Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Just in:

Inna lillahi waina ilaihi rajiun.

Ajali ya boti iliyokuwa ikitokea Pangani Tanga imezama watu wanane wamefariki wakiwemo watoto watatu. Na watu kumi na moja wamepotea baharini. Wengine wameokolewa na boti ilikuwa na jumla ya watu 35. Chombo hicho kimezama kutokana na hali ya hewa ya upepo,Mammlaka ya hali ya hewa jana mwanzoni mwa week hii imetoa tahadhari ya kuwepo kwa mvua kubwa na upepo.
[ Read More ]

Gas City: Hospitali ya Apollo kujengwa Kilwa


Wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi na wakaazi wa mikoa ya kusini kwa ujumla, wanatarajia kunufaika na ugunduzi wa gesi katika visiwa vya Zafaran na Lavan vilivyopo wilayani huo. Kampuni ya Statoil kutoka nchini Norway ikishirikiana na Exxon Mobil imegundua gesi katika Visiwa vya Zafaran na Lavan vilivyopo Kitalu namba 2, Ukanda wa Pwani ya Tanzania, hususan Pwani ya Kilwa mkoani Lindi. Kutokana na ujio wa wageni hao, Watanzania hususan wakazi wa Kilwa, Lindi na Mtwara kwa jumla hawana budi kupata faida za moja kwa moja na zingine zisizo za moja kwa moja ikiwemo gesi hiyo kutumika kutengeneza umeme utakaopatikana kwa uhakika na kuuzwa kwa wananchi wote. 
Akizungumza mjini Kilwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Kilwa, Adoh Mapunda amesema kuwa, madiwani, watendaji na mkuu wa wilaya wamekaa na kutafakari kwa kina juu ya faida ya kudumu itakayoonekana wilayani humo kutokana na ujio wa mradi wa gesi. Amefafanua zaidi kuwa mradi huo ni ujenzi wa hospitali ya kimataifa itakayolingana na ile ya Apollo nchini India ambayo viongozi mbalimbali duniani hukimbilia kwenda kutibiwa ambayo itajengwa na mwekezaji na itaendeshwa na taasisi nyingine ya kimataifa huku halmashauri ikiwa na hisa za kupata gawiwo la kila mwaka kutokana na faida. Mpango huo unatekelezwa kupitia utaratibu uliopo katika mikataba kwa wawekezaji kuhusu uwajibikaji na ushiriki katika masuala ya kijamii. Amesema kuwa, tayari Statoil imetenga Sh18 bilioni kuanza ujenzi wa hospitali hiyo mjini Kilwa wakati wowote kuanzia mwaka huu ambapo michoro ya hospitali hiyo ipo tayari huku ikitarajia madaktari bingwa kutoka ndani na nje ya nchi na itakuwa na wafanyakazi wataalamu, pamoja na wahudumu ambao wengi watatoka Halmashauri ya Kilwa.

[ Read More ]

Dr Shein swears in permanent secretaries for national unity government


Zanzibar President Dr Ali Mohammed Shein swears in Dr Abdulhamid Yahya Mzee at a ceremony at Zanzibar State House yesterday after appointing him Isles’ Revolutionary Council Permanent Secretary. (Photo: Ramadhan Othman)
 

Employment History

  • President
    Zanzibar

Board Memberships and Affiliations

  • Chief Secretary
    Zanzibar
  • Chief Secretary
    Zanzibar Revolutionary Council
  • Permanent Secretary
    Revolutionary Council
Zanzibar President Dr Ali Mohammed Shein yesterday sworn in the newly appointed permanent secretaries for the government of national unity.
The new permanent secretaries were appointed on Thursday evening, whereby he re-appointed all the permanent secretaries, who had saved in the sixth phase government.
According to a press statement availed to the media, Abdulhamid Yahya Mzee was appointed Chief Secretary and Secretary of the Zanzibar Revolutionary Council, while Salum Maulid Salum was appointed as Permanent Secretary in the President’s Office and Chairman for the Revolutionary Council, State House.
Others are Abdalla Juma Abdalla, Deputy Permanent Secretary (Special Government Departments), Said Abdalla Natepe, Deputy Permanent Secretary (International Cooperation and Coordination of activities of Zanzibaris living abroad), Mwinyiusi Abdalla Hassan, Deputy Permanent Secretary (Regional Administration and Local Governments).
Other permanent secretaries include Khami Mussa Omra, who has been re-appointed as Permanent Secretary in the Ministry of Finance, Economy and Development Plans and Abdi Khamis Faki Deputy Secretary in the Ministry of Finance.
Dr Shein also appointed Amina Khamis as Executive Secretary for Zanzibar Planning Commission and Joseph Abdalla Meza as Permanent Secretary in the President’s Office Civil Servant and Good Governance and his Deputy is Yakout H Yakout, Dr Omar Dadi Shajak, Permanent Secretary in First Vice President Office and Dr Ismal Seif Salum as his deputy.
Dr Khalid Said Mohammed has been appointed as Permanent Secretary in the Second Vice President Office and his deputy is Said Shaaban Said.
Dr Shein also has appointed Asaa Ahmada Rashid as Permanent Secretary in the Ministry of Constitution and Justice and his deputy is Abdughani Msoma, while Mwanaidi Saleh Abdalla has been appointed Permanent Secretary in the Ministry of Education and Vocational Training and his deputy is Mzee Abdalla Mzee Abdalla.
Mohammed Saleh Jidawi has been re-appointed in the Ministry of Health, while Dr Malik Abdalla Juma as Director General in the Ministry.
Others appointed are Vuai Idd Lila, the Ministry of Infrastructure and Communication and his deputy is Msanif Haji Mussa.
Rahma Mohammed Mshangama had been appointed to the Ministry of Social Welfare, Youth Development, Women and Children and her deputy is Msham Abadalla Khamis.
Other permanent secretaries are Ali Saleh Mwinyikai in the Ministry of Information, Culture, Tourism and Sports and his deputy is Issa Mlingoti Ali.
Other appointed permanent secretaries and their deputies are Mwalimu Ali Mwalimu (Ministry of Land, Housing, Water, and Energy), his deputy is Tahir M. Abdalla, Julian Raphael (Ministry of Trade, Industries, and Marketing), his deputy is Rashid
Ali Salum, Asha Ali Abdalla (Ministry of Labour, Peoples Economic Empowerment and Cooperatives), his deputy is Ali Khamis Juma, Othman Maalim (Ministry of Agriculture and Natural Resources), his deputies are Juma Ali Juma and Dr Bakar Asseid (Natural Resources).
The president also appointed Dr Kassim Gharib as permanent secretary in the Ministry Livestock and Fisheries, his deputy is Dr Omar Ali Ameir.
The newly appointed permanent secretaries and their deputies come from the main political CCM and CUF that form the national unity government.
Isles Constitution as amended also allows the new power-sharing government to distribute ministerial positions to the respective parties in accordance with percentage of votes scored by the parties in the general elections.
[ Read More ]

Two die in helicopter crane crash in Vauxhall, London

 
Two people have died after a helicopter crashed into a crane at a building site in central London in misty conditions, police have said.
read more http://www.bbc.co.uk/news/uk-england-21040410
[ Read More ]

Saikolojia: Namna ya kutambua tabia ya mtu


Hakuna anayependa kusahihishwa, kugombana au kukemewa mbele za watu, hii ndiyo tabia ya watu wajeuri na walio na tabia za kitukutu. Mara nyingine hudhani wanapata sifa. Wako watu wa jinsi hii ambao hawawezi kukugombeza au (kukupa vidonge vyako) mkiwa wawili peke yenu, watangoja watu wengine wawepo ndiyo waanze kubwabwaja, cha kufanya jiepushe nao.


Kwa kule kukimbiwa na marafiki, na kuwa mpweke, huongeza tabia za kitukutu na kijeuri na hii huwafanya watu hawa kutambulika haraka na kiurahisi zaidi.

Zifuatazo ni alama zitakazokutambulisha mtu jeuri na mtukutu:

a) Alama za kimaneno
Mara kwa mara hupendelea kusema maneno haya vinywani mwao.
Nakwambia bora unge…”
Wewe sichochote, silolote…”
Nakwambia, lazima u...”
Fanya vile ninavyokuambia mimi…”
Nataka u...”
Wewe endelea tu tutaona...”

b) Alama za kimwili
Hupendelea kusimama wima
Huwa wenye pozi kavu, ngumu (still and rigid pause)
Hupenda kukunja mikono
Hupenda kupayuka au kupigia wengine kelele
Hupenda kuwanyooshea wengine vidole.
Hupenda kuwazodoa wengine na vidole (hawezi kukuelekeza hadi kidole chake kikusukume)
Hupenda kupiga au kugonga meza na viti akizungumza



2. Watu wapole, waliotayari kukubali kushuka (Submissive)
Hawa ni watu wanaopenda kujitoa sadaka kwa ajili ya manufaa ya wengine. Kwa hali hii ni rahisi watu hawa kujikuta wanatumiwa vibaya na watu wengine hasa wale wajeuri na watukutu tulio waangalia awali.

Mara nyingi watu walio wapole na wanaokubali kushuka hupenda kuwatia moyo wengine wawe kama wao. Katika vizazi vilivyopita, wanawake walitegemewa zaidi kuwa watu wa kundi hili. Ni mabadiliko ya maisha na ya jamii ya leo ambayo yamemfanya hata mwanamke kuwa mjeuri na mshindani tofauti na jamii za awali.

Kwa upande mwingine mfumo wa maisha wa vizazi vya nyuma ulimweka chini mwanamke na kuzuia maendeleo yake hasa katika kujiendelezea vipawa alivyonavyo kwa vigezo tu kwamba yeye ni wakukubali chochote na wakati wowote sasa tunayaona mabadiliko kwa kiasi fulani.

Mara kwa mara watu wapole, na waliotayari kushuka wamekuwa wenye hisia za kinyonge na kutengwa, wakijihisi kutokuwa salama wakati mwingi. Kujijali, kujipenda na kujithamini kwa watu hawa siyo kwa kudumu, bali kunakuwa na nyakati za kuyumbayumba kutokana na mazingira. Hawa siyo watu wenye ujasiri ndani yao wenyewe na hata katika vile wavifanyavyo.

Mara mtu wa kundi hili anapokutana na mtu mjeuri na mtukutu, hofu na ujasiri wake hupungua sana, na anaweza kukubali kupingwa hata kama alikuwa ana haki. Kwa sababu mara nyingi watu wa jinsi hii wanajua kuwa kwa upole wao watu wengi wamekuwa wakiwatumia na kuwachezea, hii imewafanya wawe ni watu wenye vihasira vya mara kwa mara.

Kwa sababu wameunganishwa na hisia zao zaidi, ni rahisi wao kuzielezea hisia zao kwa mtu mwingine, hata kama hisia zao ni za kujutia kile walicho kifanya wenyewe. Mara nyingi husikia amani kwa yale wanayofanya au kuyaamua.

Ingawa mara nyingine mambo huwaendela tofauti na walivyopanga, watu hawa hufahamu kuwa hawanabudi kukubali kosa au na kuwa tayari kujifunza kutokana na yale makosa.

Mambo yanapowaendea vema hupenda kujisifia na kujiona walio juu. Mara nyingine misimamo yao huwashawishi na kuwavutia wengine watazame kama wao, sio watu wanaopenda kuwatumia wengine vibaya (being manipulative) kama vile kuwasema au kuwasengenya wengine, hii huwafanya kuwa na wafuasi au washabiki wengi zaidi.

Kule kujiamini kwao na kuwa na ujasiri hupunguza sana msongo wa mawazo maishani mwao na hii huwasaidia kuelekeza nishati na nguvu zao zote katika kufikia malengo waliojiwekea.

Mara kwa mara sio watu wenye mabadiliko ya hisia (change of attitude) na hii hufanya mahusiano yao na wengine kuwa yasiyoyumba na mawasiliano baina yao na wengine huwa wazi, sio watu wakuficha wanachokiona, uwazi walionao kuwaweka huru.

Hujisikia vema hujipenda na kujithamini muda mwingi. Hujijengea hisia za usalama na imani kwa sababu ya mawasiliano bora walionayo na wale wanaowazunguka, hii pia husababishwa na wao kuelewa fika wajibu wao na wajibu wa wengine pia.

Ingawa wanaweza kuwa wabishi, lakini huheshimu misimamo ya wengine na kupenda ya kwao iheshimiwe pia na hii huwafanya kuwa na ushirika na wale wanaowazunguka. Mara nyingi ni wazuri katika kuwatia wengine moyo kujitahidi zaidi.

Alam za kuwatambua:
Alama za maneno
Nahisi……. Najisikia kuu……………”
Ningependa kuu…………”
Wewe unaonaje hapa/mawazo yako nini…………..”
Unadhani njia gani bora kulishuhulikia hili ………..”
Nafikiri………..”
Hembu tu……………..”

Alama za kimwili
Hupenda kuwa wima ila wenye pozi laini (relaxed stance)
Huangalia kijasiri na kuangalia usoni (kukodoa macho).
Huwa na hisia za upole, kujitawala na kujimiliki wenyewe

Kwa vyovyote vile, mara zote unapokutana na mtu mwenye tabia yeyote kati ya hizi tatu kumbuka una haki ya kufanya yafuatayo;

Jifunze kuelezea hisia zako njema (usiogopoe au kuona aibu kwakuwa hutokuwa umejitendea haki)
Jifunze kuzielezea hisia zako mbaya au za hasira, kamwe usifunike. Mfano; “Sipendi kabisa unavyokula”
Jifunze kusema hapana, Mfano; “Hapana sitaweza kufika leo”

Toa wazo la kweli, usipake watu mafuta kwa mgongo wa chupa. Mfano; “Mimi siliafiki hilo jambo hata kidogo”
Kiri kuwa umekasirika, hasa pale ambapo haunabudi kukasirika.

Mfano: “Kweli umeniudhi sana baada ya kusema hayo maneno”. Usitoe tabasamu la mamba tu, kutabasamu wakati ndani yako unahisi kuungua moto.

source: Jamii forum.
[ Read More ]

TANZANIA YASHINDA KATIKA SHINDANO LA KUTAFUTA MAAJABU SABA YA ASILI YA BARA LA AFRIKA

Bodi ya Utalii Tanzania inapenda kuwaarifu wananchi na umma kwa ujumla kuwa Tanzania itakuwa ni
miongoni mwa nchi ambazo angalau moja ya vivutio vyake kitaingia katika orodha ya Maajabu Saba ya Asili
Barani Afrika baada ya kukamilika kwa upigaji wa kura katika shindano la kutafuta Maajabu Saba ya Asili
Barani Afrika Desemba31, 2012 na Tanzania kuwa miongoni mwa washindi

Kampeni ya kutafuta Maajabu Saba ya Asili ya Bara la Afrika ilikuwa iikiendeshwa na Taasisi ya Seven
Natural Wonders yenye makao yake makuu nchini Marekani tangu mwaka 2008 ambapo upigaji wa kura
ulihusisha Taasisi za Kimataifa ikiwemo taasisi ya uhifadhi asili wa Mazingira (IUNC) na wataalamu wengine
duniani ambao walipiga kura kwa kuzingatia zaidi umuhimu wa asili, upekee na uzuri wa kivutio husika.
Taasisi hiyo ya Seven Natural Wonders imewasiliana na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania,
Dr. Aloyce Nzuki na kumfahamisha kuhusu matokeo ya awali na kumthibitishia kuwa Tanzania ni kati ya nchi
zilizoshinda na kwamba vivutio vyake zaidi ya kimoja vitakuwa miongoni mwa Maajabu hayo Saba ya Asili
Barani Afrika. Tanzania itakuwa mwenyeji wa sherehe za tukio la utangazaji wa vivutio vilivyoshinda katika
shindano hili na kwamba itakuwa ni fursa kwa Watanzania na Afrika kwa ujumla kufurahia tukio hilo na
Maajbu yatakayoshinda.
Sherehe za utangazaji wa washindi zitafanyika jijini Arusha katika Hotel ya Mt Meru Februari 11, 2013 ambapo
watu mashuhuri kutoka nchi mbalimbali Barani Afrika, na wandishi kutoka vyombo vya habari vya Kimataifa
na ndani ya nchi wataalikwa kushiriki katika sherehe hizo na kushuhudia utangazaji wa vivutio vya Tanzania na
vingine vya Afrika kuwa Maajabu Saba ya Asili Barani Afrika.
Bodi ya Utalii Tanzania inapenda kuwashukuru watu wote ndani na nje ya Tanzania walioshiriki katika kupigia
kura vivutio vya Tanzania. Vivutio vya Tanzania vilivyokuwa katika shindano hili ni Mlima Kilimnajaro,
Bonde la Ngorongoro, na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mwendeshaji
Bodi ya Utalii Tanzania
Jengo la IPS ghorofa ya tatu
Mtaa wa Samora/Azikiwe
S.L.P 2485 D’slaam, Tanzania
[ Read More ]

MHE. MWANRI AZITAKA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUSIMAMIA VIZURI FEDHA ZA MIRADI YA SERIKALI




Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri akipima kwa tape maalum urefu wa moja ya barabara zilizojengwa na Manispaa ya Sumbawanga katika Mji huo kuhakikisha kama barabara hiyo imejengwa kwa vipimo vilivyoanishwa kwenye mpango wa ujenzi huo (BOQ). Naibu Waziri huyo alitumia fursa hiyo kuziasa halmashauri zote nchini kusimamia vyema fedha za Serikali katika miradi kuhakikisha inafanana na thamani ya fedha zilizotumika, alilazimika kusema hayo baada ya kubaini mapungufu mbalimbali katika mradi huo wa barabara na miradi mingine aliyofanikiwa kuitembelea Mkoani Rukwa.
Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe. Agrey Mwanri akikagua barabara za lami zilizo chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga zilizojengwa hivi karibuni. Katika ukaguzi huo alibaini mapungufu mbalimbali katika ujenzi huo na kuagiza Halmashauri hiyo kuhakikisha mapungufu hayo yanaondolewa. Aliitaka pia halmshauri hiyo kusimamia vyema kazi za Serikali kuepusha minong’ono inayotoka kwa wananchi juu ya utendaji mbovu wa baadhi ya watendaji Serikalini.
Mhe. Agrey Mwanri akiweka jiwe la msingi kiwanda cha unga cha Malangali kinachomilikiwa na muwekezaji wa ndani mapema hivi leo. Kwa sasa Mkoa wa Rukwa una viwanda vitatu vya unga vinavyomiliwa na wawekezaji wa ndani.  
Naibu wa Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Agrey Mwanri akikagua kiwanda cha unga cha Malangali Mjini Sumbawanga leo alipotembelea kiwandani hapo kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi.
Mhe. Mwanri akizungumza na wakazi wa Mji wa Sumbawanga katika Stendi kuu ya mabasi ya Mjini hapo ambapo alipokea kero mbalimbali ikiwepo ubovu wa miundombinu ya umeme na barabara katika stendi hiyo. Aliuagiza uongozi wa Manispaa ya Sumbawanga kufanya Mkutano wa hadhara na wananchi hao kuskiliza kero zao zote pamoja na kuzitaftia ufumbuzi na kumpelekea taarifa ya utekelezaji.
Katika hali isiyotegemewa msafara wa Mhe. Mwanri ulipowasili katika kijiji cha Mlanda katika Manispaa ya Sumbawanga kwa ajili ya Mkutano wa hadhara ulikuta msiba ambapo walishiriki na kutoa ubani ambapo Mhe. Mwanri alitoa laki moja na alfu mbili na aliyekuwa Mbunge wa Sumbawanga Mjini CCM ambaye pia ni Mjumbe wa halmashauri kuu Taifa ya CCM (NEC) kupitia Mkoa wa Rukwa Aeshi Hillal alikabidhi shilingi alfu hamsini. 
(Picha na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa – rukwareview.blogspot.com)
[ Read More ]

RAIS SHEIN AZINDUA MRADI WA ONE WORLD FOOTBAL


shein akiongea
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohammed Shein ameuagiza uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzi ya Amali kuhakikisha michezo yote inayoruhusiwa kisheria Zanzibar kuchezwa mashuleni isipokuwa mchezo wa Ngumi (Boxing).
Amesema michezo yote inafaa kuchezwa wala haipunguzi kasi ya mwanafunzi kusoma na kwamba Wizara inapaswa kulisimamia agizo hilo ili Zanzibar iweze kupata vipaji vitakavoiletea nchi Medali za mashindano ya kitaifa na kimataifa.
Rais Shein ameyasema hayo alipokuwa akizindua Mradi wa “Mpira Mmoja” “One World Football ball Project for Africa”  Wenye lengo la kupambana na Ukatili dhidi ya Watoto kupitia mchezo wa Mpira katika Uwanja wa Aman mjini Zanzibar ikiwa ni shamra shamra za miaka 49 ya Mapinduzi Zanzibar.
Amesema Mradi huo ambao umewalenga zaidi Wanafunzi wa Shule umefufua matumaini mapya ya kuibua vipaji vya michezo mbalimbali Zanzibar na kwamba kinachohitajika kwa sasa ni mipangilio mizuri kutoka kwa Walimu na wasimamizi wa michezo mashuleni.
Aidha amesisitiza kuwa michezo haimzuii mwanafunzi kufanya vizuri darasani hivyo Wazazi na walezi waendelee kutoa mashirikiano kwa watoto wao kuhusu michezo stahiki wanayoipenda.
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akizindua Mradi Mkubwa wa Ugawaji wa Mipira ya kuchezea kwa Vikundi mbalimbali vya Michezo hadi Mashuleni kwa  kuanza kumgawia kijana  Yunus Fadhil Juma kutoka Mkoa wa Kusini Pemba hafla iliofanyika hapo Uwanja wa Amani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akizindua Mradi Mkubwa wa Ugawaji wa Mipira ya kuchezea kwa Vikundi mbalimbali vya Michezo hadi Mashuleni kwa kuanza kumgawia kijana Yunus Fadhil Juma kutoka Mkoa wa Kusini Pemba hafla iliofanyika hapo Uwanja wa Amani Zanzibar.

“Jukumu lenu Wizara ya Elimu ni kuhakikisha kuwa Michezo yote ile iliyoruhusiwa kisheria chini ya Wizara ya Habari Utalii Utamaduni na Michezo kuwa inachezwa Mashuleni..Wala michezo haimzuii mwanafunzi kufanya vyema Darasani ” Alisema Rais Shein.
Rais Shein alifahamisha kuwa mradi huo pia utasaidia sana kujenga kikosi imara cha Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) kwa vile vipaji vya Soka vitaibuka vingi mashuleni vitakavyosaidia Timu hiyo kuwa tishio Afrika Mashariki na Kati.
Akigusia suala la Zanzibar Heroes na ushindi wa nafasi ya tatu uliyoipata katika Mashindano ya SECAFA Rais Shein amesema timu hiyo ilicheza vizuri kiasi cha kumvutia sana na kuongeza kuwa Zawadi yao ipo kinachohitajika ni kumalizwa tofauti baina ya Wachezaji na Viongozi wa Timu hiyo.

Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk akitoa hotuba ya Kumkaribisha Rais wa Zanzibar ili kuwahutubia wananchi  waliohudhuria katika Uzinduzi wa Mradi mkubwa wa Ugawaji Mipira ya kuchezea kwa Vikundi mbalimbali vya Michezo hadi Mashuleni kwa Zanzibar nzima, hapo Uwanja wa Amani Zanzibar.
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk akitoa hotuba ya Kumkaribisha Rais wa Zanzibar ili kuwahutubia wananchi waliohudhuria katika Uzinduzi wa Mradi mkubwa wa Ugawaji Mipira ya kuchezea kwa Vikundi mbalimbali vya Michezo hadi Mashuleni kwa Zanzibar nzima, hapo Uwanja wa Amani Zanzibar.
Kwa upande wake Waziri wa Habari na Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema Mradi huo umelenga kuleta vuguvugu la michezo na kuondoa tatizo la vifaa vya michezo Zanzibar ili kuibua vipaji vitakavyoifanya Zanzibar iwe tishio katika michezo mbalimbali.
Aidha ameongeza kuwa Mipira hiyo itagaiwa katika maeneo yote ya Unguja na Pemba bila ya upendeleo na kwamba Timu zote zilizosajiliwa na Makundi maalum watanufaika na mipira hiyo.
Mradi huo ambao umefadhiliwa na One World Futbal,Shirika la Kusaidia Watoto Duniani kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar unajumuisha Mipira-Elfu 20, itakayogaiwa kwa Wanafunzi wa shule na Timu za Soka za Unguja na Pemba.

IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
[ Read More ]

NAIBU WAZIRI ASISITIZA RESI ZA NGALAWA KUENDELEZWA

Naibu Waziri wa Ardhi,Makazi,Maji na Nishati Haji Mwadini Makame akipuliza filimbi kuonyesha ishara ya kuanza kwa mashindano hayo.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Naibu Waziri wa Ardhi,Makazi,Maji na Nishati Haji Mwadini Makame akipuliza filimbi kuonyesha ishara ya kuanza kwa mashindano hayo.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Naibu Waziri wa Ardhi Makazi, Maji na Nishati Haji Mwadini Makame amewataka Manahodha wa Ngarawa waendelee kudumisha utamaduni wao wa kufanya mashindano ya Resi za Ngalawa kila ifikapo nuda wa maadhimisho ya shererhe za Mapinduzi ya Zanzibar. 
Wito huo aliutoa jioni ya jana wakati alipokuwa akitoa nasaha zake kwa Manahodha walioshiriki mashindano hayo huko Forodha Mchanga Mjini Zanzibar ikiwa ni shamra shamra za kutimiza miaka 49 ya Mapinduzi Zanzibar. 
Alisema kuwa Resi za Ngarawa ni moja ya utamaduni wa Zanzibar hivyo ipo haja ya kuenziwa mchezo huo ili kukuza utamaduni na kudumisha Mapinduzi ya Zanzibar yaliyo wakomboa wananchi wa Zanzibar kutoka kwa Wakoloni.
“Udumisheni utamaduni huu kwani unaleta mshikamano na furaha miongoni mwenu na ni njia nzuri ya kudhihirisha utamaduni wetu kwani Zanzibar watu wake ni wavuvui kihistoria” alisema Mwadini
Alifahamisha kuwa kuudumisha mchezo huo ni kuwapa umuhimu Wavuvi ilikuona na wao wanathaminiwa na taifa lao kwavile viongozi wa Serikali ndio wanaokuwa Wageni rasmi na Wadhamini wa mchezo huo.
 Waziri Mwadini aliwaomba Washriki wa mchezo huo kuwahamasisha wenzao kutoka Vitongoji mbalimbali vya Zanzibar kushiriki mchezo huo ili kuunogesha zaidi.
Aidha aliwataka pia Washirikia kujiandaa vyema zaidi katika mashindano yanayokuja na kuuthamini mchezo wao huo ambao amedai kuwa hauna tofauti na michezo mingine inayochezwa Zanzibar  
Mchezo huo ulishirikisha ngalawa 10 kutoka vitongoji mbali mbali vya unguja kama vile Dimani ,chukwani ,Nyamazi Bumbwni ambapo Mshindi wa mchezo huo Fundi Abubakari kutoka Bubwini alizawadiwa Shilingi Laki 2.

 IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR  11/01/2012

[ Read More ]

MUUNGANO WA MAKAMPUNI YA OMAN KUWEKEZA SHIRIKA LA NDEGE ATCL SHS. BILIONI 160

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Oman Oktoba mwaka 2012 baada ya kualikwa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said ambapo aliambatana na ujumbe wa mawaziri na viongozi waandamizi wa biashara.
Katika ziara hiyo Rais Kikwete alibadilishana uzoefu wa uhusiano na kuangalia namna ya kudumisha
ushirikiano wa nchi hizo mbili kuhusiana na biashara, elimu, utamaduni na mambo mengine.
Hiyo ilikuwa ni ziara ya pili muhimu ya kiongozi wa Tanzania kutembelea nchi hiyo tangu mwaka 1985 wakati Rais wa kwanza, hayati Julius Nyerere akiwa madarakani.
Ziara hiyo ya Rais Kikwete inaonyesha umuhimu wa namna nchi hizo mbili zinavyojenga mahusiano makubwa na undugu baina yao.
Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na Oman lililofanyika Oktoba 16 katika Hoteli ya Al Bustan Palace wakati Rais Kikwete akitoa hotuba yake.
Kongamano hilo liliangalia fursa za kibiashara katika rasilimali zilizopo katika nchi hiyo iliyopo Ukanda wa
Afrika Mashariki zikiwemo kilimo, viwanda, utalii, usafirishaji, mafuta na gesi.

Kituo cha Uwekezaji (TIC)Tanzania kiliwasilisha namna uwekezaji katika kiuchumi na nafasi za uwekezaji nchini Tanzania.
Mwishoni mwa tukio hili muhimu, malaka za nchi hizi mbili zilisaini na kukubaliana kuanzisha Baraza la Biashara kati ya Oman na Tanzania ambalo litakuwa ni hatua muhimu katika kuanzisha uhusiano wa mataifa hayo mawili katika ngazi ya juu.
Madhumuni mengine muhimu ya ziara hiyo yalikuwa ni pande hizo mbili kusaini makubaliano ya kukuza na kuulinda uwekezaji jambo ambalo ni kichochezi katika Baraza hilo la Biashara la Oman na Tanzania, itarahisisha kutoa fursa za kibiashara na uwekezaji kati yao.
Pia makubaliano ya kupeana ushauri katika masuala ya siasa yamesainiwa hivyo itakuwa ni njia nzuri ya uzileta nchi hizo mbili zenye undugu karibu katika jambo hilo
muhimu.
Walisaini makubaliano kuhusu Utunzaji kumbukumbu na Nyaraka ambazo zinatunza kumbukumbu za historia muhimu kwa vile nchi hizo mbili zina historia inazofanana kiasi fulani.
Kubadilishana huko kwa nyaraka na kumbukumbu za historia kunaweza kusaidia kuchimbua matukio
ya kihistoria yaliyotokea zama hizo. Walisaini makubaliano ya kushirikiana katika elimu ya juu.
Oman na Tanzania zimekuwa na uhusiano wa muda mrefu hivyo ziara hiyo ya Rais Kikwete inalenga
kufungua fursa nyingi na hatimaye kufikia ngazi wanazostahili wananchi.
Nchi hizo zinafaidika na upendo baina ya watu wake kwa sababu Oman ni nchi pekee nje ya Afrika ambako wananchi wengi wanazungumza Kiswahili na Wa-Oman wamezaliana na Watanzania pamoja
na kuwa na utamaduni wa aina moja.
Kuna uwezekano mkubwa wa kufungua fursa za usafiri wa ndege ndani na nje ya Afrika katika uwekezaji na biashara katika juhudi za kibinadamu.
Tanzania ina fursa kubwa za uwekezaji katika sekta za
mifugo, uvuvi na kilimo.
Ikiwa imebarikiwa kuwa na eka za ardhi yenye rutuba, maji na hali nzuri ya hewa, Tanzania ni mahali
pazuri kwa Oman kuwekeza na kukuza shughuli za kilimo ili kufanikisha mahitaji yake.
Hii ni namna Oman inavyoweza kujibadilisha yenyewe kutoka kuwa muingizaji wa bidhaa nchini na kuwa muuzaji wa bidhaa za matunda na mboga mboga nje ya
nchi hivyo kujihakikishia kutokuwa tegemezi wa chakula.
Kwa vile Tanzania imegundua visima kadhaa vya Mafuta na gesi, na nchi hizo mbili zinaweza kuanzisha
ushirikiano katika suala hili ambalo litawanufaisha wote kwa pamoja.
Oman inaweza kuwekeza katika miundombinu iliyokua nchini Tanzania kama barabara, madaraja, hoteli,
resort na pia katika usafirishaji, na sekta ya usafiri wa njia ya meli.
Pia sekta ya viwanda itatoa fursa za uwekezaji kwa Serikali ya Oman na jamii ya biashara.
Cha muhimu ni kwamba nchi ya Tanzania yenye ananchi 44,929,002 inahudumia soko la watu milioni 150 katika nchi zake za jirani kupitia Bandari ya Dar es
Salaam.
Tanzania ni nyumbani kwa baadhi ya maeneo muhimu duniani kwa shughuli za utalii na miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la wageni kutoka Oman wakienda nchini Tanzania jambo ambalo limefanya safari za ndege za Ndege ya Oman ziwe nyingi.
Tanzania ni nchi kubwa zaidi Afrika Mashariki ikiwa na jiografia inayoruhusu uwekezaji katika sekta ya utalii ambapo pia inasifika kuwa na hali nzuri ya hewa, ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha na rasilimali
ambayo inavutia uwekezaji.
Baada ya ziara Rais Mheshimiwa Dk.Jakaya Kikwete, Umoja wa wadau wa biashara nchini Oman umeamua kuwekeza fedha kiasi cha sh.bilioni 160 ili kuendeleza Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).
Hatua hiyo ilikuja baada ya mkutano kati ya Kikwete na ujumbe wa wafanyabiashara hao.
Akizungumza wiki hii, Mwenyekiti wa Al Hayat Development na kampuni yake ya uwekezaji, Sheikh
Salim Al Harthy alisema wanashukuru kwa msaada huo uliotolewa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said Sultan wa Oman.
Alisema wanashukuru kwa vile msaada huo utasaidia na kuimarisha ushirikiano wa kibiashara kati ya mataifa hayo mawili hasa baada ya makubaliano kufikiwa kati ya viongozi wa nchi hizo.
Na kama sehemu ya kujitolea kwao huko wanadhamiria kusaini makubaliano na Air Tanzania na kuwekeza
dola milioni 100 na kuongoza wawekezaji ambao tumekuwa na uhusiano nao wa karibu.
Alisema uekezaji huo utatumika katika kukodisha na kununua ndege ambazo zitatumika katika safari za
ndani na nje ya Afrika kukuza biashara ndani ya Tanzania na nchi
nyingine.
Sheikh Salim Al Harthy aliongeza kuwa fursa hiyo ilikuja kwa ukarimu na matarajio mazuri ya Rais Kikwete na Serikali ya Tanzania kwa kutuamini kuja kuwekeza
katika kushughuli za kiuchumi nchini Tanzania.
“Tunamshukuru Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said wa Oman na Rais Kikwete wa Tanzania kutupa nafasi
hiyo hasa ukizingatia kipindi hiki tuna mpango wa kujenga kituo cha mafunzo ya masuala ya ndege, ofisi
nzuri kwa ajili ya ATCL, kununua ndege na kufanya shughuli nyingine za maendeleo tunazotarajia kuanza
ndani ya miezi sita hadi kumi” alisema.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akiwa na Mtukufu Sultan Qaboos Bin Said wakati wa
ziara yake nchini Oman.
Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Al Hayat, Shaikh Salim Al Harthy, wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mkuu wa ATCL, Kapteni Milton Lazaro. Wa kwanza kushoto ni Al Sayyid Fahar Bin Taimur Al Said na kulia ni Bwana Saeed S. Bawazir kama wa wakilishi wa Al Hayat inchini Tanzania.
[ Read More ]

SMZ UIMARIKAJI WA SECTA YA UTALII UMEANZA KUSHAMIRI ZANZIBAR


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akishusha Nanga kuashiria kuweka jiwe na nanga la ujenzi wa chumba cha chini ya bahari katika Hotelai ya Manta Resort iliyoko Makangale Kaskazini mwa Kisiwa cha Pemba.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akishusha Nanga kuashiria kuweka jiwe na nanga la ujenzi wa chumba cha chini ya bahari katika Hotelai ya Manta Resort iliyoko Makangale Kaskazini mwa Kisiwa cha Pemba.
Harakati za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha Sekta ya Utalii zimeanza kuonyesha dalili za mafanikio kufuatia uwekezaji wa daraja la juu katika sekta hiyo kuanza kushamiri kidogo kidogo hapa Nchini.
Ujenzi wa chumba cha chini ya bahari { under water room} ulioanzishwa kama mradi maalum wa kuvutia watalii wa daraja la kwanza unaofanywa na Uongozi wa Hoteli ya Manta Resort iliyopo Makangale Mkoa wa Kaskazini Pemba ni miongoni mwa dalili hizo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikuwa mgeni rasmi katika uwekaji wa jiwe la nanga la ujenzi wa chumba hicho kitakachokuwa chini ya Bahari ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya kutimia miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Balozi Seif akiambatana na Viongozi mbali mbali wa Serikali, Wizaraya ya Habari wakiwemo maafisa wa sekta ya Utalii na wanasiasa alionekana kufarajika na mradi huo mpya ndani ya Bara la Afrika na ni wa pili kufanywa Duniani ukitanguliwa na ule wa Sweden ulioko katika maji ya ziwa.
Chumba cha chini ya Bahari kikionekana kwa mbali kikiendelea na matengenezo kwenye Hoteli ya Manta Resort Makangale iliyoko Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Chumba cha chini ya Bahari kikionekana kwa mbali kikiendelea na matengenezo kwenye Hoteli ya Manta Resort Makangale iliyoko Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Akizungumza katika hafla hiyo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema ni jambo la kutia moyo kuona Kisiwa cha Pemba hivi sasa kinanza kupanuka Kiutalii kufuatia kuimarika kwa miundombinu iliyowekwa.
Aliwataka wananchi wa Kisiwa cha Pemba kuchangamkia sera ya Utalii kwa wote kwa lengo la kuitumia fursa hiyo adhimu kabla haijavamiwa na wafanyakazi wa nje ya Visiwa hivi.
‘’ Pemba sasa ni eneo ambalo Serikali inaliangalia katika kufunguka kiutalii hasa kutokana na kukamilika kwa miundombinu ya umeme na Bara bara’’. Alifafanua Balozi Seif.
Alikumbusha kwamba Zanzibar bado haijatangazwa kiutalii nje ya Nchi na watu wanaofikia hatua za kufanya hivyo huitangazia kwa
maslahi yao binafsi.
Balozi Seif ameiagiza Taasisi inayosimamia uwekezaji vitega uchumi Zanzibar { ZIPA } kuziangalia upya sheria zilizopo za uwekezaji ili kuwepuka kurejea makosa yaliyojitokeza tokea kuimarishwa kwa sekta ya Utalii Nchini.
Alisema ipo miradi ya uwekezaji ambayo imekuwa mtihani kwa serikali kwa vile imeshindwa kutoa huduma zilizokusudiwa akiutolea mfano mradi wa Hoteli ya Mawimbini ambao kmwa sasa umeshindwa kufanya kazi.
Akimkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Mh. Said Ali Mbarouk alisema mradi huo wa chumba cha chini ya Bahari masafa ya Mita 100 ni wa majaribio.
Mh. Said alieleza kuwa mradi huo wa chumba kimoja  utakapofaulu Uongozi wa Hoteli ya Manta Resort umekusudia kujenga vyumba vingi zaidi ili kufanikisha utali wa daraja la juu.
Mapema Meneja wa Hoteli ya Manta Resort Makangale Bwana Metthew Saus Maarufu kwa jina la Babu kwa nini alisema wazo la ujenzi wa mradi huu lilichukuwa takriban miaka saba kwa kufanywa utafiti chini ya bahari.
Babu kwani alisema Kisiwa cha Pemba kina mazingira mazuri ya kuendeleza mradi huo ikilinganishwa na mradi wa mwanzo Duniani kama huo ulioanzishwa Nchini Sweden.
Amewapongeza wananchi wa Zanzibar kwa kusherehekea miaka 49 ya mapinduzi Matukufu ya mwaka 1964 yaliyowatoa katika makucha ya wakoloni.
 Meneja wa Hoteli ya Manta Resort Makangale mkoa wa kaskazini Pemba Bwana Metthew Saus { Maarufu Babu kwanini na msaidizi wake  wakiwa tayari kumsubiri mgeni rasmi Balozi Seif Ali Iddi kuweka jiwe la nanga katika ujenzi wa chumba cha chini ya bahari.
Meneja wa Hoteli ya Manta Resort Makangale mkoa wa kaskazini Pemba Bwana Metthew Saus { Maarufu Babu kwanini na msaidizi wake wakiwa tayari kumsubiri mgeni rasmi Balozi Seif Ali Iddi kuweka jiwe la nanga katika ujenzi wa chumba cha chini ya bahari.
[ Read More ]