungwana, na kwamba wananchi hao hawakupaswa kufanya fujo na badala yake walikuwa wasubiri.
Naye msanii anayetikisha katika igizo la ‘Husdaa’ Bi Tele, alilaani vitendo hivyo na kuongeza kuwa akili za vijana waliohusika navyo zinasumbuliwa na bangi.
Kwa upande wao, baadhi ya wapenzi wa sanaa waliokuwepo, walidai kuwa walilazimika kufanya hivyo kwani tayari walikwishalipa fedha ili kupata burudani hiyo, na kwamba waliamua kuwapa fundisho wasanii hao.
A doctor entered the hospital in hurry after being called in for an urgent surgery. He answered the call asap, changed his clothes and went directly to the surgery block. He found the boys father going and coming in the hall waiting for the doctor. Once seeing him, the dad yelled: Why did you take all this time to come? Dont you know that my son's life is in danger? Don't you have the sense of responsibility??The doctor smiled and said: I am sorry, I wasn't in the hospital and I came as fast as I could after receiving the call. And now, I wish you would calm down so that I can do my work??Calm down?! What if your son was in this room right now, would you calm down? If your own son dies now what will you do??? said the father angrily. The doctor smiled again and replied: From dust we came and to dust we return. Doctors cannot prolong lives. Go and pray to God for your son, we will do our best by Gods grace??Giving advice when we're not concerned is so easy? Murmured the father. The surgery took some hours after which the doctor went out happy, Thank God!, your son is saved!?And without waiting for the father.s reply he carried on his way running. If you have any question, ask the nurse!!??
Father: Why is he so arrogant? He couldnt wait some minutes so that I ask about him my son's state? commented the father when seeing the nurse minutes after the doctor left. The nurse answered, tears coming down her face: His son died yesterday in a road accident, he was in the burial when we called him for your son's surgery. And now that he saved your son's life, he left running to finish the formalities.
We sometimes feel we have the worst moments and yet there are people whose lives are really messed up but they remain strong enough to carry on our burdens!
When you are really focused with what you believe and want to achieve then there is a point in life that you have to eliminate some people no matter how close they are you have to free them and it hurts but its healthy as long as they make you loose focus then they should go....come back to them when you are satisfied with your achievements....and they will understand and be happy and proud of you and if NOT then they were never real and true to your life.
ZANZIBAR imefanikiwa kuwa mshindi wa kwanza na kujinyakulia tuzo ya Utalii nchini Russia kwa mwaka 2011, ‘Star Travel.ru 2011’.
Tuzo hiyo hushindaniwa kila mwaka kwa maeneo yalio bora zaidi kwa shughuli za kiutalii barani Afrika, ambapo watalii na waongoza watalii wa nchi hiyo hutembelea.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Mkurugenzi Mkuu wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Ali Khalil Mirza, amesema amepokea taarifa hiyo kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Russia, ikielezea Zanzibar kuchaguliwa kuwa mshindi wa tuzo hiyo, kama eneo lililo bora kwa shughuli za kiutalii barani Afrika.
Alisema kuwa kinyang’anyiro hicho kilihusisha maeneo 23 yalio bora zaidi kwa shughuli za kiutalii, ispokuwa nchi ya Misri haikushirikishwa.
Alisema tayari tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Ubalozi wa Tanzania nchini humo tangu juzi katika hafla maalum ilioambatana na kuanza kwa maonyesho ya Kimataifa ya Utalii nchini.
Mirza alisema ushindi wa tuzo huyo unatokana na msukumo mkubwa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Russia pamoja na hatua ya Kamisheni hiyo kufanya ziara maalum ya kuutangaza utalii wa Zanzibar mnamo 2009.
Alisema makubaliano yaliofikiwa kati ya Kamisheni ya Utalii na Makampuni ya kutembeza watalii yamelifanya soko la Utalii nchini Russsia kuimarika, ambapo wastani wa watalii 300 hufika nchini kila mwaka tangu wakati huo.
Alieleza kuwa hayo ni mafanikio makubwa kwa soko la utalii nchini Russia kwa kuzingatia watalii wanaokuja ni wale wanaotumia zaidi, ambao hufikia katika Hoteli zenye hadhi za juu kama vile Plan Hotel,Lagema,Green of Zanzibar na The Residents.
Aidha alisema Kamisheni yake ina matumaini makubwa kuwa ifikapo 2013 idadi ya wataalii kutoka nchi hiyo itaongezeka, hususan pale Shirika la ndege la Uturuki litakapoanza kufanya safari zake moja kwa moja hadi Zanzibar, ikizingatiwa watalii hao hivi sasa hutumia usafiri wa Shirika la Emirates, na kutembelea kwanza katika Mbuga za wanyama na hatimae kuja Zanzibar.
Mkurugenzi huyo alivitaja baadhi ya vigezo muhimu vinavyozingatiwa katika kumpata mshindi wa tuzo hiyo, kuwa ni pamoja na hali ya usalama, kufikiwa kwa matarajio ya wageni, vivutio vya utalii ikiwemo michezo mbali mbali (pwani na ufukweni), huduma katika mahoteli pamoja na tamaduni za wenyeji.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wanaoshiriki Semina ya Siku Moja inayohusu utekelezaji wa Mkuza wakisikiliza Hotuba ya Ufunguzi iliyotolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hayupo Pichani huko kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika Picha pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar baada ya kuifungua Semina ya Utekelezaji wa Mkuza nje wa ukumbi wa Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani.
Juhudi za kupambana na Umaskini hapa Nchini ni vyema zikajikita zaidi katika kuimarisha Uchumi sambamba na huduma za Kijamii kwa lengo la kustawisha maisha bora ya Wananchi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema hayo wakati akiifungua Semina ya siku mbili ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayohusu utekelezaji wa Mpango wa Kupunguza Umaskini Zanzibar { MKUZA } inayofanyika katika Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani.
Balozi Seif alisema wimbi la umaskini hushamiri iwapo jamii itakosa huduma za Elimu, ongezeko la uzazi katika umri mdogo, ukosefu wa usawa wa kijinsia pamoja na uchumi duni kwa akina mama ambao ndio wengi katika familia.
Balozi Seif alisema Umoja wa Mataifa umepitisha Azimio la utekelezaji wa Malengo la Milenia ili Dunia iondokane na umaskini ifikapo mwaka 2015 na kuzitaka Nchi Wanachama hasa zinazoendelea kujipangia mikakati ya kuuondoa Umaskini kwa kupitia utekelezaji wa Mipango yao ya maendeleo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisisitiza kwamba Serikali imo katika hatua za kupambana na umaskini kupitia utekelezaji wa Mkuza ingawa Wananchi waliowengi bado hawajaelewa Mpango huu.
Alieleza kwamba yapo mafanikio makubwa yamepatikana katika huduma za Kijamii zikiwemo Elimu, Afya na huduma za Maji safi mafanikio yanayoonekana zaidi kwenye kupunguza umaskini usio wa kipato.
Akizungumzia changamoto zilizojichomoza wakati wa utekelezaji wa Mkuza Balozi Seif alisema Mfumko wa bei umekuwa bado tatizo kinyume na lengo la chini ya asilimia 10% ukiathiriwa zaidi na ongezeko la bei ya mafuta na chakula katika soko la Dunia.
Akigusia Ukuaji mdogo wa Sekta ya Kilimo wa asilimia 4.6 Balozi Seif alisema unaonekana kushusha mchango wa Sekta hiyo katika pato la Taifa wakati Sekta ya Kilimo bado ni muajiri Mkuu wa nguvu kazi ya Taifa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alifahamisha kwamba hali hiyo imechangia kuwa na mafanikio madogo katika kuhakikisha kuwepo kwa usalama wa chakula.
Semina hiyo ya siku mbili inahusisha Mada kadhaa ikiwa pamoja na Mipango ya Maendeleo, Mapitio ya Dira
ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020, Matokeo muhimu katika uchagumbuzi wa matumizi ya kaya pamoja na maandalizi ya Bajeti na mahusiano na Mkuza.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
MJANE Specioza Kamala ameendelea kusotea mafao ya mume wake aliyefariki miaka 13 iliyopita, huku mwaka huu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikimwandikia marehemu barua ya kumtaka ajaze fomu ya kulipwa mapunjo ya mshahara baada ya kupanda daraja.
Marehemu Richard Mutakulemberwa aliyekuwa mwalimu katika shule ya sekondari Kahororo iliyopo Manispaa ya Bukoba, alikutwa na mauti August,19 mwaka 1998 wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na T.Kagumisa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ambayo Fikra Pevu ina nakala yake, pamoja na mambo mengine inamtaka marehemu kujaza fomu kutokana na utaratibu mpya wa malipo ya malimbikizo.
Pia barua hiyo ya Januari 4, 2012 iliyotumwa kupitia shule aliyokuwa akifundisha marehemu ya Kahororo inamtaka kufuata maelekezo kwa mujibu wa barua hiyo ili madai yake yaweze kushughulikiwa.
“Tafadhali mara upatapo barua hii jaza na utume kwa Katibu Mkuu fomu halisi na nakala moja (photocopy), pia ambatanisha barua yenye maelezo sahihi ya madai,nakala ya barua ya kupandishwa na kukubali cheo na ‘salary slip’ ya karibuni,” inaeleza sehemu ya barua hiyo kwenda kwa marehemu.
Pia mbali na barua hiyo kumtakia marehemu ushirikiano mwema katika kukamilisha zoezi hilo, inamkumbusha kuwa nyaraka zote lazima zipite kwa mkuu wake wa kituo na kutumwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Naye mjane wa Marehemu, Specioza Kamala mbali na kusikitishwa na hali hiyo, alisema tangu kufariki kwa mume wake mwaka 1998 ameendelea kufuatilia madai ya mume wake bila mafanikio na hata kufika Wizarani huku akipewa kauli za ahadi.
Alisema kuwa mbali na kuwa alishapata barua hiyo aliyoandikiwa marehemu mume wake, anachokumbuka ni kuwa mme wake alifariki kabla hajalipwa mapunjo ya mshahara baada ya kupandishwa daraja ambayo ameendelea kuyafuatilia bila mafanikio na kuwa mirathi ya marehemu ilishatolewa.
“Alipanda daraja mwaka 1996 na kufariki kabla ya kulipwa mapunjo yake ya mshahara,suala hili nilishawaeleza hata watu wa Utumishi wa Umma kutoka Dar es salaam na kunielekeza niende Wizarani na baada ya kwenda walisema faili lake halipo,” alisema mama huyo ambaye pia ni mwalimu katika moja ya shule za msingi Mkoani Kagera.
Alipoulizwa kama suala hilo liliwahi kufika katika Ofisi za Chama cha Walimu Mkoani hapa, Katibu wake wa Mkoa Aaron Masalu alisema halijafika katika ofisi hiyo huku akilihusisha na mfumo mbovu wa utunzaji wa takwimu za watumishi.
Pia alidai vyombo vinavyomshughulikia mwalimu havina utaratibu mzuri wa mawasiliano na kusema kuwa sasa wakati umefika wa mwalimu kushughulikiwa na chombo kimoja tofauti na ilivyo sasa.
Alisema mbali na kuwa utaratibu uliopo unaweza kuchelewesha malipo ya mhusika au kuyakosa kabisa alidai suluhisho ni kuwa namwajiri mmoja ambapo hivi sasa walimu wanashughulikiwa na Tamisemi,Utumishi wa Umma na Wizara yenyewe.
Imeandikwa na Phinias Bashaya-Kagera
[ Read More ]
Marehemu Richard Mutakulemberwa aliyekuwa mwalimu katika shule ya sekondari Kahororo iliyopo Manispaa ya Bukoba, alikutwa na mauti August,19 mwaka 1998 wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na T.Kagumisa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ambayo Fikra Pevu ina nakala yake, pamoja na mambo mengine inamtaka marehemu kujaza fomu kutokana na utaratibu mpya wa malipo ya malimbikizo.
Pia barua hiyo ya Januari 4, 2012 iliyotumwa kupitia shule aliyokuwa akifundisha marehemu ya Kahororo inamtaka kufuata maelekezo kwa mujibu wa barua hiyo ili madai yake yaweze kushughulikiwa.
“Tafadhali mara upatapo barua hii jaza na utume kwa Katibu Mkuu fomu halisi na nakala moja (photocopy), pia ambatanisha barua yenye maelezo sahihi ya madai,nakala ya barua ya kupandishwa na kukubali cheo na ‘salary slip’ ya karibuni,” inaeleza sehemu ya barua hiyo kwenda kwa marehemu.
Pia mbali na barua hiyo kumtakia marehemu ushirikiano mwema katika kukamilisha zoezi hilo, inamkumbusha kuwa nyaraka zote lazima zipite kwa mkuu wake wa kituo na kutumwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Naye mjane wa Marehemu, Specioza Kamala mbali na kusikitishwa na hali hiyo, alisema tangu kufariki kwa mume wake mwaka 1998 ameendelea kufuatilia madai ya mume wake bila mafanikio na hata kufika Wizarani huku akipewa kauli za ahadi.
Alisema kuwa mbali na kuwa alishapata barua hiyo aliyoandikiwa marehemu mume wake, anachokumbuka ni kuwa mme wake alifariki kabla hajalipwa mapunjo ya mshahara baada ya kupandishwa daraja ambayo ameendelea kuyafuatilia bila mafanikio na kuwa mirathi ya marehemu ilishatolewa.
“Alipanda daraja mwaka 1996 na kufariki kabla ya kulipwa mapunjo yake ya mshahara,suala hili nilishawaeleza hata watu wa Utumishi wa Umma kutoka Dar es salaam na kunielekeza niende Wizarani na baada ya kwenda walisema faili lake halipo,” alisema mama huyo ambaye pia ni mwalimu katika moja ya shule za msingi Mkoani Kagera.
Alipoulizwa kama suala hilo liliwahi kufika katika Ofisi za Chama cha Walimu Mkoani hapa, Katibu wake wa Mkoa Aaron Masalu alisema halijafika katika ofisi hiyo huku akilihusisha na mfumo mbovu wa utunzaji wa takwimu za watumishi.
Pia alidai vyombo vinavyomshughulikia mwalimu havina utaratibu mzuri wa mawasiliano na kusema kuwa sasa wakati umefika wa mwalimu kushughulikiwa na chombo kimoja tofauti na ilivyo sasa.
Alisema mbali na kuwa utaratibu uliopo unaweza kuchelewesha malipo ya mhusika au kuyakosa kabisa alidai suluhisho ni kuwa namwajiri mmoja ambapo hivi sasa walimu wanashughulikiwa na Tamisemi,Utumishi wa Umma na Wizara yenyewe.
Imeandikwa na Phinias Bashaya-Kagera



