Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook


 
‘’ASalaammu Alaikum’’ 
Jummuah Mubarak 
  

O Allah!
On this blessed day we ask of you... 
Guide us among those, whom you have guided, 
And grant us protection among those whom you have protected. 
  
Befriend us among those whom you have befriended. 
Grant us blessings in that, which you have given us, 
And save us from the evil which you have ordained. 
  
For, surely, your decree matters and no one decrees over you. 
Indeed the one whom you befriend will never be dishonored, 
And the one with whom you have enmity will never be honored. 
  
You are Most blessed our Lord and You are Most Exalted.. 
We seek your forgiveness and turn towards you in repentance. 
  
And may Allah send salutations upon the most Honorable Prophet Muhammad (S.A.W). 
  
O Allah! Grant respect to Islam and the Muslims. 
O Allah! Assist Islam and the Muslims. 
O Allah! Create love among the hearts of the believers, 
O Allah! Destroy the unbelievers, who prevent people 
From the path of your religion, reject your Messengers, 
And who fight against your friends.
O our Beloved Allah! Hear our dua’s..
Aameen .. Ya Rabul-Aalimeen (Oh Creator of Everything)
[ Read More ]

Mashindano ya kusoma Qur'an London.




Hafla ya matokeo ya kusoma Qur'an ya mwaka 2010 (1431 AH) yamefanyika siku ya Alhamisi ya tarehe 03/02/2011 katika ukumbi wa Town Hall, East Ham, jijini London.

Washiriki wasiopungua 18 walishiriki mashindano hayo ya kusoma Qur'an yaliyoandaliwa na kituo cha kujitolea na kinachosaidia Waislamu waishio nchini Uingereza (Salama Trust).

Mashindano hayo yaligawanyuka katika makundi matatu. Mshindi wa kwanza katika kundi la kwanza alikuwa Khayrat Juma ambaye alipata kura 99%, mshindi wa pili katika kundi la kwanza alikuwa Yaaqub Abeid ambaye alipata kura 98% na mshindi wa tatu alipata kura 85%.

Kundi la pili, mshindi wa kwanza Rashid Mohammed alipata kura 100%, Mujahidi Mujahidi alitokea mshindi wa pili kwa kupata kura 94% na mshindi wa tatu Faisal Issa aliyepata kura 85%.

Ashraf Khalifa ndiye mshindi katika kundi la tatu kwa kupata kura 100%, Mohammed Yusuf alitokea mshindi wa pili kwa kupata kura 87% na Abdulmajid Yusuf alitokea mshindi wa tatu kwa kupata kura 64%.

Mwenyekiti wa Salama Trust Bw. Salehe Jaber aliwapongeza washiriki wote kwa kujitolea kushiriki mashindano hayo ya kusoma Qur'an.

"Umoja na ushirikiano ndiyo chanzo cha maendeleo" alisema Bw. Jaber na kusisitiza mshikamano kwa waislamu dunia kote.

Ally Muhdin - WWW.TZ-ONE.BLOGSPOT.COM
[ Read More ]

Taarifa Ya Habari Yasomwa Gizani Nepal


''Ifuatayo ni taarifa ya habari ikisomewa gizani, kwa kuwa umeme umekatwa.'' Mojawapo wa vituo vikuu vya televisheni nchini Nepal kimeanza kutangaza taarifa zake za habari za usiku katika mazingira ya nusu kiza ili kubainisha athari za ukataji mkubwa wa umeme.

Tangu mwanzoni mwa mwezi wa February, kituo cha televisheni cha Kantipur kimetumia taaa zinazotumia mafuta kutoa mwanga wakati wa taarifa yake ya habari ya dakika 30 saa moja usiku.

Mkuu wa kituo hicho alisema shabaha ni kutia shinikizo kwa serikali ikabiliane na tatizo hili.

Kwa sasa Nepal inakabiliwa na mpango wa kukata umeme kwa saa 12 kila siku.

"tunaitaka serikali izalishe umeme zaidi kwa haraka" mkuu wa Kantipur News Tirtha Koirala aliiambia BBC.

"hadi sasa watazamji wetu wamepokea vizuri hatua hii;lakini serikali bado haijasema chochote."

Licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kuzalisha umeme kutokana na mito, Nepal huzalisha nusu tu ya mahitaji yake ya umeme.

Miaka kumi ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya waasi wa Kimao na serikali ya Nepal vilivyomalizika mnamo mwaka 2006, imemaanisha uwekezaji mdogo sana katika sekta ya umeme ya Nepal.

Juu ya yote hayo mtandao wa kusambaza umeme nchini uliathiriwa vibaya sana baada ya kuharibiwa na mafuriko ya mto Kosi mnamo mwaka 2008.

Hii imesababisha kuwepo na mgawo wa umeme kuwa ni jambo la kawaida katika maisha ya kila siku.

Tatizo ni kubwa zaidi katika majira ya baridi ambapo ukosefu wa mvua na kina cha chini cha mito inamaanisha mabwawa yaliyopo hayawezi kuendesha shughuli zao kikamilifu.

Mamlaka ya nguvu za umeme ya Nepal yanayomilikiwa na serikali yamesema kuwa nchi inaweza kutazamia kukatwa umeme kwa kipindi cha saa 14 kila siku katika muda wa wiki chache zijazo.

"tunasumbuka sana kwa sababu ya mgawo wa umeme ," amesema Bwana Koirala .

"Takriban wanafunzi 400,000 hivi sasa wanajitayarisha kwa mtihani wa shule za sekondari na hawana mwanga wowote wa taa usiku".

"Halikadhalika wafanyibiashara wadogo wadogo ambao hawawezi kumudu jenereta au kifaa cha "inverter"nao pia hawawezi kuendesha shughuli zao."

Bwana Koirala alisema taarifa za habari za kituo chake zitaendelea kutangazwa katika mazingira ya kiza mpaka serikali itakapochukua hatua .
[ Read More ]