Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

HAPPY ISLAMIC NEW YEAR.Muharaam


                                     Nawatakia wadau wote furaha ya mwaka mpya wa kiislam.
                                          MAY ALLAH BLESS YOU ALL...AMIN.
            
[ Read More ]

ZANZIBAR BILA YA UMEME KWA MARA NYENGINE TENA.




Tanzania bila Ufisadi tutafika?Je Zanzibar Bila Umeme inawezekana?Kuchaji simu 500,Saluni kichwa 2000,Soda 1000,Juice 500,Barafu 200,Maji ya kawaida hayapatikani,Wanaofaidika sasa ni Wazinifu na wizi,Sasa wewe ulioko nje ukijaribu kupiga simu kwa ndugu zako ZNZ usishtuke zikiwa zimefungwa ufahamu hakuna matatizo ila ni umeme tu.


Waziri wa maji ameshatangaza mapema mwakani (2010) umeme utapatikana,Je tatizo kama hili sasa linataka kupelekwa Pemba?Tayari Mh.Karume ashapokea kila nyenzo za kutandaza umeme kutoka Tanga,lakini Je hafahamu kwanza usipoziba ufa,Utajenga Ukuta?



mdau.

[ Read More ]

Miss Gibraltar is Miss World '09


Miss Gibraltar, Kaiane Aldorino has been crowned the Miss World 2009. The first runner up is Miss Mexico Perla Beltran and South Africa's Tatum Keshwar came up second runner up.
[ Read More ]

[ Read More ]

[ Read More ]

Mahakama yaamuru hoteli ya Bwawani ipigwe mnada


Mahakama Kuu Zanzibar, imeamuru kupigwa mnada Hoteli ya Kimataifa ya Bwawani inayomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) baada ya kushindwa kulipa deni la mchele la Sh. trilioni 1.6 kwa muda mwafaka.

Uamuzi huo ulitolewa baada ya kampuni ya Leamthore Rice Ltd kutoka nchini Thailand kushinda kesi ya madai namba 4 ya mwaka 1997, dhidi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Katika kesi hiyo, kampuni hiyo ilifungua mashitaka dhidi ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Zanzibar, baada ya Serikali kuchukua mchele kutoka kampuni hiyo na kushindwa kulipa kwa muda mwafaka.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilifunga mkataba wa kibiashara kuchukua mchele kutoka katika kampuni hiyo na kuuza katika soko la ndani la Zanzibar.

Amri ya kupigwa mnada hoteli hiyo ya Serikali ilitolewa na Mrajisi wa Mahakama Kuu ya Zanzibar Yesaya Kayange kufuatia hukumu iliyotolewa Mei 16, mwaka 1997 na Jaji Walfong Dourado.

Kwa mujibu wa barua ya Novemba 12, mwaka huu, uongozi wa Ushirika wa Mnada wa Kumekucha, umetakiwa kupiga mnada hoteli ya Bwawani ambayo ipo mita chache kutoka katikati ya Mji mkongwe wa Zanzibar.

“Ili haki itendeke, uendelee na utekelezaji wa hukumu ya kuuza Hoteli ya Bwawani Zanzibar”, alisema Mrajis huyo katika barua yake hiyo.

Mrajis huyo alieleza kuwa awali Mahakama iliamuru kupigwa mnada Shamba la Serikali liliyopo katika kijiji cha Kijichi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, lakini ilishindikana kutokana kutoeleweka kwa mipaka yake ya ardhi.

Akizungumza na Nipashe, Kiongozi Mwanadamizi wa ushirika wa mnada wa Kumekucha, Salim Ahmed Salim, alithibitisha kupokea amri ya Mahakama inayowataka kuipiga mnada Hoteli ya Bwawani ili kulipa deni la mchele iliyokuwa ikidaiwa Serikali.

Kampuni hiyo ilifungua kesi ya madai Januari, mwaka 1997 baada ya Wizara ya Fedha na Uchumi Zanzibar, kushindwa kulipa deni la dola za Marekani milioni 69.4 na kutaka walipwe riba ya asilimia 25 na gharama zote za kesi.

Kampuni hiyo ilikuwa ikitetewa na wakili wake, Masumbuko Lamwai na Mahakama Kuu iliamua kutoa hukumu baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi wakati huo, Omar Sheha Mussa, kushindwa kuzingatia wito wa Mahakama na kuamriwa kutolewa uamuzi huo.

Hata hivyo, upande wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ulichukua juhudi za kutaka kukata rufaa lakini muda ulikuwa umepita na hivyo kuamuliwa kulipwa kiwango hicho cha fedha pamoja na asilimia 25 ya riba tangu kutolewa kwa hukumu hiyo.

Kutokana na deni hilo kutolipwa kwa muda mwafaka, riba ya deni hilo iliendelea kuongezeka kutoka deni ya dola za Marekani milioni 69.4 hadi dola za Marekani biloni 1.6 sawa na bajeti ya miaka mitatu ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliingia mkataba wa kibiashara na kampuni hiyo wakati wa Utawala wa Serikali ya awamu ya nne chini ya uongozi wake marehemu Idrissa Abdul Wakil na aliyekuwa Waziri Kiongozi, Maalim Seif Sharif Hamad.

Iwapo amri hiyo ya Mahakama itatekelezwa, kampuni nyingi zitaathirika kwa vile hoteli hiyo hivi sasa imepangishwa baadhi ya makampuni yanayofanya biashara ya utalii na uwakala wa mizigo.

Tayari wafanyabiashara marufu Zanzibar na wengine kutoka nje ya nchi, wameanza kufanya matayarisho ya kuinunua hoteli hiyo ambayo ilijengwa kwa nguvu za wazalendo baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964.


source;nipashe.

[ Read More ]

HOTTEST HEADS OF STATE..


  1. Yulia Tymoshenko Prime Minister of Ukraine
    -
  2. Stoltenberg
    Jens Stoltenberg Prime Minister of Norway
    -
  3. Wangchuck
    Jigme Khesar Namgyel Wangchuck King of Bhutan
    -
  4. Kabila
    Joseph Kabila President of the Democratic Republic of the Congo
    -
  5. Kirchner
    Cristina Fernández de Kirchner President of Argentina
    -
  6. Correa
    Rafael Correa President of Ecuador
    -
  7. Henri
    Henri Grand Duke of Luxembourg
    -
  8. Skerrit
    Roosevelt Skerrit Prime Minister of Dominica
    -
  9. Macapagal-Arroyo
    Gloria Macapagal-Arroyo President of the Philippines
    -
  10. Topi
    Bamir Topi President of Albania
    -
  11. Bachelet
    Michelle Bachelet President of Chile
    -
  12. Lukashenko
    Alexander Lukashenko President of Belarus
    -
  13. Gusmão
    Xanana Gusmão Prime Minister of East Timor
    -
  14. Nasheed
    Mohamed Nasheed President of the Maldives
    -
  15. Obama
    Barack Obama President of the United States of America
    -
  16. Loong
    Lee Hsien Loong Prime Minister of Singapore
    -
  17. Funes
    Mauricio Funes President of El Salvador
    -
  18. Putin
    Vladimir Putin Prime Minister of Russia
    -
  19. Nkurunziza
    Pierre Nkurunziza President of Burundi
    -
  20. Kikwete
    Jakaya Kikwete President of Tanzania
    ree-
[ Read More ]

Child actor of Slumdog Millionaire loses his father


Mohmmed Azharuddin played the role of elder brother of the protagonist in the first half of the Oscar winning film Slumdog Millionaire. He lost his father on Friday.

The child actor was away at school at the time of his father’s death. According to family members the child was not aware of the declining health of his father.

Ismail Shaikh, 46, died due to tuberculosis. He was suffering from advanced tuberculosis for past two years. Apart from Azharuddin, Shaikh is survived by his wife Shamim, an older son and two daughters.

Shamim said that Shaikh had neglected his health and was totally immersed in making a bright future for Azharuddin, especially after the Slumdog Millionaire became an international box-office hit.

The child actor recently shifted to his new Santacruz home. Director Danny Boyle of the film has sent his condolences to the family. He will be visiting the family next month to express his support to the family.

[ Read More ]

Wachomana Sindano Zenye Damu Yenye Ukimwi China

Mashambulizi ya watu kuchomwa sindano zinazohofiwa kuwa na damu yenye virusi vya ukimwi, yamezidi kuongezeka katika jimbo lililokumbwa na vurugu za kikabila la Xinjiang lililopo magharibi mwa China. Kumekuwa na kuongezeka kwa idadi ya watu wanaoshambuliwa kwa kuchomwa sindano zinazohofiwa kuwa zina damu yenye virusi vya ukimwi au kemikali zenye sumu katika mji wa Urumqi uliopo kwenye jimbo la Xinjiang magharibi mwa China pamoja na kwamba serikali ya China imeweka ulinzi mkali kwenye jimbo hilo kuzuia mashambulizi hayo.

Mashambulizi hayo yanatokana na vurugu za kikabila kati ya kabila dogo la Uygur ambalo wengi wao ni waislamu na kabila kubwa la Han.

Wakazi wa mji huo wa kabila la Han wamekuwa wakiwalaumu watu wa kabila la Uygur kufanya mashambulizi hayo ya kuwachoma watu sindano.

Jumla ya watu 45 kutoka makabila yote mawili wameishakamatwa katika mji huo wakituhumiwa kuhusika na mashambulizi hayo ya kutumia sindano.

Polisi katika jimbo la Xinjiang walitangaza kupokea ripoti ya watu 77 kushambuliwa na kuchomwa sindano hizo katika kipindi cha kuanzia jumapili mchana mpaka jumatatu mchana.

Taarifa za awali zilisema kwamba kulikuwa na jumla ya watu 531 waliokumbwa na mashambulizi hayo ya kuchomwa sindano katika wiki chache zilizopita.

Baada ya wiki iliyopita maelfu ya watu kuandamana kwenye mji huo kutaka serikali iongeze ulinzi kukomesha mashambulizi hayo, serikali ya China iliamua kupeleka majeshi yake na polisi wengi sana katika mji huo kulinda amani.

Mashambulizi hayo yamesababisha hali tata kwenye mji huo na kutishia kutokea tena kwa vurugu kubwa za kikabila kama zilizotokea julai 5 mwaka huu ambazo zilisababisha vifo vya takribani watu 200 wengi wao wakiwa ni watu wa kabila la Han.

Taarifa iliyotolewa na serikali ya China ilisema kuwa watu watakaopatikana na hatia ya kuwadhuru watu kwa kutumia sindano, watahukumiwa adhabu ya kifo.

Hofu ya sindano hizo kuwa na damu yenye virusi vya ukimwi imetokana na kwamba jimbo la Xinjiang ndilo jimbo linaloongoza kwa waathirika wa ukimwi nchini China kukiwa na jumla ya waathirika 25,000 katika jimbo hilo kwa mujibu wa takwimu za mwaka jana. Idadi hiyo kubwa inasababishwa na watumiaji wengi wa madawa ya kulevya katika jimbo hilo kutumia sindano zilizotumiwa na wenzao.

source:nifahamishe
[ Read More ]

Urembo wamtumbukia nyongo.


Jitihada za kutafuta urembo wa ziada za mwanamke mmoja wa nchini Marekani zilimtokea puani baada ya sura yake kuharibika vibaya kiasi cha kuwa vigumu kutambulika alipoamua kujidunga sindano za urembo za silikoni.Mary Johnson mwenye umri wa miaka 54 mkazi wa California nchini Marekani katika jitihada zake za kutafuta urembo wa ziada aliamua kufanya upasuaji wa kurekebisha sura yake aonekane kijana na mrembo. Lakini Mary ambaye ni mama wa watoto watatu alipoambiwa kuwa upasuaji wa kurekebisha sura yake utamgharimu maelfu ya dola za Marekani, aliamua kughairi kufanya upasuaji huo hospitalini na kuamua kutumia njia za kujidunga sindano za silikoni. Baada ya kufanya utafiti kwenye Internet Mary alinunua sindano za kimiminika cha silikoni kwa dola 10 tu na kujidunga mwenyewe kwenye mdomo wake na kwenye mashavu yake. Badala ya sindano hizo kumfanya aonekane mrembo kama alivyotarajia, ziliiharibu kabisa sura yake na kuifanya iwe vigumu kwa mtu kumtambua. Baada ya muda mfupi sura yake ilianza kubadilika rangi na kuvimba na kwenye kona za mdomo wake kulitokea vidonda vikubwa visivyoeleweka. Hali ilikuwa mbaya kiasi cha kusababisha Mary awahishwe hospitali na kufanyiwa upasuaji wa kuifanya sura yake irudie hali yake ya zamani. Hivi sasa ingawa sura ya Mary imerudia hali yake ya zamani, Mary anakiri kujutia uamuzi wake wa kutafuta urembo wa ziada.

source:nifahamishe.com
[ Read More ]