Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook


When you are really focused with what you believe and want to achieve then there is a point in life that you have to eliminate some people no matter how close they are you have to free them and it hurts but its healthy as long as they make you loose focus then they should go....come back to them when you are satisfied with your achievements....and they will understand and be happy and proud of you and if NOT then they were never real and true to your life.
[ Read More ]

[ Read More ]

Zanzibar Yajinyakulia Tuzo ya Utalii Nchini Russia


ZANZIBAR imefanikiwa kuwa mshindi wa kwanza na kujinyakulia tuzo ya Utalii nchini Russia kwa mwaka 2011, ‘Star Travel.ru 2011’.
Tuzo hiyo hushindaniwa kila mwaka kwa maeneo yalio bora zaidi kwa shughuli za kiutalii barani Afrika, ambapo watalii na waongoza watalii wa nchi hiyo hutembelea.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Mkurugenzi Mkuu wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Ali Khalil Mirza, amesema amepokea taarifa hiyo kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Russia, ikielezea Zanzibar kuchaguliwa kuwa mshindi wa tuzo hiyo, kama eneo lililo bora kwa shughuli za kiutalii barani Afrika.

Alisema kuwa kinyang’anyiro hicho kilihusisha maeneo 23 yalio bora zaidi kwa shughuli za kiutalii, ispokuwa nchi ya Misri haikushirikishwa.
Alisema tayari tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Ubalozi wa Tanzania nchini humo tangu juzi katika hafla maalum ilioambatana na kuanza kwa maonyesho ya Kimataifa ya Utalii nchini.
Mirza alisema ushindi wa tuzo huyo unatokana na msukumo mkubwa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Russia pamoja na hatua ya Kamisheni hiyo kufanya ziara maalum ya kuutangaza utalii wa Zanzibar mnamo 2009.
Alisema makubaliano yaliofikiwa kati ya Kamisheni ya Utalii na Makampuni ya kutembeza watalii yamelifanya soko la Utalii nchini Russsia kuimarika, ambapo wastani wa watalii 300 hufika nchini kila mwaka tangu wakati huo.
Alieleza kuwa hayo ni mafanikio makubwa kwa soko la utalii nchini Russia kwa kuzingatia watalii wanaokuja ni wale wanaotumia zaidi, ambao hufikia katika Hoteli zenye hadhi za juu kama vile Plan Hotel,Lagema,Green of Zanzibar na The Residents.
Aidha alisema Kamisheni yake ina matumaini makubwa kuwa ifikapo 2013 idadi ya wataalii kutoka nchi hiyo itaongezeka, hususan pale Shirika la ndege la Uturuki litakapoanza kufanya safari zake moja kwa moja hadi Zanzibar, ikizingatiwa watalii hao hivi sasa hutumia usafiri wa Shirika la Emirates, na kutembelea kwanza katika Mbuga za wanyama na hatimae kuja Zanzibar.
Mkurugenzi huyo alivitaja baadhi ya vigezo muhimu vinavyozingatiwa katika kumpata mshindi wa tuzo hiyo, kuwa ni pamoja na hali ya usalama, kufikiwa kwa matarajio ya wageni, vivutio vya utalii ikiwemo michezo mbali mbali (pwani na ufukweni), huduma katika mahoteli pamoja na tamaduni za wenyeji.
[ Read More ]

Balozi Seif Afungus Semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Kuhusiana na MKUZA




Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wanaoshiriki Semina ya Siku Moja inayohusu utekelezaji wa Mkuza wakisikiliza Hotuba ya Ufunguzi iliyotolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hayupo Pichani huko kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika Picha pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar baada ya kuifungua Semina ya Utekelezaji wa Mkuza nje wa ukumbi wa Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani.
Juhudi za kupambana na Umaskini hapa Nchini ni vyema zikajikita zaidi katika kuimarisha Uchumi sambamba na huduma za Kijamii kwa lengo la kustawisha maisha bora ya Wananchi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema hayo wakati akiifungua Semina ya siku mbili ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar inayohusu utekelezaji wa Mpango wa Kupunguza  Umaskini Zanzibar { MKUZA } inayofanyika katika Hoteli ya Neptune Pwani Mchangani.
Balozi Seif alisema wimbi la umaskini hushamiri iwapo jamii itakosa huduma za Elimu, ongezeko la uzazi katika umri mdogo, ukosefu wa usawa wa kijinsia pamoja na uchumi duni kwa akina mama ambao ndio wengi katika familia.

Balozi Seif alisema Umoja wa Mataifa umepitisha Azimio la utekelezaji wa Malengo la Milenia ili Dunia iondokane na umaskini ifikapo mwaka 2015 na kuzitaka Nchi Wanachama hasa zinazoendelea kujipangia mikakati ya kuuondoa Umaskini kwa kupitia utekelezaji wa Mipango yao ya maendeleo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisisitiza kwamba Serikali imo katika hatua za kupambana na umaskini kupitia utekelezaji wa Mkuza ingawa Wananchi waliowengi bado hawajaelewa Mpango huu.
Alieleza kwamba yapo mafanikio makubwa yamepatikana katika huduma za Kijamii zikiwemo Elimu, Afya na huduma za Maji safi mafanikio yanayoonekana zaidi kwenye kupunguza umaskini usio wa kipato.
Akizungumzia changamoto zilizojichomoza wakati wa utekelezaji wa Mkuza Balozi Seif alisema Mfumko wa bei umekuwa bado tatizo kinyume na lengo la chini ya asilimia 10% ukiathiriwa zaidi na ongezeko la bei ya mafuta na chakula katika soko la Dunia.
Akigusia Ukuaji mdogo wa Sekta ya Kilimo wa asilimia 4.6 Balozi Seif alisema unaonekana kushusha mchango wa Sekta hiyo katika pato la Taifa wakati Sekta ya Kilimo bado ni muajiri Mkuu wa nguvu kazi ya Taifa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alifahamisha kwamba hali hiyo imechangia kuwa na mafanikio madogo katika kuhakikisha kuwepo kwa usalama wa chakula.
Semina hiyo ya siku mbili inahusisha Mada kadhaa ikiwa pamoja na Mipango ya Maendeleo, Mapitio ya Dira
ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020, Matokeo muhimu katika uchagumbuzi wa matumizi ya kaya pamoja na maandalizi ya Bajeti na mahusiano na Mkuza.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
[ Read More ]