Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

MISS YOU.



[ Read More ]

Friends Of Mafia: TAMKO KUHUSU TAMASHA LA MASHOGA.


Kisiwa cha Mafia


Sisi kama wenyeji wa kisiwa hichi na wenye nia uchungu na kisiwa hiki
tumesikitishwa na hatua ya baadhi ya wenye mahoteli ya kitalii kwenye
kisiwa hichi pamoja na uongozi mzima wa wilaya (DC) na halmashauri kutoa
kibali kwa kundi la burudani toka Ugiriki kuja kufanya vitendo vya ushoga
kwa kutumia mgongo wa Tamasha la muziki. 
Pia tumesikitishwa uongozi hapa Mafia kukubali kutoa kibali kwa hawa vijana
3,000(revelers) bila kupata ridhaa ya wenyeji wa Kisiwa hichi (Public
consultation). Tungependa ifahamike kuwa sisi kama wenyeji wa Kisiwa hichi
tunakaribisha wageni lakini ni LAZIMA wazingatie na waheshimu mila na
taratibu zetu na moja kati ya hizo mila zetu USHOGA haumo!
Kitendo cha kutaka kuleta vijana hawa mashoga hapa kisiwani kufanya
vitendo vyao kwa siku 14 mfululizo hakikubaliki kimaadili na tunawaunga
mkono wana Mafia na hasa wazazi ambao hawako tayari kuona watoto wao
wakishuhudia vitendo vya kishoga, utumiaji wa madawa ya kulevya ambavyo
ni si mila na desturi yetu kama waTanzania.
Kama mjuavyo Mafia ni kisiwa cha amani na ndio maana kimekuwa kinaongoza kwa utalii wa scuba diving duniani na tunaendelea kuwakaribisha watalii ambao wanakuja na kutuheshimu na wanaoelewa umuhimu wa kutunza mazingira ya kisiwa hichi.
Kisiwa hichi hakina uwezo wala fedha za kuweza kutoa huduma za afya kwa
watu wake iweje leo tamasha hili la mashoga 3,000 ambao itabidi wajisaidie
kwenye mashamba ya watu kwani hakuna public toilets za kuweza kuhimili
kishindo hichi.
Hivi kwa mfano mazingira yashachafuliwa ni sisi watu wa Kisiwa hiki ndio
tutasafisha au halmashauri? je wanazo pesa za kusafisha na kuokota toilet
papers zitakazo achwa na hawa Mashoga kwenye mashamba yetu?
Hospitali zetu hapa zinatia aibu na mbaya zaidi huduma za afya kwa mama
zetu na dada zetu wanapojifungua zipo katika hali duni, hivi kweli
mheshimiwa DC na timu yake wameona kwa sasa tunachohitaji ni hili Tamasha?
Kwa kawaida ya Mashoga hawatokaa sehemu moja hapa kisiwani na watataka
kwenda kufanya uchafu wao kwenye fukwe zetu hapa kisiwani, hivi Uongozi wa
Kisiwa hichi utatoa polisi wangapi kwa kila kundi la hawa mashoga kufanya
mambo yao? kwani sidhani kama wananchi watakaa na kushangilia vitendo
hivi vikifanyika hadharani.
Tungependa kuufahamisha umma kuwa hawa waandaji tamasha hili lilipofanyika kwenye kisiwa cha Skyros, watu walililalamika sana pamoja na kuwa Wagiriki wana mitizamo ya ku liberali kwenye mambo haya lakini hali ilikuwa mbya kiasi cha Polisi kuvamia na kusitisha lile Tamasha kwani lilikuwa linaelekea kuvujinka kwa amani.
Katika kipindi hichi ambacho tunaelekea kwenye Uchaguzi je ni kweli
Serikali inataka kuona uvunjikaji wa amani katika kipindi hichi
tunachoelekea kwenye Uchaguzi kwa kukubali hili tamasha la Mashoga?
Je jeshi la polisi linazo resources za kulinda mashoga 3,000 usiku na
mchana kwa siku saba mfulululizo?
Kwa nini mratibu wa hili Tamasha hili la Mashoga hataki kukutana na viongozi wa Kisiwa hichi na kuwaeleza kwa
kinagaubaga nia yake?
Maandaji wa Tamasha hili wamesema wamepata ushirikiano wa karibu na
kampuni ya uwindani na utalii inayojiita KARIBUSANA ambayo iko chini ya
Costa Coucoulis,Angela Damas,Chyrista Batou na Mark Evans ambao wanajiita
wahifadhi wa mazingira kwenye tovuti yao lakini wakati huo huo wako tayari
kuhakikisha kuwa mazingira ya kisiwa chetu yanachafuliwa na hawa wageni.
Je Mbunge na DC wa Kisiwa hichi watakuwa wanatekeleza ilani ya chama gani
kulikubali hili Tamasha la Mashoga?
Je wilaya iliyo masikini kuliko zote Tanzania inahitaji Tamasha la muziki
au tunahitaji miradi ya Maendeleo?
Je BASATA na Wizara ya Utalii wameamua
[ Read More ]