Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

MISS YOU.



[ Read More ]

Friends Of Mafia: TAMKO KUHUSU TAMASHA LA MASHOGA.


Kisiwa cha Mafia


Sisi kama wenyeji wa kisiwa hichi na wenye nia uchungu na kisiwa hiki
tumesikitishwa na hatua ya baadhi ya wenye mahoteli ya kitalii kwenye
kisiwa hichi pamoja na uongozi mzima wa wilaya (DC) na halmashauri kutoa
kibali kwa kundi la burudani toka Ugiriki kuja kufanya vitendo vya ushoga
kwa kutumia mgongo wa Tamasha la muziki. 
Pia tumesikitishwa uongozi hapa Mafia kukubali kutoa kibali kwa hawa vijana
3,000(revelers) bila kupata ridhaa ya wenyeji wa Kisiwa hichi (Public
consultation). Tungependa ifahamike kuwa sisi kama wenyeji wa Kisiwa hichi
tunakaribisha wageni lakini ni LAZIMA wazingatie na waheshimu mila na
taratibu zetu na moja kati ya hizo mila zetu USHOGA haumo!
Kitendo cha kutaka kuleta vijana hawa mashoga hapa kisiwani kufanya
vitendo vyao kwa siku 14 mfululizo hakikubaliki kimaadili na tunawaunga
mkono wana Mafia na hasa wazazi ambao hawako tayari kuona watoto wao
wakishuhudia vitendo vya kishoga, utumiaji wa madawa ya kulevya ambavyo
ni si mila na desturi yetu kama waTanzania.
Kama mjuavyo Mafia ni kisiwa cha amani na ndio maana kimekuwa kinaongoza kwa utalii wa scuba diving duniani na tunaendelea kuwakaribisha watalii ambao wanakuja na kutuheshimu na wanaoelewa umuhimu wa kutunza mazingira ya kisiwa hichi.
Kisiwa hichi hakina uwezo wala fedha za kuweza kutoa huduma za afya kwa
watu wake iweje leo tamasha hili la mashoga 3,000 ambao itabidi wajisaidie
kwenye mashamba ya watu kwani hakuna public toilets za kuweza kuhimili
kishindo hichi.
Hivi kwa mfano mazingira yashachafuliwa ni sisi watu wa Kisiwa hiki ndio
tutasafisha au halmashauri? je wanazo pesa za kusafisha na kuokota toilet
papers zitakazo achwa na hawa Mashoga kwenye mashamba yetu?
Hospitali zetu hapa zinatia aibu na mbaya zaidi huduma za afya kwa mama
zetu na dada zetu wanapojifungua zipo katika hali duni, hivi kweli
mheshimiwa DC na timu yake wameona kwa sasa tunachohitaji ni hili Tamasha?
Kwa kawaida ya Mashoga hawatokaa sehemu moja hapa kisiwani na watataka
kwenda kufanya uchafu wao kwenye fukwe zetu hapa kisiwani, hivi Uongozi wa
Kisiwa hichi utatoa polisi wangapi kwa kila kundi la hawa mashoga kufanya
mambo yao? kwani sidhani kama wananchi watakaa na kushangilia vitendo
hivi vikifanyika hadharani.
Tungependa kuufahamisha umma kuwa hawa waandaji tamasha hili lilipofanyika kwenye kisiwa cha Skyros, watu walililalamika sana pamoja na kuwa Wagiriki wana mitizamo ya ku liberali kwenye mambo haya lakini hali ilikuwa mbya kiasi cha Polisi kuvamia na kusitisha lile Tamasha kwani lilikuwa linaelekea kuvujinka kwa amani.
Katika kipindi hichi ambacho tunaelekea kwenye Uchaguzi je ni kweli
Serikali inataka kuona uvunjikaji wa amani katika kipindi hichi
tunachoelekea kwenye Uchaguzi kwa kukubali hili tamasha la Mashoga?
Je jeshi la polisi linazo resources za kulinda mashoga 3,000 usiku na
mchana kwa siku saba mfulululizo?
Kwa nini mratibu wa hili Tamasha hili la Mashoga hataki kukutana na viongozi wa Kisiwa hichi na kuwaeleza kwa
kinagaubaga nia yake?
Maandaji wa Tamasha hili wamesema wamepata ushirikiano wa karibu na
kampuni ya uwindani na utalii inayojiita KARIBUSANA ambayo iko chini ya
Costa Coucoulis,Angela Damas,Chyrista Batou na Mark Evans ambao wanajiita
wahifadhi wa mazingira kwenye tovuti yao lakini wakati huo huo wako tayari
kuhakikisha kuwa mazingira ya kisiwa chetu yanachafuliwa na hawa wageni.
Je Mbunge na DC wa Kisiwa hichi watakuwa wanatekeleza ilani ya chama gani
kulikubali hili Tamasha la Mashoga?
Je wilaya iliyo masikini kuliko zote Tanzania inahitaji Tamasha la muziki
au tunahitaji miradi ya Maendeleo?
Je BASATA na Wizara ya Utalii wameamua
[ Read More ]

Wanajeshi Wawili Wapoteza Maisha Katika Ajali Ya Ndege

sehemu ya ndege iliyopata ajali baada ya kutua barabarani kwa dharura na kugonga basi la watalii ambalo linaonekana juu kushoto likiwa limeanguka



Askari wawili ambao ni marubani wa Jeshi la Wananchi Tanzania wa Kambi ya Ngerengere ya Morogoro, wamekufa baada ya ndege waliyokuwa wakisafiria kutua barabarani kwa dharura na kugonga gari la watalii na kupinduka jana katika eneo lijulikanalo kama Zimbabwe katika kijiji cha Manga wilaya ya Handeni, Mkoa wa Tanga.

Katika basi la watalii inasemekana kulikuwa na watu 24 ambao 19 kati yao ni raia kutoka Uholanzi, wanne kutoka Kenya na mmoja Mtanzania. Wote walinusurika kufa.

Inasemekana kuwa marubani hao walikuwa katika mazoezi ya kawaida katika anga ya eneo hilo, na kwamba wakati ikiwa angani ndege ilipata hitilafu ndipo rubani akaamua atue barabarani ili kuokoa maisha yao, kabla gari hiyo ikiwa kwenye mwendo mkali iliigonga.

Ndege hiyo ndogo ya JWTZ yenye namba F59119 ilikuwa inatumika katika mafunzo ya kijeshi. Kaimu kamanda wa polisi mkoani Tanga, Afande Jafari Mohammedi, aliwataja waliokufa kuwa ni rubani wa ndege hiyo Meja Kathbet Leguna (41) na mwanafunzi wake Luteni Andrew Yohana Kijangwa (31).

Taarifa zinasema Meja Leguna alikuwa ni mwalimu wa mafunzo ya ndege za kivita katika kikosi hicho cha Ngerengere na alikuwa anamfundisha urubani Luteni Kijanga.

source:issa michuzi blog.
[ Read More ]

TANZANIAN CHINESE YOGA..so funny

[ Read More ]

MESSAGE OF THE DAY.



[ Read More ]

from nubia group.

[ Read More ]

Wanted: Dark & handsome Imams!





Malaysia swoons over reality search for hottest Imam. The prize: A university scholarship, a job leading prayers at a Kuala Lumpur mosque and a trip to Mecca


 They’re young, tall-ish, dark and handsome and they’ve captured the hearts of Malyasian TV viewers mesmerized by the quest to be declared a nation’s hottest up-and-coming imam.


 Contestants on the new reality show Young Imam are judged by one man— the former grand mufti of Malaysia’s national mosque—and are ranked by their knowledge of Islamic theory, the quality of their voices citing Koran verses and intellectual feats. Their reward? A university scholarship, a job leading prayers at a Kuala Lumpur mosque and a trip to Mecca to perform the Haj pilgrimage. 

The show is an odd mix of Hollywood razz matazz with ancient religion as the nation juggles the demand of faith and the modern world. “These young imams are modern, and we need that. Muslims are very progressive,” one fan tells the Wall Street Journal. “After 9/11, it’s good for us to show the true picture of Islam.” Thought the program has the look of Survivor meets Britain’s Got Talent, the feats are unique. In one episode, contestants had to prepare unclaimed corpses for burial—an essential rite in Islam. “It’s a tough contest, but if we want to be imams and lead our community, we should expect to face difficult challenges any time, any place,” declared one brash contender.
[ Read More ]

MR II ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI,AWEKA WAZI KUKAMATWA KWAKE NA POLISI





Joseph Mbilinyi a.k.a Mr II


TAARIFA KWA VYOMBO HABARI
.NATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI KUPITIA CHADEMA
· NATOA TAMKO RASMI KUHUSU KUHOJIWA KWANGU NA POLISI
Mimi, Joseph Mbilinyi ambaye najulikana zaidi katika anga ya muziki kama “Sugu” ama “Mr II” leo tarehe 29 Juni 2010 natangaza rasmi nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Mbeya Mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Kwa muda mrefu katika maisha yangu ya kimuziki pamoja na kuimba nyimbo za kuburudisha nimekuwa zaidi mstari wa mbele kuimba nyimbo za kutetea haki za makundi mbalimbali katika jamii na taifa kwa ujumla.
Wakati umefika sasa wa kuhamisha jukwaa la mapambano ya kudai haki kutoka jukwaa la muziki mpaka jukwaa la siasa kwa dhamira ile ile ya kutumia kipaji changu alichonijalia Mwenyezi Mungu kuimba na kuhutubia kwa ajili kuleta mabadiliko ya kweli katika taifa letu.
Nyimbo zangu zimekuwa zikibeba sauti ya watu wasio na sauti ili zisikike na watawala; lakini hata hivyo kwa kipindi chote ambazo nimekuwa nikifanya harakati hizi watunga sheria na wafanya maamuzi ya kisera chini ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameshindwa kuongoza vizuri taifa kuweza kufanya mabadiliko ya kweli yenye kuhakikisha watanzania wananufaika na vipaji vyao ambavyo Mwenyezi Mungu amewajalia na taifa linanufaika na rasilimali na maliasili ambazo tumejaliwa kuwa nazo.
Hivyo natangaza nia ya kugombea ubunge ili kuchangia katika kuongeza nguvu ya chama mbadala katika Bunge letu; niwe sehemu ya sauti mbadala katika kutunga sheria, kuwawakilisha wananchi, kuandaa sera na kuiwajibisha serikali kuweza kutekeleza yale ambayo mimi na wanaharakati wenzangu katika sanaa tumekuwa tukiyapigia kelele muda mrefu kupitia muziki wetu na maisha yetu.
Uamuzi wangu wa kugombea ubunge Mbeya Mjini ni haki yangu ya kikatiba na natambua kuwa kwa kuwa mbunge nitafanya kazi ya kuwawakilisha wananchi wenzangu na kama ambavyo wakati wote nimekuwa nikipambana katika harakati mbalimbali ndivyo ambayo nataka niwe mstari wa mbele kupambana katika kuleta maendeleo.
Huu si wakati wa kampeni hivyo niwaahidi wananchi wa Mbeya kwamba nitaeleza mengi kuhusu sera zangu na ahadi zangu kwao mara baada ya kupitishwa na CHADEMA kugombea ubunge katika jimbo letu.
Hivyo, nachukua fursa hii kuwajulisha watanzania wenzangu kwamba siku chache sijazo nitachukua fomu ya chama ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini.
Lakini kwa ujumla uamuzi wangu wa kugombea umesukumwa na harakati zangu za miaka mingi na ufahamu wangu kuhusu hali halisi ya maisha yetu wananchi wa Mbeya Mjini.
Natangaza nia ya kugombea nikiwa ni mgombea mpya kutoka chama mbadala ili kushirikiana na wananchi wenzangu wa Mbeya Mjini kuondokana na siasa za makundi, ukabila, ubaguzi, na migogoro ambazo zimekuwa zikitawala katika Jimbo letu na Mkoa kwa ujumla na hatimaye kusababisha tuwe na uongozi mbovu unaokwamisha maendeleo.
Jiji la Mbeya linakabiliwa na ubovu wa barabara ukiondoa barabara kuu inayokwenda Tunduma; barabara za mitaani ni mbovu wakati ambapo kuna fursa ya kuwa mkoa wenye makaa ya mawe ambayo mabaki yake yangeweza kutumika kukarabati barabara za mitaani Uyole, Soweto na kwingineko.
Natambua kwamba wafanyabiashara wa Mbeya Mjini wanamalalamiko mengi kuhusu kubambikiziwa kodi huku wafanyabiashara wadogowadogo wakiwa wananyanyaswa katika maeneo wanayofanyia biashara kwa kuwa hata mimi mwenyewe nimewahi kuwa mfanyabishara katika soko letu la Mwanjelwa.
Natambua kwamba jiji letu la Mbeya ni kitovu cha elimu katika mkoa wetu hata hivyo lugha zinazotolewa na uongozi wa Mkoa zinawadhalilisha walimu wakati uongozi huo unashindwa kuweka mazingira bora ya elimu na kusababisha Mbeya mjini kuanza kudorora kielimu. Kwa upande mwingine, kadiri mji unavyopunuka ndivyo kero ya usafiri wa wanafunzi inakithiri na shule za pembezoni zinakosa walimu.
Natambua kwamba kwa muda mrefu Mbeya Mjini yetu ina kero ya umeme wakati ambapo tupo jirani na Mgodi wa Kiwira ambao ungeweza kuzalisha umeme wa kututosheleza lakini kutokana na ufisadi tunashindwa kuondokana na hali hii ambayo inasababisha ugumu na kupanda kwa gharama za maisha na kukosa taa za barabarani hali ambayo inaweka mazingira ya kuongezeka kwa uhalifu.
Natambua kwamba viwanda vyetu vya Mbeya Mjini vimeuzwa kwa bei chee na vingine vimeshindwa kuendeshwa na kubaki magovu na kusababisha vijana kukosa ajira na uchumi kuathirika kama ilivyokuwa kwa viwanda vya pamba, mafuta na nyama.
Natangaza nia ya kugombea ubunge wa Mbeya Mjini kwa kuwa naamini kwamba kero ya maji inayotukabili inaweza kuondolewa tukiwa na uongozi mbadala ambao utaweza kutumia vyanzo mbadala vya maji kama mto Mzovwe, Ivumwe na kutoka katika Mlima Igamba.
Natangaza nia ya kugombea Ubunge ili pamoja na kuingia bungeni niweze kuingia katika halmashauri ya Jiji la Mbeya nishirikiane na wananchi wenzangu kuibua ufisadi na udhaifu iliopo unaosababisha ubadhirifu wa fedha za wananchi na mali za umma kama ilivyotokea kwa milioni 68 zilizobaishwa kwenye ripoti ya mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2007/08; tuhuma za kutaka kuuza kiwanja cha wazi eneo la Sokoine na kushindwa kulipa fidia wananchi wa Kata ya Kalobe waliondolewa katika viwanja vyao.
Wakati huo huo; napenda kuchukua fursa hii kuwafahamisha wananchi wenzangu wa Mbeya Mjini, wapenzi wa muziki wangu, wanachama wenzangu wa CHADEMA na watanzania kwa ujumla kwa jana tarehe 28 Juni 2010 nilikamatwa na polisi kwa kile walichonieleza kuwa kuna malalamiko dhidi yangu kuwa nimemtishia kwa maneno kumuua Ruge Mutahaba kupitia wimbo uitwao “Wanna Kill” uliopo kwenye album iitwayo “Anti Virus”.
Walinikamata saa 5 asubuhi nikiwa naingia ukumbi wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa ajili ya kutoa Mada kuhusu “Tathmini ya Muziki wa Kizazi Kipya na Hatma yake nchini” na kunihoji kwa takrabani masaa matano mpaka saa 10 jioni.
Wameniachia kwa kile walichonieleza kuwa ‘dhamana ya kujidhamini mwenyewe’ na kunitaka niripoti kwao siku ya jumatano tarehe 30 Juni saa 5 asubuhi siku ambayo nilipanga kwenye ratiba zangu kurejea nyumbani Mbeya Mjini kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge kabla ya tarehe ya mwisho ya utoaji na upokeaji fomu ndani ya CHADEMA.
Katika mahojiano nao yaliyofanyika Makao Makuu ya Upelelezi Wizara ya Mambo ya Ndani; maofisa usalama (CID) walionihoji walirejea mstari mmoja katika kiitikio cha wimbo husika wenye maneno “I Wanna Kill Right Now” na kusema kwamba mlalamikaji ameutafsiri mstari huo kuwa ni tishio la kutaka kumuua.
Napenda kuwajulisha mashabiki wangu na watanzania wenzangu kwamba nimelieza wazi jeshi la polisi kwamba hakuna wimbo wala maneno niliyowahi kutamka kwa lengo la kukusudia kumuua binadamu yoyote. Niliwaeleza jeshi la polisi kwamba sanaa ya muziki inalugha zake zake za kifasihi.
Maadhui ya wimbo mzima yamejikita katika harakati zangu za siku zote za kupambana na wanyonyaji dhidi ya maslahi ya wasanii Tanzania na wimbo huo una maudhui ya kutaka “Kuondoa ama kuiua dhamira ya mbovu na nia zao ovu”.
Ni vyema mashabaki wangu, wanachama wenzangu na watanzania kwa ujumla wakarejea katika Kamusi mbalimbali za kimataifa ambapoo neno KILL linamaana zaidi ya 10 zikibeba pia maana ya KUKOMESHA, KUONDOA nk.
Katika wimbo huo nimeghani kwa kutumia fasihi mambo ya ukweli yanayotokea katika sekta ya sanaa na wala hauna dhamira yoyote wala maudhui ya kufanya kosa lolote la jinai; hivyo kama kuna mtu ameguswa na ukweli uliomo katika wimbo huo na hakubaliani nao basi aupinge kwa hoja ama akafungue madai badala ya kukimbilia kutaka kuliingiza jeshi la polisi kwenye masuala ya sanaa.
Aidha nimeshangazwa na hatua ya jalada hilo la polisi kufunguliwa ndani ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Wizara ya Mambo ya Ndani yaliyopo Wilaya ya Ilala wakati mimi na mlalamikaji wote ni wakazi wa Wilaya ya Kinondoni.
Baada ya maelezo niliyoyatoa ni matumaini yangu kuwa jeshi la Polisi ambalo lina kazi muhimu zaidi ya kukabiliana na ujambazi na vitendo vingine vya uhalifu ambavyo vinazidi kuongezeka katika Mkoa wa Dar es salaam ambapo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi yapo litaelekeza nguvu zake katika kukabiliana na vitendo hivyo vya makosa ya Jinai badala ya kupoteza muda wake kushughulikia masuala ya kifasihi ambayo yana sura ya madai yasiyo na uzito wowote.
[ Read More ]

Stara Thomas - Tupendane....za kale...

[ Read More ]

AT Feat Stara Thomas - Nipigie

[ Read More ]

Police to question Viveka Babajee's boyfriend

The police in Mumbai are likely to question the boyfriend of former supermodel Viveka Babajee who was found dead at her Bandra home on Friday.
They have already confirmed that it as a case of suicide and are now investigating the reasons behind the extreme step. The former Miss Mauritius is said to have fought over the phone with a close friend on June 24 evening.
Police have recovered her laptop, mobile phone, a bag with medicines including sleeping pills and a diary with reportedly had 'I kill' written on the last page.
She was living alone in the rented flat. The 37-year-old model shot to fame in the 90s when she featured in an advertisement for Kamasutra condoms.

[ Read More ]

Young, Famous and Dead



A tribute to those who lost their lives at the crest of fame... Even as we are still coming to terms with the shocking suicide of model Viveka Babaji. Here's a look at some young talents whose lives were cut short too soon, by accident or self destruction. Most of these young celebrities died, even before they could ride the crest of fame befitting their talent.
[ Read More ]

Gelly & AT feat Ray C - Mama Ntilie

[ Read More ]

ZANZIBAR ALLSTARS - We Are Together (Tuko Pamoja)


Baada ya makubaliano kati ya Rais wa Zanzibra na Seif sharif hamadi juu ya mstakbali wa ZANZIBAR. Wasanii wakizazi kipya kwa moyo mmoja wameamua kushirikiana na kutengeneza wimbo huu kwa ajili ya kuhamasisha kuwa ZANZIBAR NI MOJA .
[ Read More ]



[ Read More ]

RING ROAD MYSORE: WORK IN PROGRESS

na hivi ndivyo itakavyokua baada ya kukamilika kwa ujenzi.
[ Read More ]

GOOD MORNING, HAVE A NICE DAY.



[ Read More ]

HAVE A NICE DAY.

[ Read More ]

Mtukuu wa Nelson Mandela afariki dunia.



(Pichani Mzee Nelson Mandela na Mtukuu wake Zanani mwaka 2008)

Habari za kusikitisha kutoka Afrika Kusini. Mtukuu wa Nelson na Winnie Mandela, Zenani mwenye miaka 13 amefariki katika jali ya gari. Habari kutoka huko zinasema kuwa walikuwa wanarudi kutoka kwenye sherehe za ufunguzi wa mashindano ya World Cup. Dereva wa gari alikuwa amelewa!

Pole sana familia ya Mandela. Mungu ailaze roho ya Zenani mahala pema . AMEN.


[ Read More ]

Mtanzania auwawa........


Takribani mwezi mmoja uliopita kulikuwa na tangazo kwenye blogs na hapa JF kwamba kuna dada yetu mmoja alipotea na akawa anatafutwa na ndugu zake.

Taarifa iliyotolewa kwenye local TV stations za Southern California zinasema kwamba mwili wa huyo dada ulipatikana jana nyuma ya nyumba aliyokuwa akiishi. Ulikuwa umefungwa kwenye mifuko ya plastic na blanket kama takataka.

Mume wa marehemu anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuhusika na mauaji hayo. Dada huyo alikuja kwa ajili ya kusomea kozi ya Uuguzi na alikuwa anasoma ili awe Registered Nurse. Ameacha watoto 2.

Lilian Mgonjwa alihojiwa na kituo cha TV kutoka makazi yake huko Long Beach. Kama kutakuwa na taarifa za ziada ninatumaini tutaendelea kujulishana
[ Read More ]

IJUMAN NJEMAA........

[ Read More ]

Shakira - Waka Waka | Official Video | World Cup South Africa 2010 | HD

[ Read More ]

Shakira - Waka Waka | Official Video | World Cup South Africa 2010 | HD

[ Read More ]

K'Naan ft. Nancy Ajram - Waving Flag [FIFA World CUP 2010]

[ Read More ]

MESSAGE OF THE DAY.

[ Read More ]

MTOTO ALIETIA FORA KWENYE MECHI KATI YA TZ NA BRAZIL.

[ Read More ]

Aliyemkumbatia Ricardo Kaka Neshno Apata Dhamana




Kombo akiwa kwenye gari na babake (kulia) pamoja na Askari kanzu wakielekea Polisi Chang'ombe kupewa dhamana.

picha kutoka kwa Issa michuzi.
[ Read More ]

ALIYEMVAA KAKA KATIKATI YA UWANJA AWA SHUJAA

  KIJANA Mtanzania aliyeingia uwanjani na kwenda moja kwa moja kumkumbatia kiungo nyota wa Brazil, Ricardo Kaka amekuwa gumzo na ‘shujaa’ kwa mashabiki wa soka nchini.

Kijana huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja aliingia uwanjani wakati mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya Taifa Stars na Brazil inaendelea na kwenda kumkumbatia Kaka.


Mashabiki walionyesha kuvutiwa naye na kuanza kumshangilia kwa nguvu, kama hiyo haitoshi mashabiki uwanjani hapo waliwazomea askari Polisi walipoanza kumpiga wakitaka wasifanye hivyo.

”Wale askari hawajui mapenzi, yule kaonyesha ustaarabu, kamkumbatia Kaka halafu katoka zake uwanjani wala hajafanya kitu chochote. Anastahili sifa,” alisema shabiki mmoja akiunga mkono na wenzake ambao waliendelea kuwazomea askari Polisi.

Hata baada ya mechi kijana huyo ambaye alikamatwa na Askari Polisi alikuwa gumzo kubwa huku watu wengi wakimpongeza kwamba ametimiza ndogo yake kwa kuwa Mtanzania wa kwanza kumkumbatia Kaka tena katikati ya uwanja lakini kwa amani ya kutosha.
Kijana huyo alitokea Magharibi ya uwanja huo na aliruka uzio baada ya kuvua viatu na kutoa kila kitu alichonacho mfukoni akihofia kuonekana anakwenda kumdhuru Kaka.

Baada ya hapo alianza kuingia uwanjani akiita, “Kaka, Kaka, Kaka”, huku akionyesha kama anataka kulia. Baada tu ya kumfikia, alimkumbatia kama mtu wanayefahamiana siku nyingi, Kaka hakuwa na hiyana alimpokea vizuri.

Halafu Kaka anayechezea Real Madrid, alimuomba shabiki huyo atoke uwanjani ili waendelee kusukuma gozi, naye taratibuu alitoke nje upande wa Magharibi kama mtu aliyefunga bao, mikono juu na mwenye furaha.

Waliokuwa wamekaa naye karibu walieleza kuwa kijana huyo alifanya maandalizi ya takribani dakika 15 akijiandaa kuingia uwanjani na mwisho aliapa, “potelea mbali kama nitafungwa au nife sawa, mimi naenda kwa Kaka.”

Kupata picha zaidi za tukio hilo bonyeza hii 'Link' hapa chini
http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/jamaa-aweka-histori...

habari kwa hisani ya global publishers
[ Read More ]

Tank up, petrol, diesel prices set to rise



Petrol and diesel prices are almost certain to increase after an empowered group of ministers (EGoM) meets to decide on fuel pricing on Monday, Oil Ministry sources tell CNN-IBN.

The EgoM, which is headed by Finance Minister Pranab Mukherjee and includes the Oil Minister, will meet on Monday afternoon to consider a Kirit Parikh Committee report that calls for freeing of petrol and diesel prices from government control.

If petrol prices are decontrolled, rates may go up by Rs 3.35 per litre, which being the difference between the retail price and imported cost. Mukherjee may even push for freeing pricing of diesel - the nation's most consumed fuel that is used in transport sector and hence has inflationary impact.

Also on cards is a Rs 50 per cylinder hike in domestic LPG prices, which may be moderated if Railway Minister Mamata Banerjee and other allies in the ruling United Progressive Alliance insist. A marginal increase in politically sensitive kerosene, which is used by the masses for lighting and cooking purposes, may also be proposed at the EGoM.

The EGoM will have to raise the price of petrol by Rs 3.35 per litre and that of diesel by Rs 3.49 a litre to free them from government control.


habari ndio hiyo...

[ Read More ]

PHOTO OF THE DAY.

[ Read More ]

YUSUF CHUCHU AFARIKI DUNIA




HABARI ZIMETUFIKIA PUNDE TOKA ZENJI ZIKISEMA KWAMBA MSANII MAARUFU WA HUKO VISIWANI YUSUF AHMED ALLEY MAARUFU KAMA BWAN'CHUCHU HATUNAYE TENA. HABARI HIZO ZINASEMA BWAN'CHUCHU AMEFIA JIJINI NAIROBI, KENYA, ALIKOKUWA AMEKWENDA KIKAZI. CHANZO CHA MAUTI YAKE HATUJAAMBIWA ILA IMETHIBITISHWA KWAMBA MWILI WAKE UMESHAREJESHWA ZENJI NA MSIBA UKO KWAO SEHEMU ZA KISIMA MAJONGOO NA MAZIKO YATAFANYIKA LEO SAA 10 KWENYE MAKABURI YA MWANAKWEREKWE.
BWAN'CHUCHU ATAKUMBUKWA KWA UHODARI WAKE KATIKA MUZIKI HASA ALIPOUNDA BENDI YA CHUCHU SOUND ILIYOTAMBA SANA KWA VIBAO VYAKE VIKALI NA CHAPUO ZA MAONGEZI KATI YAKE NA OMARI MKALI YALIYOKUWA YAKIHITIMISHWA NA NENO LA 'EE! KWAHERI'.
MAREHEMU CHUCHU PIA ALIKUWA MMOJA WA WAJUMBE WA BODI YA TAMASHA LA KILA MWAKA LA SAUTI ZA BUSARA NA PIA ALIKUWA ANAMILIKI STUDIO YA KUREKODIA MUZIKI PAMOJA NA STESHENI YA REDIO.
MOLA AIWEKE MAHALA PEMA ROHO YA MAREHEMU
-AMIN
[ Read More ]

PHOTO OF THE DAY.

[ Read More ]

PHOTO OF THE DAY.

[ Read More ]