Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Serikali ya Zanzibar yazuia waandishi kuingia bandarini

BAADA ya waandishi wa habari kupinga kunyanyaswa na askari wa vikosi vya serikali ya mapinduzi wakati wa ziara ya Rais Amani Abeid Karume juzi, Idara ya Habari ya serikali hiyo, jana ilizuia waandihi wa habari wa vyombo mbalimbali kuingia bandarini.

Miongoni mwa waandishi waliozuiwa ni wa vyombo vya habari binafsi pamoja na vya serikali ya Jamhuri ya Muungano, likiwepo Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Hatua hiyo ilidhihirika bada ya waandishi kadhaa kuzuiwa kuingia katika Bandari ya Zanzibar ambako kwa zaidi ya wiki sasa wamekuwa wakifika kufuatilia mwenendo wa harakati za uokoaji kutokana na ajali ya kupinduka kwa meli ya Mv Fatih.

Waandishi hao walipofika kwenye bandari hiyo walikuta orodha ya majina ya waandishi zaidi ya 10, ambao wamepigwa marufuku kuingia bandarini.

“Aah! Leo mmeumia, hamtaweza kuingia humu ndani kwa mujibu wa maelekezo tuliyopewa,” alisema mmoja wa askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambao walikuwa wakiongoza ulinzi bandarini hapo.

Askari huyo ambaye hakutaka kutaja jina alisema amepewa majina ya watu ambao wasingeruhusiwa kuingia bandarini humo jana.

“Sisi tunafanya kazi kwa maagizo. Amekuja Bosi wenu Juma (Afisa habari wa Maelezo Zanzibar) kasema wenye majina haya wasiingie labda muwasiliane naye,” alifafanua.

Waandishi waliozuiliwa ni wa magazeti, vituo binafsi vya televisheni na redio, lakini vyombo vinavyomilikiwa na SMZ waliruhusiwa ingawa nao waliungana na wenzao katika kugomea kufanya kazi wakati wa ziara ya Rais Karume.

Mkurugenzi wa Maelezo Zanzibar, Hassan Mitawi alisema hakuwa na taarifa zozote kuhusu kuzuiwa kwa waandishi hao, lakini akaahidi angefuatilia suala hilo.

Pia Mkurugenzi wa Shirika la Bandari la Zanzibar, Mustpha Aboud Jumbe alipopigiwa simu alisisitiza kuwa uongozi wa bandari haujatoa ilani yoyote ya kuwazuia waandishi wa habari na wala hawana taarifa juu ya kizuizi hicho.

Hata hivyo, juzi jioni baada ya askari hao kuwazuia waandishi katika ziara ya Rais Karume, alikuja Makamu wa Rais Ali Shein na kutembelea eneo hilo, lakini hali ilibadilika kwani waandishi waliachwa kuendelea na kazi na hata kufanya mahojiano naye.

Dk Shein alipongeza jitihada zilizofanywa na wataalamu wa Shirika la Bandari Zanzibar kwa kushirikiana na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na vikosi mbalimbali vya majeshi.

Dk Shein alisema watu wawe na subira na wawape nafasi wataalamu wafanye kazi yao na baadaye itakapomalizika watapata taarifa.

Habari zilizopatikana jana jioni zilieleza kuwa operesheni hiyo imefungwa baada ya wazamiaji kuingia melini na kukuta hakuna maiti iliyosalia.

Kazi iliyofanyika ni kuondoa baadhi ya mali zilizokuwamo miongoni zikiwemo nondo na mbao.

Kwa sasa inasubiriwa Jumatatu ili kuiondoa meli hiyo katika eneo la bandari ili kuweza kuruhusu shughuli nyingine kuendelea kama kawaida.

[ Read More ]

Mabomu yadhibitiwa, 17 hoi kwa mshtuko


Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), jana lililipua mabomu 11 yaliyokuwa katika kambi yake iliyopo Mbagala Kuu ambapo wakazi 17 wa Mbagala walikumbwa na mshtuko na baadhi yao akiwamo mjamzito wa miezi tisa, walizimia na kupelekwa hospitalini.

Awali mamia ya wakazi wa eneo hilo lililopo wilayani Temeke mkoani Dar es Salaam, waliamua kuyahama maeneo yao pamoja na kuwapo taarifa kuwa watulie majumbani kwa kuwa mabomu hayo yangedhibitiwa na yasingekuwa na madhara.

Mabomu yaliyolipuliwa jana, yaliokotwa katika makazi ya watu baada ya kutokea ajali katika kambi hiyo Apili 29 mwaka huu, iliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 20 na uharibifu wa mali zikiwamo nyumba na samani za wananchi. Askari wa JWTZ jana walilipua mabomu hayo kati ya saa nne na saa tano asubuhi na kusababisha vishindo vikubwa na moshi mzito angani.

Wakati yanalipuliwa, mamia ya wakazi wa Mbagala hawakuwapo kwenye makazi yao, nyumba zilikuwa zimefungwa, baadhi wakiwamo wanawake na watoto waliokuwa njiani kwenda mbali na kambi hiyo wakikimbia athari za mabomu.

Bomu la kwanza lililipuliwa saa nne na dakika nne asubuhi, la 11 lililipuliwa saa tano na dakika 15 asubuhi, na ilipofika saa sita na dakika 11, Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Said Mkumbo alitangaza kuwa kazi ya kuyalipua imekwisha. Mkumbo alisema, kazi hiyo ilifanywa vizuri, na kwamba uongozi wa wilaya ulijiandaa kuwahudumia waathirika na kulinda makazi ya wananchi ili vibaka wasiibe.

“Tulijiandaa kwa maana kwamba tulichukua tahadhari…tulijiandaa kwa sababu tulijua dharura yoyote inaweza kutokea,” alisema Mkumbo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye eneo la kambi ya Chama cha Msalaba Mwekundu ya kuwadumia waathirika wa mabomu hayo.

Wakati yanalipuliwa, sehemu nyingi za biashara jirani na kambi ya JWTZ zilikuwa zimefungwa, kulikuwa na watu wachache katika barabara iliyo jirani na kambi hiyo, na kwa ujumla jana asubuhi Mbagala ilikuwa kwenye hali ya tahadhari.

Kazi hiyo ya kulipua ilipokuwa ikiendelea, waandishi wa habari waliongozwa na Skauti kwenda jirani na eneo lililotumika kuyalipua, wakati wanakaribia, bomu lililipuka, wote wakatimua mbio kunusuru maisha. “Yaani wee, tulikuwa tumefika kabisa, nimechanganyikiwa kabisa, yaani hata sijajua tumesambaratika vipi, naona tu vyuma taap, yaani hata sijui wameondoka vipi (waandishi wengine),” alisema Anne Robi wa gazeti la Daily News.

“Yaani mimi naona watu wanakimbia ikabidi na mimi nikimbie…nilikuwa nakimbia naona viatu vinanichelewesha, nikajiuliza nivue nini,” alisimulia Robi. “Nilihisi kila bomu likilipuka hereni yangu inafunguka kwa nini?” Aliuliza Kusiluka wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), mwenzake kutoka katika shirika hilo, Rachael Mhando alimjibu huku wakionekana kuogopa” eti eeh, let’s go my dear, stori tutapata huko.”

Mkazi wa Mtoni Kijichi, Juma Mdelele alidai kuwa, taarifa ya JWTZ kuhusu ulipuaji ilikuwa tofauti na hali halisi kwa sababu kama wananchi wangeifuata kauli hiyo na kuendelea na shughuli zao athari zingekuwa kubwa. Mdelele alidai kuwa, alikwenda katika Hospitali ya Temeke kumpeleka mmoja wanawake walioathiriwa na milipuko hiyo akakuta wengine 10 na akashauri kuwa JWTZ ingewaamuru wananchi wawe umbali fulani kutoka kambini hapo ili kuepusha madhara.

“Wangetoa tu tangazo jamani tutalipua, kaeni mbali, halafu waongeze tu ulinzi, lakini kuwambia watu waendelee na shughuli zao hapana,” alisema. Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano JWTZ Jumatano wiki hii iliwahakikishia wakazi wa Mbagala kuwa, milipuko ingekuwa salama kwa kuwa ingedhibitiwa lakini iliwataka wananchi wakae mbali na eneo la kulipulia.

Jana alasiri, Msemaji wa JWTZ, Alfred Mbowe alisema, kwa ujumla kazi ya kulipua mabomu ilifanywa vizuri na hakukuwa na madhara kwa askari na wananchi. Meneja Habari wa Red Cross, Stella Marialle alisema, inawezekana baadhi ya wananchi walibaki kwenye makazi yao kulinda mali zao na walizingatia pia taarifa ya JWTZ kuwa yasingekuwa na madhara.

“Majeruhi wameletwa na tumewapeleka Temeke hospitali, tathmini ya haraka hawapungui kumi, lakini taarifa kamili tutaipata Temeke hospitali,”alisema Marialle wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kambi ya kuhudumia waathirika wa mabomu. “Nafikiri mabomu ni mabomu, ikitokea wakati mwingine wananchi waondolewe hata kama ni kwa nguvu,” alishauri.

Akizungumza kwa niaba ya Mwakilishi wa Kamishna wa Skauti Wilaya ya Temeke, Rehema Marango, aliyewasimamia Skauti jana, Alphonce Mabula alisema, baadhi ya waathirika walikutwa katika makazi yao, na kwamba, wakazi wengi wa Mbagala waliondoka jana asubuhi kwenda mbalii na eneo la kambi ya Jeshi.

Wakati mabomu yakilipuliwa, magari ya Polisi yenye namba za usajili, PT 1524 na PT 1161 aina ya Land Rover 110 yalikuwa yakifanya doria, wafanyakazi 25 wa Chama cha Msalaba Mwekundu na Skauti 15 walikuwa wakiwahudumia waathirika wakiwamo waliopoteza fahamu.

Magari matatu ya Red Cross yenye namba za usajili, T 563 AMA, T 127 ARS na T590 AFM yalikwenda maeneo mbalimbali kuwachukua waathirika na kuwapeleka katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke. Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk. Asha Mahita alisema, waathirika 17 wa mabomu hayo walifikishwa katika hospitali hiyo akiwamo mjamzito huyo, Mboni Chano (23) anayeishi Njia Panda ya Kijichi, wanawake wengine 14 na wanaume wawili.

Kabla ya kufikishwa hospitalini hapo, 'Habari Leo Jumapili' ilimwona mjamzito huyo akiwa hajitambui jirani na ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Mbagala Kuu. Gazeti hili lilikuta waathirika hao wakiwamo wanawake 14, wakiwa katika hospitali hiyo, wengi wao walikuwa wamepata fahamu, Dk. Mahita alisema walikuwa wakiendelea vizuri.


[ Read More ]

Mgombea wa urais auawa Guinea Bissau


Taarifa kutoka kwa wizara ya mambo ya ndani inasema Bwana Dabo na wenzake watatu walikuwa wakipanga kuipindua Serikali na kuwa walikuwa wamekataa kutiwa nguvuni wakati walipouawa.

Hata hivyo mlinzi wa mwanasiasa huyo amesema Bwana Dabo alikuwa amelala na mke wake nyumbani kwake wakati watu waliokuwa na sare za kijeshi walipomfumania na kumuua.

Waziri wa zamani wa Ulinzi Helder Procea na walinzi wake wawili pia waliuawa kwenye operesheni hiyo.

Wizara ya Mambo ya Ndani imemtaja Bwana Proenca kama kiongozi wa njama ya kuipindua serikali.

Bwana Dabo alikuwa waziri wa Serikali na mwandani wa karibu wa Rais Joao Bernado Viera ambaye aliuawa na wanajeshi mwezi Machi.

Mauaji hayo yametekelezwa wiki tatu kabla ya uchaguzi wa urais kufanywa, hali inayozua wasi wasi kuwa huenda jeshi likaendelea kuingilia siasa nchini hiyo.

Guinea Bissau imetajwa kama moja ya maeneo muhimu ya ulanguzi wa mihadarati na hasa, Cocaine. Wadadisi wanahofia kuwa taifa hilo sasa liko katika hatari ya kudhibitiwa na mababe wa biashara hiyo haramu
[ Read More ]

Watoto wanne Dar watiwa mbaroni

Jeshi la Polisi Jijini limewatia nguvuni watoto wanne wakituhumiwa kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.

Kukamatwa kwa watoto hao ni muendelezo wa msako unaendelea kwa ajili ya kukabiliana na watu wanaofanya vitendo vya kihalifu katika maeneo mbalimbali ya Jiji.

Akiongea na gazeti hili, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile amesema watoto hao ni mingoni mwa watu 12 waliokamatwa katika msako uliofanywa kwenye maeneo tofauti ndani ya wilaya ya Ilala.

Amesema katika tukio la kwanza, mtoto Omar Ramadhani, 16, alikamatwa akiwa na wenzake saba wakiwa na bangi kete 24, misokoto 400 pamoja na pombe ya gongo lita 11.

Amesema watu hao walikamatwa jana majira ya saa 3:00 asubuhi baada ya raia wema kutoa taarifa zao.

Amewataja watuhumiwa wengine kuwa ni Khamis Maulidi, 20, Issah Athumani, 21, Joseph Nakati, 23 na wenzao wanne.

Kamanda Shilogile amesema katika tukio la pili, watu wanne walikamatwa huko eneo la Gerezani wakiwemo watoto watatu wakiwa na bangi puli moja na misokoto 211.

Amesema watu hao walikuwa katika harakati ya kutafuta wateja.
Amewataja watu hao kuwa ni Yahaya Ali, 16, Pascal Haruna, 26, Aidina Mgaika, 15 na Abdul Khalfani, 14, wote wakazi wa eneo hilo.

Kamanda Shilogile amesema jeshi hilo linaangalia namna nzuri ya kuwafungulia kesi watoto hao huku watuhumiwa wengine wakitarajia kufikishwa mahakamani wakati wowote.

[ Read More ]

Vatican fires bishop of Same

The Vatican has removed from office Bishop Jakob Koda of Same Catholic Diocese in Kilimanjaro region for alleged violation of church moral teachings.The Vatican Apostolic Nuncio to Tanzania Archbishop Joseph Chennoth told the 'Daily News' in Dar es Salaam yesterday that Bishop Koda has now been ‘advised to take time for rest, reflection and personal study.’Following Bishop Koda’s removal, Archbishop Chennoth said that the Holy Father, Pope Benedict XVI has appointed Father Rogath Kimaryo CSSp to be Apostolic Administrator of the Same Catholic diocese until the diocese gets new bishop.

Father Kimaryo, who was until recently the parish priest of Kipawa Parish in Dar Es Salaam will be ‘authorised’ tomorrow during Holy Mass at Same Cathedral Church, to be presided over by Cardinal Polycarp Pengo. Archbishop Chennoth will also attend the liturgy.Without elaborating, Archbishop Chennoth said that the Catholic Church normally grants such occasion to its leaders ‘when necessary.’"We have advised him to leave the Diocese, and Father Kimaryo will lead the See for a short while, until the Holy Father announces (the appointment of) a new bishop," he said.

Pope John Paul II nominated Koda as the new bishop of Same in September 1999, to succeed Bishop Josaphat Louis Lebulu who had been transferred to Arusha Archdiocese the previous year.Father Kimaryo who is a member of the Holy Ghost Fathers’ congregation holds a doctorate in Law, obtained from the Rome-based Pontifical Gregorian University. He has also laboured at the General House of his Order in Rome for six years as Counsellor.

According to the Catholic teachings, an Apostolic Administrator in the Roman Catholic Church is a prelate appointed by the Pope to serve as the ordinary. He can either be in an area that is not yet a diocese (a stable apostolic administration) or for a diocese that either has no bishop (an apostolic administrator sede vacante) or, in very rare cases, has an incapacitated bishop (apostolic administrator sede plena).

Strictly in Canon Law, An Apostolic Administrator is equivalent to a diocesan bishop, meaning he has essentially the same authority as a diocesan bishop, serving in their role until a newly chosen diocesan bishop takes possession of the diocese. However, he is restricted by the Canon Law in what he can do to the diocese he temporarily administers. For example, an administrator may not sell real estate owned by the diocese.
[ Read More ]

ATAPELI MILIONI 5/- AKIDAI ANAWEZA KUMFUFUA MTOTO

MGANGA wa Kienyeji, Jongo Salum, maarufu kwa jina la Dk. Manyaunyau, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam kwa tuhuma za kujipatia sh milioni 5 kwa njia ya udanganyifu, kwamba angeweza kumfufua mtoto aliyefariki dunia.

Mwendesha Mashitaka Mkuu wa mahakama hiyo, Naima Mwingi, alidai kuwa Dk. Manyaunyau (29), alijipatia kiasi hicho cha pesa kutoka kwa Zufa Abubakari, ili amfufue mtoto wake aliyedai amefariki dunia katika mazingira ya kishirikina.

Naima, alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Samwel Maweda, kwamba Dk. Manyaunyau, mkazi wa Tabata Mawenzi, alitenda kosa hilo kati ya Agosti 2, 2007 na Machi 3 mwaka jana, maeneo ya Tabata Mawenzi katika Wilaya ya Ilala.

Hata hivyo, mtuhumiwa alikana kosa hilo na kuachiwa huru kwa dhamana hadi Julai 21, kesi yake itakapotajwa tena, na upepelezi bado haujakamilika.

Wakati huohuo, mfanyabiashara Henry Hadson Mwasongwe (42) mkazi wa Tabata, amepandishwa katika mahakama hiyo kwa tuhuma za kujipatia milioni 14/- kwa njia ya udanganyifu.

Mwendesha Mashtaka, Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga, alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi, Joyce Minde kwamba, mtuhumiwa alitenda kosa hilo kati ya Desemba 11 na Machi 3, mwaka huu katika eneo la Ukonga, jijini Dar es Salaam.

Mtuhumiwa alikana kosa hilo na kurudishwa rumande baada ya kukosa dhamana hadi Juni 15 kesi hiyo itakapotajwa tena.

[ Read More ]

MABOMU ZAIDI LEO,MBAGALA WALILIA CHAKULA.



Wakati mchakato wa kukamilisha ripoti ya fidia kwa wananchi walioathirika kwa milipuko ya mabomu katika eneo la Mbagala, Dar es Salaam ikiendelea kufanyiwa kazi, baadhi ya wakazi hao jana ‘walivamia’ ofisi za kata wakidai kutopatiwa msaada wa chakula kama inavyostahili. Wakazi hao walikusanyika kwa wingi katika ofisi hizo, kuanzia majira ya saa 2:00 asubuhi huku miongoni mwao wakiwa wanawake waliokuwa wamebeba watoto. Aidha, wakati wamekusanyika, wengine walisikika wakisema sio wote wenye matatizo ingawaje hawawezi kufikia kiwango kikubwa kama ambavyo walikusanyika katika eneo hilo. Akizungumzia hali hiyo, Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu, Anderson Chale aliwasihi wananchi hao kurudi katika makazi yao na kwamba kazi ya ugawaji chakula ingewafikia huko baada ya kuwasiliana na viongozi wao wa mitaa kwa kuwa baada ya kuzungumza na viongozi wenzake, wamebaini kuwa sio wote wenye madai hayo. Hata hivyo, tamko hilo la Diwani lilipingwa na wananchi hao waliopiga kelele za kukataa, wakidai kutokuwa na imani na viongozi hao badala yake kutakiwa kuchagua viongozi watakaowaamini miongoni mwao, jambo ambalo walilifurahia kwa pamoja na kukubaliana nalo. Diwani aliwatahadharisha kutoingiza majina ya ndugu zao katika suala hilo ili kwamba waonekane kuwa wako wananchi wengi wenye matatizo ya aina hiyo, na kwamba wazingatie taratibu za kupatiwa chakula kwa kuwa tayari zilishaelezwa tangu awali. Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Temeke, Said Mkumbo, alisema watakachofanya ni pamoja na kuangalia orodha ya majina waliyonayo ya wakazi wa kata hiyo na kazi ya kuwagawia chakula itafuata utaratibu huo maalumu. Alisema watendaji husika wanaendelea kufuatilia suala hilo kwa maana kuwa si kila mmoja akifika hapo adai chakula apewe bila kuzingatia taratibu zinazotakiwa. Naye mkazi wa Mwanamtoti, Abdallah Hafidh, alisema ni kweli wapo wenye matatizo ambao hawajapata kabisa chakula na wengine kidogo, lakini kwa waliokusanyika jana siyo wote wenye shida. Mkazi wa Mbagala Kuu, Neema Makofa, alisema tangu kazi ya ugawaji chakula ianze katika kata hiyo kwani hajapata chakula hivyo, alitoa mwito kwa uongozi huo kupatiwa huduma hiyo. Kuhusu ulipuaji wa mabomu leo, Mkuu wa Wilaya alisema ofisi yake ikishirikiana na Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ), wamejiandaa kwa kuweka tahadhari za kutosha huku baadhi ya wakazi wakisema wana taarifa na wengine wataondoka katika makazi hayo ili kupisha usumbufu unaoweza kujitokeza.



[ Read More ]

KESI ZA ALBINO KUANZA J'TATU


Mahakama Kuu ya Tanzania inatarajia kuanza kusikiliza kesi tano za mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi ‘albino’ katika miji ya Wilaya za Kahama na Shinyanga mkoani Shinyanga kuanzia Jumatatu. Kwa mujibu wa Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu, John Utamwa, kesi tatu zitasikilizwa mjini Kahama na Jaji Gabriel Rwakibarila kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza na zimepangwa kusikilizwa kwa muda wa siku 35.

Utamwa alisema Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Kanda ya Dodoma, Gadi Mjemas anatarajiwa kusikiliza kesi nyingine mbili katika Mahakama Kuu mjini Shinyanga zilizopangwa kusikilizwa kwa muda wa siku 21. “Taratibu zote kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hizo zimekamilika,” alisema Utamwa.

Akizungumza jana Dar es Salaam, Msemaji wa Wizara ya Katiba na Sheria, Omega Ngole alisema tayari Mawakili wa Serikali wameshawasili katika miji ya Kahama na Shinyanga kwa ajili ya kuendesha kesi hizo ambazo upelelezi wake umekamilika. Kuanza kusikilizwa kwa kesi hizo, kunaifanya Tanzania kuungana na nchi za Rwanda na Burundi ambazo zimeanza kusikiliza kesi za aina hiyo hivi karibuni.

Katika siku za hivi karibuni kumekuwapo na malalamiko ya kuchelewa kusikilizwa kwa kesi za mauaji ya albino nchini. Pia Mbunge kutoka Canada ambaye ni albino aliishinikiza nchi yake kuinyima misaada Tanzania kwa kile alichodai tatizo la mauaji hayo kutomalizika nchini. Licha ya malalamiko hayo, tayari serikali ilishafanya kura za maoni nchi nzima kwa watu kuwataja wanaohusika na biashara ya viungo vya albino.
[ Read More ]