Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

MHE. MWANRI AZITAKA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUSIMAMIA VIZURI FEDHA ZA MIRADI YA SERIKALI




Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri akipima kwa tape maalum urefu wa moja ya barabara zilizojengwa na Manispaa ya Sumbawanga katika Mji huo kuhakikisha kama barabara hiyo imejengwa kwa vipimo vilivyoanishwa kwenye mpango wa ujenzi huo (BOQ). Naibu Waziri huyo alitumia fursa hiyo kuziasa halmashauri zote nchini kusimamia vyema fedha za Serikali katika miradi kuhakikisha inafanana na thamani ya fedha zilizotumika, alilazimika kusema hayo baada ya kubaini mapungufu mbalimbali katika mradi huo wa barabara na miradi mingine aliyofanikiwa kuitembelea Mkoani Rukwa.
Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri akikagua barabara za lami zilizo chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga zilizojengwa hivi karibuni. Katika ukaguzi huo alibaini mapungufu mbalimbali katika ujenzi huo na kuagiza Halmashauri hiyo kuhakikisha mapungufu hayo yanaondolewa. Aliitaka pia halmshauri hiyo kusimamia vyema kazi za Serikali kuepusha minong’ono inayotoka kwa wananchi juu ya utendaji mbovu wa baadhi ya watendaji Serikalini.
Mhe. Agrey Mwanri akiweka jiwe la msingi kiwanda cha unga cha Malangali kinachomilikiwa na muwekezaji wa ndani mapema hivi leo. Kwa sasa Mkoa wa Rukwa una viwanda vitatu vya unga vinavyomiliwa na wawekezaji wa ndani.  
Naibu wa Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Agrey Mwanri akikagua kiwanda cha unga cha Malangali Mjini Sumbawanga leo alipotembelea kiwandani hapo kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi.
Mhe. Mwanri akizungumza na wakazi wa Mji wa Sumbawanga katika Stendi kuu ya mabasi ya Mjini hapo ambapo alipokea kero mbalimbali ikiwepo ubovu wa miundombinu ya umeme na barabara katika stendi hiyo. Aliuagiza uongozi wa Manispaa ya Sumbawanga kufanya Mkutano wa hadhara na wananchi hao kuskiliza kero zao zote pamoja na kuzitaftia ufumbuzi na kumpelekea taarifa ya utekelezaji.
Katika hali isiyotegemewa msafara wa Mhe. Mwanri ulipowasili katika kijiji cha Mlanda katika Manispaa ya Sumbawanga kwa ajili ya Mkutano wa hadhara ulikuta msiba ambapo walishiriki na kutoa ubani ambapo Mhe. Mwanri alitoa laki moja na alfu mbili na aliyekuwa Mbunge wa Sumbawanga Mjini CCM ambaye pia ni Mjumbe wa halmashauri kuu Taifa ya CCM (NEC) kupitia Mkoa wa Rukwa Aeshi Hillal alikabidhi shilingi alfu hamsini. 
(Picha na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa – rukwareview.blogspot.com)
[ Read More ]

RAIS SHEIN AZINDUA MRADI WA ONE WORLD FOOTBAL


shein akiongea
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohammed Shein ameuagiza uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzi ya Amali kuhakikisha michezo yote inayoruhusiwa kisheria Zanzibar kuchezwa mashuleni isipokuwa mchezo wa Ngumi (Boxing).
Amesema michezo yote inafaa kuchezwa wala haipunguzi kasi ya mwanafunzi kusoma na kwamba Wizara inapaswa kulisimamia agizo hilo ili Zanzibar iweze kupata vipaji vitakavoiletea nchi Medali za mashindano ya kitaifa na kimataifa.
Rais Shein ameyasema hayo alipokuwa akizindua Mradi wa “Mpira Mmoja” “One World Football ball Project for Africa”  Wenye lengo la kupambana na Ukatili dhidi ya Watoto kupitia mchezo wa Mpira katika Uwanja wa Aman mjini Zanzibar ikiwa ni shamra shamra za miaka 49 ya Mapinduzi Zanzibar.
Amesema Mradi huo ambao umewalenga zaidi Wanafunzi wa Shule umefufua matumaini mapya ya kuibua vipaji vya michezo mbalimbali Zanzibar na kwamba kinachohitajika kwa sasa ni mipangilio mizuri kutoka kwa Walimu na wasimamizi wa michezo mashuleni.
Aidha amesisitiza kuwa michezo haimzuii mwanafunzi kufanya vizuri darasani hivyo Wazazi na walezi waendelee kutoa mashirikiano kwa watoto wao kuhusu michezo stahiki wanayoipenda.
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akizindua Mradi Mkubwa wa Ugawaji wa Mipira ya kuchezea kwa Vikundi mbalimbali vya Michezo hadi Mashuleni kwa  kuanza kumgawia kijana  Yunus Fadhil Juma kutoka Mkoa wa Kusini Pemba hafla iliofanyika hapo Uwanja wa Amani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akizindua Mradi Mkubwa wa Ugawaji wa Mipira ya kuchezea kwa Vikundi mbalimbali vya Michezo hadi Mashuleni kwa kuanza kumgawia kijana Yunus Fadhil Juma kutoka Mkoa wa Kusini Pemba hafla iliofanyika hapo Uwanja wa Amani Zanzibar.

“Jukumu lenu Wizara ya Elimu ni kuhakikisha kuwa Michezo yote ile iliyoruhusiwa kisheria chini ya Wizara ya Habari Utalii Utamaduni na Michezo kuwa inachezwa Mashuleni..Wala michezo haimzuii mwanafunzi kufanya vyema Darasani ” Alisema Rais Shein.
Rais Shein alifahamisha kuwa mradi huo pia utasaidia sana kujenga kikosi imara cha Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) kwa vile vipaji vya Soka vitaibuka vingi mashuleni vitakavyosaidia Timu hiyo kuwa tishio Afrika Mashariki na Kati.
Akigusia suala la Zanzibar Heroes na ushindi wa nafasi ya tatu uliyoipata katika Mashindano ya SECAFA Rais Shein amesema timu hiyo ilicheza vizuri kiasi cha kumvutia sana na kuongeza kuwa Zawadi yao ipo kinachohitajika ni kumalizwa tofauti baina ya Wachezaji na Viongozi wa Timu hiyo.

Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk akitoa hotuba ya Kumkaribisha Rais wa Zanzibar ili kuwahutubia wananchi  waliohudhuria katika Uzinduzi wa Mradi mkubwa wa Ugawaji Mipira ya kuchezea kwa Vikundi mbalimbali vya Michezo hadi Mashuleni kwa Zanzibar nzima, hapo Uwanja wa Amani Zanzibar.
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk akitoa hotuba ya Kumkaribisha Rais wa Zanzibar ili kuwahutubia wananchi waliohudhuria katika Uzinduzi wa Mradi mkubwa wa Ugawaji Mipira ya kuchezea kwa Vikundi mbalimbali vya Michezo hadi Mashuleni kwa Zanzibar nzima, hapo Uwanja wa Amani Zanzibar.
Kwa upande wake Waziri wa Habari na Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema Mradi huo umelenga kuleta vuguvugu la michezo na kuondoa tatizo la vifaa vya michezo Zanzibar ili kuibua vipaji vitakavyoifanya Zanzibar iwe tishio katika michezo mbalimbali.
Aidha ameongeza kuwa Mipira hiyo itagaiwa katika maeneo yote ya Unguja na Pemba bila ya upendeleo na kwamba Timu zote zilizosajiliwa na Makundi maalum watanufaika na mipira hiyo.
Mradi huo ambao umefadhiliwa na One World Futbal,Shirika la Kusaidia Watoto Duniani kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar unajumuisha Mipira-Elfu 20, itakayogaiwa kwa Wanafunzi wa shule na Timu za Soka za Unguja na Pemba.

IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
[ Read More ]

NAIBU WAZIRI ASISITIZA RESI ZA NGALAWA KUENDELEZWA

Naibu Waziri wa Ardhi,Makazi,Maji na Nishati Haji Mwadini Makame akipuliza filimbi kuonyesha ishara ya kuanza kwa mashindano hayo.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Naibu Waziri wa Ardhi,Makazi,Maji na Nishati Haji Mwadini Makame akipuliza filimbi kuonyesha ishara ya kuanza kwa mashindano hayo.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Naibu Waziri wa Ardhi Makazi, Maji na Nishati Haji Mwadini Makame amewataka Manahodha wa Ngarawa waendelee kudumisha utamaduni wao wa kufanya mashindano ya Resi za Ngalawa kila ifikapo nuda wa maadhimisho ya shererhe za Mapinduzi ya Zanzibar. 
Wito huo aliutoa jioni ya jana wakati alipokuwa akitoa nasaha zake kwa Manahodha walioshiriki mashindano hayo huko Forodha Mchanga Mjini Zanzibar ikiwa ni shamra shamra za kutimiza miaka 49 ya Mapinduzi Zanzibar. 
Alisema kuwa Resi za Ngarawa ni moja ya utamaduni wa Zanzibar hivyo ipo haja ya kuenziwa mchezo huo ili kukuza utamaduni na kudumisha Mapinduzi ya Zanzibar yaliyo wakomboa wananchi wa Zanzibar kutoka kwa Wakoloni.
“Udumisheni utamaduni huu kwani unaleta mshikamano na furaha miongoni mwenu na ni njia nzuri ya kudhihirisha utamaduni wetu kwani Zanzibar watu wake ni wavuvui kihistoria” alisema Mwadini
Alifahamisha kuwa kuudumisha mchezo huo ni kuwapa umuhimu Wavuvi ilikuona na wao wanathaminiwa na taifa lao kwavile viongozi wa Serikali ndio wanaokuwa Wageni rasmi na Wadhamini wa mchezo huo.
 Waziri Mwadini aliwaomba Washriki wa mchezo huo kuwahamasisha wenzao kutoka Vitongoji mbalimbali vya Zanzibar kushiriki mchezo huo ili kuunogesha zaidi.
Aidha aliwataka pia Washirikia kujiandaa vyema zaidi katika mashindano yanayokuja na kuuthamini mchezo wao huo ambao amedai kuwa hauna tofauti na michezo mingine inayochezwa Zanzibar  
Mchezo huo ulishirikisha ngalawa 10 kutoka vitongoji mbali mbali vya unguja kama vile Dimani ,chukwani ,Nyamazi Bumbwni ambapo Mshindi wa mchezo huo Fundi Abubakari kutoka Bubwini alizawadiwa Shilingi Laki 2.

 IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR  11/01/2012

[ Read More ]

MUUNGANO WA MAKAMPUNI YA OMAN KUWEKEZA SHIRIKA LA NDEGE ATCL SHS. BILIONI 160

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Oman Oktoba mwaka 2012 baada ya kualikwa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said ambapo aliambatana na ujumbe wa mawaziri na viongozi waandamizi wa biashara.
Katika ziara hiyo Rais Kikwete alibadilishana uzoefu wa uhusiano na kuangalia namna ya kudumisha
ushirikiano wa nchi hizo mbili kuhusiana na biashara, elimu, utamaduni na mambo mengine.
Hiyo ilikuwa ni ziara ya pili muhimu ya kiongozi wa Tanzania kutembelea nchi hiyo tangu mwaka 1985 wakati Rais wa kwanza, hayati Julius Nyerere akiwa madarakani.
Ziara hiyo ya Rais Kikwete inaonyesha umuhimu wa namna nchi hizo mbili zinavyojenga mahusiano makubwa na undugu baina yao.
Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na Oman lililofanyika Oktoba 16 katika Hoteli ya Al Bustan Palace wakati Rais Kikwete akitoa hotuba yake.
Kongamano hilo liliangalia fursa za kibiashara katika rasilimali zilizopo katika nchi hiyo iliyopo Ukanda wa
Afrika Mashariki zikiwemo kilimo, viwanda, utalii, usafirishaji, mafuta na gesi.

Kituo cha Uwekezaji (TIC)Tanzania kiliwasilisha namna uwekezaji katika kiuchumi na nafasi za uwekezaji nchini Tanzania.
Mwishoni mwa tukio hili muhimu, malaka za nchi hizi mbili zilisaini na kukubaliana kuanzisha Baraza la Biashara kati ya Oman na Tanzania ambalo litakuwa ni hatua muhimu katika kuanzisha uhusiano wa mataifa hayo mawili katika ngazi ya juu.
Madhumuni mengine muhimu ya ziara hiyo yalikuwa ni pande hizo mbili kusaini makubaliano ya kukuza na kuulinda uwekezaji jambo ambalo ni kichochezi katika Baraza hilo la Biashara la Oman na Tanzania, itarahisisha kutoa fursa za kibiashara na uwekezaji kati yao.
Pia makubaliano ya kupeana ushauri katika masuala ya siasa yamesainiwa hivyo itakuwa ni njia nzuri ya uzileta nchi hizo mbili zenye undugu karibu katika jambo hilo
muhimu.
Walisaini makubaliano kuhusu Utunzaji kumbukumbu na Nyaraka ambazo zinatunza kumbukumbu za historia muhimu kwa vile nchi hizo mbili zina historia inazofanana kiasi fulani.
Kubadilishana huko kwa nyaraka na kumbukumbu za historia kunaweza kusaidia kuchimbua matukio
ya kihistoria yaliyotokea zama hizo. Walisaini makubaliano ya kushirikiana katika elimu ya juu.
Oman na Tanzania zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu hivyo ziara hiyo ya Rais Kikwete inalenga
kufungua fursa nyingi na hatimaye kufikia ngazi wanazostahili wananchi.
Nchi hizo zinafaidika na upendo baina ya watu wake kwa sababu Oman ni nchi pekee nje ya Afrika ambako wananchi wengi wanazungumza Kiswahili na Wa-Oman wamezaliana na Watanzania pamoja
na kuwa na utamaduni wa aina moja.
Kuna uwezekano mkubwa wa kufungua fursa za usafiri wa ndege ndani na nje ya Afrika katika uwekezaji na biashara katika juhudi za kibinadamu.
Tanzania ina fursa kubwa za uwekezaji katika sekta za
mifugo, uvuvi na kilimo.
Ikiwa imebarikiwa kuwa na eka za ardhi yenye rutuba, maji na hali nzuri ya hewa, Tanzania ni mahali
pazuri kwa Oman kuwekeza na kukuza shughuli za kilimo ili kufanikisha mahitaji yake.
Hii ni namna Oman inavyoweza kujibadilisha yenyewe kutoka kuwa muingizaji wa bidhaa nchini na kuwa muuzaji wa bidhaa za matunda na mboga mboga nje ya
nchi hivyo kujihakikishia kutokuwa tegemezi wa chakula.
Kwa vile Tanzania imegundua visima kadhaa vya Mafuta na gesi, na nchi hizo mbili zinaweza kuanzisha
ushirikiano katika suala hili ambalo litawanufaisha wote kwa pamoja.
Oman inaweza kuwekeza katika miundombinu iliyokua nchini Tanzania kama barabara, madaraja, hoteli,
resort na pia katika usafirishaji, na sekta ya usafiri wa njia ya meli.
Pia sekta ya viwanda itatoa fursa za uwekezaji kwa Serikali ya Oman na jamii ya biashara.
Cha muhimu ni kwamba nchi ya Tanzania yenye ananchi 44,929,002 inahudumia soko la watu milioni 150 katika nchi zake za jirani kupitia Bandari ya Dar es
Salaam.
Tanzania ni nyumbani kwa baadhi ya maeneo muhimu duniani kwa shughuli za utalii na miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la wageni kutoka Oman wakienda nchini Tanzania jambo ambalo limefanya safari za ndege za Ndege ya Oman ziwe nyingi.
Tanzania ni nchi kubwa zaidi Afrika Mashariki ikiwa na jiografia inayoruhusu uwekezaji katika sekta ya utalii ambapo pia inasifika kuwa na hali nzuri ya hewa, ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha na rasilimali
ambayo inavutia uwekezaji.
Baada ya ziara Rais Mheshimiwa Dk.Jakaya Kikwete, Umoja wa wadau wa biashara nchini Oman umeamua kuwekeza fedha kiasi cha sh.bilioni 160 ili kuendeleza Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).
Hatua hiyo ilikuja baada ya mkutano kati ya Kikwete na ujumbe wa wafanyabiashara hao.
Akizungumza wiki hii, Mwenyekiti wa Al Hayat Development na kampuni yake ya uwekezaji, Sheikh
Salim Al Harthy alisema wanashukuru kwa msaada huo uliotolewa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said Sultan wa Oman.
Alisema wanashukuru kwa vile msaada huo utasaidia na kuimarisha ushirikiano wa kibiashara kati ya mataifa hayo mawili hasa baada ya makubaliano kufikiwa kati ya viongozi wa nchi hizo.
Na kama sehemu ya kujitolea kwao huko wanadhamiria kusaini makubaliano na Air Tanzania na kuwekeza
dola milioni 100 na kuongoza wawekezaji ambao tumekuwa na uhusiano nao wa karibu.
Alisema uekezaji huo utatumika katika kukodisha na kununua ndege ambazo zitatumika katika safari za
ndani na nje ya Afrika kukuza biashara ndani ya Tanzania na nchi
nyingine.
Sheikh Salim Al Harthy aliongeza kuwa fursa hiyo ilikuja kwa ukarimu na matarajio mazuri ya Rais Kikwete na Serikali ya Tanzania kwa kutuamini kuja kuwekeza
katika kushughuli za kiuchumi nchini Tanzania.
“Tunamshukuru Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said wa Oman na Rais Kikwete wa Tanzania kutupa nafasi
hiyo hasa ukizingatia kipindi hiki tuna mpango wa kujenga kituo cha mafunzo ya masuala ya ndege, ofisi
nzuri kwa ajili ya ATCL, kununua ndege na kufanya shughuli nyingine za maendeleo tunazotarajia kuanza
ndani ya miezi sita hadi kumi” alisema.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akiwa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said wakati wa
ziara yake nchini Oman.
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Al Hayat, Shaikh Salim Al Harthy, wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mkuu wa ATCL, Kapteni Milton Lazaro. Wa kwanza kushoto ni Al Sayyid Fahar Bin Taimur Al Said na kulia ni Bwana Saeed S. Bawazir kama wa wakilishi wa Al Hayat inchini Tanzania.
[ Read More ]