
baadhi ya wananchi wa manispaa ya mji wa Zanzibar wamelalamikia kupanda kwa bei ya mazao ya kilimo siku moja baada ya kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani. Baadhi ya wateja katika soko la Mwanakwerekwa wamesema bidhaa nyingi zinazotumika kwa ajili futari zimepanda bei ikilinganishwa na siku za kawaida. Wamesema mazao yaliopanda bei ni pamoja na ndizi ya mkono mmoja inayouzwa kati ya