Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Barcelona mabingwa wa ulaya 2009, yaichapa Man United 2-0

MABAO ya Samuel Eto'o,dakika ya 10 ya kipindi cha kwanza na Lionel Messi, dakika ya 70 yameipa ubingwa wa tatu wa Ulaya Barcelona na kuivua ubingwa huo Manchester United. Mpira wa kwanza wa Barca, uliomaliza utawala wa dakika 10 za kwanza za mchezo huo lilifungua mlango kwa mabingwa hao wa Hispania kuonyesha dhamira ya ushindi. Eto'o, alibashiriwa mapema na mkongwe Rui Costa wa Ureno kuwa ndiye

[ Read More ]

Kikwete ashutumiwa vikali kwa kuendekeza ziara za nchi za nje

WAKATI Rais Jakaya Kikwete akirejea nchini kutoka Marekani kwa ziara ya siku takriban nane, jarida maarufu la uchambuzi wa kiuchumi, The Economist limehoji safari za mkuu huyo wa nchi, likisema kuwa anatumia muda mwingi katika kutangaza jina la nchi nje badala ya kutatua matatizo ya ndani. Kikwete, ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa

[ Read More ]

Huu ndio mguu bandia

Mtaalamu wa tibamaungo wa Kituo cha Tiba cha Kijeshi cha Walter Reedy jijini Washington, DC, Marekani, Annette Bergenon, akimwonyesha Rais Jakaya Kikwete jinsi mguu bandia unavyofanya kazi, wakati Rais alipotembelea kituo hicho hivi karibuni.Wanaoshuhudia kushoto, ni Dk. Mohamed Janabi wa Chuo Kikuu cha Afya na Tiba Muhimbili (MUCHS) na Waziri wa Kazi, Vijana,Wanawake na Watoto wa Zanzibar, Asha Juma,

[ Read More ]

JK kuongoza mkutano wa kujadili kilimo

Rais Jakaya Kikwete wiki ijayo ataongoza mkutano wa kujadili kilimo kuwa nguzo kuu ya uchumi wa Tanzania. Mkutano huo wa siku mbili ulioandaliwa na Baraza la Biashara la Taifa (TNBC), pia utahudhuriwa na Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, mawaziri, wakuu wa mikoa, wajumbe wa baraza hilo, wawekezaji wa ndani, wadau wa maendeleo, wasambazaji wa mazao na wasindikaji. Akizungumza

[ Read More ]

Wabunge waondolewa ulaji

Wabunge wameanza kunyang’anywa sehemu ya ulaji kutokana na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kutoa waraka unaowaelekeza wabunge wote ambao ni wajumbe kwenye bodi za mashirika na taasisi za fedha kuondolewa mara moja. Hatua hiyo inatokana na ushauri uliotolewa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kushauri wabunge wasiwe wajumbe wa mashirika yoyote ya umma, ili kuondoa mgongano wa maslahi.

[ Read More ]