Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

UN yalaani hatua ya Korea Kaskazini


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya kukutana kwa dharura, hatimaye limeshutumu vikali hatua ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la kinyuklia.

Baraza hilo lilikutana kwa dharura saa chache tu baada ya jaribio hilo kufanywa na limeonya hatua kali zitachukuliwa dhidi ya Korea Kaskazini.

Kauli ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa imetolewa muda mfupi tu baada ya serikali ya Korea Kaskazini kutangaza imefanya jaribio lililofanikiwa la Kombora la nyuklia lililo kubwa zaidi ya lile iliyolipua mnamo mwaka wa 2006.

Mataifa wanachama sasa wanataka hatua kali zichukuliwe dhidi ya Korea Kaskazini ambayo tayari iko chini ya vikwazo vya baraza hilo la usalama la Umoja wa Mataifa. Lakini serikali ya Korea Kaskazini imepuuza kauli hiyo na kusema iko tayari kukabiliana vilivyo na wapinzani wake wote.

Wataalamu wa makombora wa Urusi wanasema kombora lililolipuliwa lina uwezo sawa na yale yaliyoangushwa na Marekani katika miji ya Hiroshima na Nagasaki nchini Japan wakati wa vita vya pili vya dunia.

Hata China ambayo imekuwa ikiunga mkono Korea Kaskazini chinichini sasa imesema itakubaliana na azimio lolote la Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa.

Ili kuelewa wasiwasi huu ambao umekumba jamii ya kimataifa ni muhimu kuelewa uwezo wa zana za Kinyuklia.

Kulingana na shirika moja la utaalamu wa kivita la Marekani, Center for Defense Information, makombora matano au sita ya aina iliyofanyiwa majaribio siku ya Jumatatu, yakilipuliwa mara moja yana uwezo wa kuharibifu duniani kote na kuwaacha manusura wachache sana.

Ikiwa na silaha kama hizi, si ajabu Korea kaskazini sasa imeionya Marekani itakabiliana nayo kivita iwapo serikali ya Rais Obama itajaribu kuishambulia

[ Read More ]

Uchumi wa Afrika kusini umekumbwa na mdororo


Uchumi wa Afrika kusini umekumbwa na mdororo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1992, kufuatia kupungua kwa kasi ya uzalishaji viwandani halikadhalika sekta ya madini.

Uchumi wa nchi yenye Uchumi bora barani Africa imerekodi upungufu wa kiwango cha hadi asili mia 6.4% kati ya mwezi Januari na March, ikilinganishwa na kipindi kama hiki mwaka jana.

Hiki ndio kiwango kikubwa cha upungufu tangu mwaka 1984 kikifuatiwa na mdororo wa asili mia 1.8% kila mwaka katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.

Sekta ya ujenzi hata hivyo imeimarika kutokana na mashindano ya mpira ya Kombe la Dunia yanayopangwa kufanyika huko.

Afrika kusini imenufaika chini ya mpango kabambe wa serikali wa uwekezaji katika mipango ya mashindano ya mpira ya mwaka 2010.

Takwimu zilizofanywa na kampuni huru 'Statistics South Africa, imebaini kupungua kwa uzalishaji viwandani pamoja na uwindaji wanyama pori vimechangia mno mdororo huo.

Makampuni ya kuchimba migodi yameathiriwa na mdororo wa uchumi duniani.

[ Read More ]