Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

READ 4 REASONS TO AVOID ALL SODA (EVEN DIET)…!!!



From Kitchen Cabinet Cures

That innocent-looking can of soda pop-no matter what it’s sweetened with-may be taking a toll on your immunity. Here’s why:

1. People who drink sodas instead of healthy beverages (think low-fat milk and pure fruit juice) are less likely to get adequate vitamin A, calcium, and magnesium. What’s more, soda contains phosphoric acid that depletes calcium and magnesium. These two nutrients help keep your immunity operating at peak efficiency.

2. Sodas containing high-fructose corn syrup also contain high levels of free radicals linked to tissue damage, the development of diabetes, and diabetic complications.

3. Plastic soda (and water) bottles contain a toxic chemical called bisphenol A (BPA) that can leach from bottles into soda…into you. Emerging evidence links BPA to a myriad of maladies, including immune system depression. Public health experts recommend that we protect children from exposure to products containing BPA-especially those they consume or use every day.

4. Diet soda actually contributes to weight gain. A study of 1,550 people concluded that people who drink diet soda have a 41 percent increased risk of being overweight or obese-for every can or bottle they drink per day! Turns out, any sweet taste signals body cells to store fat and carbohydrates, which makes you hungrier. Sweet tastes also promote insulin release, which blocks your body’s ability to burn fat. The hard truth: No published study has ever proven that drinking diet soda will help you lose weight.

Study: Diet Soda May Increase the Risk of Stroke.
[ Read More ]

MAJI YASIYO SALAMA YASABABISHA KUHARISHA



WATU kutoka zaidi ya familia 10 katika Shehia ya Mikunguni, wamekumbwa na maradhi ya kuharisha baada ya kutumia maji yasiyo salama yanayosadikiwa kuchanganyika na kinyesi cha binadamu.

Tatizo hilo limewakumba zaidi watoto baada ya kutumia maji hayo yaliyokuwa na ladha ya uchungu pamoja na rangi ya udongo.

Katika taarifa yake kwa Zanzibar Leo, Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), imesema hali hiyo imesababishwa na mwananchi mmoja katika eneo hilo kujenga shimo la karo na kusababisha kinyesi kuchanganyika na maji safi baada ya bomba la maji la chini ya ardhi kupasuka kwa kemikali za kinyesi.

Afisa Uhusiano wa ZAWA, Zahor Suleiman alisema katika kukabiliana na tatizo hilo, Mamlaka lichukua hatua ya kufunga laini ya maji katika eneo hilo na kubadilisha mfumo mzima wa usambazaji maji ili yasipite kwenye karo hilo.

Mabadiliko hayo, yamesababisha wananchi wa shehia hiyo kukosa huduma za maji na kusababisha usumbufu mkubwa, hata hivyo hatua hiyo imechukuliwa ili kunusuru maisha ya wananchi na kuhakikisha wanapata huduma ya maji safi na salama kwa wote.

Shehia ya Mikunguni kwa muda mrefu imekuwa ikikosa huduma za maji safi kutokana na uchakavu wa miundombinu, lakini wakati ZAWA ikiweka laini mpya baada ya siku tatu tu hali ya maji ilibadilika na kuwa na ladha ya uchungu
[ Read More ]

ALBINO ALIEPOTEA APATIKANA MSITUNI


MTOTO mwenye ulemavu wa ngozi (albino), Juma Kapela (3) aliyekuwa ameibwa tangu Jumatano iliyopita wilayani Mpanda mkoani Rukwa, amepatikana akiwa hai, lakini akiwa amechanjwa chale mwili mzima na ametelekezwa msituni.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Daniel ole Njoolay, jana alithibitisha kupatikana kwa mtoto huyo na kumpokea ofisini kwake, lakini akiwa amechanjwa chale mwili mzima, kutokana na kile kinachoaminika kuwa ni imani za kishirikina na jitihada za kumdhuru kushindikana.

Njoolay alisema alimpokea Juma na dada yake ambaye pia ni albino, Wande Kapela (5), ambao walikuwa wamefuatana na bibi yao ambaye pia ni mlezi wao, Maria Elias (60) na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda, Naomi Nnko.

Juma na dada yake, Wande, wamekuwa wakilelewa na bibi yao kijijini Itunya kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika wilayani Mpanda, na Juma aliliripotiwa kuibwa Jumatano iliyopita na mtu asiyefahamika kwa kile kinachodaiwa ni imani za kishirikina.

Mkuu wa Mkoa alisema awali mkoa ulipendekeza kuwa watoto hao wapelekwe kuishi kwenye Shule ya Msingi ya Malangali mjini hapa pamoja na wenzao ambao ni albino, lakini baada ya kubaini kuwa bado ni wadogo haikufanyika hivyo lakini sasa wamekubaliwa na wataishi kwenye nyumba ya watoto yatima mjini hapa ya Mt Martin de Pores iliyopo Katandala.

“Hii ni faraja kubwa, hata Waziri Mkuu Pinda nilipomfahamisha kuhusu kupatikana kwa Juma akiwa hai, alisema tu ‘Mungu ni Mkubwa’. Nimekuwa nikimjulisha kuibwa kwa mtoto huyu tangu Jumatano iliyopita.

Pia nimeendelea kufanya hivyo hadi alipopatikana akiwa hai juzi, na leo muda mfupi ujao nitamtaarifu kuwa watoto hawa sasa wataishi na kutunzwa kwenye nyumba hiyo ya watoto yatima,” alisema Njoolay.


Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, kupatikana kwa Juma kunatokana na msako mkali uliofanywa siku nne mfululizo ukijumuisha Jeshi la Polisi , Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na wananchi wa maeneo ya vijiji vilivyopo si tu mwambao wa Ziwa Tanganyika bali pia wilayani Mbozi, Mbeya.

Akizungumza kwa Kiswahili kidogo huku akichanganya na Kisukuma, bibi wa watoto hao, Maria, alidai kuwa amekuwa akiishi na kuwatunza watoto hao tangu miaka miwili baada ya baba mzazi wa watoto hao aitwaye Kwangulija Kapela kumtelekeza mama wa watoto hao na kwenda kuishi Urambo, Tabora.

Alisema baba huyo ambaye ni mwanawe, alimtelekeza mkewe, Mbaru Busagija, akimtuhumu kumzalia mfululizo watoto albino ambapo alidai kuwa uzazi wa watoto hao umetia nuksi familia yao. Mama yao huyo ameolewa na anaishi pia Urambo .

Akielezea mkasa huo, bibi alisema siku ya tukio, Juma alikuwa na dada yake Wande karibu na nyumba yao wakati yeye amekwenda kutafuta mboga ndipo alipotokea mtu wasiyemfahamu na kuwafukuza na kumkamata Juma na kutoweka naye.

“Nilipojulishwa kuibwa kwa mjukuu wangu nililia sana ndipo majirani walipokuja na kwenda kutoa taarifa kwa viongozi wa kijiji ambao waliitaarifu Polisi na msako ukaanza,” alisema bibi huyo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Isuto Mantage, alisema hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusika na tukio hilo na kwamba msako wa kumtafuta mtuhumiwa unaendelea.
[ Read More ]