Wahitimu wa Uhasibu na Fedha wa Chuo Kikuu Mzumbe (MU), wameshauriwa kujiendeleza kwa kufanya mitihani ya juu ya Uhasibu (CPA) na baadaye kusajiliwa katika Bodi ya Uhasibu (NBAA) ili watambulike wanataaluma. Changamoto hiyo ilitolewa na Meneja wa Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF), Kanda ya Mashariki na Kati, Meshack Bandawe, wakati wa hafla maalumu ya wanafunzi wanaotarajia kumaliza masomo
Polisi mkoani Singida inamshikilia dereva teksi kwa kosa la gari lake kuhusika na uporaji wa fedha Sh milioni nne mali ya mfanyabiashara wa alizeti, na baadaye kuvamia baa ya Kairo mjini hapa, na kutoweka na mauzo ya siku nzima. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Singida, Celina Kaluba matukio hayo yalitokea Jumanne na Jumatano wiki iliyopita katika eneo la Kibaoni na Mitunduruni katika Manispaa
Wizara ya Fedha na Uchumi Zanzibar imewatuhumu wahasibu wa kigeni wanaofanya kazi nchini kwa kushirikiana na wawekezaji kukwepa kulipa kodi na hivyo kuikosesha serikali mapato. Akizungumza katika ufunguzi wa semina kwa jumuiya ya wahasibu na wakaguzi wa hesabu iliyofanyika jana mjini hapa, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi, Abdi Khamisi Faki alisema zipo dalili zinazoashiria kuwa wahasibu
Zaidi ya asilimia 50 ya wanawake wajawazito mkoani Singida hujifungulia majumbani na kwa wakunga wa jadi, hali inayohatarisha usalama wa maisha yao na watoto wanaozaliwa. Hayo yalibainishwa na daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi Mkoa wa Singida, Dk. Christopher Mgonde kwenye mafunzo ya kuokoa maisha ya mama na mtoto wakati wa kujifungua. Dk. Mgonde alisema ingawa takwimu zinaonyesha kuwa
Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wameiomba Serikali kuimarishia ulinzi katika eneo la mahakama hiyo na wao binafsi. Maombi hayo yalitolewa jana na watumishi hao, mbele ya Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe, alipotembelea mahakama hiyo. Akizungumza kwa niaba ya watumishi hao, Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Addy Lyamuya, aliiomba serikali kupitia kwa Chikawe, kuwaimarishia
Watu wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, wakikabiliwa na mashitaka ya kula njama za kutaka kuiba zaidi ya Sh bilioni 6 mali ya Benki ya Stanbic. Akisoma mashitaka jana mbele ya Hakimu Nyigumalila Mwaseba, Mwendesha Mashitaka, Epifras Njau, alidai kuwa washitakiwa hao walikula njama za udanganyifu ili kutaka kuiba kiasi hicho cha fedha, jambo ambalo ni kinyume
Askari wawili wa Kikosi cha Valantia kinachomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), wameuawa na majambazi wakati wakilinda kituo cha mafuta cha Mwanakwerekwe mkoa wa Mjini Magharibi kisiwani Unguja. Askari waliouawa ni Taibani Mikidadi Ali (23) na Juma Mcha Ali (25) ambao walijeruhiwa na majambazi hao kwa risasi kichwani na kifuani.Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Bakari

Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lolesia Bukwimba, ametangazwa kuwa Mbunge Mteule wa Jimbo la Busanda, baada ya kuwashinda wagombea wa vyama vingine vilivyokuwa vikishiriki uchaguzi huo mdogo wilayani Geita.Mgombea huyo alitangazwa jana kwa kupata kura 29,242 wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambacho hata hivyo kiliyakataa matokeo, kilishika nafasi ya pili kwa kupata kura 22,799.