Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

UTATA WAGUBIKA KIFO CHA MWANAFUNZI ALIYEFIA HOTELINI


UTATA mkubwa umegubika kifo cha mwanafunzi Jackline Musa Matiko (15) aliyekuwa akisoma katika Shule ya Sekondari Juhudi iliyopo Gongo la Mboto Wilaya ya Ilala aliyekutwa amekufa katika Hoteli ya Southern Resort, Kigamboni Dar es Salaam baada ya wazazi wake kudai kuwa hakufa maji bali alinyongwa.
Ndugu na jamaa wa marehemu Jackline Musa Matiko, wakitoa mwili wa ndugu yao katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, baba wa marehemu, Mussa Matiku alisema baada ya kuikuta maiti ya mtoto wake kando ya bwawa katika hoteli hiyo na kuichunguza shingo yake aliiona imelegea na tumbo lake halikujaa maji kama watu wanaokufa kwa maji wanavyokuwa.
Alisema kwa vigezo hivyo ni wazi kwamba mwanaye hakufa maji na amelitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini waliomuua kikatili binti yake.
 Naye mjomba wa marehemu ambaye alikuwa na Jackline kabla ya kifo chake aliyejitambulisha kwa jina moja la Abdul, alisema  binti huyo alitoka nyumbani kwa wazazi wake maeneo ya Mazizini Ukonga kwenda Gongo la Mboto kwa bibi yake kusherehekea Sikukuu ya  Mwaka  Mpya.
Jackline Musa Matiko (15) enzi za uahi wake.
“Baada ya kufika pale na kupata chakula cha mchana pamoja  na ndugu zake, Ilipangwa kwenda  kutembea kokote walikohitaji ambapo walichagua  kwenda Quality Centre.
Aliongeza kuwa walipofika huko waliamua kwenda Southern Beach Resort Kigamboni ambako ndiko waliposherehekea siku hiyo ya mwaka mpya.
 Akadai kuwa wakati wakiwa huko walikuwa wakinywa vinywaji laini, kucheza muziki pamoja na kuogelea lakini akawapa  tahadhari kuwa kila anayetoka kwenda sehemu yoyote ahakikishe anarejea walipokuwepo wenzake.
Akaongeza: “Ilipofika saa moja usiku Jackline hakuonekana ndipo nikawa na hofu na kuanza kumtafuta huku nikiwa nimewaambia wenzake wasitoke eneo nililowaacha.
“Kutafuta kwangu hakukuzaa matunda nikaenda kwa uongozi wa bichi kueleza kuhusiana na tukio hilo nao pia wakatangaza  kwa kutumia kipaza sauti kuwa mtoto amepotea huku akiwa  anatajwa  jina lake pia hapakuwa na mafanikio.”
Baada ya kuona jitihada za kumpata Jack hazikuzaa matunda walikwenda kutoa taarifa Kituo Kidogo cha Polisi Vijibweni kisha wakarudi nyumbani.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Jackline Musa.
Abdul aliongeza kuwa anachohisi uongozi ulishajua kuwa tukio  hilo lilitokea lakini waliamua  kumficha kwa kuhofia  kama wangesema ukumbi ungefungwa na biashara  ingekuwa ndiyo mwisho kwa siku hiyo.
Aliongeza kuwa asubuhi walipigiwa simu na polisi wakielezwa kuwa kuna mtoto aliokotwa akiwa amekufa na walipokwenda kuhakikisha wakakuta ni Jackline.
Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Kipolisi Temeke, ACP Engelbert Kiondo alipohojiwa na gazeti hili alisema upelelezi wa tukio hilo ulisubiri ripoti ya madaktari ili kujua kama mtoto huyo alikufa maji au aliuawa kisha kutupwa karibu na bwawa la hoteli hiyo.
Marehemu Jackline alizikwa Januari 3, mwaka huu eneo la Moshi Bar Ukonga.

Habari na global.
[ Read More ]

Disappointment Misses No One.



Each of us experiences disappointments in our life,Disappointment springs up regularly in the workplace because many of us have limited control over our work surroundings.
You get passed over for leading a task force, even though you have all the requisite skills and experience. Someone else gets the raise that you thought you deserved. Your co-worker says she is going to support you on a task and she ducks out. That manuscript you submitted was rejected by a third journal. One of your clients pulled the plug – he doesn’t want to work with you anymore .
None of this feels good.
Ever notice how you don’t like the feeling of disappointment? How incredibly discomforting it is? What you will do to avoid it? Me too.
As humans, we squirm away from disappointment. Oftentimes we get disheartened and start obsessing about the story line that led to our disappointment instead of connecting with the actual feeling. We blame – others, the economy, our childhood, traffic — even the dog. We think of ourselves as failures. We push disappointment away turning it into anger. Or we push it down turning it into depression. Just having it near us can be so scary.

Life is a constant changing wave – with the high tide of joys and the low tides of disappointment and everything else in between. When we keep pushing disappointment away from us at work, we also give our human wholeness  a shove. That part of us that contains our essential goodness.
I don’t want to get carried away with the eye story, but last year I had a lot of disappointments. separated from my family, hospitalized more than six time,  Diagnosed With Keratoconus , undergo c3r surgery, good-bye chocolate, ice-cream and all delicious food .
In my reflection time during treatment, I realized that the more pushed the feelings of disappointment away, the more miserable I became. And when I tried to hide from them, they started to creep toward me like King Kong. When I shunned them, they were so persistent – tapping me on the shoulder.
And so I started snuggling up with them, just like a good book. I leaned in, got comfortable, and remained still. No pushing. No blaming. Some moments, disappointment would be stuck in my body – not budging. I’d need to breathe into it and invite it in a bit closer. Holding my vulnerability, being with the tenderness. Soothing, without a story. Tuning into the sensation. Naming the feeling, “Aah, that was disappointment.” And off it would go.
What I experienced over and over again is that disappointment doesn’t want to stick around. It wants to get its running shoes on and trek out away from us. But sometimes it’s us that keep dragging our disappointments through our muddy storylines. We won’t let go of it. We are tethered to its pay-off. More suffering.
It’s truly our choice.

I’ve had enough disappointments professionally and personally to know they are transitory. What is a disappointment one day may turn out to be an opportunity the next. Think about when you thought a window was closing and then all of a sudden a big door of opportunity swung open. Perhaps your job was getting grueling and laborious but it was just the spark plug for you to seek a better one. Sometimes a disheartening event gets us ready to take the next big leap – the next big jump toward bigger joy, more appreciation, and greater kindness.
I can’t imagine a more perfect this day – with my  friend and a heart full of gratitude for each step of the way. All year’s disappointment transformed into this year’s magnificent joy.

May your disappointments circle back as blessings. And this day, as always, may you be wise at work.

Remember Inspire Me Daily.One Person Can Make a Difference

[ Read More ]

RAIS DK. SHEIN AZINDUA BOHARI KUU YA DAWA ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kama ishara ya uzinduzi
wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa,Maruhubi Nje ya Mji wa Zanzibar jana
ikiwa ni shamra shamra za kilele  cha miaka 49 ya Mapinduzi Matukufu
ya zanzibar,(kulia)  Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Alfonso
Lenhardt.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akikata utepe kama ishara ya uzinduzi
wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa,huko Maruhubi Nje ya Mji wa Zanzibar
jana ikiwa ni shamra shamra za kilele  cha miaka 49 ya Mapinduzi
Matukufu ya zanzibar,(kulia) ni Naibu waziri wa Afya Sira Ubwa Mamboya
na  Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Alfonso Lenhardt.[Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa
Bohari Kuu,Said Mohamed,(kulia) alipotembela sehemu ya kuhifadhia
Dawa,baada ua uzinduzi wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa huko Maruhubi
Nje ya Mji wa Zanzibar,ikiwa ni shamra shamra za kilele  cha miaka 49
ya Mapinduzi Matukufu ya zanzibar,(wa tatu kushoto)  Balozi wa
Marekani Nchini Tanzania Alfonso Lenhardt.[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa tatu Kulia)pamoja na Viongozi
wengine akiwemo Balozi wa Marekani Nchini  Alfonso
Lenhardt.wakiangalia namna ya uchukuwaji dawa kwa kutumia mashine
maalum na kutoa nje ya Bohari kuu ya Dawa,baada ya ufunguzi rasmi jana
huko Maruhubi Nje ya mji wa Zanzibar,ikiwa ni shamra shamra za kilele
cha miaka 49 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzíbar  
………………………………………………
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema uzinduzi wa Bohari kuu ya Dawa utaiwezesha Serikali ya Mapinduzi Zanzíbar kupanga bajeti yake vyema ya dawa na kusaidia utoaji wa huduma za afya kwa ubora wa hali ya juu.
 Rais Shein ameyasema hayo katika hafla ya uzinduzi wa Bohari Kuu ya Dawa iliyopo Maruhubi mjini Zanzibar ikiwa ni mwendelezo wa shamra shamra za kutimiza miaka 49 ya Mapinduzi Zanzibar.
 Amesema Bohari hiyo ya kisasa ni matunda ya kujivunia ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo kwa hakika italeta tija katika upatikanaji wa dawa na uimarisha wa afya za wananchi.
 Dkt. Shein ameelezea matumaini yake kwa sekta ya afya kupitia Bohari hiyo na kwamba anaamini baada ya miaka mitatu Zanzibar itakuwa haipeleki tena Wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu.
 Aidha Dkt. Shein amewataka watumishi wa Serikali kubadilika kiutendaji kulingana na kasi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wa Bohari hiyo kuitunza vyema ili iendelee kutoa huduma kama inavyotakiwa.
 Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya Sira Ubwa amesema Bohari hiyo itaboresha utoaji wa huduma kwa uhakika kutokana na ubora wa vifaa na mitambo ya kisasa ambapo wataalamu wataweza kubaini mahitaji ya Dawa zinazohitajika katika kila Hospitali za Unguja na Pemba.
 Kwa upende wao Mabalozi wa Marekani na Denmark wameelezea kufurahishwa kwao na juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha afya ya Wananchi hasa katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Malaria na Ukimwi.
 Aidha wameahidi kuendelea kutoa mashirikiano kwa Serikali hasa katika huduma za Afya kwa Mama na Watoto, Elimu,Mapambano dhidi ya magonjwa ya maambukizi pamoja na uzazi wa mpango.
 Bohari hiyo iliyojengwa na Serikali ya Mapinduzi kwa msaada wa Shirika la USAID na NIDA inaelezewa kuwa ya tatu duniani katika viwango vya ubora ambapo jumla ya Dolla za Kimarekani Milion 1.2 zimetumika kukamilisha ujenzi wake.
[ Read More ]

YUSUF OMAR CHUNDA AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUWA NA VITAMBULISHO (PRESSCARD)


 
.                                     Mkurugenzi Idara ya Habari,Maelezo Zanzibar Yusuf  Omar Chunda amewataka waandishi wa Habari Nchini kuhakikisha kwamba wanafanya kazi zao wakiwa na leseni za uwandishi wa habari (PRESSCARD) ilikuhakikisha kwamba wanafanya kazi zao hizo    kwa mujibu wa sheriaNo5 ya mwaka 1988 ya magazeti .
 Hayo ameyaeleza leo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali huko katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Chake chake Pemba.juu ya utendaji wa kazi za Idara hiyo kwa mwaka 2012na kuomba mawazo yao kwa utendaji wa kazi kwa mwaka 2013.
 Amesema kuwa na kitambulisho   kitamrahishia mwandishi huyo kufanya kazi kwa mujibu wa sheri  na kupata habari anazozihitaji kwa wahusika bila ya matatizo ambazo  zitachapishwa na kutangazwa katika vyombo mbalimbali vya habari.
 Mkurugenzi huyo amewataka waandishi hao kutopuuza agizo hilo la kuwa na kitambulisho kwani ni kwa faida yao wenyewe kutokana na kazi zao wanazo zifanya kila siku.
 Chunda amesema kuwa viongozi wasionekane wagumu pale wanapotaka kutoa habari kwanza kwa kuuliza waandishi vitambulisho vyao kwani wao wanahitaji kupata uhakika wa mwandishi huyo kama amepata kibali cha kuandika habari nchini kama sheria inavyotaka .
 Amesema kuwa ni vyema kwa waandishi kuelewa kazi zote zinakwenda kwa mujibu wa sheria kwa hivyo waandishi kama kioo cha jamii na wao wanastahiki kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria na wawe mfano.
 Mkurugenzi huyo amewashukuru waandishi wa habari wote kisiwani Pemba kwa mashirikiano mazuri walioipa idara yake katika utendaji wa kazi kwa mwaka 2012 na amewataka mashirikiano hayo yawe endelevu ili kufanikisha shughuli za idara hiyo na Taifa kwa Ujumla .
 Aidha amewashukuru pia waandishi wa habari, viongozi wa dini pamoja na NGOs za habari kwa mashirikiano walioyatoa wakati wakutoa mawazo yao juu ya mabadiliko ya sheria No5 ya mwaka 1988 ya magazeti na Majarida Zanzibar

[ Read More ]