Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Matokeo Ya Kidato Cha Nne.

Matokeo ya Kidato cha nne 2009 yamewekwa hadharani leo huku takwimu zikionesha kuwa kiwango cha ufaulu kwa kidato cha nne yameshuka na yale ya mtihani wa maarifa(QT) kiwango kikiongezeka kwa asilimia 3.9 ukilinganisha na mwaka 2008.

Akitangaza matokeo hayo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa, Dk Joyce Ndalichako (pichani) amepasha, mwaka 2009 ufauli kwa watahiniwa wa shule ni asilimia 72.51 ya watahiniwa 248,336 ikiwa imeshuka kwa tofauti ya asilimia 11.18 ukilinganisha na mwaka 2008 ambayo ilikuwa asilimia 83.69 na wale wa kujitengemea ni asilimia 54.12 ya watahiniwa 91,589 ikiwa imeshuka kwa asilimia 4.89 ya asilimia 59.01 ya mwaka 2008.

Kati ya watahiniwa 173, 323 waliofaulu, wasichana ni 74,696 (asilimia 67.59) na wavulana ni 98,627 kwa upande wa shule wakati kwa watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu ni wasichana 25,044 na wavulana 24,433.

Dk. Ndalichako ametaja orodha ya wanafunzi wanafunzi bora 2009, ikiongozwa na msichana Imaculate Mosha wa Marian Girls akifuatwa na Gwamaka Njobelo wa Mzumbe.

Namba 3- Wolfgang Seiya wa Majengo ya Kilimanjaro 4- ni Vanessa Chilunda, 5 ni Faith Assenga na 6 ni Doreen Philbert wote wa Marian Girls 7 ni Zahra Meghji wa Usagara na 8 ni John Kimbari wa St. James Seminali, 9 ni Said Abdallh na10 ni Evans Lwanga wote wa Feza Boys.
Dk. Ndalichako alizitaja shule kumi bora zenye watahiniwa zaidi ya 35 ikiongozwa na Marian Girls ya Pwani ambayo mwaka 2008 ilikuwa ya pili na inafuatiwa na St. James Seminary ya Kilimanjaro, Don Bosco seminary ya Iringa ambayo mwaka 2008 ilikuwa nafasi ya nane imepanda hadi nafasi ya tatu.

Alisema sekondari ya wasichana ya St. Francis ya Mbeya ambayo mwaka 2008 ilishika nafasi ya kwanza imeshika nafasi ya nne na kufuatiwa na St. Mar’y Junior Seminary ya Pwani iliyonafasi ya tano huku Uru Seminary ya Kilimanjalo imeshuka nafasi tatu na kushika nafasi ya sita wakati sekondari ya wanaume ya Feza imepanda nafasi moja hadi nafasi ya saba.

Dk. Ndalichako alisema shule zilizoshika nafasi ya nane tisa na 10 ni Anwarite Girls, Maua Seminary na St Mary Goreti zote za Kilimanjalo.
Kwa upande wa shule zenye watahiniwa chini ya 35, Dk Ndaliachoka alisema kundi hilo linaongozwa na shule ya wasichana wa Feza ya Dar es Salaam na kufuatiwa na Mafinga Seminary ya Iringa, St. Joseph-kilocha Seminari ya Kilimanjaro iliyo nafasi ya tatu na nafasi ya nne ikishikwa na Queen of Apostle-Ushirombo ya Shinyanga.

Zingine kuwa ni Dungunyi Seminari ya Singida iliyonafasi ya tano na kufuatiwa na Rubya Seminary ya Kagera, Sengerema Seminary ya Mwanza iko nafasi ya saba na kufuatiwa na sekondari ya wasichana ya Bethelsabs ya Iringa huku Thomas More Machrina ya Dar es Salaam ikishika nafasi ya tinsa na Hellen’s pia ya Dar ikiwa nafasi ya 10.

Dk Ndaliachoka alizitaja shule kumi za mwisho kwa watahiniwa 35 au zaidi kuanzia iliyoshika mkia kuwa ni Busi ya Dodoma, Milola ya Lindi, Misima ya Tanga, Kiwere ya Tabora, Potwe da ya Tanga, Masanze ya Morogoro, Mandawa ya Lindi, Msata ya Pwani, Chekelei ya Tanga na Jangalo ya Dodoma.

Alizitaja shule kumi za mwisho zenye watahiniwa chini ya 35 kuwa ni Kizara ya Tanga, Mungumbi ya Lindi, Songolo ya Dodoma, Nakuhukahuka na Marambo za Lindi, Dole ya Zanzibar, Ruponda na Mpunyule za Lindi, Ruvuma ya Singida na Viziwi Njombe ya Iringa.

“ Hapa sina mchanganuo wa ufaulu wa somo moja moja, ila somo la Civis watahaniwa wamefaulu sana wakati hisabati imeendelea kuwapiga chenga.”

Hata hivyo, Dk. Ndalichako alisema baraza hilo limesitisha matokeo ya watahiniwa 7, 242 ambao hawajalipa ada ya mtihani na wamepewa muda wa miaka mwili kulipa na kinyume cha hapo matokeo hayo yatafutwa.

“ Pia tumesitisha matokeo ya watahiniwa wawili wa kujitegemea kutokana na kuwa na sifa zao kufanana, nah ii tumeigundua dakika za mwisho, majibu yao yatatole hadi hapo watakapoleta uthibitisho. Haiwezekani kufanana majina, wamezaliwa mwaka mmoja na sifa zo za kidato cha pili zinafanana na tumeshawaandikia matokeo.”

Dk. Ndalichako alisema kuwa na hata wanafunzi wawili wakafanana kila kitu, ikiwa ni majina, tarehe na umri wa kuzaliwa,” alisema.
Baraza hilo pia limefuta matokeo ya watahiniwa 405 na watano wa mtihani maarifa(QT).

“ Baraza limegundua udanganyifu wa watahiniwa kuwa na skripti zenye miandiko tofauti au kuwa na miandiko tofauti katika skripiti ya somo moja na hili tumeshirikiana na taasisi ya kubaini miandiko.

“ Pia kunawale ambao wamekamatwa na ‘notes, na wale waliokutwa chooni wakisoma, waliokutwa na simu kwenye chumba cha mtihani. Lakini wapo ambao walibainika na mfano usio wa kawaida wa majawabu, kwa mfano kuna wengi wamefanana kila kitu labda badala ya kuandika ‘themselves’ wanaandika ‘them selves’.”

Dk. Ndalichako aliongeza kuwa: “ Pia kunawengi ambao swali la kemia ambao lilitakiwa kueleza jinsi ya kutenganisha kerosene na water wao wajibu jinsi ya kutenganisha alcohol na water, lakini kulikuwa na udanganyifu hatari sana wa watahiniwa kubadilisha namba za wenzao.”
Alisema kuwa watahiniwa 53 pia wamefutiwa kutokana na kutokuwa na sifa kutoka shule za Mkwese sekondari(25), Ruruma (15), Thaqalaini(6), Bishop Kisanji(5), St Vicent na Edmund Rice Sinon kila moja mmoja.

Dk Ndalichako alisema mwanafunzi mmoja wa shule ya sekondari ya Kadoto amefutiwa matokeo kwa kuandika matusi kwenye skripti ya somo la baiolojia ikiwa ni kinyme na kifungu cha 5(13) cha kanuni za mitihani.
Pia alisema kuwa Baraza liemevifutia usajili wa watahiniwa wa kujitegemea kwa Sinza Iteba na Dar es salaam Prime vya Dar es salaam kutokana na kuzidiwa uwezo wa kuwachukua watahiniwa wengi.

Chanzo cha habari hii www.habarileo.co.tz
[ Read More ]

Mamia Wamzika Imran Mtui Mjini Moshi

Jeneza lenye mwili wa hayati Imran kijana aliyeuawa India hivi karibuni likitoka msikitini kuelekea katika makaburi ya Njoro mjini Moshi jana. Marehemu Imran alizikwa bila kuwa na kichwa. Picha na mdau Dixon Busagaga wa Moshi.
Mtanzania aliyeuawa India azikwa bila kichwa
Na Charles Ndagulla na
Dixson Busagaga, Moshi
VILIO, simanzi na majonzi jana vilitawala mazishi ya Mtanzania Imran Mtui (31) aliyeuawa kikatili nchini India hivi karibuni, katika mazishi yaliyofanyika makaburi ya Njoro Manispaa ya Moshi.

Mwili wa marehemu huo ulizikwa bila kichwa huku pia ukidaiwa kuwa na majeraha mengi mwilini kuanzia miguuni na kwenye paja lake karibu na kiuno huku kiwiko cha mkono wa kulia nacho kikidaiwa kunyofolewa.

Mwili huo uliwasili mjini moshi usiku wa kuamkia jana baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es salaam, ukitokea nchini India huku gharama zote za kuusafirisha zikibebwa na serikali ya Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kabla ya mazishi, kaka wa marehemu, Maliki Mtui, alisema kuwa wameshtushwa na kifo cha ndugu yao hasa kutokana na marehemu kutokuwa na historia ya ugomvi.

Kwa mujibu wa kaka huyo, mwili huo pia umeonekana kuwa na alama za kamba kwenye mikono yake hali ambayo inaonyesha marehemu kabla ya kuuawa alifungwa kamba ili asiweze kujitetea.

Tukio hilo la kusikitisha linadaiwa kutokea katika mji wa Bangalore nchini India ambako marehemu alikuwa tayari amehitimu masomo yake ya biashara na utawala (Business Administration) na tayari alikuwa akijiandaa kurejea nyumbani.

Kaka huyo wa marehemu aliwaambia waandishi wa habari kuwa mdogo wake huyo alipatwa na mkasa huo akiwa njiani kuelekea mjini ambako rafiki yake wa kike ambaye pia ni Mtanzania aishie visiwani Zanzibar alikuwa akisoma.

“Niliwasiliana naye siku ya tukio kabla hajapatwa na mauti haya nikamuuliza anatarajia kurudi lini nyumbani akanijibu angerudi mapema na rafiki yake alikuwa akimsubiri lakini hakuweza kutokea” alisema.

Pamoja na kuishukuru serikali ya Tanzania kugharamia kuusafirisha mwili wa marehemu mdogo wake, Mtui ameitaka pia serikali kuwathamini raia wake walioko nje ya nchi kwa kufuatilia taarifa zao pindi wanapokumbwa na matukio kama hayo ya kuuawa kwa mdogo wake.

Naye msemaji wa familia ya marehemu Mtui ambaye pia ni shekhe wa msikiti wa Majengo, Shekhe Said Khatibu, alisema kuwa serikali haiwathamini raia wake walioko nje na ndiyo maana serikali haijatoa tamko rasmi kulaani mauaji hayo.

Shekhe huyo pia alisema katika kile kinachoonyesha kuwa idara za serikali zimelala, serikali imeshindwa kutuma hata mwakilishi kwenye mazishi hayo ambayo tukio lake lina utata.

Aidha, alipinga taarifa zote zilizotolewa na madaktari nchini India kwamba marehemu alifariki dunia kwa ajali ya treni na kusisitiza kuwa taarifa hizo sio za kweli.
                                             

source:michuzi.                                                                              







[ Read More ]