Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

BLOG YA JAMII YATUWAKILISHA VYEMA UINGEREZA



                     Mkuu wa blog ya jamii a.k.a Ankal akituwakilisha vyema Uingereza







PRESENTATION BY MUHIDIN ISSA MICHUZI AT DIASPORA 2 CONFERENCE

BACKGROUND

Since Jon Barger put online what is considered to be the first blog (known as weblog by then) in 1995, millions of blogs have been created. Today, it is estimated that over 100 million blogs are created every day. As of December 2007, Technorati was tracking more than 112,000,000 blogs.
Even though it took a bit longer for Tanzanians to embark on the social media networking scene, such as blogging, when it finally did, the results were impressive. Today, there are over 200 active blogs written for Tanzania or by people who, in one way or another, refer themselves as Tanzanians.

It is fair to estimate that at least 10 to 20 blogs or online forums are created every week by Tanzanians with the purpose of sharing information, news and personal thoughts on different issues affecting or occurring in Tanzania or by Tanzanians wherever they could be in the globe.
It is therefore pretty safe to suggest that Social Media, as of today, stands out as one of the major sources of news and information sharing among Tanzanians in the Diaspora and home. It is a significant source of meaningful discussions; a place for citizens to air their opinions, show patriotism for their beloved country, and communicate ideas while positively criticizing one another. The discussions range from political to economical and by large, social issues at hand.
WHAT TANZANIA’S HOME/DIASPORA SOCIAL NETWORKERS SHOULD STRIVE FOR

1. To involve all stake holders of the “New Media” and to discuss how to engage the government, media houses and the community at large in today’s rapidly growing and expanding social media phenomena.

2. To ensure that Social Media is formally recognized as an important tool in sharing and disseminating news and information and also a central tool for educating, entertaining and fostering freedom of expression.

3. To highlight the unique opportunity that Social Media brings on the table in contributing to social, political and economic development and also to come up with specific recommendations to the government on how it can tap in to make the “New Media’ for social change even more meaningful.

4. To forge partnership between Social Media stakeholders and media houses/outlets on information sharing, compensations, recognition and media ethics.

5. Share knowledge and the best practices of Social Media and how the “New Media” could actually be utilized in bringing social, economic and political change.

6. Promote freedom of speech and information through blogging and other social media.

7. Strengthen cooperation between the Government and Social Media Practitioners.

8. And, more importantly, Social Media should act as a bridge to allow us cross the existing information ocean flowing between Home and the Diaspora, the absence of which greatly undermines government and stakeholder’s resolve to ensuring the much cherished rapid economic and social change.

SOCIAL MEDIA RATIONALE

Information is power. As a Social Media Networker, I firmly believe that through information; a lot can be achieved and developed. And in order to acquire the intended or dreamed about success and desired economical, political and social changes, we require local, regional and international approaches.

Therefore, there is a need for developing, as soon as much as possible, a public policy platform that focuses on fostering on how meaningful dialogues which starts in the Social Media sphere can be utilized to achieve the above mentioned goals and how to achieve social empowerment of the people through the provision of equal opportunities of being heard and contributing ideas, thoughts and best practices.

We should endeavor to see that there is a strong collaboration across all media sectors so that there is effective means of disseminating useful information and news to all communities.
WHY SOCIAL NETWORKS

As a social networker, I believe that empowerment of the people through information is an important part not only for fostering democratic principles of the country but also for social, economical and political advancement both at home and abroad.

Therefore, the main intention of should be not only to give Stakeholders the opportunity to learn and appreciate even more the “power of Social Media ” but also to introduce the New Media to even larger communities and specifically to schools and other educational, social, finance and other institutions.

EXPECTED OUTCOMES SHOULD THAT BE IMPLEMENTED

• Strong partnership between the Social Networkers and the Government

• An avenue for regular dialogue between Social Networkers at home and in the Diaspora,

• Understanding the global changes when it comes to social media, as well as citizen journalism

• Discovery and deeper understanding about new media technologies, free and open source software, and many useful Web 2.0 tools

• Provide Tanzania’s Local and Diaspora Social Networkers with an opportunity to learn from each other and expend knowledge on the use of new technologies.

• Be a forum for Tanzanian Internet surfers/users and other stake holders the opportunity to interact and build their network.

• Engage attention from traditional media, civil society, development agencies and private entities to new technologies (Open Source and Web2.0) and Tanzanian Social Newtworks both home and abroad.

• Consulting and facilitation with various stakeholders in organizational change and community outreach

• Create more favorable conditions to allow for the return of Tanzania in the map of writers, thinkers etc

• Establish effective ways and means of channeling and disseminating news and information to the public and create dialogues that result into true social changes.

• Teaching and helping new writers and Social Media Networkers to establishing their own forums that are not necessarily of news in nature but informative. Think of how the potential Tanzanian investor in the Diaspora has to sweat it out to search for relevant information on how to set up a business, or a researcher who needs vital information from home for his or her thesis.
WAY FORWARD

The government should subsidize internet accessibility. Only recently the US government has put in place a policy that is aimed at ensuring rural communities have access to internet free! So, I believe, we have to move to wireless internet (it is cheaper, and fortunately we already have Fibre Optic) as not only users will have access to internet but also even those institutions that can ill afford paid for internet services would start looking for online presence. That is, without making internet affordable it will remain a luxury only to a few.

So far.. almost the same information circulated through Social Networks is not sufficient presented because information that is on Michuzi Blog, Haki Ngowi, Maggid Mjengwa is the same that is on newspapers, radio and TV. We have to widen the sources.. When we start (and its happening slowly) to obtain materials from Moshi, Tukuyu, Musoma, Muheza, Bariadi and Ukerewe and so forth then you know.. We are getting somewhere..But you know what.. It all depends on supply and demand.. For long Social Networks have been supplying certain type of information, entertainment, politics.. udaku.. (those are the 3 things that seem to be of high demand. Now.. as long as the choices remain those 3 it means stakeholders will continue to wallow in there only. So, who is to create the other info? How do they get exposure?

.The Government needs to make the net accessible and affordable to all, and social networkers be creative, innovative and passionate in what they are doing.

And this is the major challenge that the government and stakeholders have to address; including Tanzanians both at home and in the Diaspora. They should unite and come up with sustainable and affordable answers.

WAY FORWARD

1. The Government should coordinate with Home and Diaspora Social Media Networkers in creating a common forum, let’s say Tanzania Home and Diaspora Forum ( like Jamii Forum etc) to be a bridge. The Diaspora Desk at the Ministry should supervise this

2. Form a small team of networkers at Home and Abroad to run the forum. ( I Volunteer to be one such person from home)

3. Ensure a two way traffic flow of information from Home and the Diaspora is established, maintained and sustained

4. Allow all stakeholders in the Diaspora access the forum not only as readers but also by contributing news, informative articles, ideas from all over.

THANK YOU FOR LISTENING

LIBENEKE OYE!
                              source na jiachie blog




[ Read More ]

AJALI....




Mtoto Mwanaidi Ibrahim (4) (kulia), ambaye wazazi wake wote wawili walifariki dunia katika ajali ya gari, Kibamba juzi, akiwa amebebwa na Mama yake mdogo, Sharifa Ally wakati wa maombolezo ya msiba wa wazazi wake hao, Kibamba, Dar es Salaam jana. Kushoto ni ndugu yake Salha Jaffar (3). Mtoto huyo kwa sasa amebaki yatima.

Ajali ya gari iliyochukua nafasi juzi alfajiri eneo la Kibamba, Dar ndani yake kuna zaidi ya tukio, baada ya kuibuka kwa taarifa mpya kwamba kulikuwa na wanandoa watarajiwa ambao roho zao zilizimika papo papo...

ndani ya daladala lililoangukiwa na lori la mafuta, kulikuwa na wanandoa watarajiwa ambao walikuwa safarini kwenda Morogoro kwa ajili ya kukusanya michango ya harusi.

Kwa mujibu wa mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Chaudama Emanuel, wanandoa watarajiwa waliopoteza maisha ni Justin na Helen.

Akifafanua kila kitu, Chaudama alisema kuwa Justin na Helen walipata ajali hiyo walipokuwa wanakwenda kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi yanayokwenda mikoni na nchi jirani, Ubungo ambako walikuwa wapande basi la Hood kwenda Moro.

“Kwanza kulikuwa na ubishi wa wao wenyewe, masikini mdogo wangu (Justin) alitaka wasubiri basi hapa hapa Kibamba, lakini wifi akataka wakapandie Ubungo, kwahiyo Justin akamsikiliza mchumba wake kumbe walikuwa wanafuata wito wa Mungu,” alisema Chaudama.

Aliongeza: “Walikuwa wanakwenda Morogoro kufuata michango ya harusi, walitakiwa kurudi leo leo (juzi) jioni au kesho (jana) asubuhi na ndoa yao ingefungwa Jumamosi (leo) kanisani kwa sababu sisi ni Wakatoliki.”

MKOSI
Wakati hali ikiwa hivyo kwa Justin na Helen ambao pumzi yao ilikatika siku mbili kabla ya kutimiza tukio muhimu katika historia ya binadamu, yaani ndoa, ‘ishu’ nyingine ya kusikitisha ni kuwa, mwanamke aliyekuwa amesotea mtoto kwa muda mrefu, akiwa njiani kwenda kujifungua kwenye hospitali ya Mwananyamala, Dar ni mmoja wa abiria waliopoteza maisha hali inayotafsiriwa na wakazi wa Kibamba kuwa ni mkosi wa mji huo.

Katika ushuhuda wa gazeti hili baada ya ajali hiyo, mtoto mchanga akiwa amepoteza maisha, alitokeza kwenye tumbo la mama huyo, tukio ambalo liliwaliza wengi walioshuhudia.

Shuhuda mmoja aliyezungumza na gazeti hili eneo la tukio na kueleza kwamba anamfahamu mwanamke huyo aliyekuwa mjamzito, alisema kwamba alikuwa na mumewe wakienda hospitali ya Mwananyamala baada ya kushikwa na uchungu.

“Walikuwa wanakwenda hospitali Mwananyamala, sasa Mungu ana yake ndiyo maana wamepata ajali kabla ya kufika hospitali. Inasikitisha sana,” alisema mtoa habari wetu huku akijifuta machozi.

Katika ajali hiyo, Lori la kubeba mafuta lenye namba za usajili T192 ABP, lililiangukia daladala aina Hiace na kuua abiria wote waliokuwemo.


Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba, katika idadi hiyo, waliopoteza maisha ni wanaume wanane na wanawake watatu.

Kutokana na ajali hiyo, waandishi wetu walizunguka mitaa mbalimbali ya eneo la Kibamba ambako ndiko inasemekana watu wengi waliopoteza maisha wanaishi, na kushuhudia nyumba nyingi zikiwa katika hali ya utulivu.

Picha iliyoshuhudiwa na Risasi Jumamosi ni kuwa japo si kila nyumba iliyokutwa na msiba lakini uzito wa tukio hilo, ulivuta hisia za watu wengi ambao waliungana na wafiwa kuomboleza.

chanzo cha habari hii:GLOBAL PUBLISHER.





[ Read More ]

AJALI:LORI LA MAFUTA LAIANGUKIA HIACE.


mwili ukiwa umenasa kwenye gari hilo



Leo majira ya saa kumi na nusu alfajiri, lori lenye namba za usajili T 189 ABP na tela lake lenye namba za usajili T 192 ABP lililokuwa limebeba mafuta kutokea jijini Dar es Salaam kuelekea Kibaha Pwani, limepata ajali mbaya na kuliangukia basi dogo la abiria (Hiace) lenye namba za usajili T 615 AJW katika eneo la Kibamba CCM, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, na kusababisha basi hilo dogo kupondeka vibaya.

Ajali hiyo ya kutisha imesababisha vifo vya watu 7 waliokuwa ndani ya basi dogo, baada ya lori hilo kulilalia basi hilo lililokuwa likitokea Kibamba kwenda Ubungo. Akiongea na mwandishi wetu aliyefika eneo tukio, Kamanda Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani, Mohamed Mpinga , alisema kuwa basi hilo dogo aina ya Hiace lilikuwa na abiria saba ambao wote wamefariki dunia, na kati ya maiti hizo, ni maiti mbili tu ndizo zilizoweza kutolewa hadi muda huu tena zikiwa vipandevipande.

Katika maiti hizo zilizotolewa, moja ni ya mwanamke ambae hakuweza kutambuliwa kwa wakati ule na na mwanaume aliyetambuliwa kwa jina la Shukuru Hussein, maarufu kama Kibwetere, mkazi wa Kibamba. Aidha Kamanda Mpinga aliongeza kuwa bado utaratibu unaendelea kwa kuwa lori lilikuwa limejaza mafuta hivyo imeleta ugumu katika utoaji hadi mzigo wote utakapoisha na kuweza kufanya utaratibu wa utoaji.

Kamanda Mpinga aliweza kumtaja dereva wa lori ambaye amekimbia mara baada ya tukio hilo kutokea kuwa ni Kudura Adam na mmiliki wa Lori hilo ametambuliwa kwa jina la Mahamudu Mohamed.

Hata hivyo baada ya ndugu wa mmiliki wa Hiace kupatikana na kudai mwenyewe yuko Mkoani Kilimanjaro, walisema kuwa mmiliki huyo anaitwa Selemani Khalfan na Hiace yake huwa inalala Ubungo Kibo maeneo ya Rombo na kumtaja Dereva wa Hiace hiyo kwa jina moja kuwa ni Seif na Kondakta wake Faraji Ismail Kalama ambao mpaka sasa bado maiti zao hazijatolewa eneo la ajali.

SOURCE:GLOBAL PUBLISHERS.

[ Read More ]

Milango ya Zanzibar : Mji mkongwe.



gari linaloonekana ndio lilikuwa gari la Prez wa kwanza wa Zanzibar Marehemu A.Karume.


Milango ya Zanzibar ilianza kutumika katika miaka ya 1870 na kupata umaarufu mkubwa hadi sasa.Milango hii ilibuniwa na kuchongwa kufuatana na tamaduni za kihindi na kiarabu.

Katika miaka hiyo ya 18' jumla ya milango 806 ilitengenezwa. Hiki kilikuwa ni kipindi cha Sultan Bargash.
Sifa kubwa ya milango hii ni mapambo yake ambayo yalitokana na dhana ya kujikinga na madhara ya kishetani kuingia ndani ya nyumba. Mapambo mengine yaliyomo kwenye milango hiyo ni maua, matawi ya minazi, aya za Koran, jina la mwenye nyumba na mwaka uliotengenezwa mlango huo.

Zaidi baadhi ya milango hiyo imetiwa vyuma umbo la koni nyenye ncha kali ikiwa ni kama silaha ya kujikinga na uvamizi wa Tembo.


Kuna aina mbili za milango hii, moja ni umbo la mstatiri katika sehemu yake ya juu na ya pili ni umbo la nusu duara katika sehemu yake ya juu. Mlango mmoja uchukua muda wa miezi mitatu kutengenezwa na hutumia mbao ngumu aina ya Mninga. Hadi sasa milango hii hutengenezwa kwa kutumia mkono. Hata hivyo katika karakana ya Ofisi ya Hifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe, baadhi ya maandalizi ya utengenezaji wa milango hiyo hutumia mashine.


Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe, inastahili kupongezwa kwa kuhakikisha kuwa aina hii ya milango inaendelea kutumika katika Mji Mkongwe. Hii ni kutokana na kuwepo na wimbi kubwa la kung'olewa kwa milango hiyo katika miaka ya 80 kwa lengo la kuuzwa. Adhia kuwepo kwa ubadilishaji wa milango hiyo kutokana na kufanyiwa matengenezo ya nyumba.


picha na habari kutoka:kibunango.blogspot.com
[ Read More ]

Maiti ya mtoto yakutwa juu ya kaburi!!!


MAITI ya mtoto mdogo wa kike anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka miwili hadi mitatu, imekutwa juu ya kaburi katika eneo la Buguruni Madenge, Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile alisema maiti huyo ambaye hajatambuliwa, aliokotwa juzi saa 5 asubuhi.
Alisema mwili wa mtoto huyo uliokotwa ukiwa hauna jeraha lolote, ingawa alikuwa anatokwa na povu mdomoni na kwamba mpaka sasa haijajulikana maiti huyo alifikaje juu ya kaburi hilo na kwa madhumuni gani.
Aidha, Kamanda Shilogile alisema sababu na chanzo cha kifo cha mtoto huyo hakijafahamika na maiti amehifadhiwa Hospitali ya Amana kwa uchunguzi zaidi huku Polisi ikiendelea na msako dhidi ya watuhumiwa.
Akizungumza kwa simu jana kufafanua tukio hilo, Kamanda Shilogile alisema hawajamkamata mtu yeyote kuhusiana na tukio hilo ambalo lina utata. “Mtoto alikuwa amefunikwa kwa nguo.
Hakuwa na jeraha lolote. Lakini unaweza kujiuliza maswali mengi kuhusu tukio zima. Je, alitupwa hapo? Alikuwa anaumwa, au ilikuwaje,” alisema Kamanda Shilogile na kuongeza kwamba hata mazingira ya kulihusisha na ushirikina, pia inawezekana.
[ Read More ]

Drunk millionaire 'lost' £130,000 car


A wealthy property tycoon lost his £130,000 Lamborghini Gallardo supercar after a night out because he was too drunk to remember where he had parked it.
Glenn Knowles, 35, was accused of fraud when the car disappeared and has not been found since, even though it was fitted with a satellite tracking device.
Mr Knowles appeared at Guildford Crown Court with the Lamborghini's co-owner, Richard Mant.
Both were cleared of fraud when the jury accepted Mr Knowles' claim that he had been so drunk he could not recollect where he had left the Italian sports car.
When he realised the car was missing, Mr Knowles tried to cover his embarrassment by lying to his friend Mr Mant and the police, saying he didn't know what had happened to the car.
Knowles only later admitted he'd taken the car from his friend's house when the police showed him video images of the car being driven from Mr Mant's home in Epsom towards Gillingham, Kent where Mr Knowles' parents live.
After drinking heavily that night, Mr Knowles and Mr Mant then reported the car stolen and informed their insurance company of the car's theft.
Mr Knowles, who earns £160,000 per year from his property empire, said both he and Mr Mant had "no motive to commit fraud" and that they had intended to keep the Lamborghini.
The two men have shared several high performance cars since their early 20s, including a Mercedes convertible that Mr Knowles had also previously forgotten where it was parked after a night out. The Mercedes was subsequently found parked behind a nightclub in Kingston, Surrey.
Summing up, Judge Neil Stewart said: "As time went on, Mr Knowles found it harder and harder to confess and took the view that either way the car was stolen, but he said he realises it was the wrong thing to do."
[ Read More ]

WANAFUNZI WA KITANZANIA NUSURA KUUWAWA KWA MOTO BANGALORE -INDIA


TANZANIA STUDENTS ASSOCIATION BANGALORE
(TASABA)
WANAFUNZI WA KITANZANIA NUSURA
KUUWAWA KWA MOTO BANGALORE -INDIA
-----------
Tarehe 11/03/2010 majira ya saa 11:30 wanafunzi wawili ,Hamis Mbelwa Fintan mwenye na Olais Alexendra Siarra waliokuwa wanakaa No.1093/1.11th Cross,Swarnanagar,Robertsonpet,KGF-563 122. Walinusurika kuuwawa kwa moto baada ya fujo iliyofanywa na wahindi wakidai kuwachukia waAfrika.
Wahindi hao waliamua kuchukua mafuta ya petrol na kumwaga dirishani na mlangoni, walifanikiwa kuwasha moto kupitia malangoni na moto kuanza kuingia ndani wakati vijana hao wakiwa ndani. Kwa bahati nzuri walifanikiwa kuuzima moto uliokuwa unaingia ndani na ule wa nje wasamalia wema waliuzima, bahati nzuri petrol ilikuwa chache hivyo hakuna madhara makubwa yaliyotokea.

Nilipopata taarifa hii nilitoka na kufika kituo cha Police cha Hennur Cross, nilitoa taarifa hiyo wakatoka maafisa wa police na kufika sehemu ya tukio wakati huo mimi nikiwa nimebaki kituoni. Baada ya dakika 30 police walirudi bila watuhumiwa, nilipouliza walinijibu nirudi nyumbani wameshawatuliza na hawatarudia tena nilibishana sana na police juu ya hilo maana walipofika waliwakuta watuhumiwa na kuwaachia waende huru.
Nilizidi kupigania haki lakini walinijibu “This is India not Tanzania and we have to cop with them like it or not” niliwauliza kama huo ndio utamaduni wao wa kumwagia watu petrol na kuchoma moto kutaka kuwaua? Wakasema kama naona hawajanisaidia niende kutafuta msaada mahali pengine.
Nilisikitika sana kwa kauli za police hasa ukizingatia kuwa toka kifo cha mwenzetu Imran Mtui ni mwezi tu na siku 7 mpaka sasa na hatujapata taarifa ya kuridhisha kutoka kwa police halafu linatokea jaribio lingine la kuua kwa kutumia petrol.
Hali hii inatisha hasa nikiwa kama mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi kuona raia wenzangu wanatishiwa kutolewa maisha yao kwa moto na bila hatia huku police wakiona jambo hilo ni la kawaida kwao na kuwaachia watuhumiwa waende huru. Watu hawa wanaishi nchini kwetu kwa amani na kufaidi matunda ya uhuru na uchumi wa nchi yetu bila bugudha.


Baada ya kuona hakuna masaada kutoka police niliwashauri Hamis Mbelwa Fintan na Olais Alexendra Siarra wahame mahali pale kwani hapana usalama tena. Tunaomba sana msaada toka nyumabani na ofisi zetu za ubalozi zilizopo New-Delhi India kutafuta jinsi ya kufanya waTanzania waishio Bangalore –India na kwingine kote kuishi kwa amani, imezoeleka kuwa mara zote wanafunzi ni wakorofi lakini kwa tukio hili nakataa kabisa kama chanzo ni wahanga hawa bali ni chuki binafsi iliyoko dhidi ya wa Afrika ambayo inatufanya tuishi kwa uoga na wasiwasi mkubwa sana. Leo hii petrol ilikuwa chache siku nyingine itakuaje? Je wangefanikiwa kutoa roho za vijana hawa majibu kutoka vyombo vya dola vya India ingekuwa ni nini? Au wangesema wamejiua tena vijana hawa kwa moto? Haya ni maswali machache ya kujiuliza.


“Mungu ibariki Tanzania, Mungu tubariki wanafunzi wa kiTanzania tuishio Bangalore India”


Fidelis Msomekela


Mwenyekiti – TASABA

+919742176980

[ Read More ]

Meli ya m.v serengeti yawaka moto.

Meli ya MV Serengeti ilivyowaka jana ikiwa nangani.kwenye bandari ya zanzibar.
[ Read More ]

Sheikh Mkuu Wa Misri Dr Muhammad Sayyed Tantawyi Afariki Dunia


Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh I ssa Shaabani Simba (shoto) akiwa katika picha ya pamoja na Sheikh Mkuu wa Misri (Sheikhul-Azhar v-GRAND SHEIKH OF AL-AZHAR - Pr,) Dr Muhammad Sayyed Tantawyi katika Ofisi zake za Masheikhatul-Azhar zilizopo mji wa Darassa mwezi jana.
Habari zinasema Dr. Tantawyi amefariki dunia huko Misri.
Sheikh Mkuu wa Tanzania alikuwa nchini Misri kuhudhuria Mkutano Mkuu wa 22 (The 22nd General Conference. Under the Title The Objectives of Shariah(Islamic Law)And Issues of the Contemporary Age.



Marehemu amefariki leo saa 12:00 asubuhi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mjini Riadh Nchini Saudi Arabia akijiaanda kwa safari ya kurudi Nchini Misri.
Sheikh alikuwa Nchini Saudia Arabia Kuhudhulia Hafla ya ugawaji wa tunzo ya Mfalme Faisal iliyokuwa ikigaiwa kwa baadhi ya viongozi kutoka Nchi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu wa Uturuki.

Sababu za kifo chake ni Presha(Mshtuko wa Moyo) uliomtokea Ghafla akiwa kwenye ngazi ya Ndege,Taarifa zinasema hali hiyo imetokana na Uchovu aliopata kutokana na Shughuli hiyo ya jana.      


source:michuzi                                               




[ Read More ]

MAALIM SEIF YU HAI NA ANAENDELEA VIZURI

Uvumi ulioenea nchini ya kwamba Maalim Seif emefariki dunia unaonekana hauna ukweli wowote baada ya kuthibitika kwamba Maalim anaendela vizuri katika Hospitali ya Hindu Mandal.
Uvumi huo uliokua ukisambazwa leo hii kwa njia ya simu (SMS)unaeleza kua Maalim Seif amefariki dunia leo katika Hospitali ya Hindu Mandal ambapo alikua amelazwa tokea jana baada ya kuanguka jana Uwanja wa Ndege Jijini Dar-es-salaam alipokua akisubiri ndege kuelekea nchini Oman.
Maalim alikua anasumbuliwa na tatizo la Presha pamoja sukari, lakini kwa sasa anaendelea vizuri na anatarajia kuruhsiwa kwenda nyumbani hii leo.
InshaaAllah Mungu ampe afya njema......Amiin
[ Read More ]

UMEME ZANZIBAR KUREJEA JUMANNE IJAYO

Huduma ya umeme visiwani Zanzibar inatarajiwa kurudi Jumanne ijayo baada ya kukamilika kazi za utengenezaji wa kituo cha kupokea umeme kilichopo Fumba, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.

Kaimu Meneja wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), Hassan Ali Mbarouk, aliwaambia waandishi wa habari waliotembelea katika kituo chenye kufanyiwa matengenezo cha Fumba kwamba ikiwa kazi ya kurejesha huduma hiyo itafanyika kama ilivyopangwa basi huduma hiyo itarejea siku hiyo.

Alisema kazi hiyo iliyobakia ni kuunganisha waya za umeme kutoka nchi kavu na baharini na kazi hiyo ya kuunganishwa kwa waya kutoka katika vituo vya Fumba hadi Ras Kiromoni Tanzania Bara itachukua muda wa siku tatu.

Akitaja hatua zitakazochukuliwa za kurejesha huduma hiyo, Kaimu Meneja huyo alisema hadi Jumapili ijayo kazi ya matengenezo itakuwa imemalizika na matarajio Machi 8 kutafanyika vipimo vya majaribio na Machi 9 ndiyo huduma hiyo inatarajiwa kuwashwa.

Aliwaeleza waandishi wa habari kuwa kuchelewa kwa huduma hiyo kumesababishwa na mafuta yaliyokuwemo ndani ya waya zinazoleta umeme kutokuwa safi na kulazimika kusafishwa kwa muda wa siku tatu.

Wakazi wa visiwa hivyo wamekosa huduma ya umeme tangu Desemba mwaka jana, baada ya kutokea hitilafu katika kituo cha kupokea umeme huo kutoka Ras Kiromoni hadi Funmba mjini Unguja.
[ Read More ]