
Umoja wa Afrika umesema unasitisha ushirikiano na mahakama ya kimataifa inayoshughulikia uhalifu wa kivita, kuhusiana na uamuzi wa mahakama hiyo wa kumshtaki Rais wa Sudan Omar Al- Bashir. Rais Omar Al- Bashir alishtakiwa kwa madai ya ukatili dhidi ya raia katika eneo la Darfur, magharibi mwa Sudan mwezi wa tatu. Lakini wajumbe katika mkutano wa AU