Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Hausigeli Amuangukia Mtoto, Mtoto Afariki





Katika tukio ambalo si la kawaida, hausigeli mmoja wa nchini Marekani ambaye alikuwa ni mnene sana, alizimia ghafla na kumuangukia mtoto mchanga wa mwezi mmoja na kupelekea kufariki kwa mtoto huyo kutokana na kuelemewa na uzito.
i na ni

Baba wa mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Michael Baldwin II ambaye ni mwandishi wa habari jijini New York, alikuwa nyumbani kwake akimuangalia mtoto wake mchanga wa mwezi mmoja kabla kutakiwa aende kazini mara moja na mwajiri wake.

Michael alilazimika kumuita hausigeli Teresa Coffey, ambaye pia alikuwa ni rafiki wa mke wake ili aje amtunzie mwanae huyo wa kiume.

Alipofika kazini, Michael alijaribu kumpigia simu Teresa mara kadhaa ili kujua hali ya mtoto wake.

Baada ya kuona simu haipokelewi, Michael alirudi nyumbani ili ajue nini kimetokea mpaka hausigeli hapokei simu.

Michael alimkuta Teresa akiwa amefariki amelalia uso chini kwenye kochi huku akiwa amepiga magoti sakafuni.

Michael hakumuona mwanae, alijaribu kuzunguka kila chumba kumtafuta mwanae lakini hakufanikiwa kumuona.

Hisia zilimtuma amnyanyue Teresa na ndipo alipomkuta mwanae akiwa amefunikwa na uzito wa Teresa akiwa tayari ameishafariki.

"Nilimnyanyua Teresa na kumkuta mwanangu chini yake, alikuwa amelala huku mikono yake akiwa ameiweka tumboni mwake", alisema Michael.

"Alikuwa amebadilika rangi kuwa kama wa bluu, nilimnyanyua na kumuita jina lake , nilijua tayari mwanangu ameishafariki", aliongeza Michael.

Taarifa ya polisi ilisema kuwa Teresa alikuwa ni mnene sana na alikuwa na matiti makubwa sana huenda nyama nyama za mwili wake zilimfunika mtoto na kumfanya akose pumzi.

Taarifa zaidi zilisema kuwa Teresa alikuwa akijulikana kuwa alikuwa akisumbuliwa na matatizo mbalimbali ya kiafya na chupa ya dawa alizokuwa akizitumia ilikutwa pembeni yake.

habari na nifahamishe.

[ Read More ]

Ufafanuzi Zaidi Juu Ya Keratoconus.

         baada ya kuandika makala ya kwanza kuhusu keratoconus nimegundua kuwa kuna idadi kubwa ya watu wanaohitaji kujua zaidi juu ya hili tatizo na vilele juu ya tiba yake. na wapo wengine 
ambao hawana ufahamu wowote juu hili na wapo wale ambao amegundulika na hili tatizi ila kwa njia moja ama nyengine wamekosa ufumbuzi wake.na leo nitaongea zaidi juu ya dalili na tiba yake.




kama nilivyokwisha eleza maana ya keratoconus ni hali ya kuendelea ambayo inafanya muundo wa kawaida
wa cornea ambao ni curve kwenda kwenye muundo wa cone.na vilevile nikatoa mambo yanayopelekea tatizo hili  kuwa
ni urithi na mazingira..na sababu nyengine pia ni ukunaji wa macho kupindukia.
ukunaji wa macho kupindukia, kwa mtu mwenye matatizo ya macho ni kawaida kwake kujikuta na uwasho katika macho ambapo inapelekea yeye kutumia muda mwingi sana kujikuna.kitu ambacho ningependa kuwashauri ni kwamba kupunguza kufanya kujikuna na kujitahidi kuacha kabisa  kwani ni sababu moja apo inayosemekana kupelekea keratoconus.



na miongoni mwa dalili za keratosconus ni;

*maumivu ya kicha na macho kwa ujumla


*kuwashwa kwa macho na kujikuna kupindukia.



*kushindwa kuendesha chombo wakati wa usiku

*kuona vitu viwiliviwili

*kuumizwa na muangaza

*kushindwa kusoma alama za barabarani


* blurring vision ambayo haitaweza kurekebishika kwa mawani isipokua kwa 20/20 with rigid,contact lenses.



*mabadiliko ya namba za miwani mara kwa mara.



 kwa upande wa matibabu ya keratoconus yapo mengi na kwa hatua mbali mbali.kwanza kabisa mgonjwa pindi anapogundulika na keratoconus changa hutakiwa kuvaa miwani au contact lens,ambazo mara nyingi huwa si suluhisho ya tatizo hili,pia kuna treatment nyengine ambayo inaitwa Intacs,c3-r,na cornea transplant.

intacs ring


contact lens


classes


C3-R. Corneal Collagen Crosslinking with Riboflavin.


in 2008 FDA clinic ya nchini marekani ulikuja na tiba ya kuzuia tatizo hili ambalo kwa kitaalam inaitwa  corneal collagen cross-linking (C3-R).


C3-R huzuia kuendelea kwa ukuaji wa kertocunus,naomba ifahamike kwamba c3-r  haitabadisha shape ya cornea iliyoharibika na wala haitoondoa athari iliyotokezea bali inazua kabisa maradhi haya kuendelea kukua tena,na pia huondoa ulazima wa cornea transplant.vilevile c3-r inasaidia kupunguza namba ya miwani yako.ingawa wataalamu wanasema keratoconus inaendelea na baada ya muda inasita but hawezi jua hadi kipindi itakoposita yaweza kuwa imeshakuathiri kiasi gani.

\


watu wengi wamekua na uelewa wa tiba corneal transplant lakini ningependa kuwaambia kuwa tiba hii ni ya mwisho kabisa kwa tatizo hili pindi tiba zote zitakaposhindikana ingawa ma daktari wengi nchini tanzania wanawashauri wangonjwa kufanya cornea transplant.

Cornea Transplant.




ni surgery inayofanywa ku replace cornea  kwa kutumia tissue ya mchangiaji mwengine mnaoendana.kusema ukweli cornea transplant  sio suluhisho kamili ya keratoconus ila ndio hivyo lisilobudi kwani mgonjwa anaetakiwa kufanyiwa tiba hii ni yule ambae amekosa kabisa uwezo wa kuona na ameshatumia njia zote,


napenda kusema ukweli kuwa cornea transplant ni tiba yenye hasara nyingi pia,naomba ifahamike kwamba baada ya kufanyiwa cornea transplant bado utakua unahitaji miwani ili kuona vizuri.na pia huwa inachukua muda mkubwa ili ku recover na pia hata kama cornea transplant itafanikiwa kufanyika bila ya tatizo lolote hutarudi kwenye hali 
yako ya kawaida kabisa..nakumbusha tena corneal transplant ni tiba ya mwisho kwa mgonjwa wa keratoconus.



kama una mtu mwenye tatizo hili nyumbani kwako au mtu yeyote unaemfahamu basi mshauri aende hospital na aulizie hii C3-R  treatment na doctor atamueleza kama ni candidate mzuri
wa kufanyiwa  hii treatment au la.

kwa maelezo haya nadhani yanaweza kusaidia kidogo kwa wale wenye utata juu ya tatizo hili.. kwa taarifa zaidi ya tatizo hili btajaribu kuwaletea kadri ya uwezo wangu ili nanyi mfaidike.


kupata makala ilopita bofya hapa.http://fromcoast.blogspot.com/2011/08/sharing-this-story-may-save-some.html

Inspire Me Daily.One Person Can Make a Difference.

[ Read More ]

HAWA MALAIKA WANAHITAJI MAZIWA TU...!!!



Familia ya Bw. na Bibi Edwin Dosantos wakazi wa Kimara jijini Dar es Salaam wanaomba msaada wa maziwa au fedha kwa ajili ya kuwasaidia kuwatunza watoto wao mapacha watatu ambao wana Umri wa miezi miwili.
Akizungumza na MO BLOG jijini Dar es Salaam  Baba wa watoto hao Bw. Dosantos amesema kwa sasa yeye na mkewe hawana kazi na inawawia vigumu kutimiza mahitaji ya watoto hasa lishe kutokana na kwamba mama mzazi wa watoto hao hana maziwa ya kutosha kuwakidhi watoto hao.

MO BLOG inaomba kuwashirikisha wadau ambao wataguswa na malaika hawa kuwasaidia chochote kupitia namba  ya mzazi wa kiume wa watoto hao             +255719909085       au             +255714940992       kwa kuwasiliana au kuwasilisha mchango wowote hasa maziwa.

Tunaamini kutoa ni moyo na si utajiri.
[ Read More ]