Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Ujumbe wa Oman Wawasili Zanzibar kwa matayarisho ya Mkutano wa Kimataifa wa Historia ya Oman na Zanzibar, Historia ya Kiislam na Utamaduni wake.



Kaimu Balozi Mdogo wa Oman Zanzibar Saleh Suleiman, akisalimiana na Kiongozi wa Msafara wa Wajumbe wa Oman waliowasili Zanzibar leo kwa ajili ya matayarisho wa Mkutano wa Historia na Utamaduni wa Kiislam. unaotarajiwa kufanyika mwezi wa september 2013 Zanzibar. 
 BALOZI wa Oman  nchini Tanzania Yussuf Al Bakar ( katikati) akiongozana na Ujumbe kutoka Nchini Oman ukiwasili Zanzibar kwa ajili ya matayarisho ya Mkutano wa Kimataifa wa utakaozungumzia Historia na Utamaduni wa Kiislam Zanzibar kulia Kiongozi wa Ujumbe huo Dk. Hamed Mohammed Al Dhawiyaniy, ni Mwenyekiti wa Taifa wa Mamlaka ya Makumbusho ya Taifa ya Oman. Na kushoto Kaimu Balozi Mdogo wa Oman Zanzibar Saleh Suleiman

 Ujumbe wa Oman ukiwa katika ukumbi wa Wageni katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume wakibadilishana mawazo baada ya kuwasili Zanzibar leo.
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Dkt. Haji Mwevura Haji,akizungumza katika mkutano na Ujumbe wa Oman, uliowasili Zanzibar kwa matayarisho ya mkutano wa Historia na Utamaduni wa Kiislam, kushoto Dk. Hamed Mohammed Al Dhawiyaniy, ni Mwenyekiti wa Taifa wa Mamlaka ya Makumbusho ya Taifa ya Oman,na kulia Mkurugenzi Mkuu wa Kitengo cha Historia ya Uislam Oman Dkt.Halit Eren.
 Mkuu wa Msafara wa Ujumbe wa Oman uliowasili Zanzibar kwa matayarisho wa Mkutano wa Kimataifa utakaozungumzia Historia na Utamatudi wa Kiislam, Dk. Hamed Mohammed Al Dhawiyaniy, ni Mwenyekiti wa Taifa wa Mamlaka ya Makumbusho ya Taifa ya Oman,Zanzibar ina mahusiano ya Kihistoria na Mataifa ya Kiarabu katika historia na Utamaduni wa Kiislam.kulia  Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Dkt. Haji Mwevura Haji na  Mkurugenzi Mkuu wa Kitengo cha Historia ya Uislam Oman Dkt.Halit Eren,
 Mkuu wa Skuli ya Kiswahili na Lugha za Kigeni Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar Dkt. Issa Haji Zidi, akitafsiri katika mkutano huo kutoka katika lugha ya Kiarabu, wakati wa mkutano huo wa matayarisho ya Mkutano wa Kimataifa wa Historia na Utamaduni wa Kiislam unaotarajiwa kufanyika Zanzibar mwezi wa September 2013.  
 Mkurugenzi Mkuu wa Kitengo cha Historia ya Uislam Oman Dkt.Halit Eren, akizungumza katika mkutano huo uliowashirikisha Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA,  
 Ujumbe wa Oman wakimsikiliza Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa Dkt. Haji Mwevura Haji, akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa SUZA Majestiki Zanzibar. 
Ujumbe wa SUZA wakiwa katika Mkutano na Ujumbe kutoka Oman uliofika Zanzibar kwa maandalizi ya Mkutano wa Kimataifa wa Historia ya Uislam na Utamaduni wake baina ya Nchi hizi mbili.mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa mkutano Chuo Kikuu cha Taifa Kampasi ya Majestic Zanzibar. 
[ Read More ]