Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Shambulio la bomu hotelini Pakistan


Takriban watu kumi na mmoja wameuawa na wengine zaidi ya sitini kujeruhiwa katika shambuli la bomu la kujitoa mhanga katika hoteli moja nchini Pakistan.

Kwa mujibu wa maafisa waandamizi nchini humo, shambulio hilo lilitokea katika mji wa Peshawar kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.

Ripoti za vyombo vya habari nchini humo, zimeeleza watu waliokuwa wamejihami waliwashambulia walinzi karibu na hoteli ya kifahari ya Pearl Continental kabla ya kulipua gari liliokuwa limebeba shehena ya mabomu eneo la kuegeshea magari.

Walioshuhudia tukio hilo waliiambia BBC, mlipuko huo ulionekana hadi umbali wa kilomita tano. Sehemu moja ya hoteli hiyo imeporomoka kabisa.

Mwandishi wa BBC nchini Pakistan amesema hoteli hiyo ndiyo maarufu zaidi katika mji wa Peshawar na ni mojawapo ya majengo yanayotambuliwa zaidi ya mji huo.

Miji kadhaa nchini Pakistan ukiwemo ule wa Peshawar imekumbwa na mashambulio ya mabomu tangu jeshi la nchi hiyo lilipoanza harakati za kupambana na wanamgambo wa Taliban.

Hata hivyo hakuna aliyekiri kuhusika na mashambulio hayo.

[ Read More ]

Ghailani lands in New York


UNITED States authorities have announced that Ahmed Khalfan Ghailani, a Tanzanian national accused of involvement in the 1998 US embassy bombing in Dar es Salaam arrived early yesterday morning in New York to face criminal charges. Ghailani had been held at the notorious Guantanamo Bay detention facility in Cuba since September 2006. After a thorough review of his case, the Tanzanian was recently referred for criminal prosecution in the Southern District of New York pursuant to a March 12, 2001 indictment against him. Ghailani was transferred from the custody of the US Department of Defence to the Southern District of New York by America’s Marshals Service. He is currently in custody at the Metropolitan Correctional Centre in New York, which has housed numerous terror suspects over the years during their prosecutions in the city’s Southern District. The Tanzanian was later yesterday expected to make his initial appearance in Manhattan federal court. Ghailani faces 286 separate counts in the indictment. Among other violations, the superseding indictment charges him with conspiring with Osama bin Laden and other members of al-Qaeda to kill Americans anywhere in the world, as well as separate charges of murder for the deaths of each of the 224 people killed in the simultaneous US embassy bombings in Tanzania and Kenya and various other offences related to the bombings. ’’With his appearance in federal court today, Ahmed Ghailani is being held accountable for his alleged role in the bombing of US embassies in Tanzania and Kenya and the murder of 224 people,’’ said US Attorney General Eric Holder. ’’The Justice Department has a long history of securely detaining and successfully prosecuting terror suspects through the criminal justice system, and we will bring that experience to bear in seeking justice in this case.’’ Ghaliani has already admitted having once met bin Laden, but apologized for his role in the bomb explosion. He insisted that he had been kept in the dark about the purpose of the attack on the US embassy in Tanzania. ’’It was without my knowledge what they were doing, although I helped them,’’ said Ghailani, according to official court transcripts. He added: ’’I’m sorry for what happened to those families who lost...who lost their friends and their beloved ones.’’ Ghailani also said he once met Osama bin Laden. More than a decade ago, a federal grand jury in New York indicted Ghailani on charges that he helped plan the bombing of the US embassy in Dar es Salaam on August 7, 1998. At the time, he was still a fugitive. He was finally captured in Pakistan in 2004, held in secret prisons run by the Central Intelligence Agency (CIA), and transferred in 2006 to the naval base at Guantanamo Bay. Last year, US military prosecutors filed war crimes charges against him in connection with the embassy bombing episode. Ghailani thus became a rare detainee facing similar charges in both military and civilian courts, for the same act. The baby-faced and diminutive Tanzanian -- known as ’’Fupi’’ -- faced a bounty of $25m when he was nabbed after a 12-hour shoot-out at an Al Qaeda safe house in Pakistan. Ghailani rose from an Al Qaeda ’’rank-and-file soldier’’ in Afghanistan before the September 11, 2001 (9/11) attacks in the US to become Bin Laden’s cook and his most prolific passport forger and travel agent, according to official records. He was among the original 22 ’’most wanted’’ terrorists designated by ex-President George W. Bush’s Federal Bureau of Investigations (FBI) after 9/11, even though the US government admits he ’’was not directly involved in operational planning’’ by Al Qaeda. US President Barack Obama has come under sharp criticism from Congress for allowing Ghailani to be transferred to America to face criminal charges.
[ Read More ]

Shahidi aeleza maiti ya albino alivyookotwa

KESI inayowakabili washitakiwa wa mauaji ya albino mkoani Shinyanga iliendelea kusikilizwa jana ambapo shahidi wa kwanza alianza kutoa ushahidi wake mbele ya Jaji Gadi Mjemas wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Akitoa ushahidi huo huku akiongozwa na wakili wa Serikali Bi. Veritas Mlay shahidi huyo Bw. Mayenga Matongo ambaye alikuwa Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Harawa alidai kuwa Desemba 4 mwaka juzi akiwa ofisini kwake alipokea taarifa kutoka kwa Yusuph Ramadhani kuwa kuna maiti imeonekana imetupwa katika mto Kidamlida.

Bw. Matongo alidai baada ya kupokea taarifa hizo aliandika barua kwa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Isanga Bw.Sayi Gamanya kumtaka aende kuangalia sehemu ya tukio ili kuthibitisha tukio hilo.

Aidha Shahidi aliongezea kuwa Bw. Gamanya hakutii agizo hilo ndipo shahidi alikwenda na baadhi ya watu katika mto wa kidamlida na kuanza kuusaka mwili ambapo saa 12:00 jioni Mei 4 mwaka jana walifanikiwa kuuona ukiwa kwenye kisima cha kunyweshea mifugo.

Bw.Matongo aliendelea kudai kuwa alitoa taarifa polisi wa Wilaya ya Bariadi Aprili 5 saa 7 mchana polisi walifika eneo hilo na zoezi la kuutoa mwili huo lilianza ambapo ilikutwa imekatwa kichwa na miguu yote miwili na kuhifadhiwa kwenye mfuko wa ambao ulikuwa umeanza kuoza.

Matongo alidai kuwa Diwani wa kata hiyo Bw. Juma Mapilipili kwa kushirikiana na wananchi wengine waliweza kuutambua mwili huo kuwa ni wa marehemu Lyaku Willy ambapo polisi walianza upelelezi wao ambapo iligundulika Mboje Mawe na Masahi Magumba waliokuwa wakiishi kijijini hapo walikuwa hawaonekani.


Alidai kuwa Desemba 6 mwaka jana alipata taarifa kuwa watuhumiwa hao walikuwa wamejificha katika milima ya kijiji cha Harawa na aliwachukua wanamgambo wawili wa vijiji vya Nkwindabuye na Harawa ili kumsaidia kazi ya kuwatafuta watuhumiwa hao.

Alidai tarehe hiyo hiyo majira ya jioni wanamgambo ho waliweza kumkamata Mboje kwenye milima ya kijiji cha Harawa ambapo
inadaiwa aliwataja watu wengine alioshirikiana nao katika mauaji hayo kuwa ni Sayi Mafizi,Chenyenye Maganyale,Sayi Gamanya,Gumbo Nzige na Masihi Magumba.


Kesi hiyo iko Mbele ya Jaji wamahakama Kuu ya Tanzania Bw. Gadi
Mjema ambapo mashahidi wanaendelea kutoa ushahidi wao. Hukumu ya kesi hiyo inatarajiwa kutolewa mwezi ujao.
[ Read More ]

Mama ajinyonga kwa wivu

MKAZI wa Kijiji cha Ukata katika kata ya Ukata wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, Bi. Rehema Ndunguru (40) amejinyonga na kufa kwa kinachosadikiwa ni kutokana na mgogoro wa mapenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Bw. Michael Kamuhanda amesema tukio hili lilitokea Juni 8, mwaka huu saa 3 asubuhi kijijini humo.

Alisema, Bi. Ndunguru alikutwa akiwa amejinyonga chumbani kwakwe kwa kutumia kanga na chanzo kimetokana na wivu wa kimapenzi ambapo imedaiwa mara nyingi alikuwa akimtuhumu mumewe kuwa si mwaminifu katika ndoa yao.

Alifafanua kuwa wakati mama huyo anajinyonga mume wake hakuwepo na kwamba watoto wake waliokuwa wakicheza nje walipoingia ndani walimwona mama yao akiwa ananing'inia chumbani na kutoa taarifa kwa majirani waliotoa taarifa Polisi.

Bw. Kamuhanda ameongeza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.
[ Read More ]

Mv Fatih yaundiwa tume

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeunda tume ya watu 8 kuchunguza chanzo cha ajali ya Mv. Fatih ambayo ilisababisha vifo vya watu 6 pamoja na hasara ya mali.

Akitangaza kuundwa kwa tume hiyo, Waziri wa Nchi, Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, Bw. Machano Othman Said alisema tume hiyo imepewa kazi ya kujua chanzo cha ajali ya Mv Fatih

Bw. Machano alisema tume hiyo imepewa muda wa mwezi mmoja kukamilisha kazi yake na kuwasilisha ripoti kwa wizara husika ambapo Mwenyekiti wa tume hiyo ni Jaji Omar Makungu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar akisaidiwa na nahodha mkongwe ambaye, Meneja Mkuu wa Shirika la Meli la Zanzibar Alhaji
Masoud Sururu.

Wajumbe wengine katika tume hiyo ni Bw. Abdalla Kombo, Bw. Mohamed Mahmoud Juma, Bw. Nahodha Hatib
Katundula kutoka katika kikosi cha jeshi la majini la KMKM, Meneja wa Ufundi wa Shirika la Bandari Zanzibar, Bw. Abdi Maalim.

Meli ya Mv Fatih ilipata ajali wakati ikikaribia eneo la Bandari ya Malindi mjini Zanzibar ambapo watu 34 walifanikiwa kutoka katika chombo hicho na wengine kuokolewa baada ya kuzama baharini.
[ Read More ]