Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

300 dead in massive quake in Chile, search on for survivors.


SANTIAGO: Rescue teams hunted for survivors on Sunday after one of the largest earthquakes on record killed at least 300 people in Chile and sent giant waves roaring across the Pacific Ocean.

In an address to the nation on Saturday, President Michelle Bachelet said two million Chileans had been affected but, after touring the worst-hit areas by plane, she found it hard to spell out the magnitude of the disaster.

In Pics: Massive quake in Chile

"The power of nature has again struck our country," Bachelet said, declaring six of Chile's 15 regions "catastrophe zones" in the aftermath of the 8.8-magnitude quake.

Highways in the South American nation of 16 million were sliced to pieces, bridges imploded and buildings collapsed as the earthquake struck at pre-dawn hours Saturday some 325 kilometers (200 miles) southwest of the capital Santiago.

"This is a catastrophe of immense proportions, so it will be very difficult to give precise figures," Interior Minister Edmundo Perez Yoma said. Officials later said at least 300 people had been killed.

Waves well over two meters (seven feet) high crashed into the Chilean coast after the quake struck at 3:34 am (0634 GMT) and tore out into the Pacific, killing at least five people in the remote Robinson Crusoe islands.

In the Chilean port of Talcahuano, trawlers were sent shooting inland to the town square where they lay oddly marooned next to abandoned cars.

About 50 countries and territories along an arc stretching from New Zealand to Japan braced for giant waves, five years after the Indian Ocean tsunami disaster that killed more than 220,000 people.

More than 70,000 people fled vulnerable coastal areas of Japan Sunday as a tsunami slammed into the country's long Pacific coastline.

"Please do not approach the coast at any cost," Prime Minister Yukio Hatoyama said in nationally televised comments as Japan, one of the world's most quake-prone nations, went on its first major tsunami alert in 15 years.

The first tsunami wave, 30 centimetres (one foot) high, hit Nemuro on the northern island of Hokkaido in the early afternoon, the Meteorological Agency said.

The massive quake plunged much of Santiago into darkness, snapping power lines, severing communications. The international airport was closed after sustaining significant damage to the terminal.

Many Chileans were still in nightclubs partying at the start of the weekend when the quake struck before dawn, ripping up roads, bringing roofs crashing down and toppling power lines.

"It was the worst experience of my life," said 22-year-old Sebastian, standing outside his house in eastern Santiago.

"Friends who were at clubs said it was pandemonium," said Santiago resident Maren Andrea Jimenez, an American expert working for the United Nations. "It was scary! Plaster began falling from the ceiling."

President Barack Obama said the United States "stands ready to assist in the rescue and recovery efforts, and we have resources that are positioned to deploy should the Chilean government ask for our help."

"Early indications are that hundreds of lives have been lost in Chile and damage is severe. On behalf of the American people, Michelle and I send our deepest condolences to the Chilean people," he said at the White House.

The total value of economic damage caused by the quake is likely to range between 15 billion and 30 billion dollars, a US risk modeling firm predicted.

Despite officials saying up to 1.5 million homes could be affected, Chile's Foreign Minister Mariano Fernandez asked countries that had offered aid to hold off until local authorities could assess the emergency needs.

Chile does not want "aid from anywhere to be a distraction" from disaster relief, Fernandez said, adding: "Any aid that arrives without having been determined to be needed really helps very little."

The European Union said it would provide three million euros (four million dollars) in immediate assistance. Unlike Haiti, struck by a devastating earthquake last month, Chile is one of Latin America's wealthiest countries.

The US Geological Survey said it had recorded more than 51 aftershocks ranging from 4.9 to 6.9 since the quake.

Earthquake-prone Chile lies along the Pacific rim of fire and is regularly rocked by quakes, but damage is often limited as they mostly hit in remote desert regions.

It was the second major earthquake to hit the Western hemisphere in seven weeks after more than 200,000 people were killed in Haiti last month by a 7.0-magnitude quake.

The epicentre was just a few hundred miles north of the biggest earthquake on record, a 9.5-magnitude monster in May 1960 that killed between 2,200 and 5,700 people and triggered a huge tsunami that reached as far as eastern New Zealand.
[ Read More ]

Joti wa ze comedy alazwa moi....


[t.JPG]
Msanii maarufu wa kundi la vichekesho la Orijino Komedi,Lukac Mhavile a.k.a Joti (pichani) anahofiwa kuvunjika shingo,baada ya kupata ajali alipokuwa akirekodi kipindi pamoja na wenzake eneo la daraja la Salender,jijini Dar.




Joti aligongwa na lori aina ya Scania malai ya Ubalaozi wa Ubelgiji nchini,saa 5:30 jana asubuhi.Amelazwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa matibabu,akiwa amefungwa kifaa maalum cha kuzuia shingo kukunja na kugeuka.


Akizungumzia tukio hilo,Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni,Sebastian Masinde,alisema ajali hiyo ilitokea wakati msanii huyo akiwa na wenzake wakiigiza tukio lililodaiwa kutokea eneo hilo la Mwanamke kuoata Manyoya baada ya kumpa ombaomba pesa.


Alisema walipokuwa wakiigiza wakiwemo pia wasanii wenzake Masanja na Mpoki,ombaomba waliokuwa karibu walichachamaa na kuwazuia wasiigize ambapo katika kufanya hivyo waliwavamia na Joti na wenzake wakalazimika kukimbia.


"walipokuwa wakikimbia ndipo alipogongwa na gari,wamekasirika kwa sababu sasa mwenye kila gari lake anayepita pale anafunga vioo,hivyo hawakupenda Komedi waigize tukio hilo na kuanza kuwafukuza.
kamanada Masinde alisema kuwa baada ya tukio hilo, Majeruhi walipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako amelazwa MOI,na dereva wa Lori hilo anashikiliwa na polisi pamoja na gari lililosababisha ajali hiyo.
source michuzi.
[ Read More ]

PRESIDENT JK CONFERRED PHD IN INTERNATIONAL RELATION IN TURKEY!

President Jakaya Mrisho Kikwete prepares to deliver his acceptance speech shortly after he was conferred with Honorary Doctorate Degree in International Relations yesterday at Fatih University, in Instabul, Turkey Friday evening. Photo by Freddy Maro.


The Rector of Fatih University in Instabul, Turkey, Professor Shariff Ali confer upon President Jakaya Mrisho Kikwete a honorary Doctorate Degree (Honoris Causa) in International Relations during a colourful ceremony held at Fatih Univesity in Instabul Turkey Friday evening.Photo by Freddy Maro.
[ Read More ]

JK Ziarani Uturuki






Rais wa Uturuki Abdullah Gul na mkewe wakiwakaribisha ikulu ya jıjını Ankara JK Mama Salma leo asubuhi

JK na mwenyeji wake Raıs wa Uturuki Abdukkah Gul wakıkagua gwaride la heshima muda mfupi baada ya Rais Kıkwete kuwasili katika ikulu ya nchı hıyo iliyopo jijini Ankara leo asubuhi.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo 18 Feb, 10 anaanza ziara ya siku tatu nchini Uturuki kwa makaribisho rasmi ambapo Rais wa Uturuki Mheshimiwa Abdullah Gul atamkaribisha Rais Kikwete katika kasri ya nchi hiyo.

Mara baada ya makaribisho hayo, viongozi hao wawili watafanya mazungumzo rasmi ya kiserikali na kushuhudia utiaji saini kwa mikataba mitano kati ya nchi mbili hizi shughuli ambazo zitafanywa na mawaziri.


Mchana wa leo, (18.2.10) Rais na ujumbe wake utakutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Uturuki, Mheshimiwa Recep Tayyid Erdogan kabla ya kukutana na kufanya mazungumzo na spika wa Bunge la Uturuki Mheshimiwa Mehmet Ali Sahin.

Rais Kikwete pia atakutana na kufanya mazungumzo na Umoja wa Wafanyabiashara wa Uturuki na baadaye kukutana na mabalozi wa Nchi za Afrika waliopo Uturuki na baadaye jioni hii Rais Kiwete na ujumbe wake watahudhuria dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa kwa heshima yake na mwenyeji wake.



[ Read More ]

Ajiua baada ya kumchinja mkewe kwa wivu

MKAZI wa Kitefu wilayani Arumeru mkoani hapa, George Lukas (27), anatuhumiwa kumuua mkewe kwa kumchinja na kisu na kisha kuacha ujumbe mzito, kabla naye kujiua kwa sumu kutokana na wivu wa mapenzi.

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Basilio Matei alisema tukio la kuuawa kwa mke huyo, Asumin Hussein (36), limetokea juzi saa 12 jioni katika Kitongoji cha Kitefu, Maroroni wilayani Arumeru.

Akielezea chanzo cha tukio hilo, Kamanda Matei alisema wanandoa hao wamekuwa na ugomvi wa mara kwa mara, huku mume akimtuhumu mkewe kuwa sio mwaminifu kwani amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume mwingine, na kwamba amewahi kutoa ujauzito wake ili aolewe na mwanamume mwingine.

Alisema siku ya tukio, mwanamume huyo alifika nyumbani na kuanza kudai ujauzito wake kutokana na majibizano, kulitokea ugomvi wa kutoelewana, na kusababisha mume kuchukua kisu na kumchinja mkewe, na kusababisha kifo cha mwanamke huyo.

Baada ya tukio hilo, Kamanda alisema Lukas alichukua karatasi na kuandika ujumbe kabla ya kujiua kwa sumu, ambayo haikufahamika.

Polisi baada ya kupata taarifa, walifika eneo la tukio na kukuta karatasi yenye ujumbe uliosomeka kuwa “nimeamua kumuua mke wangu kwa sababu ametoa mimba yangu na ana uhusiano na mwanamume mwingine.’’

Katika tukio jingine, Lembrisi Taiko (25), mkazi wa Sanawari Moivo katika Manispaa ya Arusha, ameuawa kwa kukatwakatwa na panga na wananchi baada ya kujeruhi kwa panga.

Kamanda Matei alisema tukio hilo limetokea juzi saa 4:30 usiku baada ya Taiko kukutwa akimshambulia kwa panga, Saimoni Lizer (45) na kumjeruhi vibaya kwa sababu ambazo hazikufahamika.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru kwa uchunguzi zaidi.
[ Read More ]

Mtoto aliyenusurika mauaji Musoma asimulia alivyookoka

MTOTO wa miaka minne aliyenusurika katika mauaji ya watu 17 wa familia tatu za ukoo mmoja katika eneo la Buhare, nje ya Manispaa ya Musoma, mkoani Mare, ameeleza namna alivyojiokoa dhidi ya wauaji kwa kuingia uvunguni.

Kituo cha Redio Clouds jana kilirusha sauti ya mtoto huyo (jina lake limehifadhiwa) akijieleza kwamba alifanikiwa kuingia uvunguni mwa kitanda mara baada ya wahalifu hao kuanza kuwakata kwa mapanga ndugu zake.

Mtoto huyo ambaye kwa mujibu wa mwandishi wa kituo hicho alionekana kisaikolojia kuathirika kutokana na tukio hilo, alisikika akisema hakuweza kuwatambua wavamizi kutokana na jinsi walivyojifunika makoti meusi.

Akielezea walivyoonekana, mtoto huyo ambaye kwa mujibu wa mahojiano redioni alikuwa amefuatana na watu wazima, akiwamo kiongozi wa ukoo, alidai kuwa aliwaona watu wanne waliokuwa na makoti meusi na viatu alivyovitaja kwamba vinafanana na vya kuchezea mpira.

Alisema aliwasikia wakiwataka wanafamilia hao kutoa fedha na kuwaambia wasipotoa, watawaua.

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Enos Mfuru, wakati wa maziko ya miili ya watu waliouawa kwenye tukio hilo ambalo kati ya marehemu 17, kati yao, 11 ni watoto wenye umri wa kati ya miezi 11 na miaka 13 wakiwamo wazazi wake, aliahidi kwamba Serikali itamhudumia mtoto huyo.

Mfuru alisema mtoto huyo atasomeshwa na Serikali. Naye Mbunge wa Musoma Vijijini, Vedastus Mathayo (CCM), aliahidi kumsaidia.

Mfuru alisema Serikali itahakikisha inagharimia matibabu kwa majeruhi wa tukio hilo waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mara mjini Musoma. Maiti hao 17 walizikwa juzi katika tukio lililohudhuriwa na mamia ya watu.

Taarifa zinasema mauaji hayo yalifanyika kutokana na kinachosadikiwa kuwa ni kulipiza kisasi. Polisi katika taarifa yake ya juzi, ilisema watu watano walikuwa wamekamatwa wakihojiwa juu ya tukio hilo.

Miili 16 ilizikwa katika kijiji cha Mgaranjabo nje kidogo ya Musoma na aliyekuwa mwanafunzi wa sekondari ya Mkirira, Joseph Sofareti, alisafirishwa kwenda kijijini kwao Kome, Musoma Vijijini baada ya heshima za mwisho kutolewa.
[ Read More ]

Aanguka toka ghorofa ya tisa

FUNDI ujenzi aliyefahamika kwa jina moja la Ally, amekufa baada ya kuanguka kutoka ghorofa ya tisa wakasti akiwa katika shughuli za ujenzi katika ghorofa hiyo.

Fundi huyo alikuwa katika ya nyumba ya Shubas Patel iliyokuwa na ghorofa 12 na alianguka wakati akiwa kazini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, amesema ajali hiyo ilitokea jana, saa 10 jioni, Mtaa wa Sewa na Zanaki Ilala jijini Dar es Salaam.

Alisema fundi huyo, akiwa na wenzake wakiendelea na kazi kwenye ghorofa ya tisa, ghafla alidondoka hadi ghorofa ya tatu ambapo alinasa kwenye kizuizi cha mabati.

Alisema alipata majeraha kwenye paji la uso pamoja na kuvunjika mkono wake wa kushoto.

Hata hivyo wenzake walimkimbiza Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu na alikufa muda mfupi baada ya kufikishwa hospitalini hapo.


SOURCE;NIFAHAMISHE.COM
[ Read More ]

Mstaafu JWTZ mbaroni kwa tuhuma za kumuua mkewe

ASKARI mstaafu wa Jeshi la la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Matiko Ng'eng'e (55) anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumuua mkewe kwa kisu.

Ng'eng'e ambaye alikuwa sanjenti wa jeshi hilo anadaiwa kufanya hivyo saa 11:00 alfajiri ya jana nyumbani kwake Ukonga Mazizini, jijini Dar es Salaam.

Habari ambazo Mwananchi imezipata na kuthibitishwa na Polisi zilisema mauaji hayo yalifuatia mgogoro wa shamba ambalo mtuhumiwa alikuwa ashinikiza liuzwe huku mkewe akipinga vikali mpango huo.

Akisimulia mkasa huo nyumbani kwao, mtoto wa mtuhumiwa huyo, Joyce Matiko (22) alidai kuwa baba yake ana wake wawili wa ndoa na kwamba marehemu alikuwa ni mke mdogo.

Kwa mujibu wa Joyce, mke mkubwa wa baba yake anaishi Banana.

Alisema hata hivyo familia hizo zimekuwa katika mgogoro wa muda mrefu kuhusu eneo ambalo mke mdogo na watoto wake wamekuwa wakiishi na kwamba mgogoro huo ulitokana na baba yao kutaka eneo liuzwe ili apate fedha za kusafirisha familia kwenda kijijini.

"Muda mfupi kabla ya mauaji ya mama yetu, baba alituita watoto wote watano pamoja na mama na kutukanya tusithubutu kuuza eneo tunaloishi hata kama itatokea yeye amekufa.

Tulishangazwa sana baba kutuita na kutukanya eti tusithubutu kuuza eneo hilo, wakati yeye ndiye kinara wa kutafuta madalali kwa siri ili afanikishe zoezi hilo,"alisisitiza mtoto huyo.

Alisema mara baada ya kikao hicho, baba yao aliwataka warudi ndani wakalale na kwamba walifanya hivyo.

Mtoto huyo alisema ilipofika saa 9:30 usiku alisikia kelele za mama yao akiomba msaada kwamba anakufa na kuomba asaidiwe jambo lilowashtua mno.

Alisema baada ya kusikia kelele hizo waliamua kutoka na kumkuta mama yao akiwa amelala chini huku damu zikiwa zinamtoka kwa wingi mwilini.

"Tulimkuta mama akiwa amelala chini katika dimbwi la damu, lakini baba hakuwepo alikuwa amejifungia chumbani, tulipiga kelele za kuomba msaada na muda mfupi tu majirani walifika na kutusaidia kumtoa kabla polisi kufika," alisema.

Alisema baada ya polisi kufika walimchukua mtuhumiwa (baba yao) na mama yao ambaye kwa wakati huo alikuwa ameshapoteza maisha.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile, alisema polisi wanamshikilia mtuhumiwa huyo katika Kituo cha Polisi cha Staki Shari, wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Kamanda Shilogile alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Amana, kwa uchunguzi na kwamba upelelezi ukikamilka mtuhumiwa atafikishwa mahakamani mara moja.

[ Read More ]

GIZA ZANZIBAR LASABABISHA NDEGE YA NAHODHA KUKWAMA KUTUA

Ndege ya Serikali ikiwa imembeba Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha, imeshindwa kutua katika Uwanja wa Kimataifa wa Zanzibar kutokana na giza baada ya jenereta ya kufua umeme wa dharura kuharibika.

Waziri Kiongozi alikuwa akitokea mkoani Dodoma kuhudhuria kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM akiwa amefuatana na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Zanzibar, Shawana Buheit Hassan ambaye pia ni mjumbe wa NEC.

Taarifa zilizopatikana zimeeleza kwamba ndege hiyo iliondoka juzi saa 12:00 jioni mjini Dodoma na ilitarajia kutua saa 1:00 usiku katika Uwanja wa Kimataifa wa Ndege Zanzibar.

Hata hivyo, kutokana na uwanja huo kuwa gizani, ndege hiyo ilizunguka mara kadhaa katika anga ya Zanzibar na baadaye kwenda kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Meneja wa Mamlaka ya Usalama wa Usafiri wa Anga Zanzibar, Said Sumri, alithibitisha kuwa ndege hiyo ilishindwa kutua Zanzibar ikiwa na wajumbe wa NEC.

Hata hivyo, Sumari hakutaka kuingia kwa undani zaidi juu ya suala hilo kwa madai kwamba si msemaji.

Lakini vyanzo vya habari katika tukio hilo vilieleza kwamba ndege hiyo ililazimika kuzunguka katika anga ya Zanzibar na baadaye kurejea Dar es Salaam na kutua katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

“Tulilazimika kulala Dar es Salaam baada ya ndege yetu kushindwa kutua kutokana na tatizo la giza kufuatia jenereta ya uwanja kuharibika,” chanzo kimoja cha habari kilikaririwa kikisema.

Hata hivyo, abiria wote waliokuwemo katika ndege hiyo baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam, walilazimika kujihudumia gharama za hoteli na kulazimika kusafiri Zanzibar siku iliyofuata na kuwasili Zanzibar saa 4:00 asubuhi jana.

Baadhi ya viongozi waliokuwemo ndani ya ndege hiyo ni wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Salmin Awadh Salmin (Magomeni), Ali Suleiman Ali (Kwahani), Thuwaiba Kisasi (Viti Maalum), Zainab Shomari (NEC), Issa Ahmed Othman (NEC) na wasaidizi kadhaa wa Waziri Kiongozi.

Lakini Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege Zanzibar, Malik Mohammed Hanif, alisema ndege hiyo ilishindwa kutua Zanzibar kwa vile uwanja wa ndege upo katika matengenezo.

Alisema tangu kuanza matengenezo katika uwanja huo, umekuwa ukifungwa kuanzia saa 1:00 usiku ili kuweka mazingira ya utulivu wakati mafundi wakitekeleza majukumu yao.

“Ndege ilishindwa kutua kutokana na matengenezo yanayoendelea katika uwanja huo na sio kweli kama jenereta liliharibika ghafla," alisema Mkurugenzi huyo.

Zanzibar haina huduma za umeme tangu Desemba 10, mwaka jana na kuathiri sekta za kiuchumi na kijamii, baada ya waya unaopokea umeme kutoka Tanzania Bara kulipuka katika kituo cha Fumba Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.

Kutokana na tatizo hilo, taasisi mbalimbali zimekuwa zikitumia umeme wa dharura wa majenereta, ikiwemo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar ambao hivi sasa upo katika matengenezo makubwa yanayofanywa na Kampuni ya Sogea Satom ya nchini Ufaransa.

Uwanja huo wa ndege unatarajiwa kuongezwa urefu kutoka mita 2,662 hadi 3,022 na mradi huo unatarajiwa kukamilika Agosti, mwaka huu.
[ Read More ]

NGUZA VIKING NA MWANAE PAPII WAFUNGWA MAISHA.WAWILI WAACHIWA HURU

HUKUMU IMETOLEWA! Papii Kocha na Baba yake, Babu Seya wameonekana na hatia hivyo wataendelea kukaa jela for the rest of your lives!! Wakati wawili hao wakiendelea kusota, watoto wake wawili Francis Nguza na Mbangu Nguza wameachiwa huru baada ya kuonekana hawakuwa na hatia.
















[ Read More ]

Matokeo Ya Kidato Cha Nne.

Matokeo ya Kidato cha nne 2009 yamewekwa hadharani leo huku takwimu zikionesha kuwa kiwango cha ufaulu kwa kidato cha nne yameshuka na yale ya mtihani wa maarifa(QT) kiwango kikiongezeka kwa asilimia 3.9 ukilinganisha na mwaka 2008.

Akitangaza matokeo hayo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa, Dk Joyce Ndalichako (pichani) amepasha, mwaka 2009 ufauli kwa watahiniwa wa shule ni asilimia 72.51 ya watahiniwa 248,336 ikiwa imeshuka kwa tofauti ya asilimia 11.18 ukilinganisha na mwaka 2008 ambayo ilikuwa asilimia 83.69 na wale wa kujitengemea ni asilimia 54.12 ya watahiniwa 91,589 ikiwa imeshuka kwa asilimia 4.89 ya asilimia 59.01 ya mwaka 2008.

Kati ya watahiniwa 173, 323 waliofaulu, wasichana ni 74,696 (asilimia 67.59) na wavulana ni 98,627 kwa upande wa shule wakati kwa watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu ni wasichana 25,044 na wavulana 24,433.

Dk. Ndalichako ametaja orodha ya wanafunzi wanafunzi bora 2009, ikiongozwa na msichana Imaculate Mosha wa Marian Girls akifuatwa na Gwamaka Njobelo wa Mzumbe.

Namba 3- Wolfgang Seiya wa Majengo ya Kilimanjaro 4- ni Vanessa Chilunda, 5 ni Faith Assenga na 6 ni Doreen Philbert wote wa Marian Girls 7 ni Zahra Meghji wa Usagara na 8 ni John Kimbari wa St. James Seminali, 9 ni Said Abdallh na10 ni Evans Lwanga wote wa Feza Boys.
Dk. Ndalichako alizitaja shule kumi bora zenye watahiniwa zaidi ya 35 ikiongozwa na Marian Girls ya Pwani ambayo mwaka 2008 ilikuwa ya pili na inafuatiwa na St. James Seminary ya Kilimanjaro, Don Bosco seminary ya Iringa ambayo mwaka 2008 ilikuwa nafasi ya nane imepanda hadi nafasi ya tatu.

Alisema sekondari ya wasichana ya St. Francis ya Mbeya ambayo mwaka 2008 ilishika nafasi ya kwanza imeshika nafasi ya nne na kufuatiwa na St. Mar’y Junior Seminary ya Pwani iliyonafasi ya tano huku Uru Seminary ya Kilimanjalo imeshuka nafasi tatu na kushika nafasi ya sita wakati sekondari ya wanaume ya Feza imepanda nafasi moja hadi nafasi ya saba.

Dk. Ndalichako alisema shule zilizoshika nafasi ya nane tisa na 10 ni Anwarite Girls, Maua Seminary na St Mary Goreti zote za Kilimanjalo.
Kwa upande wa shule zenye watahiniwa chini ya 35, Dk Ndaliachoka alisema kundi hilo linaongozwa na shule ya wasichana wa Feza ya Dar es Salaam na kufuatiwa na Mafinga Seminary ya Iringa, St. Joseph-kilocha Seminari ya Kilimanjaro iliyo nafasi ya tatu na nafasi ya nne ikishikwa na Queen of Apostle-Ushirombo ya Shinyanga.

Zingine kuwa ni Dungunyi Seminari ya Singida iliyonafasi ya tano na kufuatiwa na Rubya Seminary ya Kagera, Sengerema Seminary ya Mwanza iko nafasi ya saba na kufuatiwa na sekondari ya wasichana ya Bethelsabs ya Iringa huku Thomas More Machrina ya Dar es Salaam ikishika nafasi ya tinsa na Hellen’s pia ya Dar ikiwa nafasi ya 10.

Dk Ndaliachoka alizitaja shule kumi za mwisho kwa watahiniwa 35 au zaidi kuanzia iliyoshika mkia kuwa ni Busi ya Dodoma, Milola ya Lindi, Misima ya Tanga, Kiwere ya Tabora, Potwe da ya Tanga, Masanze ya Morogoro, Mandawa ya Lindi, Msata ya Pwani, Chekelei ya Tanga na Jangalo ya Dodoma.

Alizitaja shule kumi za mwisho zenye watahiniwa chini ya 35 kuwa ni Kizara ya Tanga, Mungumbi ya Lindi, Songolo ya Dodoma, Nakuhukahuka na Marambo za Lindi, Dole ya Zanzibar, Ruponda na Mpunyule za Lindi, Ruvuma ya Singida na Viziwi Njombe ya Iringa.

“ Hapa sina mchanganuo wa ufaulu wa somo moja moja, ila somo la Civis watahaniwa wamefaulu sana wakati hisabati imeendelea kuwapiga chenga.”

Hata hivyo, Dk. Ndalichako alisema baraza hilo limesitisha matokeo ya watahiniwa 7, 242 ambao hawajalipa ada ya mtihani na wamepewa muda wa miaka mwili kulipa na kinyume cha hapo matokeo hayo yatafutwa.

“ Pia tumesitisha matokeo ya watahiniwa wawili wa kujitegemea kutokana na kuwa na sifa zao kufanana, nah ii tumeigundua dakika za mwisho, majibu yao yatatole hadi hapo watakapoleta uthibitisho. Haiwezekani kufanana majina, wamezaliwa mwaka mmoja na sifa zo za kidato cha pili zinafanana na tumeshawaandikia matokeo.”

Dk. Ndalichako alisema kuwa na hata wanafunzi wawili wakafanana kila kitu, ikiwa ni majina, tarehe na umri wa kuzaliwa,” alisema.
Baraza hilo pia limefuta matokeo ya watahiniwa 405 na watano wa mtihani maarifa(QT).

“ Baraza limegundua udanganyifu wa watahiniwa kuwa na skripti zenye miandiko tofauti au kuwa na miandiko tofauti katika skripiti ya somo moja na hili tumeshirikiana na taasisi ya kubaini miandiko.

“ Pia kunawale ambao wamekamatwa na ‘notes, na wale waliokutwa chooni wakisoma, waliokutwa na simu kwenye chumba cha mtihani. Lakini wapo ambao walibainika na mfano usio wa kawaida wa majawabu, kwa mfano kuna wengi wamefanana kila kitu labda badala ya kuandika ‘themselves’ wanaandika ‘them selves’.”

Dk. Ndalichako aliongeza kuwa: “ Pia kunawengi ambao swali la kemia ambao lilitakiwa kueleza jinsi ya kutenganisha kerosene na water wao wajibu jinsi ya kutenganisha alcohol na water, lakini kulikuwa na udanganyifu hatari sana wa watahiniwa kubadilisha namba za wenzao.”
Alisema kuwa watahiniwa 53 pia wamefutiwa kutokana na kutokuwa na sifa kutoka shule za Mkwese sekondari(25), Ruruma (15), Thaqalaini(6), Bishop Kisanji(5), St Vicent na Edmund Rice Sinon kila moja mmoja.

Dk Ndalichako alisema mwanafunzi mmoja wa shule ya sekondari ya Kadoto amefutiwa matokeo kwa kuandika matusi kwenye skripti ya somo la baiolojia ikiwa ni kinyme na kifungu cha 5(13) cha kanuni za mitihani.
Pia alisema kuwa Baraza liemevifutia usajili wa watahiniwa wa kujitegemea kwa Sinza Iteba na Dar es salaam Prime vya Dar es salaam kutokana na kuzidiwa uwezo wa kuwachukua watahiniwa wengi.

Chanzo cha habari hii www.habarileo.co.tz
[ Read More ]

Mamia Wamzika Imran Mtui Mjini Moshi

Jeneza lenye mwili wa hayati Imran kijana aliyeuawa India hivi karibuni likitoka msikitini kuelekea katika makaburi ya Njoro mjini Moshi jana. Marehemu Imran alizikwa bila kuwa na kichwa. Picha na mdau Dixon Busagaga wa Moshi.
Mtanzania aliyeuawa India azikwa bila kichwa
Na Charles Ndagulla na
Dixson Busagaga, Moshi
VILIO, simanzi na majonzi jana vilitawala mazishi ya Mtanzania Imran Mtui (31) aliyeuawa kikatili nchini India hivi karibuni, katika mazishi yaliyofanyika makaburi ya Njoro Manispaa ya Moshi.

Mwili wa marehemu huo ulizikwa bila kichwa huku pia ukidaiwa kuwa na majeraha mengi mwilini kuanzia miguuni na kwenye paja lake karibu na kiuno huku kiwiko cha mkono wa kulia nacho kikidaiwa kunyofolewa.

Mwili huo uliwasili mjini moshi usiku wa kuamkia jana baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es salaam, ukitokea nchini India huku gharama zote za kuusafirisha zikibebwa na serikali ya Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kabla ya mazishi, kaka wa marehemu, Maliki Mtui, alisema kuwa wameshtushwa na kifo cha ndugu yao hasa kutokana na marehemu kutokuwa na historia ya ugomvi.

Kwa mujibu wa kaka huyo, mwili huo pia umeonekana kuwa na alama za kamba kwenye mikono yake hali ambayo inaonyesha marehemu kabla ya kuuawa alifungwa kamba ili asiweze kujitetea.

Tukio hilo la kusikitisha linadaiwa kutokea katika mji wa Bangalore nchini India ambako marehemu alikuwa tayari amehitimu masomo yake ya biashara na utawala (Business Administration) na tayari alikuwa akijiandaa kurejea nyumbani.

Kaka huyo wa marehemu aliwaambia waandishi wa habari kuwa mdogo wake huyo alipatwa na mkasa huo akiwa njiani kuelekea mjini ambako rafiki yake wa kike ambaye pia ni Mtanzania aishie visiwani Zanzibar alikuwa akisoma.

“Niliwasiliana naye siku ya tukio kabla hajapatwa na mauti haya nikamuuliza anatarajia kurudi lini nyumbani akanijibu angerudi mapema na rafiki yake alikuwa akimsubiri lakini hakuweza kutokea” alisema.

Pamoja na kuishukuru serikali ya Tanzania kugharamia kuusafirisha mwili wa marehemu mdogo wake, Mtui ameitaka pia serikali kuwathamini raia wake walioko nje ya nchi kwa kufuatilia taarifa zao pindi wanapokumbwa na matukio kama hayo ya kuuawa kwa mdogo wake.

Naye msemaji wa familia ya marehemu Mtui ambaye pia ni shekhe wa msikiti wa Majengo, Shekhe Said Khatibu, alisema kuwa serikali haiwathamini raia wake walioko nje na ndiyo maana serikali haijatoa tamko rasmi kulaani mauaji hayo.

Shekhe huyo pia alisema katika kile kinachoonyesha kuwa idara za serikali zimelala, serikali imeshindwa kutuma hata mwakilishi kwenye mazishi hayo ambayo tukio lake lina utata.

Aidha, alipinga taarifa zote zilizotolewa na madaktari nchini India kwamba marehemu alifariki dunia kwa ajali ya treni na kusisitiza kuwa taarifa hizo sio za kweli.
                                             

source:michuzi.                                                                              







[ Read More ]

HABARI YA MSIBA..


Binti wa Marehemu Rashid Kawawa , Habiba Kawawa amefariki  jioni ya Leo siku chache kabla ya arobaini ya baba yake katika hospitali Ya Taifa ya Muhimbili majira ya saa kumi na Mbili Jioni….
Msiba upo nyumbani kwa Marehemu Habiba huko Tegeta
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi..Amin..
[ Read More ]

Mwili Wa Imran Mtui Wawasili Dar Leo, Wasafirishwa Kuelekea Moshi Kwa Mazishi



Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Imran Mtui likiingizwa kwenye gari tayari kwa kusafiri kwenda Moshi.
Dada wa marehemu na waombolezaji wakilia kwa uchungu wakati jeneza likiingizwa kwenye gari tayari kwa kusafirisha mwili kwenda moshi Mjini kwa mazishi. 


Rais Mstaafu wa Chama cha Wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) Bw. Baraka Kange akizungumza na waandishi wa habara mara wakati wakisubiri kupokea mwili wa Mwanafunzi aliyeuwa nchini India katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo. Kushoto kwake ni Babu wa marehemu, Balozi Abubakar Abrahim.

source:michuzi.
[ Read More ]

MOTHER, DAUGHTER, SON COMMIT SUICIDE


  In a heart-rending incident, three members of a family committed suicide by consuming poison in Bogadi near here last night.
The deceased have been identified as Mangalamma (48), wife of Shivanna, her son Bhyrava (28) and daughter Lakshmi (22), wife of Swamy.
They allegedly ended their lives in their house behind Government School on Bogadi. Lakshmi is survived by two sons Preetham, 7, and Varun, 3. Her husband Swamy is said to be the main reason behind the trio taking the extreme step. The incident came to light when a neighbour Anitha reportedly went to the house of Mangalamma at about 6 am today.
Preetham opened the door for Anitha who found the three persons lying dead. She then informed neighbours who in turn alerted the Police.
Lakshmi, who was married to Swamy 7 years ago, was being constantly ill-treated by her husband who had turned into an alcoholic two years ago. Swamy, who owns a chicken stall in Bharathi Nagar, is said to have been assaulting Lakshmi and two children almost everyday. Attempts to reconcile the couple went in vain, according to neighbours.
Lakshmi, apparently fed up with her husband's ill-treatment, is said to have left for her parents' house along with her two children on Jan. 29.
Her father Shivanna, also said to be an alcoholic and totally non-chalant about his family affairs, was reportedly sleeping outside the house when the family members consumed poison last night.
[ Read More ]

Wanne wa familia moja wateketea kwa moto wa jenereta

WATU wanne wa familia moja wamekufa kwa moto baada ya jenereta lililokuwa limefungiwa katika moja ya chumba ndani ya nyumba hiyo kupasuka na kuwaka moto
Tukio hilo la kusikitisha limetokea usiku wa kuamka leo, huko maeneo ya Kibwenzini Zanzibar wakati watu hao wakiwa wamelala ndani humo.

Ilidaiwa kuwa jenereta hilo liliripuka majira ya saa 11 za alfajiri na kuzua moto uliosababisha vifo hivyo.

Ilidaiwa kuwa familia hiyo ilinunua jenereta hilo kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kutokana na kukosekana kwa umeme visiwani Zanzibar.

Katika ajali hiyo waliopoteza maisha walitajwa kuwa ni Safia Shabani, Ahmed Shaban na mtoto ambaye hakuweza kupatikana jina lake, akiwemo na msichana wa kazi Sikudhani Nasorro.

Hadi habari hii inarushwa hewani, kamanda wa Polisi wa wilaya husika hakuweza kupatikana kuongelea juu ya tukio hilo juhudi zaidi zinafanyika ili kuweza kupata maelezo yake.
[ Read More ]

RIPOTI RASMI YA KIFO CHA BWANA “IMRAN MTUI”

Mnamo siku ya jumapili ya tarehe 31/01/2010, majira ya 9:30 alasiri uongozi wa wanafunzi waishio Bangalore India (TASABA) tulipokea taarifa ya kusikitisha kutoka kwa ndugu wa karibu wa marehemu kuwa kaka yetu mpendwa IMRAN MTUI kuwa tena duniani.
Mnamo majira ya saa tatu usiku mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) Mh. Fidelis Msomekela aliwasiliana na ubalozi wa Tanzania New Delhi kuwafahamisha juu ya msiba wa mpendwa kaka yetu marehemu IMRAN MTUI.
Tarehe 1/02/2010 ofisi ya Ubalozi ilituma mwakilishi wake anayesimamia maswala ya wanafunzi India ili kusaidiana na serikali ya wanafunzi waishio Bangalore kujua chanzo zaidi juu ya kifo cha marehemu Imran Mtui.
Tarehe 2/01/2010, Mwakilishi wa ubalozi pamoja a mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi Bangalore (TASABA) walifika katika kituo cha polisi kiitwacho ‘Cantonment Railway Police’ ili kupata ripoti kamili juu ya chanzo cha kifo cha marehu Imran Mtui. Ripoti ya polisi ilieleza kuwa mnamo majira ya saa 3:35 asubuhi mkaguzi wa reli alitoa taarifa kwa msismamizi mkuu wa reli kuwa ameona mwili wa marehemu IMRAN MTUI pembeni ya reli K.M No. 339/700-800 karibu na KRISHNARAJAPURAM LOCO SHED (MAHADEVAPUR, BANGALORE).
Taarifa za awali za polisi zinaeleza kuwa chanzo cha kifo cha marehemu Imran Mtui ni Ajali ya kawaida, uchunguzi zaidi unaendelea ili kujua chanzo kamili cha kifo cha ndugu yetu marehemu IMRAN MTUI.
Taratibu zote za kusafirisha mwili wa marehemu IMRAN MTUI zimekamilika, kesho (3/01/2010) majira ya jioni, mwili wa marehemu IMRAN MTUI utasafirishwa kuelekea nyumbani Tanzania kupitia kampuni la shirika la ndege la Emirates mpaka Dar es Salaam na baadae kusfirishwa kuelekea Killimanjaro kwa mazishi.
Uongozi wa Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) unatoa shukrani za dhati kwa ubalozi wa Tanzania New Delhi kwa ushirikiano na msaada mkubwa walioutoa ili kufanikisha taratibu zote za kisheria na kutoa usafiri wa kumsafirisha ndugu yetu maarehemu IMRAN MTUI mpaka nyumbani kwao Kilimanjaro. Pia uongozi wa Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA), unatoa shukrani za dhati kwa wale wote walioungana na familia ya ndugu yetu mpendwa marehemu IMRAN MTUI kwa hali na mali.
Jumuiya ya wanafunzi waishio Bangalore (TASABA),unaomba wanajumuiya wote kuwa watulivu na kuacha kutoa habari za kizushi juu ya kifo cha marehemu IMRAN MTUI kwa kuwa uchunguzi zaidi bado unaendelea na mpaka sasa hakuna mtuhumiwa yoyote Yule anaye shutumiwa au kushikiliwa na polisi juu ya kifo hicho.
Uongozi wa wanafunzi waishio Bangalore (TASABA) unatoa pole kwa familia ya marehemu IMRAN MTUI. Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya ndugu yetu mpendwa marehemu IMRAN MTUI. Amin

Fidelis Msomekela
President – TASABA
[ Read More ]

SURA ZA HUZUNI NA MAJONZI - BANGALORE-INDIA.

Baadhi ya wanafunzi waliokusanyika katika msiba huo wakiwa na nyuso za huzuni.


Sura za Huzuni na Majonzi kwa wanafunzi wa India waliopo Bangalore na Wenzao wa Mysore baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Muwakilishi wa Ubalozi Mr. Amon Mwamunenge juu ya maendeleo ya uchunguzi na taratibu za kusafirisha mwili wa Marehemu Imran Mtui kurudi nyumbani kwa ajili ya mapumziko ya amani.
[ Read More ]

Mwanafunzi Mtanzania, Imran Mtui auawa India



Habari zilizopo katika blogu ya Watanzania waishio Bangalore (TASABA), pia katika mtandao wa Twitter zinathibitisha kuwa, mwanafunzi wa Kitanzania, Imran Mtui (31) aliyekuwa anasoma katika Chuo kishiriki Cha Chuo Kikuu cha Bangalore nchini India, amekutwa amekufa huku mwili wake ukiwa hauna kichwa.
Taarifa zinasema kuwa mwili huo ulikutwa kando kando ya reli katika eneo la Shivajinagar katika mji wa Bangalore ukiwa hauna kichwa huku mguu mmoja ukiwa umejeruhiwa vibaya.Balozi wa Tanzania nchini India, John Kijazi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

"Mimi nilipata taarifa hizo juzi jioni ambapo jana tulifanya kikao na wenzangu na kumtuma Ofisa wetu Mzee Amon Mwamanenge na mwanasheria wetu wamekwenda huko kupata undani wa tukio hilo," alisema Balozi Kijazi.

Alisema kuwa kwa sasa hawezi kutoa picha kamili lakini mwili wa kijana huyo umekutwa ukiwa hauna kichwa na mguu umebondeka. Kijana huyo aliyefariki alikuwa amemaliza Shahada ya Usimamizi wa Biashara (BBM) na alitambulika kwa jina la Imran Mtui. Aliwahi kuwa Mtunza Fedha wa Chama Cha Wanafunzi wa Kitanzania Waishio Bangalore (TASABA).

Habari hizi zimedhibitishwa na mdogo wa marehemu, Issa Mtui, kwa njia ya simu akiwa safarini kuelekea Marangu, Moshi. Alieleza kuwa mwili wa marehemu unategemewa kuwasili nchini Alhamisi ya wiki hii kwa ajili ya taratibu za mazishi ambayo yatafanyikia Marangu.
Imrani ni wa pili kuzaliwa kati ya watoto wanne kwenye familia hiyo. Inadaiwa kuwa kabla mauti haijamkuta alitarajiwa jana angekuwa amerejea nchini baada ya kuwa amechukua vyeti vyake vya masomo ambavyo alikuwa akivisubiri baada ya kuhitimu masomo yake.

Polisi nchini India wanaendelea na jitihada za kuwatafuta watuhumiwa wa tukio hilo.
[ Read More ]

TANGAZO..

TAARIFA KAMILI YA KAMATI YA KUFUATILIA MSIBA WA KAKA YETU IMRAN MTUI CHINI RAIS WA TASABA NA MUWAKILISHI WA UBALOZI MR.AMON MWAMANENGE ITATOLEWA BAADAE USIKU HUU.TAARIFA ITAHUSISHA TAARIFA ZILIZOTOLEWA NA POLISI,HOSPITALI NA KAMPUNI YA RELI KUHUSU KIFO CHA KAKA YETU IMRAN MTUI.TUNAOMBA RADHI KWA KUCHELEWESHWA KWA TAARIFA KWANI TULIKUA HATUWEZI KUZUNGUMZA LOLOTE MPAKA TUPATE RIPOTI RASMI YA KAMATI HII AMBAYO IMECHELEWA KUTOKANA NA SABABU ZILIZO NJE YA UWEZO WAO.TUNAKUMBUSHA YA KWAMBA TUSINGEWEZA KUANDIKA TETESI TULIZO SIKIA KUHUSIANA NA MSIBA HUU KWANI ZILIKUA NI TAARIFA ZISIZO RASMI.

TASABA SPOKESMAN
JUMANNE MTAMBALIKE
[ Read More ]

TAARIFA YA MSIBA




INNA LILAHI WA INNA ILAIHI RAJI'UNA!.


Tunasikitika kutanga kifo cha mpendwa wetu wanafunzi mwenzetu.Imran Mtui.kilichotokea huko Bangalore India kwa ajali. .Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda Tanzania kwa ajili ya mazishi zinaendelea.

fromcoast inatoa pole kwa Familia,ndugu, jamaa na marafiki wote.Mungu awape uvumilivu hasa katika kipindi hichi kigumu..

habari zaidi zitawajia hapo baadae

Sisi tulimpenda lakini Mungu amempenda zaidi..
mungu ailaze roho ya marehemu pahala pema peponi.

AMIN.


[ Read More ]