Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Wanafunzi 70 Mbagala kutibiwa Muhimbili kutokana na mabomu

KARIBU wanafunzi 70 kati ya 1,000 waliobainika kuwa na matatizo mbalimbali yaliyotokana na milipuko ya mabomu iliyotokea Aprili 29 kwenye kambi ya Jeshi la Wananchi (JWTZ), Mbagala Kuu, watatibiwa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Mwananchi imeelezwa.

Habari ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa baada ya kufanyika kwa uchunguzi wa watu walioathirika na milipuko hiyo, karibu wanafunzi 900 walibainika kuwa na matatizo na kutibiwa na timu ya madaktari iliyopelekwa eneo hilo baada ya kuripotiwa kuwa watoto wengi walipata matatizo ya kutoona, kutosikia vizuri na maumivu ya kichwa.

Milipuko hiyo ilisababisha vifo vya watu zaidi ya 26 na kujeruhi watu kadhaa huku ikiharibu nyumba za wakazi wengi wa maeneo yanayozunguka kambi hiyo.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zinasema kuwa idadi kubwa ya wanafunzi waliopewa rufaa hiyo ni wale waliobainika kuwa na matatizo ya kutosikia na kutoona vizuri.

“Wanafunzi sita wamepelekwa Muhimbili kutokana na kugundulika kuwa hawasikii vizuri kutoka na kuathirika na milipuko ya mabomu hayo na madaktari wamesema watoto wengine 20 hawataweza kuona vizuri hadi wapate matibabu zaidi na kupewa miwani,” alisema mwalimu mmoja wa Mbagala Kuu ambaye alikataa kutajwa gazetini.

Katika Shule ya Msingi Maendeleo habari zinasema kuwa wanafunzi 30 wamebainika kuwa na matatizo ya macho huku 14 wakiwa na matatizo ya kutosikia vizuri.

Kwa mujibu wa walimu hao, baadhi ya wanafunzi waliokuwa wakisumbuliwa na tatizo la masikio kuvuma wakati wote, kuwa na nta nzito na macho kuwasha walitibiwa shuleni hapo na kuendelea vizuri.

Baadhi ya walimu wa shule hizo waliliambia gazeti hili jana kwa nyakati tofauti kuwa tangu kutokea milipuko hiyo Aprili 29 mwaka huu, baadhi ya wanafunzi bado hawajafika shule.

Wamesema kuwa miongoni mwa wanafunzi hao ni pamoja na Majaliwa Petro (10) Mwanafunzi wa darasa la nne katika Shule ya Msingi Maendeleo ambaye tangu kutokea milipuko hiyo hajafika shule.

Hata hivyo, dada wa Petro, Siwema Petro (13) anayesoma Maendeleo alisema mdogo wake ameathirika kisaikolojia na kuwa wakati wote anataka kukimbia na mara kadhaa anaongea mwenyewe.

“Wakati milipuko inatokea Majaliwa alikuwa shuleni, lakini tunasikia katika harakati za kujiokoa aliona mtu aliyekatwa shingo na bomu, sisi tunadhani ndicho kilichomuathiri zaidi,” alisema Siwema.

Milipuko hiyo pia imefanya miguu ya mwanafunzi wa darasa la kwanza wa Mbagala Kuu, Quntinea Livingston, 7, kupooza na hivyo kusaidiwa kwa kubebwa.

Margareth Gilbert, 28, mama mzazi wa Livingston alisema mwanaye aliangukiwa na ukuta akiwa katika harakati za kukimbia baada ya kusikia milipuko ya mabomu.

Katika hatua nyingine, meya wa manispaa ya Temeke, Jerome Bwanausi amesema Mbagala sasa iko shwari na anasikitishwa na baadhi ya watu kutoa kauli za uongo na kuwatisha wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya hiyo, Bwanausi alisema taarifa zinazosambaa Mbagala kwamba mabomu yatalipuka wakati wowote ni za uongo.

“Msemaji mkuu wa suala zima la mabomu ni mkuu wa mkoa na mpaka sasa hajatoa taarifa yoyote ya ulipuaji mwingine wa mabomu kwa hiyo eneo hilo ni shwari,” alisema.

Naye mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi jana alilazimika kuiongezea muda kamati inayofanya tathimini ya mali na majengo yaliyoteketezwa kwa mabomu hadi Juni 3 mwaka huu.

Lukuvi aliliambia gazeti hili jana kuwa amelazimika kuiongezea kamati hiyo muda baada ya mwenyekiti wake kuomba muda zaidi kwa ajili ya kukamilisha kazi.

“Nilitegemea kupokea taarifa ya kamati hiyo kesho (leo), lakini mwenyekiti wa kamati Cleophace Rweye alifika ofisini kwangu na kuomba muda zaidi wa kufanya kazi hiyo,” alisema Lukuvi.

“Moja ya mambo aliyodai hajayakamilishwa ni uandaaji wa taarifa na kufikisha taarifa yao kwa mtathimini mkuu wa serikali.”

Alisema ili waathirika hao waondokane na shida ya kuishi kwenye mahema hayo, serikali inahitaji kuwalipa fidia zao mapema, hivyo taarifa ya kamati hiyo ndiyo itakayokuwa mwongozo wa malipo.

Baadhi ya wakazi wa Mbagala Kuu jana waliendelea kuilalamikia kamati hiyo kuwa haikufanya tathimini kwenye nyumba zote zilizokumbwa na maafa hayo.

Wakizungumza na Mwananchi katika ofisi za kata hiyo wakazi hao walisema nyumba zao hazijafanyiwa tathimini tangu zoezi hilo lilipoanza.

Swaum Husein, 32, mkazi wa kitongoji cha Mwanamtoti alisema: “Sijafanyiwa tathimini yoyote katika nyumba yangu mpaka leo hii tunatangaziwa kuwa kazi hiyo imefikia ukomo wake.”

Lusian Matius mkazi wa mwanamtoti alisema: “Unavyotuona hapa tumelazimika kumchukuwa mjumbe wetu aje atueleze kwa nini mpaka leo hii nyumba zetu hazijafanyiwa tathimini.”

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, mjumbe wa shina namba moja, Mohamed Likata, 48, alikiri kuwa wakazi hao hawajafanyiwa tathimini na kwamba lina nyumba 34 zinazohitaji.

[ Read More ]

CWT, HakiElimu wasaka chimbuko la kuvuja mitihani

Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kwa kushirikiana na asasi ya HakiElimu, wamezindua shindano la kufahamu chimbuko la kuvuja kwa mitihani ili kukusanya maoni yatakayosaidia kupata ufumbuzi wa tatizo hilo nchini. Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja wa Idara ya Upatikanaji wa Habari wa HakiElimu, Robert Mihayo alisema lengo la shindano hilo ni kupata mawazo na maoni ya wananchi kujua sababu za kuvuja kwa mitihani nchini na kupata ufumbuzi na kuhimiza wananchi kuboresha elimu.

Alisema taifa linahitaji elimu iliyo bora ambayo siyo tu kufaulu mitihani, bali pamoja na kumjengea uwezo mwanafunzi wa kutumia elimu aliyoipata kutatua changamoto anazokumbana nazo katika maisha ya kila siku ambapo mfumo wa elimu nchini sasa umejikita zaidi katika kufaulu.

“Katika shindano hilo litakalowashirikisha Watanzania wote bila kujali umri wala uwezo wa kitaaluma yaani kuanzia wanafunzi hadi maprofesa, linawataka washiriki kutumia kurasa mbili au michoro kuelezea chanzo cha uvujaji wa mitihani, athari zake na nini kifanyike kutatua tatizo hilo,” alisema. Alisema mwisho wa shindano hilo ni Agosti 15, mwaka huu na washindi wawili wa kwanza watapata Sh 500,000 kila mmoja, washindi 10 wanaofuata watapata Sh 200,000 kila mmoja na washindi hao na wengine 50 watakaofuata watapatiwa redio moja kila mmoja zinazotumia umeme wa jua.

Alisema mawazo ya washiriki yatachambuliwa na kutengeneza kitabu kitakachosambazwa nchini ili maoni hayo yawafikie wananchi wengi na kupelekwa serikalini ili watendaji wayafanyie kazi kupata ufumbuzi wa tatizo hilo. Akizindua shindano hilo, Rais wa CWT, Gratian Mukoba alisema ingawa serikali imechukua hatua mbalimbali zikiwamo za kuwafukuza kazi wakuu wa shule zilizohusika, kuwafutia matokeo ya mitihani wanafunzi waliobainika kuiba, lakini uvujaji na wizi umeendelea kutokea mwaka hadi mwaka.


[ Read More ]

Barcelona mabingwa wa ulaya 2009, yaichapa Man United 2-0


MABAO ya Samuel Eto'o,dakika ya 10 ya kipindi cha kwanza na Lionel Messi, dakika ya 70 yameipa ubingwa wa tatu wa Ulaya Barcelona na kuivua ubingwa huo Manchester United.

Mpira wa kwanza wa Barca, uliomaliza utawala wa dakika 10 za kwanza za mchezo huo lilifungua mlango kwa mabingwa hao wa Hispania kuonyesha dhamira ya ushindi.

Eto'o, alibashiriwa mapema na mkongwe Rui Costa wa Ureno kuwa ndiye angeweza kuipatia timu yake bao la dakika za nyongeza na kuwaduwaza Man United.

Mshambuliaji huyo wa Cameroon aliweza kutimiza ubashiri huo, kwa kuipa Barca bao muhimu ambalo hatimaye lilireejeshea jeuri timu yake na kuanza kutawala sehemu kubwa ya mchezo kipindi cha kwanza.

Mchezo ulianza kwa timu hizo kuonyesha makali, ingawa ilikuwa Man United ambayo ilikuwa na uchu kwa kulishambulia lango la Barca na kupata mikwaju kadhaa ya adhabu ndogo ambayo 'mtaalam' wake, Cristiano Ronaldo alishindwa kuitumia.

Katika mchezo huo, mwamuzi Massimo Busacca, ambaye kabla ya mchezo alikwenda Vatican, makao ya Kanisa Katoliki, kuomba baraka kwa Papa Benedict XVI akimwonyesha kadi ya njano Gerrard Pique kwa kumchezea vibaya Ronaldo.

Nao Ronaldo na Paul Scholes walionyeshwa kadi za njano kwa mchezo mbaya dhidi ya wapinzani wao.

Mabadiliko ya kipindi cha pili ya kocha Alex Ferguson kuwatoa Ji- Sung Park na Anderson na kuwaingiza Carlos Tevez na Scholes hayakusaidia.

Vikosi:

Barcelona - Victor Valdes, Carles Puyol, Gerrard Pique, YayaToure, Sylvinho, Xavi Hernandez , Sergio Busquets, Andres Iniesta, Lionel Messi, Samuel Eto'o, Thierry Henry.

Manchester United: Edwin Van der Sar, John O'Shea, Rio Ferdinand, Nemanja Vidic, Patrice Evra; Anderson, Michael Carrick, Ryan Giggs, Ji- Sung Park, Cristiano Ronaldo, Wayne Rooney.

[ Read More ]

Kikwete ashutumiwa vikali kwa kuendekeza ziara za nchi za nje




WAKATI Rais Jakaya Kikwete akirejea nchini kutoka Marekani kwa ziara ya siku takriban nane, jarida maarufu la uchambuzi wa kiuchumi, The Economist limehoji safari za mkuu huyo wa nchi, likisema kuwa anatumia muda mwingi katika kutangaza jina la nchi nje badala ya kutatua matatizo ya ndani.

Kikwete, ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kabla ya kuingia Ikulu, ameshakwenda Marekani zaidi ya mara sita tangu ashike serikali ya awamu ya nne, ikiwa ni baadhi ya safari zake nje ya nchi alizofanya katika kipindi cha miaka mitatu na nusu hadi sasa.

Safari hizo zimewafanya watu mbalimbali, wakiwemo wanasiasa na wachumi kuhoji sababu za safari hizo, ambazo wakati fulani aliwahi kuzitetea kuwa zina tija katika kuitangaza nchi na kuvutia wawekezaji.

Katika habari ya uchambuzi wa toleo la Mei 7, gazeti la The Economist limeeleza jinsi Tanzania inavyohaha kusaka misaada nje ili kukabiliana na kuyumba kwa uchumi duniani wakati bajeti yake inafadhiliwa kwa asilimia 40.

"Ni kiasi gani kinatosha," inahoji habari hiyo ya uchambuzi yenye kichwa cha habari kisemacho, "Tanzania: Waiting for That Great Leap Forward (Tanzania: Ikisubiri Kupiga Hatua Kubwa Mbele)."

Habari hiyo inasema: "Nchi tayari inapata asilimia 40 ya bajeti yake ya serikali kutokana na misaada, lakini inataka fedha zaidi ili iweze kukabiliana na kuporomoka kwa uchumi. Ni kiasi gani kinatosha?"

Baadaye gazeti hilo linaloheshimika kwa uchambuzi wa mambo ya kiuchumi duniani, linamkariri Rais Kikwete akizungumza katika moja ya hotuba zake kwa kusema: "Tunajaribu kupunguza utegemezi wetu, lakini tunashukuru kwa kila tunachokipata."

Bajeti ya mwaka huu ya serikali ilikuwa Sh7.22 trilioni huku asilimia 33.6 ikiwa ni fedha kutoka kwa wahisani na mwaka ujao wa fedha bajeti ya serikali inatazamiwa kuwa Sh8.14 trilioni, huku kiasi cha fedha kutoka kwa wahisani kikitegemewa kupanda kutoka asilimia 33.6 hadi asilimia 34.3.

Mwaka jana, wahisani hawakutoa karibu dola 2.4 bilioni za Marekani walizoahidi na hali inaweza kuwa mbaya zaidi katika mwaka mpya wa fedha kutokana na nchi wahisani kulazimika kutoa fedha kuokoa taasisi zao za kifedha zilizoathiriwa na mtikisiko wa kifedha duniani ulioyumbisha uchumi wa dunia.

Katika uchambuzi wake, linasema Tanzania, ikiwa na idadi ya watu milioni 44, ina utulivu kulinganisha na nchi jirani ya Kenya, yenye watu milioni 40.

"Inachokosa kiuwezo ndicho kinasaidia kuwa na utulivu na utambulisho wa utaifa. (Nchi) haiwezi kusambaratika wakati wa uchaguzi au wakati wowote ule," linaandika gazeti hilo.

Linasema chama kilichopigania uhuru, CCM, ambacho zamani kilijulikana kama Tanu, bado kinahangaishwa na vyama hohehahe vya upinzani.

"Bwana Kikwete ni mtu wa CCM; kazi aliyoibukia ni ya kiongozi wa vijana aliyehusika na kutangaza siasa kwenye jeshi. Ni wazi kuwa atarejea madarakani kwa ushindi mkubwa katika Uchaguzi Mkuu ujao. Bado anashawishi wawekezaji kwa kutumia kipaji chake kama mtu wa (idara ya) masoko," linaandika The Economist.

"Lakini bado wale walioanzisha maduka nchini kila mara wanakerwa. Wengi wanalalamika kuwa Tanzania ni goigoi au hata kueleza kuwa ni sehemu mbaya kufanya biashara na haina shukrani kwa misaada (inayopata) au uwekezaji.

"Hata wanaoitetea wanakiri kuwa imegubikwa na urasimu na haina wafanyakazi walio na stadi. Karibu kila mtu anasema Kikwete anatumia muda mwingi mno kutangaza nchi nje na si kutatua matatizo ya nyumbani kwa kiasi cha kutosha. Mwaka jana alikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika."

Hata hivyo, gazeti hilo la Marekani linasifu kipaji cha Kikwete katika kushawishi; na imani kubwa aliyonayo kwa maendeleo, likisema kuwa ana imani kuwa misaada itaifanya Tanzania iendelee kuwa juu kiuchumi kwa muda mrefu na hatimaye kupiga hatua kubwa kwenda mbele.

"Maghorofa mapya yanayong'aa, yaliyo hata kwenye miji midogo, sambamba na barabara na miradi mipya ya maji inadhihirisha imani hiyo (ya Kikwete). Hali ya siasa ni imara. Wapinga Muungano kwenye visiwa vya Zanzibar wametulia kwa sasa," linaeleza gazeti hilo.

Gazeti hilo pia linaeleza hali ya uharaka iliyopo sasa kwenye serikali ya Rais Kikwete, likitoa mfano wa waziri anayehusika na nishati kuwa anataka kituo kipya cha umeme katika muda mfupi ili kukabiliana na kuanguka kwa huduma ya nishati hiyo, huku JK akiita viongozi wa mashirika yanayomilikiwa na serikali kama Mamlaka ya Bandari na Kampuni ya Reli akitaka ufanisi.

Bila kufafanua zaidi, pia limeandika kuwa, Rais Kikwete anawashughulikia watu wanaoitwa "Wabenzi", likidai kuwa ni wale wanaoendesha magari ya kifahari kama ya Mercedes Benz.

Lakini linadai kuwa, Tanzania kwa kiasi fulani, imeshindwa kwenda na wakati au haikupata mafanikio.

"Ziara ya rais wa China ya hivi karibuni imeshindwa kutoa uwekezaji mwingi," linaeleza gazeti hilo. "Serikali ya China inadhani Kenya, na si Tanzania, ndio njia ya kupitia kwenda kwenye utajiri wa madini wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

"Reli mbili za Tanzania (reli ya kati na Tazara) ni mikweche. Bandari ya Dar es Salaam ilishindwa kupoka biashara kutoka Bandari ya Mombasa wakati Kenya ikiwa kwenye vurugu mwaka mmoja uliopita.

"Hakuna mtu anayeonekana kujua ni lini bandari hiyo kubwa itafikia malengo yake ya kupunguza mrundikano wa mizigo bandarini ifikapo mwaka 2030."


[ Read More ]

Huu ndio mguu bandia


Mtaalamu wa tibamaungo wa Kituo cha Tiba cha Kijeshi cha Walter Reedy jijini Washington, DC, Marekani, Annette Bergenon, akimwonyesha Rais Jakaya Kikwete jinsi mguu bandia unavyofanya kazi, wakati Rais alipotembelea kituo hicho hivi karibuni.Wanaoshuhudia kushoto, ni Dk. Mohamed Janabi wa Chuo Kikuu cha Afya na Tiba Muhimbili (MUCHS) na Waziri wa Kazi, Vijana,Wanawake na Watoto wa Zanzibar, Asha Juma, ambao walikuwa katika msafara wa Rais Marekani.
[ Read More ]

JK kuongoza mkutano wa kujadili kilimo

Rais Jakaya Kikwete wiki ijayo ataongoza mkutano wa kujadili kilimo kuwa nguzo kuu ya uchumi wa Tanzania. Mkutano huo wa siku mbili ulioandaliwa na Baraza la Biashara la Taifa (TNBC), pia utahudhuriwa na Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, mawaziri, wakuu wa mikoa, wajumbe wa baraza hilo, wawekezaji wa ndani, wadau wa maendeleo, wasambazaji wa mazao na wasindikaji. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dunstan Mrutu alisema mkutano huo utajulikana kwa jina la 'Kilimo Kwanza ' ukiwa na nia ya kufanya tathmini kwa nini sekta ya kilimo imeshindwa kukua na kupunguza umasikini.

Mrutu alisema mkutano huo utafanyika Juni 2 hadi 3 mwaka huu Dar es Salaam chini ya uenyekiti wa Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza hilo. Alisema lengo la ‘Kilimo Kwanza’ ni kuwezesha Mapinduzi ya Kijani kwa kuwa na kilimo cha teknolojia ya kisasa hasa katika kilimo na ufugaji, kutumia mbegu bora na za kisasa, uzalishaji kwa chupa, dawa za kilimo, mbolea na kukuza kilimo cha umwagiliaji. “Mkutano huu utakaowashirikisha wakuu wa nchi na mikoa, utasaidia kuangalia matatizo mbalimbali yanayosababisha kilimo kushindwa kukua na jinsi ya kufanya ili kukuza sekta hiyo,” alisema Mrutu.

Alisema mkutano huo utasaidia kubadilisha kilimo cha Tanzania kuwa cha kisasa na kibiashara kwa kuwashirikisha wakulima wadogo na wakulima wakubwa kuachana na jembe la mkono na kutumia zana za kisasa na kuacha kuuza mazao yasiyosindikwa. Alisema baada ya mkutano huo, uamuzi utakaofikiwa utasimamiwa na wakuu wa mikoa washiriki wa mkutano huo ili kuhakikisha kilimo kinakua na kuinua uchumi na kuacha kutegemea vitu kutoka nje.
[ Read More ]

Wabunge waondolewa ulaji

Wabunge wameanza kunyang’anywa sehemu ya ulaji kutokana na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kutoa waraka unaowaelekeza wabunge wote ambao ni wajumbe kwenye bodi za mashirika na taasisi za fedha kuondolewa mara moja. Hatua hiyo inatokana na ushauri uliotolewa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kushauri wabunge wasiwe wajumbe wa mashirika yoyote ya umma, ili kuondoa mgongano wa maslahi. Kaimu Msajili wa Hazina, Godfrey Sella, alisema jana kuwa utekelezaji wa waraka huo wa BoT unaanza mara moja. Alisema kuna baadhi ya wabunge wenye maslahi katika taasisi za kifedha; hivyo si vizuri viongozi hao kuwa sehemu ya bodi za wakurugenzi.

Tayari BoT imetoa orodha ya wabunge wote ambao ni wajumbe kwenye taasisi za fedha na imepeleka waraka huo kwa Msajili wa Hazina ili aondoe majina ya wabunge hao kwenye bodi hizo. “Lengo hapa ni kutenganisha usimamizi na utekelezaji…tumepata waraka huo wa BoT na kinachofuata ni utekelezaji,” alisema Sella wakati akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC). Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Tandahimba, Juma Njwayo (CCM), aliyehoji sababu ya wabunge wapigwe marufuku kuwa wajumbe wa mashirika ya umma wakati kuna baadhi yao wana uwezo.

Mbunge huyo alisema kama kuna chama cha siasa kimeshinikiza suala hilo ni vyema kikapuuzwa; kwa kile alichodai kuwa kufanya hivyo ni kutowatendea haki wabunge, kwani nao ni sehemu ya jamii. “Kuna wabunge wana uwezo mkubwa wa kuisaidia Serikali kupitia mashirika haya, iweje waondolewe kwenye nafasi zao za ujumbe wa bodi za mashirika ya umma?” alihoji mbunge huyo. Baada ya swali hilo, Mwenyekiti wa PAC, Kabwe Zitto, alifafanua kuwa hakuna chama cha siasa ambacho kimekuwa kinashinikiza suala hilo; ila ni ushauri uliotolewa na ofisi ya CAG.

Ndipo Kaimu Msajili wa Hazina akafafanua, kwamba tayari hatua zimeanza kuchukuliwa na akaeleza kuwa zina nia nzuri ya kuwafanya wabunge wawe wasimamizi wazuri wa mashirika hayo. Wakati huo huo, Msajili huyo wa Hazina alikiri kuwa kampuni za Meremeta na Buhemba hazijawasilisha hesabu zozote katika ofisi yake kwa kile alichodai kuwa wizara ndiyo yenye jukumu la kuomba hesabu hizo. Alisema Meremeta ambayo iko chini ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, haina hesabu zozote lakini pia BoT ambayo inahusika na kampuni hiyo nayo haina hesabu zake.

“Hii inahesabika kama ni kitegauchumi cha serikali, lakini kwa mtazamo wangu, si shirika la kitega uchumi kwani hata CAG ameshindwa kuifanyia ukaguzi, kwa vile haina mali inayoonekana kwa macho,” alisema Sella. Kuhusu majukumu ya ofisi ya Msajili wa Hazina, Kaimu Msajili huyo alilalamika kuwa ofisi yake imejikuta wakati mwingine ikifanya kazi za ndani za mashirika ya umma kutokana na mfumo wa kiutendaji uliopo. Alisema kwa sasa wanajitahidi kuandaa waraka utakaosaidia kufanya mabadiliko ili ofisi ya Msajili wa Hazina ibaki kuwa msimamizi wa mashirika ya umma bila kuingilia utendaji wa mashirika hayo.

“Tunataka sisi tubaki kusimamia na kuona kama uamuzi unaofanywa na mashirika haya unazingatia maslahi ya taifa,” alisema. Hata hivyo alisema kwa sasa wizara nyingi ambazo zinatakiwa zipeleke mapendekezo ya wajumbe wa bodi wa mashirika mbalimbali kabla ya kutangazwa, hazifanyi hivyo. Alisema licha ya sheria kuzitaka kufanya hivyo kwa makusudi, mawaziri wanakaidi. “Ukihoji utaulizwa Msajili ni nani na ukisema ufuate sheria lazima utagongana na wakubwa zako, ndiyo maana tunaamua kukaa kimya.”



[ Read More ]

UN yalaani hatua ya Korea Kaskazini


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya kukutana kwa dharura, hatimaye limeshutumu vikali hatua ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la kinyuklia.

Baraza hilo lilikutana kwa dharura saa chache tu baada ya jaribio hilo kufanywa na limeonya hatua kali zitachukuliwa dhidi ya Korea Kaskazini.

Kauli ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa imetolewa muda mfupi tu baada ya serikali ya Korea Kaskazini kutangaza imefanya jaribio lililofanikiwa la Kombora la nyuklia lililo kubwa zaidi ya lile iliyolipua mnamo mwaka wa 2006.

Mataifa wanachama sasa wanataka hatua kali zichukuliwe dhidi ya Korea Kaskazini ambayo tayari iko chini ya vikwazo vya baraza hilo la usalama la Umoja wa Mataifa. Lakini serikali ya Korea Kaskazini imepuuza kauli hiyo na kusema iko tayari kukabiliana vilivyo na wapinzani wake wote.

Wataalamu wa makombora wa Urusi wanasema kombora lililolipuliwa lina uwezo sawa na yale yaliyoangushwa na Marekani katika miji ya Hiroshima na Nagasaki nchini Japan wakati wa vita vya pili vya dunia.

Hata China ambayo imekuwa ikiunga mkono Korea Kaskazini chinichini sasa imesema itakubaliana na azimio lolote la Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa.

Ili kuelewa wasiwasi huu ambao umekumba jamii ya kimataifa ni muhimu kuelewa uwezo wa zana za Kinyuklia.

Kulingana na shirika moja la utaalamu wa kivita la Marekani, Center for Defense Information, makombora matano au sita ya aina iliyofanyiwa majaribio siku ya Jumatatu, yakilipuliwa mara moja yana uwezo wa kuharibifu duniani kote na kuwaacha manusura wachache sana.

Ikiwa na silaha kama hizi, si ajabu Korea kaskazini sasa imeionya Marekani itakabiliana nayo kivita iwapo serikali ya Rais Obama itajaribu kuishambulia

[ Read More ]

Uchumi wa Afrika kusini umekumbwa na mdororo


Uchumi wa Afrika kusini umekumbwa na mdororo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1992, kufuatia kupungua kwa kasi ya uzalishaji viwandani halikadhalika sekta ya madini.

Uchumi wa nchi yenye Uchumi bora barani Africa imerekodi upungufu wa kiwango cha hadi asili mia 6.4% kati ya mwezi Januari na March, ikilinganishwa na kipindi kama hiki mwaka jana.

Hiki ndio kiwango kikubwa cha upungufu tangu mwaka 1984 kikifuatiwa na mdororo wa asili mia 1.8% kila mwaka katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.

Sekta ya ujenzi hata hivyo imeimarika kutokana na mashindano ya mpira ya Kombe la Dunia yanayopangwa kufanyika huko.

Afrika kusini imenufaika chini ya mpango kabambe wa serikali wa uwekezaji katika mipango ya mashindano ya mpira ya mwaka 2010.

Takwimu zilizofanywa na kampuni huru 'Statistics South Africa, imebaini kupungua kwa uzalishaji viwandani pamoja na uwindaji wanyama pori vimechangia mno mdororo huo.

Makampuni ya kuchimba migodi yameathiriwa na mdororo wa uchumi duniani.

[ Read More ]

Wahasibu watakiwa kuwania CPA

Wahitimu wa Uhasibu na Fedha wa Chuo Kikuu Mzumbe (MU), wameshauriwa kujiendeleza kwa kufanya mitihani ya juu ya Uhasibu (CPA) na baadaye kusajiliwa katika Bodi ya Uhasibu (NBAA) ili watambulike wanataaluma.

Changamoto hiyo ilitolewa na Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF), Kanda ya Mashariki na Kati, Meshack Bandawe, wakati wa hafla maalumu ya wanafunzi wanaotarajia kumaliza masomo yao ya Stashahada na Shahada.

Alisema taaluma ya uhasibu ni moja ya taaluma zinazohitaji kuwa na uaminifu na uadilifu wa kiwango cha juu kutokana na mazingira ya kazi yaliyojaa vishawishi vingi zaidi ukilinganisha na kazi nyinginezo.

Kwa mujibu wa Meneja huyo wa PPF Kanda ya Mashariki na Kati, wapo watu wenye taaluma ya uhasibu ambao wamekuwa wakiharibu sifa ya taaluma hiyo na kusababisha wananchi kupoteza imani.

Hivyo alisema ni wajibu wa wanafunzi wa chuo kikuu hicho kuheshimu sheria za kazi kwa kuwa waadilifu ili kuepukana na sifa mbaya katika utendaji wao kwa siku za usoni pindi watakapopata ajira.

Alisema watakapoingia kwenye ajira iwe ya sekta binafsi ama ya umma, wana wajibu wa kusimamia na kuhakikisha michango ya wanachama wa mifuko ya jamii ukiwamo wa PPF inawasilishwa kwa wakati ili kuepukana usumbufu baada ya watumishi kustaafu kazi ama kuondoka kwa sababu yoyote.
[ Read More ]

Dereva wa teksi ashikiliwa kwa gari kutumika katika ujambazi

Polisi mkoani Singida inamshikilia dereva teksi kwa kosa la gari lake kuhusika na uporaji wa fedha Sh milioni nne mali ya mfanyabiashara wa alizeti, na baadaye kuvamia baa ya Kairo mjini hapa, na kutoweka na mauzo ya siku nzima.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Singida, Celina Kaluba matukio hayo yalitokea Jumanne na Jumatano wiki iliyopita katika eneo la Kibaoni na Mitunduruni katika Manispaa ya Singida.

Alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Said Juma (28) mkazi wa Majengo mjini hapa ambaye ni dereva anayeendesha teksi yenye namba za usajili 749 ABU na ubavuni ikiwa na namba 241. Alisema dereva huyo akiwa na wenzake ambao wanaendelea kutafutwa, wakiwa na silaha mbalimbali walifika nyumbani kwa mfanyabiashara Ruben Mhai (30) na kupora kwa nguvu Sh milioni nne zilizokuwa zimehifadhiwa kwenye mkoba.

Kamanda huyo wa polisi alisema kabla ya kufanikisha unyang'anyi huo, Pendaeli Salumu (40) alijeruhiwa vibaya kwa kukatwa panga sehemu mbalimbali za mwili wake, huku mlinzi wa nyumba Rajabu Salumu (38) akivunjwa mkono wa kushoto.

Alisema baada ya uhalifu huo, wezi hao wakiwa na gari hilo hilo, Jumatano walivamia tena baa ya Kairo iliyopo Mtaa wa Mitunduruni na kupora mauzo ya siku nzima ambayo hata hivyo kiasi chake hakijafahamika hadi sasa.

Alisema watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote upelelezi utakapokamilika. Katika tukio la tatu, Kaluba alisema wanamsaka dereva teksi Richard Ngoi baada ya kutoweka na gari hilo lenye namba za usajili T777 AAE Toyota mali ya Mary Mashuda (60) mkazi wa Mtaa wa Kibaoni.

Dereva huyo anadaiwa kutoweka na gari hilo Jumanne iliyopita wakati tajiri yake akiwa ndani ya Benki ya NMB kupatiwa huduma za kifedha, na alipotoka hakumwona tena mfanyakazi wake.

Kutokana na tukio hilo, Kaluba alisema wanamshikilia fundi magari wa gereji maarufu mjini hapa 'Vijana Garage,' Peter Mlay (25) kwa madai ya kushiriki wizi huo wa gari, na upelelezi unaendelea.
[ Read More ]

SMZ yashutumu wahasibu wa kigeni kwa ukwepaji kodi

Wizara ya Fedha na Uchumi Zanzibar imewatuhumu wahasibu wa kigeni wanaofanya kazi nchini kwa kushirikiana na wawekezaji kukwepa kulipa kodi na hivyo kuikosesha serikali mapato.

Akizungumza katika ufunguzi wa semina kwa jumuiya ya wahasibu na wakaguzi wa hesabu iliyofanyika jana mjini hapa, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi, Abdi Khamisi Faki alisema zipo dalili zinazoashiria kuwa wahasibu hao hushirikiana na waajiri wao kufanya udanganyifu katika suala la kulipa kodi katika sekta mbalimbali ikiwamo hoteli za kitalii.

Alisema kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ukwepaji wa kodi kwa baadhi ya wawekezaji wakishirikiana na wahasibu wa kigeni wanaowaajiri, serikali imekuwa ikikosa mapato, jambo linaloiathiri nchi kiuchumi na kusababisha hasara kubwa kwa taifa.

“Tuna idadi kubwa ya wahasibu kutoka nchi jirani wanaokuja kutafuta ajira na tuna mashaka kuwa wanashirikiana na wawekezaji wanaowaajiri kudanganya kulipa kodi,” alisema Faki huku akisisitiza kuwa serikali inafanya jitihada kukomesha suala hilo.

Alisema serikali inatafakari hatua za kuchukua juu ya suala hilo ikiwamo kuangalia uwezekano wa kuzuia ajira kwa wahasibu wa kigeni katika sekta hizo na badala yake ajira hiyo ifanywe na wazalendo tu.

Alisema kuwapo kwa wafanyakazi wazalendo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua tatizo hilo kwa kuwa itakuwa rahisi kwao kuweka maslahi ya taifa mbele na pia kutaongeza ajira kwa vijana wa Zanzibar na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana.

“Hivi sasa serikali inaangalia uamuzi wa kuchukua juu ya tatizo hili, ikiwemo kuzuia ajira kwa wahasibu wa kigeni kwa kuwa ndio chanzo kikuu cha kukithiri kwa vitendo vya ukwepaji wa kodi nchini,” alisema.

Semina hiyo iliyowashirikisha wahasibu kutoka taasisi mbalimbali iliandaliwa na jumuiya ya wahasibu na wakaguzi Zanzibar kwa lengo la kuwaongezea uwezo wafanyakazi wa taaluma hiyo na kuwakumbusha wajibu wao.
[ Read More ]

Nusu ya wajawazito Singida wanajifungulia majumbani

Zaidi ya asilimia 50 ya wanawake wajawazito mkoani Singida hujifungulia majumbani na kwa wakunga wa jadi, hali inayohatarisha usalama wa maisha yao na watoto wanaozaliwa. Hayo yalibainishwa na daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi Mkoa wa Singida, Dk. Christopher Mgonde kwenye mafunzo ya kuokoa maisha ya mama na mtoto wakati wa kujifungua.

Dk. Mgonde alisema ingawa takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya vifo vya wanawake wakati wa kujifungua mkoani Singida imepungua kutoka 61 mwaka juzi hadi 49 mwaka jana, lakini bado kuna tatizo kubwa la wajawazito wengi kutojifungulia kwenye vituo vya tiba.

Alisema miongoni mwa mambo yanayosababisha hali hiyo ni umbali mrefu kwenda kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali, mila na desturi na matusi kutoka kwa baadhi ya watoa huduma.

Alisema pamoja na mambo mengine ikiwamo elimu duni na matatizo ya kiuchumi, hizo ndizo sababu kuu zinazosababisha wengi wa wanawake kuhudhuria vizuri kliniki wakati wa ujauzito wao na kujifungulia majumbani badala ya vituo vya tiba. Dk. Mgonde alisema katika kukabiliana na tatizo hilo, Idara ya Afya kupitia vitengo vyake mbalimbali inaendelea kutoa elimu kwa akinamama juu ya umuhimu wa kujifungulia kwenye vituo vya tiba.

Alisema lengo la hatua hiyo ni kupunguza kiwango cha vifo vya wajawazito na watoto wakati wa kujifungua ili kulinda kizazi na ustawi wa jamii kwa ujumla. Mafunzo hayo ya wiki mbili kwa watoa huduma za uzazi yameandaliwa na kuratibiwa kwa pamoja na Idara ya Afya Mkoa wa Singida na Taasisi ya Benjamin William Mkapa.
[ Read More ]

Watumishi Mahakama Kisutu waomba ulinzi

Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wameiomba Serikali kuimarishia ulinzi katika eneo la mahakama hiyo na wao binafsi. Maombi hayo yalitolewa jana na watumishi hao, mbele ya Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe, alipotembelea mahakama hiyo. Akizungumza kwa niaba ya watumishi hao, Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Addy Lyamuya, aliiomba serikali kupitia kwa Chikawe, kuwaimarishia ulinzi watumishi wa mahakama hasa ikizingatiwa uzito wa kesi zinazosikilizwa hapo. Lyamuya alisema watumishi hao wanahitaji ulinzi huo wanapokuwa kazini na hata nyumbani, ili kudhibiti jambo lolote la hatari litakalowakumba.

Aliongeza kuwa, Jeshi la Polisi linatakiwa kuboreshwa, ili lifanye kazi ndani na nje ya mahakama huku changamoto kubwa ikiwa ni ya kukosa vitendea kazi vitakavyowasaidia kuimarisha ulinzi. Lyamuya alimwambia Chikawe kuwa mbali na matatizo hayo, mahakama ina mazingira duni ambayo ndiyo yanayotegemewa kusikilizia kesi hizo. Akisoma taarifa ya maendeleo ya mchakato wa utenganishaji wa shughuli za mashtaka na upelelezi katika mahakama hiyo, Msaidizi wa Mkurugenzi wa Mashtaka, Winfrida Kasoro, alisema mchakato umeleta mafanikio mengi ikiwa ni pamoja na uharakishwaji wa kesi mahakamani hapo.

Aliongeza kuwa mbali na mafanikio hayo, mchakato huo umepata changamoto nyingi kama kutopatikana mashahidi kwa wakati na mawakili kuacha kazi kutokana na kipato kidogo. Akijibu hoja zilizowasilishwa katika kikao hicho, Chikawe alisema atawasilisha matatizo hayo katika ngazi husika na pia aliishauri mahakama kuandika barua ya maombi ya kukarabatiwa kwa jengo hilo. Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kuajiri wanasheria wapya, ili kukabiliana na utandawazi ikiwa ni pamoja na kuongeza kipato cha wafanyakazi wa mahakama.
[ Read More ]

Kortini wakitaka kuiba Sh bilioni 6 za Stanbic

Watu wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, wakikabiliwa na mashitaka ya kula njama za kutaka kuiba zaidi ya Sh bilioni 6 mali ya Benki ya Stanbic. Akisoma mashitaka jana mbele ya Hakimu Nyigumalila Mwaseba, Mwendesha Mashitaka, Epifras Njau, alidai kuwa washitakiwa hao walikula njama za udanganyifu ili kutaka kuiba kiasi hicho cha fedha, jambo ambalo ni kinyume na sheria ya nchi.

Watuhumiwa hao walitajwa kuwa ni Kunji Meena (29), mfanyabiashara na mkazi wa Kurasini na Tumsifu Kimaro(33), dereva na mkazi wa Kurasini Shimo la Udongo, Dar es Salaam. Njau alidai kuwa, kati ya Mei 16 na 17 mwaka huu, watuhumiwa hao pamoja na wenzao ambao hawajafikishwa mahakamani, walikula njama za wizi Stanbic tawi la Sukari House. Aidha, alidai kuwa Meena anakabiliwa pia na tuhuma zingine mbili za wizi wa Sh 800,000 mali ya Tumsifu Kimaro ambaye ni mtuhumiwa wa pili katika kesi ya kwanza.

Njau alidai mbele ya Mwaseba kuwa kati ya Mei 16 na 17 mwaka huu, mtuhumiwa akitumia kadi ya ATM namba 0140518196401 alichukua Sh 400,000 siku ya kwanza na kiasi hicho hicho siku ya pili katika tawi hilo. Washitakiwa wote walikana mashitaka yao na wako nje baada ya kutimiza masharti ya dhamana zilizowataka kuwa na wadhamini wawili ambao ni wafanyakazi wa Serikali au taasisi zinazotambulika na ahadi ya Sh 500,000 kila mmoja, kesi hiyo inatarajiwa kutajwa mahakamani hapo Juni 8 mwaka huu.
[ Read More ]

Majambazi waua askari 2 Zanzibar

Askari wawili wa Kikosi cha Valantia kinachomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), wameuawa na majambazi wakati wakilinda kituo cha mafuta cha Mwanakwerekwe mkoa wa Mjini Magharibi kisiwani Unguja. Askari waliouawa ni Taibani Mikidadi Ali (23) na Juma Mcha Ali (25) ambao walijeruhiwa na majambazi hao kwa risasi kichwani na kifuani.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Bakari Khatib Shaaban, alikiri jana kutokea kwa tukio hilo saa mbili usiku juzi, baada ya majambazi kuvamia kituo hicho kwa lengo la kupora fedha. Katika purukushani hizo, majambazi hao walifyatua risasi na kuwaua walinzi wawili wa Valantia waliokuwa wakilinda kituo kinachomilikiwa na kampuni ya Zanzibar Petroleum. Katika tukio hilo, majambazi hao walipora silaha aliyokuwa nayo mmoja wa walinzi hao, ikiwa na risasi 10. Jeshi la Polisi linamshikilia Gideon Simponda kwa uchunguzi baada ya kukiri kumiliki gari namba ZNZ 634 ambalo lilitumika katika tukio la ujambazi.

“Kwa sasa, Jeshi la Polisi linamshikilia Gideon Leonard Simponda kwa uchunguzi zaidi...yeye alijitokeza na kusema anamiliki gari ambalo liliporwa na baadaye kutelekezwa,” alisema Kamanda Shaaban. Aidha, polisi waliipata silaha iliyoporwa na majambazi hao aina ya Rifle yenye risasi 10. Kamanda alisema hata hivyo majambazi hao hawakuondoka na fedha ila walimjeruhi Bilali Omar ambaye alikuwa mpita njia eneo hilo, na amelazwa katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja kwa matibabu. Askari wa vikosi vya SMZ hutumiwa kulinda vituo mbalimbali vya mafuta na taasisi nyingine za watu binafsi zikiwamo benki.
[ Read More ]

CCM YAIBUA USHINDI BUSANDA


Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lolesia Bukwimba, ametangazwa kuwa Mbunge Mteule wa Jimbo la Busanda, baada ya kuwashinda wagombea wa vyama vingine vilivyokuwa vikishiriki uchaguzi huo mdogo wilayani Geita.

Mgombea huyo alitangazwa jana kwa kupata kura 29,242 wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambacho hata hivyo kiliyakataa matokeo, kilishika nafasi ya pili kwa kupata kura 22,799. Chama cha Wananchi (CUF) kilichopata kura 977 na cha United Democratic (UDP) chenye kura 271, ‘viliingia mitini’ baada ya wagombea na mawakala wake kutoshiriki mchakato wote wa kuhesabu na kuhakiki kura katika hatua za mwisho.

Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi, Dani Mollel, alisema idadi ya waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 135,163, na waliopiga kura ni 55,660, kura halali zikiwa 53,309 na zilizoharibika 2,069. Kabla ya kutangaza matokeo hayo, msimamizi huyo wa uchaguzi aliwaita wagombea wawili waliokuwapo ambao ni Bukwimba na Finias Magesa, kujaza fomu maalumu ya matokeo baada ya kupata takwimu sahihi na kuyathibitisha kabla ya kuyatangaza.

Hata hivyo, wakala wa Chadema, Basil Lema, alisimama na kueleza kwamba mgombea hatasaini fomu hizo, hadi hapo watakapopewa nafasi wagombea na mawakala wao kutoa maoni juu ya mchakato mzima wa uchaguzi na wa kuhesabu kura. Msimamizi wa uchaguzi alifafanua, kwamba hatua hiyo ilifanyika tangu asubuhi baada ya wajumbe wa kikao hicho cha kuhesabu kura kukaa kwa muda mrefu wakiwasubiri wagombea na mawakala wa vyama vingine tofauti na CCM, ikiwamo Chadema, bila kuonekana.

Kutokana na kwamba awali msimamizi huyo alishatoa ufafanuzi juu ya kilichofanyika mbele ya wakala mwingine wa Chadema, Benson Kigaila kabla ya Lema kuingia ukumbini hapo saa 7 mchana huku amechelewa, baadhi ya watu waliokuwa ukumbini walilazimika kuingilia kati kwa kusisitiza kwamba uamuzi wa msimamizi ulifuata sheria. Baada ya majibizano yaliyochukua dakika kadhaa yakihusisha baadhi ya wawakilishi wa CCM na mawakala hao wa Chadema, msimamizi aliamua kumtangaza Bukwimba kuwa mbunge mteule na akataka yeyote mwenye malalamiko, afuate utaratibu wa kujaza fomu maalumu, jambo ambalo mgombea huyo wa Chadema alilifanya.

Kulingana na maelezo yaliyokuwa yametolewa awali kabla ya Lema kuwasili ukumbini, Msimamizi alitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa kikao hicho ambacho waandishi waliruhusiwa kuingia na kusikiliza, kwamba mgombea na wakala wa Chadema walifika wamechelewa, hali ambayo iliathiri mchakato wa kutangaza matokeo. Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi, Mollel, alimfafanulia Kigaila kwamba vyama vyote vilitaarifiwa tangu Mei 15 mwaka huu, kwamba Mei 23 na 24 wakutane katika ofisi hizo za halmashauri ya wilaya kwa ajili ya kuhesabu kura, lakini wahusika (kasoro wa CCM), hawakuonekana na mtandao wa mawasiliano yao haukupatikana.

“Nikapiga kwa wajumbe wa UDP, hawakupatikana. Wiki iliyopita, wajumbe wa Chadema niliwasiliana nao sana kwa mtandao, lakini kipindi hiki (baada ya uchaguzi) wameadimika,” alisema Mollel. Akisisitiza namna alivyovihimiza vyama kushiriki mchakato huo wa kuhesabu kura, msimamizi huyo alisema pia Mei 23 mwaka huu, aliandika barua kwa makatibu wote wa vyama kuwakumbusha waje. Alisema juzi usiku, baadhi walifika akiwamo Mohamed Habib Mnyaa wa CUF ambaye hata hivyo aliondoka saa 7 usiku na kuwaacha wajumbe wengine wakiendelea na mchakato huo hadi saa 12 alfajiri.

Alisema alipompigia Mnyaa, alimwambia endeleeni hali ambayo alisema ilidhihirisha kwamba aliridhishwa na kilichokuwa kikiendelea. Kwa mujibu wa Mollel, baada ya kuona hali hiyo ya wagombea na mawakala kutofika, ilimlazimu kupiga simu kwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Rajabu Kiravu, ili kupata mwongozo wa nini kiendelee; akajibiwa kuwa hakuna sababu ya kuahirisha kama matokeo yote yamekamilika. “Mkurugenzi akashauri niwakumbushe wajumbe kwa barua na dispatch na akasema ikishapokewa, endeleeni na kikao.

Tukaendelea bila wawakilishi,” alisema msimamizi huyo wa uchaguzi. Akifafanua sababu za kikao hicho kuendelea bila mawakala, Mollel alisema walizingatia kwamba matokeo hayo yalitoka katika vituo ambavyo vyama husika vilikuwa na mawakala na akasema kwa kuchukua uamuzi huo, hawakuvunja sheria. Alisisitiza katika kikao hicho kwamba, “huu si uamuzi wa kuzuia wenzetu kushiriki. Uamuzi ulikuwa halali. Uamuzi sikuufanya kugandamiza chama, bali tumefuata taratibu na ndio wenzetu wakatokea (akimaanisha wa Chadema).”

Kwa upande wa Chadema, Lema na Kigaile walikiri kupokea taarifa ya kuwataka washiriki mchakato huo wa kuhakiki kura, lakini wakasema hawakuelezwa muda wa kufika katika ofisi hizo za Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa ajili ya kazi hiyo. Wakati msimamizi wa uchaguzi, Mollel katika taarifa yake ya awali alisema mchakato huo ulianza usiku wa kuamkia juzi hadi jana alfajiri, kwa upande wa mawakala hao wa Chadema, walidai kwamba walifika katika eneo hilo saa 5 asubuhi kwa kuwa hawakuambiwa muda halisi.

Akizungumza na waandishi wa habari juu ya uamuzi wa kukataa matokeo hayo, mgombea wa Chadema alisema uchaguzi haukuwa huru kutokana na mazingira yaliyojitokeza wakati wa kampeni. “Zoezi hili liligubikwa na matatizo yanayokiuka misingi ya utawala bora,” alisema Magesa na kuyataja matokeo hayo kuwa ni ya NEC na CCM na kwamba si ya wananchi wa Busanda. Akikariri idadi ya watu 79,703 ambao hawakupiga kura, Magesa alisema Chadema walilalamika tangu wakati wa kampeni juu ya vitendo vya ununuzi wa shahada, lakini NEC ilipuuza kilio chao.

Magesa ambaye aliomba fomu maalumu ya malalamiko kwa ajili ya kuijaza, alidai kulikuwa na vitendo vya ugawaji chumvi, vitisho kwa wapiga kura na pia akalalamikia hatua ya Serikali kuanza mchakato wa kuweka nguzo za umeme katika barabara iendayo kata ya Kamena wakati wa mchakato wa uchaguzi. Wakati huo huo, nderemo na vifijo zilitawala kabla na baada ya mgombea wa CCM kutangazwa kushinda. Kwa upande wa mgombea wa Chadema, Magesa, alionekana mnyonge ndani ya ukumbi wa kuhesabia kura huku akiwa amesindikizwa na watu watatu, tofauti na ilivyotarajiwa.

Mmoja wa viongozi wake, Tundu Lisu, siku ya kuhitimisha kampeni (Jumamosi iliyopita) aliwahimiza wafuasi wake wasikose katika ofisi hizo za halmashauri kushuhudia mchakato wa matokeo, lakini hali ilikuwa tofauti jana kutokana na mgombea wao kujitokeza akiwa na wafuasi wachache bila viongozi wa juu wa chama hicho waliokuwa wakimnadi wakati wa kampeni. CUF ambayo katika Uchaguzi Mkuu wa 2005 ilikuwa ya pili kwa mgombea wake kupata kura 26,000, safari hii imedorora na kuiachia Chadema kutamba ambayo mwaka 2005 ilipata kura 3,000 katika jimbo hilo.
[ Read More ]

Rais wa Marekani Barack Obama kuibadili sura ya Marekani katika ulimwengu wa Kiarabu.


Rais wa Marekani Barack Obama ana fursa nzuri kuibadili sura ya Marekani katika ulimwengu wa kiarabu, lakini hata hivyo ana muda mfupi wa kufanya hivyo kulingana na maoni kutoka kwa umma yaliyotokana na utafiti uliofanywa katika nchi za Misri, Jordan, Lebanon,Morocco, Saudi Arabia pamoja na miliki ya nchi za kiarabu.

Utafiti huo uliotolewa siku ya jumannne ulionyesha kuwa asilimia arobaini na tano ya waarabu wote elfu nne waliohojiwa katika mataifa matano, wana hisia nzuri juu ya rais Barack Obama kinyume na asilimia ishini na nne walio na hisia tofauti.

Hata hivyo hisia dhidi sera za marekani katika ulimwengu wa kiarabu zilionekana kubadilika kwa karibu mwaka mmoja uliopita, wakati hisia juu ya marekani na dhidi ya rais wa Zamani George Bush zikiwa mbaya zaidi.

Utafiti wa sasa ulionyesha uungwaji mkono kwa rais Barack Obama pamoja na Marekani huku asilimia sabini na nne ya nchi za kiarabu, zikiunga mkono kuundwa kwa taifa la palestina hali kadhalika zikionyesha huruma wao dhidi ya kundi la Hamas kuliko kundi la Fatah.

Watatu kati ya waarabu wanne wanaunga mkono kuundwa kwa mataifa mawili ya Israel na palestina, kama njia ya kumaliza mgogoro uliopo kati ya pande hizo mbili lakini hata hivyo kati ya walio hojiwa waanamini kuwa ni vigumu kufikiwa kwa makubaliano ya amani.

Utafiti huo pia uligundua kuongezeka kwa hisia dhidi ya mipango ya nuklia ya Iran na kupungua kwa umaarufu wa kiongozi wa Hezbollah Hassan Nasrallah hasa nchini Misri na Morocco .

Rais Obama (kushoto) pamoja na rais wa Afghanistan Hamid Karzai. Rais Obama (kushoto) pamoja na rais wa Afghanistan Hamid Karzai.

Utafiti huo uanafanyika wakati kukiwa na shughuli nyingi za kidiplomasia zianazofanywa na utawala wa rais Obama, baada ya kumteua George Mitchel kama mjumbe wa amani katika ya ulimwengu wa kiarabu na Israel. Hadi sasa micthel ameshafanywa ziara tatu katika eneo hilo tangu ateuliwe na ana mipango ya kuweka ofisi yake mjini Jerusalem.

Wiki iliyopita rais Barack Obama alimualika katika ikulu ya Marekani mfalme Abdullah wa Jordan na pia kukutana na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu siku ya Jumatatu. Wiki ijayo rais Obama anatarajiwa kukutana na rais wa mamlaka ya palestina mahmoud Abbas baada ya rais wa Misri Hosni Mubarak kuhairisha ziara yake nchini Marekani.

Juni nne mwaka huu rais Obama anatarajiwa kuhutubia ulimwengu wa kiarabu kutoka mji wa Cairo nchini Misri, katika kile kinachoonekana kama kinyume na sera za mtangulizi wake kuhusu vita dhidi ya ugaidi suala ambalo waislamu wengi waliliona kama vita dhidi ya uislamu.

Hotuba ya rais Obama pia inatarajiwa kuguzia lengo la utawala mpya nchini Marekani la kupatika kwa amani mashariki ya kati kama njia muhimu ya kuimarisha uhusiano katika ya marekani na ulimwengu wa kiarabu.

Utafiti wa hivi majuzi ulionyesha kuwa hata kama bado kuna shaka kuhusu mipango ya Marekani katika eneo la mashariki ya kati, kuchaguliwa kwa Obama na miezi ya kwanza uongozini huenda kukabadili mawazo mengi.

Wengi wa waliohojiwa, asilimia arobaini na sita walisema kuwa, wangependa wanajeshi wa Marekani waondoke nchini Iraq huku asilimia 26 wakitaka kusuluhishwa kwa mzozo uliopo katika ya Wasrael na wapalestina.

[ Read More ]

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu asisitiza kuwa Jerusalem utasalia kuwa mji mkuu wa Israel.


Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameapa hii leo kuwa mji wa Jerusalem utasalia kuwa mji wa Israel milele huku Israel ikiadhimisha miaka arobaini na mbili baada ya kulichukua kwa nguvu eneo la mashariki la mji huo lenye wakaazi wengi wa kiarabu.

Jerusalem ni mji mkuu wa Israel, umekuwa tangu hapo na utasalia hivyo milele, na kamwe hautagawanwa, alisema waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wakati wa sherehe za kuadhimisha kuchukuliwa kwa nguvu eneo lililo mashariki mwa Jerusalem, wakati wa vita vya siku sita vilivyo piganwa mwaka 1967.

Jamii ya kimataifa haiutambui mji wa Jerusam kama mji mkuu wa Israel na suala hili linaonekana kama kizingiti kwa mchakato wa amani kati ya Israel na Palestina inayotaka eneo la mashariki mwa Jerusalem kuwa mj wao mkuu baada ya kuundwa kwa taifa la Palestina.

Maelfu ya watu, wengi wao wakipeperusha bendera walijipanga katika mji wa Jerusalem wakati ambapo karibu wapalestina 200 pamoja na wanaharakati wa mrengo wa kushoto wa Israel walifanya maandamano katika mji wa zamani wa Damascus.

Uhusiano wa wayahudiu na mji wa Jerusalem ni wa tangu wa maelfu ya miaka iliyopita na mjii huu utasalia chini ya taifa letu,“ alisema Netanyahu katika mlima wa Ammunition kulikofanyika mapigano makali kati ya wanajeshi wa Israel na wa Jordan mwezi Juni mwaka 1967.

Maadhimisho hayo yanafanyika kila mwaka kuambatana na kalenda ya kiyahudi.

Rais wa mamlaka ya Palestina Mahmud Abbas. Rais wa mamlaka ya Palestina Mahmud Abbas.

Msemaji wa rais wa mamlaka ya palestina mahamoud Abbas, alisema kuwa eneo la mashariki mwa Mji wa Jerusalem linakaliwa la wapalestina kama vile Waisraeli wanavyoyakalia maeneo ya Palestina tangu Juni nne mwaka 1967.

Nabil Abu Rudeina alisema kuwa matamshi kama hayo yanavuruga mpango wa kuundwa kwa mataifa mawili na kumwomba rais wa Marekani Barack Obama kuingilia kati ili kukomesha sera za Israel, zinazohujumu juhudi za kupatikana kwa amani katika eneo hilo.

Siku ya Alhamisi wabunge wa Israel kutoka upande wa mrengo wa kulia unaotawala, waliwasilisha mswada bungeni ulio na lengo la kuzuia kugawanwa mwa mji wa Jerusalem kwa Wapalestna.

Mswada huo utahitaji mabadilo yoyote yatakayofanyiwa mipaka ya Jerusalem kupata uungwaji mkono wa asilimia 80 miongoni mwa wabunge mia na ishirini kinyume na asilimia sitini na moja iliyopo sasa.

Seriali iliyotanguliwa ilikuwa imeonyesha ishara kuwa Israel, huenda ikasalimisha eneo la masahariki mwa mji wa Jerusalam kwa waarabu.Hata hivyo serikali ya waziri mkuu Benjamin Netanyahu iliyoingia madarakani tarehe 31 mwezi machi mwaka huu, imelipinga suala hilo na hivyo kupata lawama kali za kimataifa kwa kuzuia kuidhinisha kuundwa kwa taifa la Palestina.

[ Read More ]

Maadhimisho ya miaka 60 ya Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani


Rais Horst Köhler wa Ujerumani amesema kwamba Ujerumani imestawi kuwa nchi yenye uwazi na ya kimataifa katika historia yake ya miaka 60.

Rais Köhler amesema hayo mjini Berlin leo katika maadhimisho ya miaka 60 tokea kuundwa kwa shirikisho la Jamhuri ya Ujermani.

Amesema katika miaka 60 iliyopita Ujerumani limekuwa taifa lenye uwazi kwa dunia .Ameeleza kuwa Ujerumani imeshiriki katika juhudi za kuunda jumuiya za Umoja wa Ulaya na pia imeshsiriki katika kuweka malengo ya kisiasa ya jumuiya hizo.

Amesema Ujerumani imekabiliana na uhalifu uliotendwa na mafashisti na imefikia maridhiano na taifa la kiyahudi.

Rais Köhler ameeleza kuwa wajerumani wamejifunza kutokana na historia na ndiyo sababu kwamba wakati wote itapinga maovu ya chuki dhidi ya wayahudi,ubaguzi ,na chuki dhidi ya wageni.

Juu ya katiba ya Ujerumani iliyoweka msingi wa demokrasia nchini, rais Köhler amesema kuwa hati hiyo ni mwenge wa wa uhuru.Ameeleza kuwa katiba hiyo iliwapa wajerumani wa upande wa mashariki, matumaini.

Kuhusu medani ya kimataifa rais Köhler amesema kuwa Ujerumani imeshirikiana na nchi inayofungamana nazo katika kuletekeleza majukumu ya ya kimataifa.

Imesaidia katika kutatua migogoro mbalimbali duniani na kwamba Ujerumani imetoa mchango wake katika kulinda amani na haki za binadamu duniani.




[ Read More ]

Japan fetes Wangari Maathai


Nobel Laureate Wangari Maathai this week became the first Kenyan to receive the highest decoration from the Government of Japan for her campaign to protect the environment.

Prof Maathai, a former assistant minister for the Environment and the head of the Greenbelt Movement, was decorated with “the Grand Cordon of the Order of the Rising Sun” in honour of her significant contribution in raising people’s awareness of environmental protection in Japan, and enhancing the country’s global status.

Cabinet ministers John Michuki (the Environment and Mineral Resources), Moses Wetang’ula (Foreign Affairs) and Noah Wekesa (Forestry and Wildlife) attended the ceremony at the Japan ambassador’s residence on Thursday night.

Prof Mathaai, who won the Nobel Peace Prize in 2004, played an immense role in the promotion of Japans environmental diplomacy through various activities such as the implementation of grassroot programmes using her Greenbelt Movement and made a substantive contribution to the discussion at the 4th Tokyo International Conference on African Development in May 2008.

“She is quite popular among the Japanese,” a statement from the Japanese Embassy in Nairobi said.

[ Read More ]

Food crisis whets EA’s appetite for GM crops

Worsening cereal production worldwide is swaying African countries to genetically modified crops.

Research concluded last December shows that in developing countries — excluding Brazil, China and India — cereal production has fallen by 1.6 per cent. This has worsened the global food prices and posted a deeper shock to world economies.

Many African countries are now switching from organic to GM crop production, which research says increases yields in a shorter period.

A survey by the International Food Policy Research Institute warns that prices of major cereals will increase significantly, possibly triggering a bigger food crisis.

Experts say in 2020, maize, wheat, and rice prices will be 27, 15 and 13 per cent higher, respectively. As a result of the recession, the poor are likely to have less food.

“In sub-Saharan Africa, for example, per capita calorie consumption will be 10 per cent lower in 2020. Globally, 16 million more children will be malnourished in 2020,” the survey says.

In East Africa, the Uganda government approved use of biotechnology in 2008. Laboratory trials on cotton are going on at a national research centre in Soroti to develop pest resistant varieties and increase cotton volumes.

Farmers have embraced the idea and shown willingness to adopt the techniques for commercial production.

A household survey conducted recently shows that 151 producers, 35 in Lira and 116 in Kasese, approved the use of biotechnology.

“The government approached this technology cautiously, despite appreciating that it increases productivity. We are very cautious not to compromise local production,” says Minister for Animal Industry Bright Rwamirama. He was addressing the press last week after the opening of a biotechnology conference in Entebbe.

The conference brought together scientists from all over the world to discuss the implications of GM crops on African farmers.

[ Read More ]

Obama cuts HIV funding, risks 1m lives


The lives of millions of Africans living with HIV/Aids are at risk following President Barack Obama’s underfunding of bilateral HIV/Aids programmes — among them the crucial President’s Emergency Plan for Aids Relief (Pepfar) and the Global Fund to Fight HIV/Aids, Tuberculosis and Malaria.

The Obama administration’s $3.6 trillion budget, released on May 7, created a $3.3 billion hole in US bilateral support for global HIV/Aids funding, and global health activists are now pushing for a Pan African response to fix the funding gap in the US’s fiscal year 2010 budget, already submitted to Congress.

According to Dr Paul Zeitz, the executive director of the Global Aids Alliance, President Obama is sending the wrong message to world governments — that it is acceptable to underfund global health, in particular the Global Fund. The fund is already facing a financial gap and the US move will only make it worse.

On February 26, 2009, President Obama released part of his first budget request to Congress. For fiscal year 2010, he requested $51.7 billion for the 150 Account, which funds US foreign affairs priorities.

The foreign operations section funds most of the foreign assistance programmes of concern to the Global Alliance, including the global HIV/Aids Initiative, which supports US bilateral HIV/Aids programmes and a apportions US contribution to the Global Fund to fight Aids, Tuberculosis and Malaria.

The fiscal year 2010 budget also makes it impossible for the president to meet his stated target of doubling foreign assistance by 2012.

In essence, President Obama’s request has broken four campaign promises he made to the people of Africa, putting his administration’s moral leadership to question, say the global activists. He has broken his commitment to double foreign assistance by 2012.

The proposed fiscal year 2010 funding ignores the president’s campaign promises by including only $5 billion for Pepfar, the successful US bilateral HIV/Aids programme ($1.5 billion shortfall); $900 million for the Global Fund to Fight HIV/Aids, Tuberculosis and Malaria ($1.8 billion shortfall); and $700 million for global basic education ($1.3 billion shortfall).

The Global Aids Alliance estimates that as a consequence, one million people around the world will not receive treatment for HIV/Aids, while 2.9 million women won’t receive services to prevent mother-to-child transmission of HIV.

In addition, 27 million people will not access sexual disease transmission prevention programmes and 1.9 million orphans and other children affected by or vulnerable to /HIV/Aids will not receive care and support services.

“Underfunding these critical programmes will have grave consequences, especially during the current global economic crisis and at a point in time when the world may be in the early stages of a devastating flu pandemic,” said Dr Zeitz.

Although President Obama has promised to double US foreign assistance to $50 billion by 2012, his fiscal year 2010 budget request is well below what is required to keep this promise.

[ Read More ]

NSSF undecided over return to bourse


Indecision and fear have delayed the much awaited return of Uganda’s National Social Security Fund to the local bourse even after the Ministry of Finance, Planning and Economic Development allowed the Fund to resume investment activities in its real estate and equity business.

Market sources who spoke to The EastAfrican revealed that the NSSF board and senior management are apparently undecided on when to resume trading on the Uganda Securities Exchange (USE) citing increased nervousness within the Fund towards major investment transactions in the aftermath of the Temangalo scandal that involved an irregular purchase of 460 acres in Temangalo at a cost of Ush11 billion ($5.6 million).

The land was co-owned by Minister of Security Amama Mbabazi and his business partner, Amos Nzeyi — a scenario that raised eyebrows and led to a parliamentary inquiry that culminated in the suspension of the Fund’s managing director, David Jamwa and his deputy, Prof Mondo Kagonyera.

Though the parliamentary investigation was concluded last year, additional investigations being conducted by the Auditor General’s office and private audit firm KPMG have slowed down the decision making processes leading to a near paralysis in the Fund’s investment operations.

This is reflected in apparent reluctance and nervousness among top management to endorse key transactions, including some that were approved by the former board of directors.

Though the ban was lifted, the impact of the investigations has limited our ability to make investment decisions. The appointment of a new board has also affected us because of challenges faced in persuading its members on various investment matters that were not concluded by the previous board,” said a senior NSSF official who requested anonymity.

NSSF owns about 20 per cent of all the shares listed on the USE and usually accounts for about 50 per cent of trading volumes when active on the market.

Information obtained by The EastAfrican indicates that the Ministry of Finance ban against investment in equity and real estate activities was lifted in February this year following pressure from prominent market players.

Subsequently, NSSF’s investment committee sat in March and approved its return to the local bourse. However, the appointment of a new board of directors last month stalled the process on account of pending statutory approval.

Previous meetings held by the new board have reportedly yielded no results, thereby creating fresh uncertainty about the Fund’s participation on the USE this year.

Investors’ hopes are now pinned on the next board meeting scheduled for June 2009. Similar hesitation led to NSSF’s recent decision to withdraw from a $10 million financing agreement with the Uganda Revenue Authority meant for the construction of the latter’s headquarters.

The Fund’s delayed return to the USE has also led to a backlog of huge sale offers from stockbrokers serving smaller institutional and individual investors. Such offers, estimated in millions of shares, are attributed to desperate investors eager to quit the market on account of the sustained downturn felt since the second half of last year.

[ Read More ]

Iran says foreign troops no help to region's security


TEHRAN (Reuters) - Iranian President Mahmoud Ahmadinejad attacked the presence of foreign forces in the region at a summit with his Afghan and Pakistani counterparts on Sunday aimed at tackling terrorism and other security problems.

In separate comments underscoring the Islamic Republic's deep mistrust of the United States, Supreme Leader Ayatollah Ali Khamenei told Afghanistan's Hamid Karzai and Pakistan's Asif Ali Zardari that America was hated among the region's people.

The three neighbors' first such meeting, which ended with pledges of cooperation but without any specific measures being announced, took place as Pakistan and Afghanistan are battling to stem the spread of Taliban insurgencies in their countries.

Iran and Pakistan border Afghanistan and have a large stake in its stability because of the impact of a flourishing drugs trade and because in decades of violence, millions of refugees have often spilled across borders.

Although it is a long-time foe of Iran, the United States is also pushing for a more regional approach against the growing strength of Taliban-linked militants in Afghanistan, one of the areas where Washington is seeking to engage Tehran.

"If we can save Pakistan and Afghanistan from these problems, from extremism ... then such trilateral meetings are meaningful," Karzai, the Afghan president, told the summit in comments broadcast by Iran's English-language Press TV.

"The problems come from amongst ourselves," he said.

But Ahmadinejad, who often rails against the West, took aim at outside intervention in the region, "by others who are alien to the nations and culture of our nations."

Clearly referring to tens of thousands of U.S. and mostly NATO troops in Afghanistan and Iraq, he said they were pursuing their own interests.

The United States is pouring thousands more troops into Afghanistan this year to try to reverse gains by a resurgent Taliban, particularly in its southern heartland.

"Although the presence of foreign forces in our region was under the pretext of establishing security ... it has not been much of a help to the establishment of permanent security and political and economic growth," Ahmadinejad said.

Khamenei, Iran's highest authority, later told Karzai and Zardari in a meeting that foreign military interference was one of the region's main problems.

"America ... is very much hated among the people of the region," the official IRNA news agency quoted him as saying.

At a U.N. meeting in The Hague in March, Iran offered to help Afghanistan combat the narcotics trade, which helps fund the Taliban, in a gesture that U.S. Secretary of State Hillary Clinton called promising.

Speaking after Sunday's summit in Tehran, Ahmadinejad said the three presidents had signed a declaration of "paramount importance" to increase cooperation, without giving details. Zardari said they "reached broad consensus on giving further shape to our tripartite cooperation," including working toward free trade.
[ Read More ]

11 wafariki katika tamasha Morocco


Watu wasiopungua 11 wamefariki katika mji mkuu wa Morocco, Rabat, baada ya kukanyagana katika tamasha ya kimataifa ya muziki ya Mawazine.

Kulingana na waandishi habari, inadhaniwa kwamba watu wengine 40 walijeruhiwa baada ya uzio wa senyenge kuporomoka.

Tukio hilo lilifanyika usiku wa Jumamosi, wakati zaidi ya watu 70,000 walijaa pomoni katika uwanja wa michezo wa Hay Nahda, kumtizama mwanamuziki wa Morocco, Abdelaziz Stati.

Katika tamasha mwaka huu walioshiriki ni pamoja na Kylie Minogue, Khaled na Alicia Keyes.

Wadadisi wanasema kwamba tamasha hiyo ya wiki moja ya Mawazine ni kati ya mipango ya Morocco ya kuimarisha sifa nzuri za nchi hiyo ili taifa hilo lionekana ulimwenguni kwamba linakwenda sambamba na maendeleo ya kisasa.

Kulingana na maafisa wa polisi, wanawake watano, wanaume wanne, na watoto wawili, ndio waliofariki kati hali hiyo ya mkanyagano.

[ Read More ]

Kashfa ya Richmond kuibuka tena bunge lijalo

PAMOJA na macho na masikio ya Watanzania kuelekezwa bungeni kwa ajili ya bajeti ya serikali mapema mwezi ujao, kashfa ya Richmond iliyotikisa nchi mwaka jana itaibuka tena, safari hii serikali ikieleza ilipofikia katika utekelezaji wa maazimio 23 ya bunge.

Bunge lililotoa maazimio hayo na kuitaka serikali kuyatekeleza, lakini zoezi hilo limekuwa likisuasua na mara kwa mara kuibua maswali, hasa katika eneo la kuwawajibisha vigogo na watumishi wa umma waliotajwa na Kamati ya Dk Harrison Mwakyembe iliyochunguza kashfa hiyo kuwa walihusika kwa namna fulani katika kashfa hiyo.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, alisema jana kuwa katika mkutano wa 16 wa bunge utakaoanza Juni 9, mwaka huu pamoja na taarifa hiyo ya Richmond, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo atatangaza bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2009/2010.

Taarifa hiyo ya Richmond imekuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu, kutokana na umuhimu wake kwa jamii, hasa baada ya kuwahusisha vigogo wa serikali na kusababisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na mawaziri wengine wawili kujiuzulu.

Dk Kashililah alizitaja taarifa nyingine zitakazotolewa na serikali ni juu ya utendaji usioridhisha wa Kampuni ya Kupakua Makontena Bandarini (TICTS) pamoja na kuyumba kwa uendeshaji wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), uuzwaji wa nyumba za serikali pamoja na utoaji wa vitalu vya kuwindia.

Dk Kashililah hakufafanua kwa undani kuhusu kauli hizo za serikali, lakini kumbukumbu za gazeti hili zinaonyesha kuwa suala la Richmond linatokana na maazimio 23 ya Mkutano wa 10 wa Bunge uliofanyika Februari mwaka jana.

Miongoni mwa maazinio hayo, serikali ilitangaza kwenye mkutano wa 14 wa bunge kuwa inaendelea kuyachunguza, likiwamo la uchunguzi wa tuhuma dhidi ya vigogo na watumishi wa umma ambao walitajwa kuhusika kwenye kashfa hiyo.

Vigogo wanaoendelea kuchunguzwa kuwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah.

Serikali pia inatarajia kutoa kauli juu ya uchunguzi maalumu uliofanywa ili kubaini ukweli kama taarifa halisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuhusu Richmond iliharibiwa ili kutoa nyingine inayowasafisha vigogo dhidi ya ufisadi.

Vile vile serikali inatarajiwa kutoa jibu juu ya madai kwamba jalada halisi la kampuni ya Richmond lililokuwa kwa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) nalo liliharibiwa na kuwekwa jingine kwa lengo la kuficha ukweli.

Kumekuwepo na hali ya ukosoaji juu ya serikali kuwaruhusu baadhi ya vigogo wanaotuhumiwa kwenye kashfa hiyo ya Richmond kuendelea na nyadhifa zao wakati kuna uchunguzi dhidi yao.

Hali hiyo pia ilijidhihirisha kwenye mkutano wa 14 wa Bunge, ambapo Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, William Shellukindo akisoma taarifa ya kamati, alisema hali hiyo inatia shaka.

“Kamati ina maoni kwamba uwajibishwaji wa watumishi hao upewe kipaumbele kwa kuwa wao binafsi na nafasi ambazo bado wanazishika huku wakiendelea kuchunguzwa zinatia shaka juu ya utendaji wao wakati huu wa kuchunguzwa,” alisema Shellukindo.

Bunge lilitoa maazimio 23 ya utekelezaji baada ya mjadala wa taarifa ya Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa Novemba 2007 ili kuchunguza mchakato wa zabuni ulioipa ushindi Richmond ili kuzalisha umeme wa dharura nchini mwaka 2006.

Ripoti hiyo ya Kamati Teule ya Bunge juu ya Richmond ilisababisha pamoja na Lowassa kujiuzulu kwa mawaziri Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi waliowahi kuwa mawaziri wa Nishati na Madini kwa nyakati tofauti.

Katika hatua za utekelezaji wa maazimio hayo, Agosti mwaka jana serikali ilivunja mkataba na Richmond ambao ulikuwa umerithiwa na kampuni ya Dowans.

Kuhusu kampuni ya TRL, Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawamba anatarajia kutoa taarifa kuhusu kamati ya majadiliano iliyoundwa ili kurekebisha mkataba wa ukodishwaji baina ya serikali na Shirika la Reli la India (Rites).

Kumekuwepo na hali ya kutoridhishwa juu ya uendeshaji wa kampuni ya TRL ambapo baadhi ya shughuli zimesimamishwa na kumekuwepo na msuguano wa mara kwa mara juu ya maslahi ya wafanyakazi.

Kuhusu kampuni ya Ticts, Dk Kawambwa alikuwa ameliahidi bunge kuwa wizara yake itawasilisha mbele ya Baraza la Mawaziri waraka ambao utaainisha marekebisho ya mkataba wa kampuni hiyo na serikali, ili kupitishwa.

Awali, mkataba baina ya serikali na Ticts ulionekana kuwa na mapungufu kadhaa yakiwepo ya kutoruhusiwa kuwa na mshindani jambo ambalo liliibana serikali kuongeza nguvu baada ya uwezo wa kampuni hiyo kupungua na kusababisha msururu mrefu wa meli zinazosubiri kupakuliwa.

Hali hiyo licha ya kuwakatisha tamaa watumiaji wa bandari ya Dar es Salaam, iliisababishia serikali hasara ya mabilioni ya fedha kwa kuwa kila meli iliyocheleweshwa kupakuliwa ilikuwa inalipwa Sh20 milioni kila siku.

Wakati huo huo, Dk Kashililah alisema kuwa kuanzia kesho kamati mbalimbali za bunge zitaanza kufanya vikao vyake vya kujadili kuhusu mambo mbalimbali ya bajeti.

[ Read More ]

AGNES; Alichemsha kidato cha nne na ‘kutingisha’ Taifa kidato cha sita





Naamini yupo alivyo kwa sababu ya malezi aliyopata kwenye familia yake yaliyomsaidia msichana, Agnes Dominic (20), kufanya vizuri kwenye Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka huu na kuwa mwanafunzi wa tano kitaifa. Licha ya msingi alioupata kutoka katika malezi ya wazazi wake, pia naamini kuwa juhudi binafsi na dhamira aliyoiweka ya kutorudia makosa aliyoyafanya kidato cha nne, vimechangia sehemu kubwa ya mafanikio hayo ya kitaifa.

Niliwasiliana naye kwa ujumbe mfupi wa simu ya mkononi (sms) Alhamisi iliyopita jioni na Ijumaa iliyopita asubuhi, alinipa majibu yake yaliyonipa mwanga wa awali kuhusu Agnes. Katika mawasiliano hayo ya awali kwa njia ya sms, nilitaka anieleze atakayekuja kunipokea kituoni wakati tulipokubaliana nifike kwao Mtoni kwa Dosa, wilayani Temeke, Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano naye ili wasomaji wa Jarida la Nyota la HabariLeo Jumapili wamfahamu na kujifunza kitu kutoka kwake. Alinieleza atakuja yeye na ningemtambua kwa kuwa yeye si mtu wa kujiremba awapo nyumbani.

Alipokuja kunipokea jirani na barabara ya Kilwa, nilikumbuka sms aliyonitumia, ‘hakupiga pamba’ za kupigia picha kama nilivyomtania kwenye ujumbe niliomtumia, alikuwa na nywele za rasta, alivaa sketi ndefu nyeupe, fulana nyeusi na kandambili. Saa mbili za kuzungumza na Agnes, zilinipa jibu ni kwa nini amekuwa mwanafunzi wa tano kati ya wasichana 10 bora waliofaulu mtihani huo na mwanafunzi namba moja kati ya 47 waliofanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Kibosho mkoani Kilimanjaro.

Amekuwa namba moja katika shule hiyo iliyoongoza kitaifa mwaka huu ya mkoani Kilimanjaro ikifuatiwa na Shule ya wasichana ya Marian iliyokuwa ya pili na kufuatiwa na Kibaha zilizopo mkoani Pwani, Mzumbe ya Morogoro ilishika nafasi ya nne na Ilboru ya Arusha katika nafasi ya tano. Anajiheshimu, ni mchangamfu, mstaarabu na katika dhamira yake hiyo ya kufaulu, aliweka mikakati, alisoma kwa malengo na kumtanguliza Mungu. “Sikuiba, sikuibia mtihani, nilimtegemea sana Mungu na nilisoma kwa bidii… sio kwamba kufaulu ni juhudi zangu mimi, kuna watu wengi waliojitolea na walikuwa na dhamira ya kufaulu na walimu waliwategemea,” anasema msichana huyo aliyehitimu katika shule hiyo inayoongozwa na watawa wa Kanisa Katoliki.


“Haikuwa rahisi na wala siwezi kumkufuru Mungu kwamba ilikuwa migumu sana, ilikuwa kama mitihani mingine,” anasema msichana huyo aliyezaliwa Dar es Salaam Machi 30, 1989. Alisoma mchepuo wa Historia, Kiswahili na Fasihi (HKL), alisoma pia dini na kwa mtazamo wake, mitihani ya Kiswahili na Dini (Divinity) ilikuwa migumu zaidi ya Historia na Fasihi. Alitumia vizuri muda aliopewa kujiandaa na Mtihani wa Taifa na tangu walivyokwenda shule Januari 3 mwaka huu, hakuna mwalimu aliyeingia darasani kuwafundisha, walikuwa wakijisomea baada ya kumaliza ‘topics’ za darasani. “Kuna watu wanakesha, it happens (huwa inatokea), analala saa saba usiku, anaamka saa 10 usiku,” anasema na kubainisha kwamba yeye hajawahi ‘kukesha’.

Anasema alikuwa anasoma kuanzia saa moja usiku hadi saa nne na baada ya hapo aliacha kusoma na kuandaa sare kwa ajili ya kesho yake. Baada ya maandalizi ya siku inayofuata, alijikumbusha masomo yake kwa mara nyingine hadi saa sita ambapo alilala hadi asubuhi. “Ni kuijua tu akili yako, kama wewe ukisoma mchana unaelewa vizuri zaidi kuliko usiku, inabidi usome sana mchana na usiku unalala, kama unaelewa sana usiku, pumzika mchana kisha soma usiku. “Usisome kwa sababu fulani anasoma, soma kwa sababu unataka kuelewa, cha msingi ni kuitambua akili yako,” anasema.

Tangu ameanza kusoma darasa la kwanza, hajawahi kuwa namba moja darasani na hakutarajia kufaulu kwa kiwango alichofikia kitaifa. Anasema hakudhamiria kuwa miongoni mwa wanafunzi bora kitaifa kwani lengo lake lilikuwa ni kufaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza kwa pointi zozote. Amepata daraja la kwanza pointi tatu. Ana alama ya ufaulu ya A katika Kiswahili, A katika Fasihi, A katika somo la Dini, na B katika Historia. Ni miongoni mwa wanafunzi 35 waliopata daraja la kwanza Shule ya Kibosho, saba wamepata daraja la pili, na watano wamepata daraja la tatu.

Ana malengo katika maisha yake na anatambua kuwa mchango wa wazazi wake ikiwamo nia na dhamira ya kumwezesha asome kidato cha tano na sita, vimemsaidia kupata sifa si tu kwa ndugu, jamaa, na marafiki bali Tanzania nzima. “Kingine ambacho kimenisaidia sana ni kupitia ‘past papers’ (mitihani iliyopita) na kusoma maswali kwa uangalifu… mimi nilikuwa nimezoea kufanya mitihani, nimefanya ‘a lot of papers’ (mitihani mingi),” anasema. Aliweka dhamira ya kufaulu mtihani wa kidato cha sita kwa kuwa alikuwa na mtazamo kwamba kufeli mtihani huo ni kupoteza mwelekeo wa maisha na fursa ya kuishi maisha mazuri.

“Kuna percentage (asilimia) kubwa sana ya kufaulu kama wewe mwenyewe utaijua akili yako ipo vipi,” anasema msichana huyo aliyewahi kusoma masomo ya ziada mara moja tu kwa wiki mbili. Ni mtoto wa kwanza kwa Dominic Benard na Joyce Dominic. Ana wadogo zake wawili, Happy ambaye anasoma Shule ya Sekondari ya Mtakatifu Joseph Ngarenaro iliyopo Arusha na Justine anayesoma katika Shule ya Sekondari ya Mtakatifu Anthony, Mbagala, Dar es Salaam.

“Sijui kama watakaonifuata wataiga mfano wangu, unajua kila mtu na future (maisha yake ya baadaye) yake,” anasema msichana huyo aliyependa kusoma masomo ya biashara kidato cha kwanza hadi cha nne na hakupenda masomo ya sayansi. Anawashukuru wazazi wake kwa kumpa nafasi ya kusoma kidato cha tano na sita na kumpa moyo. Anasema kwa namna alivyofeli kidato cha nne ingekuwa ni wazazi wengine isingekuwa rahisi kumpa nafasi ya kuendelea kusoma.

Baba mzazi wa Agnes ni mjasiriamali, anauza magazeti, vitabu na majarida katika barabara ya Samora jijini Dar es Salaam, mama Agnes pia anafanya biashara. Kwa kuwa Agnes alidhamiria kufaulu, ilimbidi pia asome vitu vingi kadri alivyoweza ili kujiongezea ufahamu zaidi wa yale waliyokuwa wakifundishwa darasani na anatoa changamoto kwa walimu kuwazoesha wanafunzi kufanya mitihani ili wajiamini. “Ujiamini wewe mwenyewe kwanza, ujiamini kwamba mimi nimesoma na ninaenda kufanya mtihani, uwe na hicho kitu kinasaidia,” anasema msichana huyo.

“Usitegemee vitu vya darasani tu, tafuta ‘other resources’ (vyanzo vingine zaidi ya vya darasani),” anasema msichana huyo aliyedhamiria kusoma sheria kuanzia mwaka huu wa masomo ya elimu ya juu. Kuhusu mtazamo wake kwenye masomo wakati akiwa kidato cha tano na sita, Agnes anasema umemwezesha kujiwekea historia ya maisha yake na kuipa sifa familia iliyosikitishwa na matokeo yake ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne. Alihitimu kidato cha nne mwaka 2006 katika Shule ya Mtakatifu Anthony, Dar es Salaam, akapata daraja la 3 pointi 24.

Anasema baba yake alikasirika lakini mama yake na bibi yake mzaa mama aliyemtaja kwa jina moja la Matilda, walimfariji na kumpa moyo. Kwa mujibu wa msichana huyo, mama yake alimweleza kwamba hata angepata daraja la pili katika matokeo ya kidato cha sita, lingekuwa jambo zuri kwa kuwa matokeo hayo yangemsaidia apate chuo ambacho kingemsaidia awe na maisha mazuri baadaye. Anasema kwa namna alivyosoma kidato cha tano na sita na alivyofanya Mtihani wa Taifa, alifahamu kwamba hata kama angefeli asingekosa daraja la tatu.

Licha ya kuwa na uhakika huo, aliogopa kwenda kuangalia matokeo kwa kuwa alikumbuka namna alivyoumia wakati alipokwenda kuangalia matokeo ya kidato cha nne. “Form four’ (kidato cha nne) nilikwenda kuangalia mwenyewe na nilifeli vibaya sana,” anasema msichana huyo na kubainisha kwamba, miongoni mwa mambo yaliyosababisha afeli ni kutumia muda mrefu kuangalia sinema nyumbani. Anapenda uigizaji wa Michael Scolfild na kwa sasa anafuatilia mfululizo wa sinema za Prison Break.

Anaamini kwamba amefaulu sana masomo aliyoyaona ni magumu kwa kuwa anaamini mtihani ukiwa mgumu, mtahiniwa hulazimika kutumia uwezo wa ziada wa kufikiri ili kujibu maswali, na anahisi huenda ugumu wa mtihani huo ndio ulimsaidia. Anasema mwanafunzi anapaswa kufahamu ni mazingira gani akisoma atafaulu vizuri, mtazamo huo umemsaidia kwa kuwa alitambua kuwa hakufanya vizuri kidato cha nne kwa kuwa hakusoma shule ya bweni. Alisoma St Anthony kuanzia mwaka 2003 baada ya kuhitimu elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Chang’ombe iliyopo Temeke, Dar es Salaam.

Anaamini kwamba asingesoma katika shule ya bweni asingefaulu vizuri kwa sababu kusoma huko kulimsaidia kujitambua vizuri kwa kuwa suala la kwenda shule, kula, kulala, na kupata kila unachotaka havikuwapo. Anasema, alivyokwenda shule ya bweni maisha yalikuwa magumu kwake, hakuwaona wazazi kama alivyokuwa amezoea kuwa nao, na hakuweza pia kuwasiliana nao hata kwa simu. “Hayo maisha ya ‘mshike mshike’ ndiyo yamenisaidia kusoma vizuri zaidi,” anasema na kueleza kuwa yeye alipokuwa shule ya bweni alikumbuka nyumbani lakini alijua kukumbuka nyumbani hakumpi msaada.

“You don’t go anywhere (huendi popote), yaani ukiingia ndiyo mpaka Juni, unajua watu wengine hawaamini… yaani yale ndiyo maisha yako ya miezi sita,” anasema msichana huyo anayependa kutazama kandanda. Agnes ambaye ni shabiki wa timu ya Manchester United ya Uingereza, alianza kuwapenda ‘Mashetani Wekundu’ kwa kuwa baba yake alikuwa akimnunulia zawadi timu hiyo ikishinda, mjasiriamali huyo sasa anaishabikia timu ya soka ya Liverpool ya huko huko Uingereza.

“Nampenda sana Christian Ronaldo, yaani akihama tena dah,” anasema msichana huyo. Kwa upande wa muziki anawazimia TID na Makamua, na nje ya Tanzania anampenda Akon. Anapenda kujifunza taaluma ya sheria, amewasilisha maombi katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). “Napenda kuona kila mtu anapata haki yake, hata mimi mwenyewe sipendi kunyanyaswa,” anasema na kuongeza kwamba, watu wengi wanasema masomo ya sheria ni magumu, anataka kusoma masomo hayo ili aone huo ugumu ni upi.

Anasema, miongoni mwa kazi ambazo hapendi kuzifanya ni kuwa mwalimu kwa kuwa, huwa anajisikia vibaya kuona mtu analia. “Nina moyo wa huruma, kuchapa kiboko mtu na kuona analia sipendi,” anasema. Anafuatilia maisha ya Dk. Asha-Rose Migiro, anapenda kuwa kama yeye na kufikia kiwango cha mafanikio alichofikia Mtanzania huyo ambaye sasa ni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN). Dk. Migiro pia aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kabla ya kuingia UN.

Anasema, akipata nafasi ya kuzungumza na Rais Jakaya Kikwete, atamshauri aimarishe mapambano dhidi ya rushwa ndogo kwa kuwa ni msingi wa kuimaliza rushwa kubwa. “Unajua huwezi ukafanya kitu cha ‘level’ kubwa wakati cha ‘level’ ndogo bado kinaendelea…mimi naamini kama ikiisha ya huku chini ya huko juu itaisha,” anasema. Msichana huyo anatumia muda mrefu kukaa nyumbani kutazama sinema na kusaidia kazi. Anafahamu kupika ugali, maharage, chapati, lakini anapenda kupika nyama. “Yaani nipike nyama nisionje hata vipande viwili jamani,” anasema. Anasema, ataolewa atakapokuwa tayari kuwa na familia na atapenda kupata watoto wawili.
[ Read More ]

Busanda kukata mzizi wa fitina leo

Uchanguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Busanda, wilayani Geita, mkoani Mwanza, unafanyika leo baada ya hekaheka za kampeni za takribani siku 20 huku Tume ya Uchaguzi (NEC) ikiviasa vyama vinavyohusika kuheshimu kanuni na sheria kwa kuepuka vurugu. Mwenyekiti wa Tume, Jaji Lewis Makame, jana alisema kwamba NEC ilipata taarifa juu ya kuwapo mchezo mchafu wakati wa kampeni na alivitaka vyama vya siasa kutowashawishi wafuasi wao kwenda kinyume na taratibu na kusababisha vurugu katika uchaguzi wa leo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Jaji Makame alisema, “tume imekuwa ikifuatilia kwa karibu sana wakati wote wa kampeni za uchaguzi na haikufurahishwa na matukio machache ya kuvuruga mchakato wa uchaguzi jimboni Busanda ambayo yameripotiwa katika vyombo vya habari.” Kwa mujibu wa Jaji Makame, matukio hayo ni pamoja na kutukanana, kukashifiana, mapigano, ununuzi wa shahada na utoaji wa chumvi kwa wapiga kura ambao aliutaja kwamba ni rushwa. Jaji Makame aliwataka wapiga kura kuhakikisha kwamba kila atakayeingia katika kituo cha kupigia kura anapewa karatasi iliyopigwa muhuri wa kituo nyuma yake na isiwe na alama zozote zisizohusika.

Wakati huo huo wiki hii HabariLeo Jumapili ilifuatilia habari zilizochapishwa katika magazeti yaliyo na waandishi katika kampeni hizo za Busanda na kubaini mgawanyiko mkubwa wa vyombo hivyo katika misingi ya vyama. Tathimini ya habari hizo ilionyesha kuwa vyombo hivyo vya habari viliripoti zaidi habari za kampeni za Chadema na CCM huku CUF na UDP ‘vikisuswa’ na kuonekana kama havipo katika kampeni hiyo.

Pia ilibainika kuwa viongozi wa kitaifa wa vyama hivyo vya Chadema na CCM na matukio yaliyohusu vyama hivyo viwili, yalipamba vichwa vya habari vya kurasa za mbele na picha na kuwafunika wagombea ambao ndio watakaopigiwa kura na leo na kutakiwa kuwajibika kwa wananchi. Kwa mujibu wa tathmini hiyo, licha ya habari za CCM na Chadema kuwa habari kubwa zilizotawala wiki hii, wagombea katika habari hizo walizibwa midomo kwa kutajwa majina bila kuwapo habari zao na pale walipopewa nafasi, walipewa aya zisizozidi mbili katika habari ambazo zingine zilifikia ukubwa wa aya zaidi ya 15.

Mmoja wa maofisa wa kitaifa wa CUF, Mbarara Maharagande, alipozungumza na HabariLeo Jumapili kuhusu mwenendo huo wa vyombo vya habari alisema chama hicho kimeliona na baada ya uchaguzi kitatoa tamko. Naye Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo ambaye alikuwa Afrika Kusini, alisema kampeni za chama hicho hazikuonekana kuwa habari kwa kuwa hazikuwa na matusi na vurugu.

“Ni bahati mbaya sana tumerithi vyombo vya habari vya aina hii, tukielezea sera na amani si habari lakini matusi na vurugu kwao ndio habari,” alisema Cheyo. Katika uchaguzi huo ambao idadi ya wapiga kura waliojiandikisha ni 135, 168 na vituo vya kupigia kura ni 380, Msimamizi wa Uchaguzi, Dani Mollel alisema kuwa wamejiandaa vyema kuhakikisha kwamba unakwenda kama ulivyopangwa. Gazeti hili lilishuhudia magari yaliyokuwa yakipakia vifaa mbalimbali kutoka ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita, kwa ajili ya kuvisambaza kwenda katika maeneo ya uchaguzi.

Hata hivyo mwenendo wa kampeni unaonyesha kuwa wakati vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo ni vinne, lakini CCM na Chadema ndivyo ambavyo vimekuwa vikiteka mijadala ya kisiasa na kuonyesha mwelekeo kwamba kimojawapo kitaibuka mshindi. Akizungumza na gazeti hili, mgombea wa CCM, Lolesia Bukwimba (38) alisema ana uhakika wa ushindi na kwamba atahakikisha anaendeleza shughuli mbalimbali za maendeleo kama alivyoahidi kwa kuzingatia ilani ya uchaguzi ya chama hicho ya mwaka 2005. Hata hivyo, alikiri kwamba katika uchaguzi lolote laweza kutokea na akasema yuko tayari kupokea matokeo yoyote.

Alisema ikitokea akashindwa, ataendelea kuwa mwanachama wa kawaida na kujishughulisha na shughuli mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kukijenga chama katika jimbo hilo. Naye mgombea wa CUF, Oscar Ndalahwa (52) alisema yuko tayari kwa matokeo yoyote ikizingatiwa kwamba yeye ni mwanamichezo anayeamini kwamba katika ushindani wowote lazima pawepo mshindi na atakayeshindwa. Kwa mujibu wa Ndalahwa, yeye ni Mwenyekiti wa Timu ya Mpira wa miguu wa Kijiji cha Nyarugusu ambayo imeifikisha timu hiyo katika Ligi Daraja la III ngazi ya mkoa.

Kwa upande wa Chama cha United Democratic (UDP), mgombea wake, Beatrice Lubambe ambaye ni mfanyabiashara, pia alisema yuko tayari kukubaliana na matokeo iwapo hapatakuwapo aina yoyote ya mizengwe katika uchaguzi. Ingawa gazeti hili halikumpata mgombea wa Chadema, Finias Magesa (52) kuzungumza naye moja kwa moja kuhusu msimamo wake, lakini kupitia majukwaa ya mikutano ya hadhara, alisema anajiamini na atakapochaguliwa atahakikisha kwamba anatumia fedha zake kuleta maendeleo ikiwemo kusomesha yatima.

Kuhusu mjadala juu ya nani atashinda katika uchaguzi huo, Chadema kimekuwa kikitajwa kutokana na vigezo vya namna ambavyo chama hicho kimekuwa kikiendesha kampeni zake na kuvuta hadhara hususan ya vijana na wakazi wa maeneo ya mjini. Ujio wa helikopta sambamba na ushawishi wa majukwaani na hata nje ya majukwaa unaofanywa na Chadema chenye vijana wengi, ni miongoni mwa hoja ambazo zinatumiwa kubashiri kwamba mgombea wake, Magesa atashinda.

Ingawa kumekuwapo na madai kwamba Chadema kinashabikiwa zaidi mijini na kwamba mashabiki wake wengi siyo wapiga kura, lakini Ofisa Habari wa chama hicho, David Kafulila aliliambia gazeti hili kwamba kimejiweka sawa hadi ngazi ya kituo “Sisi tunaongoza kwa kufanya kampeni ya kisayansi. CCM wao wanajivunia viongozi wa ngazi ya kijiji. Chadema tuna timu hadi ngazi ya kituo; tunafahamu ni nani atampigia Chadema na ni nani atampigia CCM,” alisema Kafulila na kusema tathmini waliyofanya, inaonyesha watashinda kwa asilimia 78. Kwa upande wa CCM ambacho mgombea wake ni Lolesia Bukwimba, kimekuwa kikitajwa na mashabiki wake kwamba kitashinda kutokana na madai kwamba kina wafuasi wengi vijijini ambao asilimia kubwa ni wapiga kura.

Wachambuzi wengine wanaoiunga mkono CCM, akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, George Mkuchika wanasema hisia kwamba Chadema itashinda inatokana na tathmini ambayo imekuwa ikifanyika kutokana na taarifa za baadhi ya vyombo vya habari. “Vipo vyombo vya habari ambavyo vimedhamiria kuibomoa CCM. Wana CCM wafahamu kwamba vipo vyombo vitasema wana CCM wanaiba kura. Wanabusanda wategemee ushindi mkubwa,” alisema Mkuchika hivi karibuni. Katika kuonyesha namna ambavyo CCM kimeweka msingi katika ngazi ya kijiji jimboni Busanda, Mkuchika alisema walikuwa na timu sita za kampeni zilizohakikisha kwamba zinazungukia vijiji vyote 70 vya jimbo hilo.
[ Read More ]