Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu Mstaafu wa Hesabu za Serikali afariki Dunia


Waumini wa Dini ya kiislamu wakiwa pamoja kwa ajili ya kumsalia maiti
Vingozi mbali mbali wa serikali waliohudhuria katika sala ya kumsalia maiti

Waumini hao wakiwa kwenye hatuwa ya mwishi ya kumsindikiza ndugu yao katika makaburi ya kisutu
Waumini wa dini ya kiislamu  wakiwa kwenye hatuwa ya mwishi ya kumsindikiza ndugu yao katika makaburi ya kisutu
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu Mstaafu wa Hesabu za Serikali wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa  Tanzania Bwana Mohd Aboud Mohd aliyefariki Dunia Nchini India  amezikwa katika makaburi ya Wangazija yaliyopo Kisutu Mjini Dar es salaam.
Mamia ya waislamu, familia, wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za  Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania walihudhuria mazishi hayo wakati wa jioni.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wake Dr. Mohd Gharib Bilal, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mwenyekiti wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere Dr. Salim Ahmed Salim na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa SMT walikuwa miongoni mwa watu waliohudhuria mazishi hayo.
Marehemu Mohd Aboud Mohd maarufu Mfaransa  alizaliwa Zanzibar Tarehe 25/1/1927 na kupata elimu zake za Dini na Dunia na alipomaliza masomo yake ya sekondari aliajiriwa serikalini mnamo tarehe 1/1/1944.
Marehemu Mohd Mfaransa kwa umahiri wake wa utumishi serikalini alipata fursa ya kupandishwa daraja hadi kufikia kuwa msaidizi Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  hadi mwanzoni mwa mwaka 1967.
Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume alimpendekeza Mzee Mohd Mfaransa  kushika wadhifa wa Msaidizi Mkaguzi Mkuu wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 1/3/1967.
Tarehe 16/10/1967 Marehemu Mohd Mfaransa  aliteuliwa rasmi Mtanzania na Mwafika wa kwanza  baada ya Uhuru wa kuwa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wadhifa aliokuwa nao hadi kustaafu kwake tarehe 25/12/1987.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Matehemu mzee Mohd Aoud Mohd    {Mfaransa }  mahala pema peponi amin.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
30/12/2012
[ Read More ]