Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

RIPOTI RASMI YA KIFO CHA BWANA “IMRAN MTUI”

Mnamo siku ya jumapili ya tarehe 31/01/2010, majira ya 9:30 alasiri uongozi wa wanafunzi waishio Bangalore India (TASABA) tulipokea taarifa ya kusikitisha kutoka kwa ndugu wa karibu wa marehemu kuwa kaka yetu mpendwa IMRAN MTUI kuwa tena duniani.
Mnamo majira ya saa tatu usiku mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) Mh. Fidelis Msomekela aliwasiliana na ubalozi wa Tanzania New Delhi kuwafahamisha juu ya msiba wa mpendwa kaka yetu marehemu IMRAN MTUI.
Tarehe 1/02/2010 ofisi ya Ubalozi ilituma mwakilishi wake anayesimamia maswala ya wanafunzi India ili kusaidiana na serikali ya wanafunzi waishio Bangalore kujua chanzo zaidi juu ya kifo cha marehemu Imran Mtui.
Tarehe 2/01/2010, Mwakilishi wa ubalozi pamoja a mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi Bangalore (TASABA) walifika katika kituo cha polisi kiitwacho ‘Cantonment Railway Police’ ili kupata ripoti kamili juu ya chanzo cha kifo cha marehu Imran Mtui. Ripoti ya polisi ilieleza kuwa mnamo majira ya saa 3:35 asubuhi mkaguzi wa reli alitoa taarifa kwa msismamizi mkuu wa reli kuwa ameona mwili wa marehemu IMRAN MTUI pembeni ya reli K.M No. 339/700-800 karibu na KRISHNARAJAPURAM LOCO SHED (MAHADEVAPUR, BANGALORE).
Taarifa za awali za polisi zinaeleza kuwa chanzo cha kifo cha marehemu Imran Mtui ni Ajali ya kawaida, uchunguzi zaidi unaendelea ili kujua chanzo kamili cha kifo cha ndugu yetu marehemu IMRAN MTUI.
Taratibu zote za kusafirisha mwili wa marehemu IMRAN MTUI zimekamilika, kesho (3/01/2010) majira ya jioni, mwili wa marehemu IMRAN MTUI utasafirishwa kuelekea nyumbani Tanzania kupitia kampuni la shirika la ndege la Emirates mpaka Dar es Salaam na baadae kusfirishwa kuelekea Killimanjaro kwa mazishi.
Uongozi wa Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) unatoa shukrani za dhati kwa ubalozi wa Tanzania New Delhi kwa ushirikiano na msaada mkubwa walioutoa ili kufanikisha taratibu zote za kisheria na kutoa usafiri wa kumsafirisha ndugu yetu maarehemu IMRAN MTUI mpaka nyumbani kwao Kilimanjaro. Pia uongozi wa Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA), unatoa shukrani za dhati kwa wale wote walioungana na familia ya ndugu yetu mpendwa marehemu IMRAN MTUI kwa hali na mali.
Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA),unaomba wanajumuiya wote kuwa watulivu na kuacha kutoa habari za kizushi juu ya kifo cha marehemu IMRAN MTUI kwa kuwa uchunguzi zaidi bado unaendelea na mpaka sasa hakuna mtuhumiwa yoyote Yule anaye shutumiwa au kushikiliwa na polisi juu ya kifo hicho.
Uongozi wa wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) unatoa pole kwa familia ya marehemu IMRAN MTUI. Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya ndugu yetu mpendwa marehemu IMRAN MTUI. Amin

Fidelis Msomekela
President – TASABA
[ Read More ]

SURA ZA HUZUNI NA MAJONZI - BANGALORE-INDIA.

Baadhi ya wanafunzi waliokusanyika katika msiba huo wakiwa na nyuso za huzuni.


Sura za Huzuni na Majonzi kwa wanafunzi wa India waliopo Bangalore na Wenzao wa Mysore baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Muwakilishi wa Ubalozi Mr. Amon Mwamunenge juu ya maendeleo ya uchunguzi na taratibu za kusafirisha mwili wa Marehemu Imran Mtui kurudi nyumbani kwa ajili ya mapumziko ya amani.
[ Read More ]