Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

WAUWAJI WA STEPHEN LAWRENCE WABAINIKA!


Baada ya miaka 18 ya upelelezi na kuendesha kesi kuhusu mauwaji ya kijana mweusi mjini London, Stephen Lawrence, wanaume wawili wamepatikana na hatia.


Gary Dobson na David Norris
Gary Dobson na David Norris

Gary Dobson na David Norris wamepatikana na hatia na jopo la mahakama baada ya kesi hio kutegemea ushahidi wa kitaalamu.
Wataalamu wa uchunguzi wa damu na alama kama hizo waligundua alama ya damu kwenye koti la Dobson ambalo bila shaka halingepatikana bila kumkaribia marehemu.

Wakati akiondolewa mahakamani, aliliambia jopo kua wamemhukumu mtu asiye na hatia. Hukumu itasomwa siku ya jumatano.


Stephen Lawrence
Stephen Lawrence

Wazazi wa marehemu Stephen, Doreen na Neville, waliangua kiliyo jopo lilipotangaza kua watuhumiwa wamepatikana na hatia. Duwayne Brooks, rafiki mkubwa wa Stephen Lawrence aliyekua naye waliposhambuliwa, alituma ujumbe kupitia mtandao wa Tweeter akisema, hatimaye, sheria imetendeka'
Mamake Dobson, Bi.Gary Dobson, aliyeiambia mahakama kua mwanawe alikua nyumbani wakati wa mauwaji, aliangua kilio mahakamani kufuatia tangazo la watuhumiwa kupatikana na hatia.

Upelelezi wa kwanza uliofanywa na polisi ulishindwa na kupelekea Polisi ya mji wa London kutuhumiwa kama Idara inayoendesha ubaguzi wa rangi.

Stephen Lawrence alikua mwenye umri wa miaka 18 alipouawa kwa kisu akiwa karibu na kituo cha basi cha Eltham, London ya kusini mnamo mwezi April mwaka 1993. Polisi walitambua watu watatu ambao baadaye walitajwa katika ripoti ya uchunguzi kama washukiwa wakuu.

Hadi wakati huo kulikuepo mfululizo wa mapungufu ya polisi kwa kushindwa kukusanya ushahidi wa kutosha mbara mbili, wa kwanza uliowasilishwa na wazazi wake Stephen Lawrence, Doreen na Neville Lawrence.

Lakini katika kuichunguza kesi hio kwa mda wa miaka minne, wataalamu wengine wa kupeleleza ushahidi waliweza kugundua ushahidi ulioweza kuwaunganisha washukiwa na mauwaji - ushahidi ambao ulia mikononi mwa polisi kwa kipindi kirefu.

Ushahidi huo wa alama za damu, nyuzi za nguo na unywele wa marehemu - vilipatikana kwenye nguo za washukiwa zilizotekwa tangu mwaka 1993.

Wataalamu wa upelelezi wa ushahidi walifanikiwa kugundua ushahidi huo kwa kutumia mitambo ya kisasa ambayo wakati ule havikuwepo.

Dobson, mwenye umri wa miaka 36, na Norris,akiwa na umri wa miaka 35, walikanusha madai ya kuua. Walidai kua damu hio ilichanganyika na nguo zao kutokana na kuchanganywa na ushahidi kupitia kipindi cha miaka mingi.

Wapelelezi walitumia mda kuchunguza jinsi ushahidi huo ulivyozungushwa na jinsi ulivyohifadhiwa kuondoa shaka ya uwezekano wa kuchanganywa kama walivyodai watuhumiwa.

Gary Dobson alikamatwa na kufungwa jela mnamo mwaka 2010 kwa kushiriki biashara ya kuuza mihadarati. Yeye ni miongoni mwa kundi dogo la wanaume waliohusishwa na uhalifu mmoja baada ya Mahakama ya rufaa kuzima ombi lake la rufani mnamo mwaka 1996.

Katika mahojiano marefu na BBC, Mamake Stephen Lawrence, Doreen alisema: "siwezi kuwasamehe vijana waliomuua mwanangu Stephen. Wao hawadhani kama wametenda uovu wa aina yoyote.

Hukumu inatazamiwa sku ya jumatano.habari ya BBC

[ Read More ]