Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Umeme waua mume, mke taabani Muhimbili

Baba mmoja amefariki dunia na mkewe kujeruhiwa vibaya baada ya kuangukiwa na waya wa umeme.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile amemtaja marehemu kuwa ni Masari Abdulhussein, 27, na aliyejeruhiwa kuwa ni Bi. Najma Swalehe, 24, wote wakazi wa Kigamboni.

Akisimulia tukio hilo, Kamanda Shilogile amesema watu hao wamekutwa na mkasa huo wakati wakiwa wamebebana kwenye pikipiki.

Amesema tukio hilo la kusikitisha limetokea katika eneo la makutano ya barabara za Uhuru na Nyamwezi, Kariakoo Jijini.

Akasema Bw. Masari ndiye aliyekuwa akiendesha pikipiki hiyo yenye namba za usajili T 311 AMS aina ya Sangly huku akiwa amembeba mkewe na kuwa walipofika eneo hilo, waliangukiwa na waya wa umeme wenye moto na kusababisha wajeruhiwe vibaya.

Kamanda Shilogile amesema wataalam wa Shirika la Umeme nchini, Tanesco waliitwa mara moja na walipofika wakawatoa na kuwakimbiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Akasema hata hivyo mwanaume, alifariki dunia wakiwa njiani na mwili wake umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Taifa, Muhimbili.

Amesema mkewe Bi. Najma naye amelazwa hospitalini hapo ambapo anaendelea kupewa matibabu.
[ Read More ]

Moto wateketeza mali za mamilioni Oysterbay Dar

Moto mkubwa umelipuka katika jengo la Golden Sand lililopo kwenye Mtaa wa Karume pale Oysterbay Jijini na kusababisha mali zenye thamani ya mamilioni ya fedha kuteketea.

Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amesema moto huo ulianza jana mishale ya saa 1:00 asubuhi na kuunguza chumba kimoja cha jengo hilo, ambalo ni mali ya Bw. Fidar Hussein.

Amesema chumba namba tisa cha jengo hilo ambacho kinatumika kama jiko, ndicho kilichoteketea kwa moto uliounguza vitu tele vilivyokuwamo ndani.

Kamanda Kalunguyeye amesema miongoni mwa vitu vilivyoteketea kwa moto ni pamoja na jokofu moja kubwa lililokuwa ndani ya chumba hicho.

Akasema chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme na kwamba thamani ya mali iliyoteketezwa na moto huo bado haijafahamika.

Kwa mujibu wa Kamanda Kalunguyeye, moto huo ulizimwa na Kikosi cha Zimamoto cha Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na wananchi wa eneo hilo.

[ Read More ]

Mama achinjwa Dar

Mwanamke mmoja Jijini ameuawa kinyama kwa kuchinjwa na kisha kichwa chake na kiwiliwili kutengenishwa.

Inadaiwa mwanamke huyo ameuawa na mtu anayedaiwa kuwa ni mume wake.

Tukio hilo la mauaji ya kinyama, linadaiwa kutokea jana katika maeneo ya Kigogo Jijini.

Taarifa ambazo Alasiri imezipata, zinaeleza kuwa aliyetekeleza mauaji hayo ya kinyama ni mume wa mwanamke huyo ambaye alitoroka baada ya tukio.

Hata hivyo, majina ya marehemu na mtuhumiwa wa mauaji hayo hayakuweza kuthibitishwa.

Aidha, taarifa zaidi zimedai kuwa chanzo cha mauaji ya mwanamama huyo anayedaiwa kuacha watoto wawili ni wivu wa kimapenzi.

Hata hivyo, Mwandishi alipojaribu kumsaka Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Mark Kalunguyeye, ili aelezee tukio hilo, hakuweza kupatikana kupitia simu yake ya mkononi.

Naye Kamanda wa Polisi katika Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema hajapata taarifa za tukio hilo.

Aliposakwa tena Kalunguyeye, mtu aliyepokea simu alidai kuwa Kamanda Kalunguyeye alikuwa ameelekea katika hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pale Mabibo ambako kulitarajiwa kufanyika mkutano wa Kamati ya Ulinzi ya Mkoa na Uongozi wa Chuo hicho.

[ Read More ]

kwa heri Beatha.


Baadhi ya waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE), Beatha Mwarabu (picha ndogo) aliyeuawa kwa kuchomwa kisu na mwanafunzi mwenzake. Heshima za mwisho zilitolewa jana chuoni hapo Chang’ombe, Dar es Salaam.
[ Read More ]

Padri akemea ngono UDSM

Padri Josephat Mosha wa Kanisa Katoliki Parokia ya Chang’ombe mkoani Dar es Salaam, amewataka wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kutambua na kuzingatia kilichowapeleka chuoni hapo na kuachana kabisa na dhana potofu ya kudanganyana kuhusu uhusiano.

“Katika maisha haya ya shule, mara nyingi sana wengi wetu huwa tunapotoshana kuhusu neno upendo na kufikia mahali mtu anasahau hata kile kilichomleta mahali hapa kutokana na kuzama katika suala hilo, itakuwa vyema kama mtajiuliza kuwa mmefuata nini mahali hapa ili kuepuka kuhatarisha maisha yenu,” alisema Padri Mosha.

Padri Mosha alikuwa akizungumza kwenye Ibada ya kumuombea marehemu Beatha Mwarabu (23), aliyekuwa mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE) cha UDSM ambaye alifariki dunia usiku wa kuamkia Jumapili kwa kuchomwa kisu na mwanafunzi mwenzake, Masaba Musiba anayedaiwa alikuwa na uhusiano naye wa kimapenzi kwa muda mrefu.

Alisema vijana wengi wa siku hizi wamekosa upendo kwa kile alichoeleza kuwa hali hiyo imetokana na vijana hao kutokuwa tayari kusikiliza maneno ya watu muhimu katika jamii, wakiwamo wazazi wao na hivyo kusababisha vijana hao kuwa na watu wenye chuki pamoja na visasi ambapo ili kuepukana na hayo yote, aliwataka kwanza kujifunza dhana itokanayo na neno upendo.

“Mtu hawezi kujipenda yeye kwanza kabla hajampenda mwenzake, hivyo mioyoni mwetu yatupasa kujenga tabia ya kuwapenda wenzetu kabla ya kujipenda sisi,” alisema Padri Mosha. Aidha, Padri Mosha aliwataka watu wote kutambua kwamba kila mmoja ataonja mauti hata kama ataishi miaka mingapi, na kuwaasa kutubu dhambi zao na kumcha Mungu.

Mapema, majonzi, simanzi na vilio vilisikika kwa wingi jana katika ukumbi uliopo katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Chang’ombe wilayani Temeke, wakati walimu, wanafunzi, ndugu na jamaa walipokuwa wakiuaga mwili wa mwanafunzi Beatha aliyefariki usiku wa kuamkia Jumapili baada ya kuchomwa kisu na Musiba aliyedaiwa kuwa ni mpenzi wake.

Hali ya huzuni chuoni hapo ilikuwa imetawala tangu tangu juzi baada ya kutolewa kwa taarifa na kubandikwa kwa matangazo yaliyoelezea tukio la kifo hicho pamoja na kilichosababisha, huku baadhi ya wanafunzi wakiwa bado wameshikwa na butwaa na kutoamini kile kilichotokea. “Inasikitisha sana yaani mpaka muda huu wengi wetu bado hatuamini kwamba kweli mwenzetu katutoka tena kwa kifo cha kinyama kiasi hiki, ila kwa upande wetu tutazidi kumuombea kwa Mungu huko aendako,” alisema mmoja wa wanafunzi wa DUCE, Mwanahamisi Shaabani.

Kwa upande wake, baba mdogo wa marehemu, Rafael Mwarabu alisema kifo hicho kimewasikitisha na zaidi wanamuomba Mungu amzidishie heri huko aendako na kueleza kuwa tangu kipindi cha uhai wake, Beatha alikuwa mtu mwenye tabia njema na heshima kwa kila mtu. Kwa upnde wake, Mkuu wa Elimu chuoni hapo, Joviter Katabalo alimwelezea Beatha kwamba alikuwa mwanafunzi mwenye bidii chuoni hapo kwa kujituma wakati wote pamoja na kushirikiana vizuri na wanafunzi wenzake hadi anakutwa na mauti.

Alisema kifo hicho kimekuwa pigo kubwa kwa upande wa wanachuo chuoni hapo. Mwili wa marehemu ulisafirishwa jana na unatarajiwa kuzikwa leo katika Kijiji cha Kibaoni kilichopo Ifakara katika Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro. Kwa mujibu wa taarifa za wanafunzi wenzao, wakiwamo marafiki wa karibu wa marehemu, Beatha na mtuhumiwa walianza mapenzi muda mrefu tangu wakiwa wanafunzi wa shule mkoani Morogoro.

Inaelezwa kuwa tangu waanze masomo chuoni hapo, uhusiano wao haukuwa mzuri kutokana na ugomvi wa mara kwa mara huku chanzo kikubwa kikidaiwa ni tabia ya ulevi aliyokuwa nayo mvulana ambayo mwenzake alichukizwa nayo. Wote wako walikuwa mwaka wa pili DUCE.

Inadaiwa Beatha alimpa mpenziwe mwezi mmoja wa kujirekebisha kutokana na tabia hiyo na kumtishia kusitisha uhusiano wao endapo angeendelea na tabia hiyo, lakini pamoja na hilo mpenzi wake huyo hakujirekebisha na ndipo msichana akachukua uamuzi wa kusitisha uhusiano huo; hatua ambayo bila ya shaka ndiyo iliyosababisha mvulana achukue hatua ya kumchoma kisu na kumuua.




[ Read More ]

UDSM yafunga barabara hosteli Mabibo

wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wamefunga barabara na kuharibu gari katika eneo la Mabibo baada ya kukasirishwa na wenzao wawili kugongwa na pikipiki na kuwajeruhi juzi usiku. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema hayo jana Dar es Salaam na kuwataja wanafunzi waliogongwa ni Ibrahimu Mkama (25) na Sayelo Daniel (30), ambao walitibiwa chuoni hapo baada ya kupewa na polisi fomu maalumu ya matibabu.

Walipata majeraha madogo. Alisema baada ya kutokea kwa tukio hilo, wanafunzi hao walizingira eneo hilo na kufanya fujo kwa magari yanayopita katika barabara hiyo na kuliharibu gari aina ya Toyota DCM ambalo walivunja vioo vya gari hiyo vya pembeni na kuongeza kuwa hakuna abiria aliyejeruhiwa kutokana na tukio hilo.

Alibainisha kuwa kutokana na fujo hizo, hakuna mwanafunzi ye yote anayeshikiliwa kutokana na tukio hilo na kuwa upelelezi kuhusu tukio hilo unaendelea ambapo Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kinondoni na Polisi inafanya mazungumzo na uongozi wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho (DARUSO) ili kubaini madai ya wanafunzi hao na chanzo cha tukio hilo. Katika tukio jingine, raia wenye asili ya Kiasia, wenye uraia wa nchi mbili tofauti wamekutwa wamekufa katika Hoteli ya Harbour View Suit iliyopo katika Mtaa wa Samora Dar es Salaam.

Kamanda Kova alisema vifo hivyo viligundulika saa 8:00 mchana juzi na kuwataja waliokufa kuwa ni Salman Zuberi (41) na Yusuph Sader (33), waliokutwa vyumbani mwao wakiwa wamekufa. Alisema raia hao walikutwa na pasipoti za kusafiria za nchi zao ambapo Zuberi alikutwa na pasipoti yenye namba JX 276017 ya Canada na Sader pasipoti yake ni namba 459639277 ya Afrika Kusini ambapo katika vyumba walivyofia kulikuwa na mazingira tofauti, yakiwamo ya maiti kukutwa na mate na dalili za matapishi. Polisi inachunguza vifo hivyo.
[ Read More ]

Wananchi wachoma nyumba na kuharibu shamba la mbunge

MAMIA ya wakazi wa kijiji cha Sing'isi kilicho wilayani Arumeru mkoani Arusha, wamevamia kwa siku mbili mfululizo shamba la Madira Estate linalomilikiwa na Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro na kuteketeza kwa moto zaidi ya nyumba 15 zilizo kuwa kwenye shamba hilo na kukata mazao kadhaa yenye thamani ya mamilioni ya fedha.

Tukio hili limetokea wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa mjini hapa kushiriki matembezi ya kuchangia mradi wa kutoa chakula mashuleni yaliyoandaliwa na Shirika la Chakula Duniani (WFP).

Wananchi hao waliokuwa na mapanga, visu, nondo na silaha nyingine kadhaa, walianza uvamizi wa shamba hilo kuanzia majira ya saa 3:00 usiku juzi na kuendelea hadi jana asubuhi, vitendo vilivyosababisha kufungwa kwa muda barabara ya Arusha-Moshi.

Licha ya polisi kumwagwa katika eneo hilo na kupiga mabomu kadhaa ya machozi na risasi kadhaa za moto hewani, wananchi hao waliendelea na uharibifu huo na kubeba mbao, mabati na mali mbalimbali zilizokuwa katika eneo hilo.

Wakizungumza katika eneo hilo, baadhi ya wananchi walisema wanapinga serikali kuliuza shamba hilo lenye ekari 50 kwa mbunge huyo wakati wao wana shida kubwa ya ardhi na eneo la upanuzi wa shule yao.

'Hatukubali... hili ni eneo letu. Tutapigana hadi mwisho na hakuna kumilikiwa tena na mbunge. Tumefunga barabara na tumevunja nyumba zote... serikali ilipaswa kutupa eneo letu wananchi baada ya Wazungu kuacha mashamba, lakini ajabu imeliuza," alisema John Akyo mkazi wa kijiji hicho.

Mkuu wa wilaya hiyo, Marcy Silla aliyefika eneo hilo jana asubuhi, alionekana kupigwa na butwaa wakati akishuhudia ujasiri wa wananchi kuendelea kubeba mali mbalimbali kutoka katika nyumba zaidi ya 15 walizovunja, nyumba ambazo zipo ndani ya shamba na nyingine ambazo mbunge huyo amezirithi.

"Sijui lolote kuhusu tukio hili. Nimepewa taarifa leo, lakini nilichoelezwa ni kwamba wananchi wanadai eneo, lakini kweli kwa nini watumie nguvu kiasi hiki," alihoji Silla.

Kimaro, akizungumza na mwandishi wa habari jana, alisema ameshangazwa na uamuzi wa wananchi kuvamia eneo lake pekee wakati jirani kuna Wazungu wana zaidi ya ekari 1,000.

"Nilipata taarifa hizi tangu juzi, nikawapa taarifa polisi, lakini nashangaa hawajachukua hatua hadi usiku wananchi walipovamia shamba. Mimi mzalendo mwenzao kumiliki heka 50 kujenga hoteli imekuwa nongwa!" alisema Kimaro.

Alisema anaamini tukio hilo sio shamba tu, bali kuna siasa ndani yake kwa kuwa anataka kujenga hoteli na ndio maana alianza kulitunza eneo kwa kupanda miti ya asili ambayo imekatwa na wananchi hao.

"Kuna miti zaidi ya 4,000 imekatwa na wananchi. Wanasema eti wanataka kulima... lile eneo ni la hoteli ya kitalii na kabla ya ujenzi nilikuwa nalirejesha kwenye uasilia wake," alisema Kimaro.

Kamanda wa polisi mkoani Arusha, Matei Basilio alikiri kutokea kwa tukio hilo na kwamba hadi jana zaidi ya watu 15 walikuwa wamekamatwa.

"Ni kweli kuna vurugu tangu usiku na vijana wangu wanashughulikia na hadi sasa watu wanakamatwa na vurugu zinaendelea," alisema Basilio jana mchana.

Diwani wa kata hiyo, Petro Kiungani na mwenyekiti wa kitongoji cha Maviruni yalipo mashamba hayo, Desaulo Akyoo, walisema kwa zaidi ya wiki wamekuwa wakitoa taarifa polisi juu ya mpango huo wa uvamizi, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa.

"Nilimweleza mkuu wa polisi wa wilaya kuna vikao vinaitishwa kuchochea vurugu. Wananchi walikuwa wakidai sisi viongozi serikalini tumeuza eneo, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa," alisema Kiungani.

Hadi jana mchana vurugu zilikuwa zikiendelea na hakuna taarifa kamili ya hasara ambayo imepatikana. Mkuu wa wilaya hiyo alikuwa akiwaomba viongozi wa serikali ya kijiji cha Singisi kuwasihi wananchi kuacha vurugu hizo.

[ Read More ]

Z`bar port authority heaps blame on sunken ship captain

The Zanzibar Port Cooperation (ZPC) yesterday said the captain of MV Fatih which capsized at Malindi Port last week was to blame for the accident.

ZPC Technical Director Abdi Omar said the captain Ussi Ali Ussi gave wrong information on the exact number of passengers who were on board before the cargo ship capsized.

Omar told this paper that Captain Ussi had told the authorities that MV Fatih carried a 55 tone cargo, 25 passengers and a crew of 13.

According to him, the names of rescued passengers are Kassim Masoud Mansour from chakechake, Bakar Shaame Mussa (Wete), Abdallah Juma Muhidini (Shangani), Sabiha Juma Khamis (Sogea), Omar Ali Khamis, Rashid Haji Makame (Mwenge), Maulid Abduli (Kisiju), Hawa Juma Saleh (Kilwa) Ramadhan Juma Mohammed and Zainab Ali Kitima both from Dar es Salaam.

Others are Fatma Ali Salum (Wete), Hassan Punga (Kisiju), Fatma Khamis Juma (Dar es Salaam), Sharif Hamad Sharif (Dar es Salaam), Omar Khamis Mohammed (Dar es Salaam), Machano Mkwai Khamis (Mkwajuni), Tiba Mussa Kitiba (Gamba), Laila Ali Hakim (Dar es Salaam), Munira Hashim Lionga, (Bububu) and Halima Mussa Johari (Arusha).

They also include Janeth Falume Mleni (Kiwengwa), Awanias Mbiro (Songea), Sjarifa Seif Mwinyi (Mpendae), Hassan Juma Hassan (Chake Chake), Rehema Juma Kabwela (Dar es Salaam) and Sharifa Juma Msham (Dar es Salaam). Shaaban Haji Abdllah, Omar Salum Said, Ismail Hassan Ndota, Abass Khamis Abas and Gora Haji Kombo from Zanzibar.
[ Read More ]

MWANAFUNZI AUWAWA MABIBO HOSTEL


Mwanafunzi wa mwaka wa pili katika Chuo Kikuu cha Elimu (Duce), jijini Dar es Salaam, Bertha Mwarabu (23), ameuawa na mwanafunzi mwenzake kwa kuchomwa kisu kwenye titi na tumboni kwa kinachodaiwa ni kutokana na wivu wa mapenzi.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana katika hosteli za chuo hicho zilizopo Mabibo, jijini Dar es Salaam.

Kamanda Kalunguyeye alimtaja mtuhumiwa wa mauaji hayo kuwa ni Masamba Musiba (27) ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo hicho, ambacho ni sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Alisema mauaji hayo yalitokea juzi saa 3:45 usiku baada ya Musiba kuingia chumbani kwa marehemu ambaye inadaiwa alikuwa mpenzi wake na kuanza kumshambulia kwa kisu. Aliongeza kuwa baada ya marehemu kuanza kushambuliwa, alipiga kelele kuomba msaada na ndipo wanafunzi wenzake walipokwenda na kumkamata mtuhumiwa wakati akijaribu kukimbia.

Alisema kelele za marehemu, ndizo zilizowashtua wanafunzi wenzake.

Kamanda Kalunguyeye alifafanua kuwa marehemu alikimbizwa hospitali kupatiwa matibabu lakini alifia njiani.

Mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mwananyamala.

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala, alisema tukio la mauaji hayo ni la kwanza kutokea chuoni hapo.

Profesa Mukandala alisema tangu aanze kufanya kazi chuoni hapo kwa miaka mingi, hajawahi kushuhudia tukio la namna hiyo na kuongeza kuwa amesikitika kwa kuondokewa na mwananfunzi huyo.

[ Read More ]