Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Mafao ya mwalimu aliyefariki yakwamishwa hadi marehemu ajaze fomu.

MJANE Specioza Kamala ameendelea kusotea mafao ya mume wake aliyefariki miaka 13 iliyopita, huku mwaka huu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikimwandikia marehemu barua ya kumtaka ajaze fomu ya kulipwa mapunjo ya mshahara baada ya kupanda daraja.

Marehemu Richard Mutakulemberwa aliyekuwa mwalimu katika shule ya sekondari Kahororo iliyopo Manispaa ya Bukoba, alikutwa na mauti August,19 mwaka 1998 wakati akipata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na T.Kagumisa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ambayo Fikra Pevu ina nakala yake, pamoja na mambo mengine inamtaka marehemu kujaza fomu kutokana na utaratibu mpya wa malipo ya malimbikizo.

Pia barua hiyo ya Januari 4, 2012 iliyotumwa kupitia shule aliyokuwa akifundisha marehemu ya Kahororo inamtaka kufuata maelekezo kwa mujibu wa barua hiyo ili madai yake yaweze kushughulikiwa.

“Tafadhali mara upatapo barua hii jaza na utume kwa Katibu Mkuu fomu halisi na nakala moja (photocopy), pia ambatanisha barua yenye maelezo sahihi ya madai,nakala ya barua ya kupandishwa na kukubali cheo na ‘salary slip’ ya karibuni,” inaeleza sehemu ya barua hiyo kwenda kwa marehemu.

Pia mbali na barua hiyo kumtakia marehemu ushirikiano mwema katika kukamilisha zoezi hilo, inamkumbusha kuwa nyaraka zote lazima zipite kwa mkuu wake wa kituo na kutumwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Naye mjane wa Marehemu, Specioza Kamala mbali na kusikitishwa na hali hiyo, alisema tangu kufariki kwa mume wake mwaka 1998 ameendelea kufuatilia madai ya mume wake bila mafanikio na hata kufika Wizarani huku akipewa kauli za ahadi.

Alisema kuwa mbali na kuwa alishapata barua hiyo aliyoandikiwa marehemu mume wake, anachokumbuka ni kuwa mme wake alifariki kabla hajalipwa mapunjo ya mshahara baada ya kupandishwa daraja ambayo ameendelea kuyafuatilia bila mafanikio na kuwa mirathi ya marehemu ilishatolewa.

“Alipanda daraja mwaka 1996 na kufariki kabla ya kulipwa mapunjo yake ya mshahara,suala hili nilishawaeleza hata watu wa Utumishi wa Umma kutoka Dar es salaam na kunielekeza niende Wizarani na baada ya kwenda walisema faili lake halipo,” alisema mama huyo ambaye pia ni mwalimu katika moja ya shule za msingi Mkoani Kagera.

Alipoulizwa kama suala hilo liliwahi kufika katika Ofisi za Chama cha Walimu Mkoani hapa, Katibu wake wa Mkoa Aaron Masalu alisema halijafika katika ofisi hiyo huku akilihusisha na mfumo mbovu wa utunzaji wa takwimu za watumishi.

Pia alidai vyombo vinavyomshughulikia mwalimu havina utaratibu mzuri wa mawasiliano na kusema kuwa sasa wakati umefika wa mwalimu kushughulikiwa na chombo kimoja tofauti na ilivyo sasa.

Alisema mbali na kuwa utaratibu uliopo unaweza kuchelewesha malipo ya mhusika au kuyakosa kabisa alidai suluhisho ni kuwa namwajiri mmoja ambapo hivi sasa walimu wanashughulikiwa na Tamisemi,Utumishi wa Umma na Wizara yenyewe.

Imeandikwa na Phinias Bashaya-Kagera
[ Read More ]

Aanguka na Kujifungua nje ya Wodi

MAMA mmoja anaetambulika kwa jina la Mwantatu Kombo mkaazi wa Miembeni ameelezea kusikitishwa kwake kwa kitendo alichofanyiwa na wauguzi wa hospitali ya Mnazimoja wodi ya wazazi wakati alipokwenda kumpeleka jamaa yake kwa ajili ya kujifungua.

Akisimulia mkasa huo Mwantatu alisema kuwa tukio hilo lilitokea wiki iliyopita majira ya saa 9 usiku, ambapo alifika hospitalini hapo kwa lengo la kumpeleka jamaa yake na hatimaye kujifungua nje ya wodi ya wazazi hospitalini hapo.

Alisema alipofika wodini hapo akiwa amefuatana na mjamzito huyo, anaejulikana kwa jina la Fatma Ali Suleiman ambaye alimuomba ampatie msaada wa kumpeleka hospitali, lakini hakupokelewa kutoka na kutokuwa na vifaa.


Alisema kutokana na kutokuwa na vifaa, aliambiwa na wauguzi hao atoke nje na hawatompokea mjamzito huyo pamoja na kuwaeleza kuwa atavilipia baada ya kujifungua kutokana na hali yake.

Pamoja na Mwantatu kudai kuwafahamisha yote hayo kuhusu mzazi wake lakini madaktari hao hawakumsikiliza kilio chake na kumtaka atoke nje yeye na mjamzito wake huku mzazi huyo akiwa na uchugu na tayari kwa kujifungua.

"Wakati nikiwa natoka nje na mjamzito wangu, alianguka mbele ya wodi ya wazazi na kujifungua hapo hapo chini, mara baada ya kujifungua nilirudi kwa wauguzi kuwambia mgonjwa wangu ameshajifungua nje naomba kuomba msaada lakini pia walikataa.

Kwa upande wake Mzazi huyo Fatma Ali alisema kuwa mwanzo wa kupata ujauzito huo alikwenda kupima na kuambiwa atoe shilingi 10,000 kwa ajili ya kununua gamba na hali yake alikuwa hana hata shilingi na ndipo akaondoka na kwenda zake hadi kujifungua kwake.

Kwa upande wake Msaidizi Katibu hospitali ya Mnazimmoja Mohammed Nadi alithibitisha kutokea tukio hilo kwa madaktari hao na alisema kitendo walichokifanya wauguzi kwa kumuacha mzazi kujifungua nje ya wodi si kitendo cha kiungwana.


Akizungumzia kadhia hiyo Katibu wa Hospitali ya Mnazimmoja, Omar Abdalla Ali, aliwashauri wananchi wanapofanyiwa vitendo vya udhalilishaji wawe na utaratibu wa kuripoti kwa ushahidi wa kutosha pamoja na kufika katika vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua za kisheria zaidi.

"Mara baada ya tukio hilo tuliwaandikia barua na kutaka wajieleze lakini hatukuridhika na maelezo yao waliyoyathibitisha kwenye barua yao, hivyo nitawaita kwenye kamati ya maadili wiki ijayo kwa ajili ya kusikiliza pande zote mbili na kulichukulia hatua za kisheria zinazofaa”, alisema Msaidizi huyo.

Aidha aliwataka madaktari kuachana na vitendo vya rushwa ambapo hivi sasa vimeonekana kukithiri kwa kiasi kikubwa na kupelekea kutothamini utu na binadamu.

Barua yenye ripoti kutoka kwa Muuguzi wa Maternity Ward ya Februari 2 mwaka huu, imeeleza kwamba siku ya tarehe saba mwezi huu wauguzi wawili (majina tunayahifadhi) walimpokea mgonjwa vizuri na wamemuweka katika kochi na kabla hawajamchunguza walimtaka atowe vifaa vyake, jamaa zake walijibu hawana na walielekezwa wakanunue hospitali ya Al-Rahma.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa walidai hawana pesa, wakati wanamuelekeza mgonjwa akalale kwenye kitanda, wauguzi hao waliitwa kwenda kumhudumia mgonjwa mwengine mwenye Eclampisia.

Ilieleza taarifa hiyo kuwa walipokuwa wakimshughulikia mgonjwa wa Eclampisia, mama wa jamaa zake walitoka nje na baadae wauguzi walipata taarifa ya mama ameshajifungua walipoulizwa wakunga aliemsaidia mama huyu ni nani, walijibu hawamjui maana wao hawakwenda tena, ilimaliza ripoti hiyo.
[ Read More ]

Kashfa ya Kuvuja Mitihani - Mtihani Mwengine


MAMIA ya vijana wa Zanzibar waliofanya mtihani wa kidato cha nne wanakabiliwa na mtihani mwingine, tena ni mkubwa zaidi kuliko ule walioufanya mwaka jana na hawajui waukabili vipi huu mtihani mpya.

Matokeo yao ya mtihani wa kidato cha nne yamefutwa na kuambiwa juhudi zao zote za kujitayarisha kwa miezi kadha zimekwenda na maji, yaani “Ajwar” (pata potea).

Hivi sasa watoto hawa, wengi wao wakiwa wanatokana na familia za kimasikini, wamebaki wakilalama huku wakiwa na huzuni na hivi sasa wanahangaika huku na kule kama kuku anayetaka kutaga na hakuna dalili za kupata mafanikio.


Watoto hawa wa kimasikini wanaona dunia imewapa mgongo na huko wanakokwenda ni kiza kitupu na hakuna mtu wa kuwaashia taa ya kuona kilipo usoni. Ni unyonge mkubwa.

Ama kweli Waswahili hawakukosea waliposema mnyonge hana haki, lakini tukumbuke walipotutahadharisha kwa kusema; ‘Mnyonge mnyongeni, lakini haki yake mpeni”.

Kwa kweli inasikitisha sana, inahuzunisha na inatisha kuona viongozi wetu wengi wanaliona suala la kufutwa matokeo ya mtihani kama vile ni jambo la kawaida na hawataki kukubali madhara yake kwa vijana wetu waliofutiwa matokeo ya mitihani.

Sishangai hata kidogo na mtazamo wao huu kwa sababu watoto wa hawa wakubwa ambao tumekuwa tukidhani na wengi kuamini watatuonea imani na kuwahurumia watoto wa kimasikini wanasoma nje ya nchi. Matatizo ya elimu tuliyonayo nchini, hayawahusu.

Ukifanya utafiti wa haraka utaona kuwa watoto wa karibu viongozi wote wa serikali na matajiri hawawapeleki watoto wao katika shule za serikali kwa sababu wanaelewa vizuri kwamba huko hakuna elimu ila kupoteza wakati.

Kwanza kuna msongamanao ndani ya madarasa, walimu ni wa kuokoteza na wanafunzi wanatumia muda mwingi kupokea wageni au kutakiwa kwenda kwenye sherehe za kitaifa zisizokwisha.

Baaadhi ya viongozi wa serikali na matajiri, bila ya aibu, wamewapeleka watoto wao katika shule zilizodhaminiwa na washirika wa maendeleo wa nchi za nje kusaidia watoto yatima.

Hii leo ukienda shule ya yatima ya OSS ya Zanzibar utashangaa na kushitushwa kuona zaidi ya asilimia 60 ya wanafunzi si yatima bali ni watoto wa viongozi na wafanyabiashara wakubwa wa nchi hii.

Hii ni aibu na ni dhambi, lakini wenye fedha na vyeo mara nyingi huwa hawajali kwa vile wanaongozwa na jeuri na kibri na si utu na ubinaadamu, imani wema au hisani. Watu hawa hawaoni kuwa wanavyofanya ni vibaya.

Wakati sasa umefika kwa serikali kulitupia macho suala hili kwa kuonyesha imani na huruma kwa watoto wa kimasikini.

Huu mchezo wa kuchezea mitihani na hatimaaye kuathiri zaidi watoto wa kimaskini ni wa hatari na hauna mwisho mwema.

Hivi sasa katika kila pembe ya Unguja na Pemba wazazi na watoto wao wanasikitika na wengine kulia kutokana na kufutwa kwa matokeo ya mithani wa kidato cha nne kwa mamia ya watoto wa kimaskini.

Ukweli ni kwamba Baraza la Mitihani Tanzania limeshindwa kazi yake na wizara zetu za elimu, Bara na visiwani zimeshindwa kuwajibika katika kuhakikisha mitihani haivuji.

Matokeo yake ni kwamba watoto wa kimasikini na wazee wao walioweka matumaini kwamba elimu ingewasaidia kutokana na umaskini (ukweli ni ufukara) na unyonge wa maisha ndio wanaoumia na kuteseka.

Hapa tujiulize ni nani wa kulaumiwa kwa kuvuja mitihani? Ni hawa wanafunzi au kutokuwepo uadilifu na ulinzi wa kutosha hata mitihani ikavuja?

Kilichojitokeza hapa ni kwamba wanaostahiki kulaumiwa na kubeba dhamana ni Baraza la Mitihani kwani ni dhahiri kuwa kazi imewashinda na kwa vile imedhihirika wazi kuwa hawawezi kusimamia mitihani kinachotakiwa ni kujiuzulu.

Lakini lililo muhimu zaidi ni kwa wahusika kuwajibishwa kikazi na kisheria na si kuwaadhibu watoto wa kimaskini.

Hapa nataka nikumbushe kwamba zama za ukoloni nilipokuwa ninafanya mitihani ya darasa la nane na baadaye kidato cha nne hizi habari za kuvuja mitihani na udanganyifu zilikuwa hazisikiki.

Kama wakoloni waliweza kudhibiti mitihani isivuje miaka ile nini kinachopelekea leo kuvuja kwa mitihani iwe jambo la kawaida kama si kutokuwapo uadilifu na kushamiri kwa uhuni?

Tujiulize kulikoni hii leo? Jawabu unayoipata na ambayo ni sahihi kwa mapana na marefu ni kutokuwepo uongozi mzuri katika kusimamia mitihani na uhuni kutawala mwenendo mzima wa kuendesha shughuli za serikali.

Hii ni aibu na fedheha, tena kubwa na wahusika hawastahili kuvumiliwa wala kuonewa huruma. Kama wao hawahurumii watoto wa kimasikini hapana sababu kwa jamii kuwaonea huruma.

Lakini ukichunguza utaona waliohusika na uvujaji wa mitihani wamepoa na hawana wasiwasi kwa vile wana uhakika wa kulindwa kwa sababu za kisiasa.

Si ajabu hivi sasa waliohusika na kuvujisha mitihani wakawa wanapanga namna bora ya kuvujisha mitihani ya mwaka huu ili kujipatia fedha za bure kwa kuwa wanaelewa na kujiamini kuwa hawatawajibishwa kikazi wala kisheria. Kwa watu hawa kuvujisha mitihani ni sehemu ya kazi yao.

Hali hii ni ya hatari na inatisha. Serikali inapaswa kuelewa kwamba uhuni wa kuvujisha mitihani na baadaye kufuta matokeo ya shule kadhaa unawaumiza na kuwadhulumu watoto wa kimasikini ambao walitegemea elimu hapo baadaye ingewakomboa na maisha duni wanayokabiliana nayo hivi sasa.

Katika nchi nyingi zinazoheshimu utawala bora na demokrasia (tofauti na ilivyo Tanzania) panapotokea aibu kama hii ya kuvuja mitihani hatua ya kwanza inayofuata ni kwa viongozi wa juu wa Wizara ya Elimu (Bara na Visiwani) na wale wa Baraza la Mitihani kuachia ngazi kwa vile kazi waliopewa imewashinda.

Lakini huu utamaduni mchafu na unaonuka tulionao wa kulindana kwa maovu tunayoyatenda au kuruhusu wasaidizi wetu kufanya uhuni na wasiwajibishwe utaendelea kutuponza na gharama zake ni kubwa.

Mpaka pale tutapoanza kutoa umuhimu kwa uwajibikaji hizi hadithi za kuvuja mitihani kila mwaka zitaendelea na matokeo yake ni kuendelea kuwaumiza watoto wa kimasikini zitaendea tena kwa kasi zaidi.

Wahusika na uvujaji wa mitihani watasema Tumethubutu na tunaweza na tutaendelea”.

Ni vizuri kama hatuwezi kuwasaidia watoto wa kimaskini tuache kufanya maovu yanayosababisha kuwakandamiza.

Leo mambo haya yananyamaziwa na hapa na pale ndiyo hupigiwa kelele, lakini tukumbuke kama leo suala hili halitazusha balaa historia hapo baadaye itatuhukumu kwa kuwadhulumu watoto wa kimaskini.

Suala la mitihani ni mtihani, lakini maisha ni kupambana na mitihani. Ni vema tukapambana na mtihani huu bila ya woga au kulindana bila ya sababu za msingi

Chanzo: Tanzania Daima
[ Read More ]

Kongamano la Kutathmini Matokeo ya Elimu, Mwanafunzi Awaliza Wazazi


 
Aziza Mohammed mwanafunzi aliyeathirika kufutiwa matokeo yake ya mtihani wa kidatu cha nne aliacha simanzi kubwa ukumbini baada ya kueleza masikitoko yake ya kufutiwa mitihani na kuelezea jeshi la polisi lilivyowanyanyasa wakati wlaipopanga kuandamana kupinga matokeo hayo ambapo licha ya kupata kibali cha maandamano lakini jeshi la polisi liliingilia kati na kuwatawanya kwa kuwarushia mabomu ya machozi na kuwanyanyasa huku wengine wakipigwa na kutupwa katika gari la polisi hivi karibuni, lakini Aziza aliwalaumu wazazi wa wanafunzi hao ambao walishindwa kuwaunga mkono watoto wao katika hilo pamoja na kuwalaumu waandishi wa habari kwa kushinda kuwapa coverage katika tukio hilo


BAADHI ya wazazi ambao watoto wao wamefutiwa matokeo ya mitihani ya kidato cha nne visiwani Zanzibar wanakusudia kulifikisha mahakamni Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) kwa kutoa adhabu hiyo kinyume cha sheria.

Wazazi hao walitoa kusudia hilo mjini hapa jana katika wakati wa mjadala uliowashirikisha wadau mbali mbali wa sekta ya elimu na wanaharakati kujadili uamuzi wa Necta wa kuwafutia matokeo wanafunzi 3,303 kutoka Tanzania bara na Zanzibar na kuwazuia kufanya mitihani kwa muda wa miaka mitatu.

Ameir Hassan Ameir alisema pamoja na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya baraza hilo , kuna haja kwa wananchi visiwani humo kuitisha maandamano makubwa kupinga kufutwa kwa matokeo hayo na kushinikiza kuondolewa kwa dhabu dhidi ya wanafunzi.


Akipinga taarifa ya Necta kwamba mitihani hiyo imefutwa kwa sababu ya udanganyifu uliofanywa na wanafunzi, Ameir alisema baraza limeshindwa kuthibitisha udanganyifu huo na hivyo haliwezi kujiondoa katika kashfa ya kuvuja mtihani.

Alisema kushindwa kwa Katibu Mtendaji wa Necta, Joyce Ndalichako kutoa maelezo juu ya idadi na majina ya wananfunzi waliofutiwa mitihani kutoka kila upande wa Muungano, kumeibua hisia kwamba Tanzania bara imeandaa njama za kuua elimu elimu Zanzibar .



“Necta wanayo majina ya shule na namba za shule zote za Zanzibar , hivyo si kweli kwamba hawajui majina ya wanafunzi waliofutiwa mitihani,” alisema Ameir huku akihoji uwepo finyu wa ushiriki wa Zanzibar katika muundo wa Bodi ya Wakurugenzi wa Necta.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana wakati wa mjadala huo, bodi ya Necta ina wajumbe 14 na kati ya hao sita wanatoka upande wa Zanzibar .

“Sisi tuna uchungu na Zanzibar yetu, kuvuja kwa mitihani na watoto kufutiwa mitihani ni matokeo ya kero za Muungano. Adhabu ya miaka mitatu itawapotezea watoto wetu muda wa kusoma, Wazanzibari tuungane tulishtaki Necta,” alisema.

Ali Hassan, Mkuu wa zamani wa Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja alisema ingawa Necta imeshindwa kutoa idadi ya wanafunzi waliathirika na uamuzi wa kufutwa matokeo, anaamini asilimia kubwa wanatoka upande wa visiwani wa Muungano.

Alisema maelezo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Necta mbele ya mkutano na waandishi wa habari Februari 14 mjini hapa yanapaswa kusikilizwa tu na mtu asiyejua chochote na kuongeza kuwa kwa hatua hiyo: “ Mama Ndalinacho amefeli astep down.” Akiwa na maana aachie ngazi.

Faisal Mohamed, ambaye pamoja na Ali walisema ni miongoni mwa waathirika wa watoto wao kufutiwa mtihani alisema alivishambulia vyombo vya habari na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa alichoeleza kuwa kushindwa kuandika kwa kina habari za kashfa ya mitihani na kupokea kutoka Necta na kusaini taarifa bila kudadisi maelezo ya baraza hilo juu ya utata wa matokeo na hatua zilizochukuliwa dhidi ya wanafunzi.

Hata hivyo walalamikaji wote hawakueleza kusudio la kulishtaki baraza litatekelzwa kwa sheria, lakini walisema chini ya makosa ya jinai ni kinyume cha sheria kutoa hukumu ya jumla kwa kosa ambalo ni la mtu mmoja mmoja. Kwa kufuatilia taarifa hii tafadhali nenda katika wall yangu ya facebook ya salma said.
[ Read More ]

whitney houston - I will always love you

[ Read More ]

WHITNEY HOUSTON FUNERAL EARLY TODAY





 Dressed in black: Two women pause to look at the memorial display before they go into the church to pay their last respects to Whitney Houston

Escort: A procession of cars with flowers - one of which is the golden hearse carrying her casket - drive down the Newark street after the service escorted by a police car

The golden hearse carrying the body of singer Whitney Houston bears a photo of her in the window as her family and friends prepare to say goodbye to the star


Death of a star: Pall-bearers carry the casket of pop singer Whitney Houston to a hearse following her funeral service at the New Hope Baptist Church in Newark, earlier today
Denied: Brown is believed to have got into an argument with Whitney's family over whether or not he could bring nine people into the church with him. He was invited and told he could bring two people but instead showed up with an entourage of nine and stormed out when he was told they could not be seated


Final journey: Whitney Houston's silver casket was carried out as her greatest hit I Will Always Love You was played

 Emotional time: Whitney Houston's mother Cissy Houston, 78, was seen arriving at the funeral home for a special private viewing with close friends and family on Friday afternoon

 Sad day: Whitney's daughter Bobbi Kristina was also seen arriving at Whigham Funeral Home in New Jersey yesterday

 Kim Burrell sings one of Whitney's favourite songs, changing the lyrics to make it more personal to the singer
 Not singing: Aretha Franklin, who performed at Radio City Music Hall in New York last night, pulled out of singing at her god daughter Whitney's funeral at the last minute, saying she was 'too ill'

Stevie Wonder said in his fantasy world he had a crush on Whitney before serenading the audience with Ribbons In The Sky
 Singer Alicia Keys was tearful as she walked to the piano and spoke about her friendship with the singer
The Bodyguard co-star: Kevin Costner paid tribute to Whitney Houston today and shared fond memories of his time with the singer with the rest of the congregation

Houston's aunt, singer Dionne Warwick, officiated the service today and took to the altar several times to welcome the singers and speakers to the congregation
First mourner: The Rev Jesse Jackson leaves Whigham Funeral Home after visiting with the family of Whitney Houston before going to the New Hope Baptist Church to prepare for the service


A year later: Whitney Houston and her daughter Bobbi Kristina Brown were pictured together at the 2011 Pre-GRAMMY Gala. She died on the day of the same event this year

Last moments: Whitney Houston's last ever public performance on Thursday February 9 with her close friend Kelly Price. She was found dead two days later

[ Read More ]

WHITNEY FUNERAL


They sang, they cried and they remembered Whitney Houston, the soulful singer who once wowed the congregation at New Hope Baptist Church in New Jersey, before she became a music icon, and a worldwide sensation.
Some of the biggest names in the entertainment industry joined Houston’s friends and family for her funeral at the same church where she first made her name, to remember the life of the woman who sold millions of albums during her life, and touched millions more with her booming voice.“You wait for a voice like that for a lifetime,” said music mogul Clive Davis.”
The funeral service ended with one of Houston’s most popular songs, “I Will Always Love You” filling the air in the packed church.

Some of the celebrities invited to say their final goodbyes to Houston included Tyler Perry, Jennifer Hudson, Kevin Costner, Alicia Keys, Stevie Wonder, and Oprah Winfrey.
“We are here today, hearts broken but yet with God’s strength we celebrate the life of Whitney Houston,” Rev. Joe A. Carter told mourners inside the church.The funeral started around noon with a choir singing to the packed room of mourners.
Houston’s biggest fans were able to mourn the singer by following the funeral live on the Internet, with the Associated Press streaming it on Live Stream.
Just after 12 p.m. Saturday more than 100,000 were viewing the live stream of the singer’s funeral.
The farewell to Houston comes just one week after she died in her hotel room at the Beverly Hilton Hotel. She was discovered underneath the water inside a bathtub. EMT’s pronounced her dead after they were unable to revive her.
Houston, who was 48 when she died last week, was scheduled to perform at Clive Davis’ pre-Grammy Awards party that night.
Her death also came one day before the Grammy’s, which is considered music’s biggest night. During the awards show, Hudson sang Houston’s “I Will Always Love You” in a moving tribute to the powerful singer.
Mourners were handed a program at the funeral, that included a letter published by Houston’s, mother, Cissy Houston, who wrote:
“I never told you that when you were born, the Holy Spirit told me that you would not be with me long. And I thank God for the beautiful flower he allowed me to raise and cherish for 48
[ Read More ]

Mjadala wa Wazi Matokeo ya Mtihani




Inshaallah Kesho Jumamosi asubuhi saa 2.30 katika ukumbi wa Beit Al Yamin Malindi kutakuwa na mjadala wa wazi wa wadau wote wa elimu kuhusu matokeo ya mtihani wa taifa kidato cha nne.

Mjadala huo utawashirikisha walimu wa skuli za serikali na binafsi, wazazi, wanafunzi na wadau wengine wa elimu karibuni katika mjadala huo ili kutoa maoni yenu katika mjadala huo.
Kwa wale watakaopenda kufuatilia tutakuwa tukirushwa moja kwa moja kupitia facebook ya Salma Said au mtandao wa www.zanzibaryetu.wordpress.com. Msikose kufuatilia kujua kinachozungumzwa katika mjadala huo muhimu.

Aidha Kesho hiyo hiyo jioni inshallah saa 4:30 eneo la Mapembeani Mwembe Tanga kutakuwa pia na mkutano wa kutoa elimu ya uraia kuhusu katiba, mkutano ambao umeandaliwa na baraza la Katiba Zanzibar

Mnaombwa kuhudhuria kwa wingi katika mkutano huo, vitabu vya KATIBA TUITAKAYO vitatolewa bure katika mkutano huo. watakaoongoza utoaji wa elimu ni pamoja na Professa Abdul Shareef, Awadh Said na Ally Saleh. Mnakaribishwa kuhudhuria kwa wingi na mnaombwa kwa kila atakayesikia tangazo hili amuarifu na mwenzake
[ Read More ]

R.I.P Whitney Houston.

 
Whitney Houston, who found fame as one of pop’s biggest voices, has died. She was 48.
Houston died Saturday afternoon, a representative for the singer told the Associated Press. Houston’s death comes on the eve of the Grammys and on the night of Clive Davis’ annual pre-Grammy gala, at which she performed last year and was expected to attend this year.
No cause of death has been announced and law enforcement sources said the singer was found in a hotel room at the Beverly Hilton, where emergency medical personnel were called sometime Saturday.

The Hilton is the scene for Davis’ annual gala. On Thursday, Houston dropped by the rehearsals to offer vocal tips for Brandy and Monica, who were slated to be one of the evening’s headliners.
Press, including The Times, were in attendance for a junket with the reunited R&B divas and Davis. Though Houston greeted people her with a warm smile, she appeared disheveled in mismatched clothes and hair that was dripping wet with either sweat or water.
The visibly bloated singer displayed erratic behavior throughout the afternoon -- flailing her hands frenetically as she spoke to Brandy and Monica, skipping around the ballroom in a child-like fashion and wandering aimlessly about the lobby. It was mentioned by a Grammy staffer that security personnel received calls of the singer doing handstands by the pool.
After leaving rehearsals, Houston returned to the ballroom -- with her teenage daughter Bobbi Kristina in tow -- as camera crews set up for interviews. The singer smelled of alcohol and cigarettes. A Grammy staffer said that during the interviews with Brandy, Monica and Clive, Houston was dancing just off camera to make the singers and Davis laugh. Grammy personnel expressed concern that she'd be caught on camera, and that reporters would write about her behavior.
Finally her daughter pulled Houston out of the room, and the singer skipped off. In our post of the event, we called Houston's behavior "loose and lively."
“She really loves and supports us both. For me, I went through a lot of very tumultuous moments and she would show up, not just with a phone call but physically when I needed,” Monica said when we asked about Houston coaching them. “That's something that I've carried with me, especially with all that she's been going through over the years herself. She's never turned her back on the people she cared about.”
Later that evening Houston appeared at Hollywood nightclub Tru, for fellow R&B singer Kelly Price’s pre-Grammy party. "Kelly Price & Friends Unplugged: For the Love of R&B" served as both a celebration and a jam session to preserve that genre, which was scaled back from eight categories to four this year.
Houston was billed as one of the evening’s special invited guests but after her appearance earlier it was shocking to see the singer arrive. More put together in her appearance, Houston briefly sang a duet with Price. In what has become her final performance, clips of the two singing a gospel hymn made the rounds because of the singer’s unsteady vocals.
SOURCE: Los Angeles Times
[ Read More ]

HATIMAE JAY-Z & BEYONCE WAMEWEKA PICHA ZA MTOTO WAO (BLUE IVY) KWENYE MITANDAO YA KIJAMII



                                   Mtoto Blue Ivy















                                Mtoto Blue Ivy.

                   Beyonce akiwa na Mwanae Blue Ivy


                     Jay-Z akiwa na mwanae  Blue Ivy

[ Read More ]

MANY CONGRATS.


Many  Congrats to  my Baby Sister Mariam Tawe  for great form 4 result ..beauty with purpose......Education is sexy.... i am so proud of you dear xoxo.....
[ Read More ]

DALILI ZA KUWA NA STRESS



Kuna mambo mengi au hali flani inaweza kuwa inajitokeza kwako mara kwa mara na usijue ni nini, au ukapuuzia lakini baadae ikaja kukuletea madhara makubwa. Ukiona mtu au kuhisi dalili zifuatazo, ujue ndio mwanzo wa stressKimbia ukapate msaada kabla mambo hayajaharibika 

1. Kutojiamini
 

2. Kujawa na mawazo mengi kichwani (Msongo wa mawazo)
3. Kuwazia mabaya wakati wote
4. Kuongea kwa sauti (Shouting)

5. Kula chakula au kunywa pombe kupindukia
6. Kushindwa kula (Kupoteza hamu ya chakula) 
7. Kushindwa kujichanganya na watu (Anti-Social)

8. Kusahau vitu mara kwa mara 
9. Kupata tabu ku concentrate katika mambo
 
10.Matatizo ya tumbo, mdomo kukauka, misuli kukaza na kutoka jasho mara kwa mara

11. Kuamka mapema 
12. Moyo kwenda mbio
 
13. Kusikia joto
 
14. Kichwa kuuma

YAFANYIE KAZI KABLA HUJACHELEWA

source jaydee.

[ Read More ]