Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

OPRAH REVEALS HER FAMILY SECRET ON HER SHOW.


Meet Oprah Winfrey's Half-Sister Patricia
Oprah Winfrey and sister Patricia
Reunion: Winfrey sits down and chats to her half-sister in front of fans on her TV talk show
She was the family secret that Oprah Winfrey called "one of the greatest surprises" of her life. 

But on Monday's 
Oprah Winfrey Show, Patricia, the media mogul's half-sister, stepped forward in a very public way. 

During the show, Winfrey revealed that she learned she had a sister last October, saying the discovery "left me speechless." 

She was 9-years-old and living with her father in Tennessee when her mother, Vernita Lee, became pregnant with a daughter, Patricia, who was given up for adoption. Born in 1963 in Milwaukee, Patricia would later live in a series of foster homes until the age of 7. She was then adopted, but said her childhood was "difficult." 

Tracing her roots took years of perseverance but Patricia finally discovered her mother – and her half-sister. 

"I received this big old package of information in the mail," Patricia said during Monday's interview. "And it has all of my birth information in it. I was like, 'Oh my God. I have a family.' " 
**************************************



OPRAH'S FAMILY HISTORY

Oprah
Oprah was born to unmarried teenagers, Vernita Lee, a housemaid, Vernon Winfrey, who was in the Armed Forces.
During her childhood was raised at various times by her grandmother Hattie Mae Lee in Mississippi, her mother in Milwaukee, and her father in Nashville.
She was raped and abused by family friends, who have not been publicly  identified, while in Milwaukee.
She moved to Nashville permanently in 1968 to live with her father while she was secretly pregnant at 14. She gave birth to a son, who died when he was just a week old.
Oprah had two half-siblings on her mother's side - Jeffrey, who died in 1989, and Patricia, who passed away in 2003.
She met her secret half-sister - who, by coincidence, is also named Patricia - in November last year.
[ Read More ]

KESI YA JERRY MURO YAZIDI ILIVYOUNGURAMA LEO

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imepokea risiti ya pingu kama kielezo cha ushahidi katika kesi ya kuomba rushwa ya sh. milioni 10 inayomkabili aliyekuwa mtangazaji wa TBC 1 Jerry Muro na wenzake Edmund Kapama na Deogratius Mgasa.

Risiti ya Pingu hiyo iliwasilishwa na shahidi wa tano katika kesi hiyo ofisa mpelelezi Anthony Mwita (45), ambaye aliieleza Mahakama kuwa risiti hiyo yenye namba 341573B, aliipata katika duka la silaha la Mzinga lililoko Upanga jeshini jijini Dar es Salaam.

Alisema alifika katika duka hilo kupata uthibitisho kama pingu aliyokutwa nayo Jerry ilinunuliwa kwao ambapo nao walithibitisha kumuuzia pingu hiyo yenye thamani ya sh.25000 Mei 26, mwaka 2009 .

Mbali na kuwasilisha risiti hiyo pia shahidi huyo alidai katika upelelezi wake alienda katika Hoteli ya Seacliff ili kuthibitisha kama Jerry alifika hotelini hapo Januari 29, mwaka 2010.

Alidai alifika hotelini hapo Januari 31, mwaka jana na kumuona mlinzi wa KK Security aliyemtaja kwa jina la Brightone Babamika na kumuomba daftari la kuandikisha magari yaliyoingia hotelini hapo Januari 29 ambapo aliwapatia na kuona gari ya Jerry yenye namba za usajili T 545
TEH aina ya Cresta ambayo iliingia saa 7:33 mchana na kukabidhiwa kadi namba 673 na kuondoka saa 8:44 mchana.

Mwita alidai aliingia hotelini na kuuomba uongozi kuwaonyesha picha katika kamera ya CCTV ya matukio ya Januari 29 ambayo walionyeshwa na kupatiwa nakala ya picha hizo, lengo likiwa ni kuthibitisha kama kweli Jerry alifika hapo siku hiyo.

Naye shahidi wa nne alidai mahakamani hapo kuwa malalamikaji Michael Wage alikuja na fedha kiasi cha Sh milioni 10 kwenye ‘briefcase’ lakini hakuzihesabu.

Kesi hiyo itaendelea tena kesho mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Gabriel Mirumbe.
[ Read More ]

KESI YA JERRY MURO ILIVYOUNGURAMA LEO

MHASIBU wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo aliyesimamishwa kazi na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa ubadhirifu wa fedha za Umma Michael Wage, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa alikubali kutoa Sh milioni 10 alizoombwa na aliyekuwa mtangazaji wa shirika la Habari Tanzania (TBC1) Jerry Muro kwa kuogopa kubambikiziwa kesi kama Liyumba.

Wage, ni shahidi wa tatu katika kesi ya kuomba rushwa ya Sh milioni 10, inayomkabili Muro na wenzake Edmund Kapama na Deogratius Mgassa, walidai mahakamani hapo kuwa alitishiwa maisha na washitakiwa hao na alikiri kutoa Sh milioni moja kwa ahadi ya kumalizia nyingine tisa
kesho yake.

Akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo Gabriel Mirumbe, alidai kuwa mfululizo wa matukio hayo ulianza Januari 28, mwaka 2010 jioni, akiwa nyumbani kwake Bagamoyo ambapo alipokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa jina la Jerry Muro na mtangazaji
wa TBC1.

Alidai Muro alimtaka kufika Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya naye mahojiano kwamba kuna taarifa za tuhuma zinazomkabili zilizoanza kusambaa ambazo alitaka kuweka sawa ambapo alikuja na kukutana na Muro katika mgahawa wa Carlifonia kama walivyoahidiana ambapo baada ya kukutana Muro alimwambia alikua akiandaa kipindi kuhusiana na tuhuma zake ambapo alimtaka waende katika Hoteli ya Seacliff ambako mahojiano hayo yangefanyika.

Alidai wakiwa njiani kwenye gari ya Muro kuelekea Seacliff Muro alimpigia mtu simu na katika maongezi yake alimtaja yeye (Wage) na alipokata simu alimuuliza alikuwa akiongea na nani, Muro akamjibu kuwa huyo ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambaye pia alikuwa na maongezi na yeye.

Wakiwa bado njiani Wage alidai kuwa Muro alimwambia kuwa yeye ni Ofisa wa jeshi, ana nyota tatu na amesomea Marekani, ambapo alifungua ‘dashboard’ ya gari akatoa pingu na kumwambia kama akifanya vurugu au fujo ya aina yoyote angemfunga pingu na kisha alitoa bastola yenye
kitako cha rangi ya damu ya mzee na kumwambia kama yote yangeshindikana basi angempiga risasi na kumuua.

Alidai walipofika Seacliff walipokelewa na mtu mmoja mrefu, mweupe na mnene aliyejitambulisha kuwa yeye ni Kaimu mkurugenzi wa TAKUKURU anaitwa Mussa na baada ya muda akaja mwingine aliyejitambulisha kuwa ni msaidizi wa Kaimu Mkurugenzi wa TAKUKURU.

Wakiwa wamekaa meza moja Kaimu Mkurugenzi akamwambia kuwa ana tuhuma za ufisadi na kwamba hajafikishwa mahakamani aseme kama atahitaji msaada wao ambapo aliwajibu kuwa yeye sio fisadi.

Wage alidai Kaimu Mkurugenzi alimwambia kuwa hata Liyumba hakufanya kosa bali alimuambukiza Ukimwi bibi wa jamaa yake ambaye wanafanya naye kazi.

Alidai baada ya maelezo hayo alimuomba Muro amsaidie ambapo alimuomba atoe Sh milioni 10, naye akawajibu hakuwa nayo pale alikuwa na Sh. milioni moja tu, na hizo nyingine angekwenda kuwatafutia na kuziwasilisha kesho yake.

Alieleza akiwa na watu hao aliamua kumpigia mke wake aliyekuwa Morogoro simu na kuweka kipaza sauti ambapo alimtaka kumletea Sh. milioni tisa kesho, mkewe huyo alidai asingeweza kupata milioni tisa kwa kesho badala yake angeleta milioni nne tu.

Alidai kutokana na matukio ya siku hiyo aliwapigia simu ndugu zake ambao walimshauri kuripoti polisi ambapo kesho yake alienda kuripoti katika kituo cha polisi kati jijini Dar es Salaam, ambapo walimwambia ampigie simu Muro amwambie wakutane katika mgahawa wa City Garden maeneo ya Posta mpya mkabala na klabu ya Billicanas.

Wage alidai alimpigia simu Muro na kukubaliana kukutana hapo ambapo alifika saa 4:30 asubuhi na kumpigia simu kumfahamisha kama ameshafika na ndipo akajitokeza akiwa na polisi waliovalia kiraia ambapo Muro alipowatambua akataka kukimbia lakini polisi wakalizuia gari lake.

Shahidi huyo aliwatambua washitakiwa hao mahakamani na pingu, bastola na miwani ambavyo viliwasilishwa na upande wa mashitaka kama utambulisho katika kesi hiyo. Shauri litaendelea kusikilizwa tena leo kwa mashahidi upande wa mashitaka kuendelea kutoa ushahidi wao.
[ Read More ]