Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Nyumba yateketea kwa moto.


Wananchi wamelazimika kuvunja nyumba ili kumuokoa Muhsin Ali Said alipoamua kujifungia ndani jana mchana baada ya nyumba yake kuungua kwa moto.
“Aliamua kujifungia ndani akisema kwamba ni heri afe na nyumba yake. Vijana walilazimika kuvunja mlango na kumtoa kabla moto haujafika chumbani kwake na kumkimbiza msikitini. Ilikuwa ni hatari,” mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Abdul ambaye ni mmoja wa wanafamilia hiyo alisema jana katika eneo la tukio.
Abdul aliiambia Nipashe kwamba kwa takriban miezi kidhaa, Saidi alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya kiharusi na hivyo wakati nyumba yake iliyoko Mtaa wa Yombo, Temeke, Dar es Salaam inashika moto alikuwa ndani huku mkewe akiwa njiani akirejea kutoka safarini Morogoro.
Akizungumza kuhusu moto huo ulioteketeza kabisa nyumba hiyo, Abdul alisema kwamba ulitokana na pasi ya umeme.
“Kuna mfanyakazi wa ndani alikuwa akinyoosha nguo… Akajisahau kuzima pasi na ndio ikawa chanzo cha tukio hili,” alisema na kuongeza kwamba hakuna mtu aliyedhurika na moto huo.
Kwa mujibu wa Abdul, vitu vilivyookolewa na majirani baada ya kuvunja eneo ambalo moto ulikuwa haujasambaa ni friji, sofa na jiko la gesi.
Majirani walikilalamikia kikosi cha zima moto kwa kuchelewa kufika katika eneo la tukio mapema licha ya kutaarifiwa mara tu baada ya nyumba hiyo kushika moto..
Walidai kwamba licha ya nyumba hiyo kuanza kushika moto saa sita na nusu mchana, kikosi cha zima moto kilifika eneo la tukio saa nane mchana (masaa mawili na nusu baadaye) na kukuta nyumba hiyo ikiwa imeshatetea kabisa kwa moto.
[ Read More ]

TVZ Daima.

televisheni ya zanzibar katika website,unaweza kutembelea

www.tvz.co.tz.
[ Read More ]

Mtoto wa miaka miwili, mvuta sigara mdogo zaidi duniani


SOTE tunafahamu kwamba mvulana mwenye umri wa miaka miwili ni dhahiri atakuwa bado anakunywa maziwa au ameanza kula vyakula vya watu wazima. Lakini, mvulana mmoja wa Kichina ameanza kuvuta sigara wakati akiwa na umri wa miezi 18...Mtoto huyo huvuta paketi moja ya sigara kila siku na hushikwa na hamaki iwapo hapewi kiburudisho chake hicho.

Mtoto huyo, Tong Liangliang, alifundishwa jinsi ya kuwasha sigara na baba yake ambaye aliamini kwamba uvutaji ungempunguzia maumivu ya ugonjwa wa ngiri (hernia).

‘Baba-mtu hakujua jinsi tabia hiyo ingekolea kwa kitoto chake hicho hadi pale alipong’amua kwamba idadi ya sigara kilichokuwa kinavuta kila siku ilikuwa imeongezeka,” kilitangaza kituo cha China Radio International.

Tong alianza kuvuta sigara yake ya kwanza akiwa na umri wa miezi 18 katika jitihada za kupunguza maumivu ya ngiri yaliyokuwa yanamsumbua. Hili lilifanyika kwa kutambua kwamba mtoto huyo alikuwa ni mdogo mno kiasi cha kutoweza kufanyiwa opasuaji.

Hata hivyo, hii ni “rekodi ya dunia isiyokuwa rasmi” kwa vile kuingizwa kwake katika Kitabu cha Rekodi za Guiness (Guinness Book of Records) kama mvutaji mdogo zaidi wa sigara duniani, kutakataliwa kwa madai kwamba kitendo hicho kilichochea tabia yenye madhara kwa watoto.

source globalpublisher
[ Read More ]

Zanzibar yakubwa na uhaba wa petroli

Zanzibar inakabiliwa na uhaba mkubwa wa mafuta ya petroli hali inayotishia kuathiri sekta za uchumi.

Uhaba huo wa petroli umekuja huku Zanzibar ikiendelea kukabiliwa na ukosefu wa umeme kwa siku 42 mfululizo.

Uhaba wa mafuta umeanza kujitokeza wiki iliyopita na kusababisha baadhi ya wananchi wanaomiliki magari kulazimika kuyafungia majumbani na kuanza kutumia usafiri wa daladala na wengine kutembea kwa miguu.

Magari yanayotoa huduma hivi sasa ya usafiri ni yale yanayotumia mafuta ya dizeli lakini idadi kubwa ya magari yanayotumia petroli yamelazimika kusitisha huduma za usafiri na kusababisha msongamano wa watu katika vituo.

Kufuatia kuadimika kwa mafuta ya petroli, kumeibuka biashara ya magendo ambapo lita moja ya petroli imekuwa ikiuzwa kwa Sh. 2,000 badala ya 1,480.

Uchunguzi wa Nipashe umegundua kuwa mafuta ya petroli yamekuwa yakiuzwa kwa bei za ulanguzi nje ya vituo vya mafuta, hasa katika maeneo ya Kijangwani, Mikunguni Gulioni.

Kampuni zinazaoingiza mafuta Zanzibar ni Zanzibar Petrolium, GAPCO, pamoja na Kampuni ya United Petroleum, lakini wateja wake wamekuwa wakifika katika vituo na kuondoka bila ya kupata huduma hiyo.

Mafuta ya petroli yamechukua nafasi kubwa katika shughuli za kiuchumi baada ya Zanzibar kukosa huduma ya umeme kuanzia Desemba, mwaka jana, baada ya kifaa aina ya spliter kulipuka katika kituo cha Fumba.

Kiongozi mmoja mwandamizi kutoka Kampuni ya United Petroleum, alisema uhaba huo wa mafuta umejitokeza baada ya nishati hiyo kuadimika katika bandari ya Mombasa, Kenya kufuatia nishati hiyo kuchelewa kuwasili kutoka nje ya nchi.

Alisema uhaba huo wa mafuta katika bandari ya Mombasa, unatarajia kumalizika kuanzia Januari 30, mwaka huu kwa vile meli zenye mafuta zinatarajiwa kuwasili katika bandari hiyo.

Hata hivyo, alisema baada ya kujitokeza upungufu huo wa mafuta, waliamua kutafuta mafuta kutoka katika meli moja iliyofunga gati, katika Bandari ya Dar es Salaam, lakini hawakufanikiwa kutokana na meli hiyo kuwa katika foleni kubwa ya kusubiri kuteremsha mafuta Tanzania Bara.

[ Read More ]

NECTA lawamani kwa kushusha ufaulu wa wanafunzi


WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe ameeleza sababu kubwa iliyosababisha kushuka kwa ufaulu wa elimu ya msingi katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka jana kuwa ni pamoja na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), kudhibiti uvujaji wa mitihani na uchache wa walimu uliopo nchini.

Profesa Maghembe alitaja sababu nyingine iliyosababisha wanafunzi kufanya vibaya katika mtihani wa darasa la saba mwaka jana kuwa ni kutokuwepo uwiano sawa wa matumizi ya vitabu katika shule za msingi kote nchini.

Akifungua mkutano wa siku tatu wa wadau wa elimu nchini mjini hapa juzi, Profesa Maghembe alisema kitendo cha Baraza la Mitihani la Taifa kudhibiti uvujaji wa mitihani, umesababisha kushuka kwa ufaulu kutokana na wanafunzi wengi kutegemea kupewa mitihani.

Alisema licha ya NECTA kudhibiti hali hiyo, bado wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakichukua mitihani iliyopita na kuichapa upya na baadaye kuiuza mitaani kwa madai kuwa hiyo ndiyo mitihani yenyewe.

Kutokana na hali hiyo, Profesa Maghembe alisema imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa kwa wanafunzi kufanya vibaya kwa kuwa wamekuwa wakitarajia kuwa mitihani waliyonunua ndiyo watakayoifanya.

Profesa Maghembe alisema hakuna utaratibu wa shule zote nchini kuwa na kitabu kimoja kinachotumika katika kufundishia na badala yake kila shule imekuwa ikinunua kitabu ambacho inaona ni kizuri na kinafaa kufundishia.

Alisema kitendo cha biashara kuingia katika shule za msingi, kimechangia kuharibu elimu ya Tanzania ambapo aliwataka maofisa elimu wa mikoa na wilaya, maofisa elimu taaluma na taasisi za elimu kuangalia na kukubaliana kuchagua vitabu vinavyowiana ambavyo vitatumika kufundishia katika shule zote nchini.

Kutokana na wanafunzi kufanya vibaya katika mtihani wa darasa la saba mwaka jana, wadau wa elimu wakiwemo maofisa elimu wa mikoa na wilaya, maofisa taaluma wa mikoa na wilaya, wakuu wa vyuo vya ualimu na wakurugenzi wa halmashauri, wanakutana mjini hapa chini ya uenyekiti wa Waziri Maghembe kujadili kwa kina sababu nyingine zilizosababisha wanafunzi kufanya vibaya katika mtihani huo.

 
[ Read More ]

Mwanajeshi aliyeshambulia polisi afungwa miaka 12

MAHAKAMA ya Wilaya ya Bukoba imemhukumu askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Koplo Katarama, kifungo cha miaka 12 jela, baada ya kupatikana na hatia ya makosa matatu likiwamo la kumchania sare za kazi askari Polisi wa kike, kuharibu simu ya upepo na kumchania nguo ya ndani.

Hukumu hiyo ilitolewa Januari 5 mwaka huu katika Mahakama hiyo na Hakimu Richard Maganga ikielezwa kuwa mtuhumiwa ambaye hakuwa mahakamani hapo siku hiyo, alitenda makosa hayo Desemba 7, 2007 saa mbili asubuhi, eneo la Rwamishenye mjini hapa wakati polisi huyo akiwa kazini.

Awali Mahakama hiyo ilielezwa na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Ibrahimu Jumanne, kuwa Koplo Katarama siku hiyo alisimamishwa Rwamishenye akiwa katika gari la kiraia na wanajeshi wengine na baada ya gari kusimama, aliteremka na kumshambulia Sajini Wigesa aliyesimamisha gari hilo.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa alimkaba polisi huyo na kumwangusha katika barabara ya lami na kumsababishia michubuko magotini na maumivu makali kichwani, huku akimchania mavazi yake, kuharibu simu, kofia ya Polisi na kumchania nguo ya ndani.

Jumanne alidai kuwa mshtakiwa alimzuia polisi huyo kufanya kazi yake na baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha mashahidi watatu, mtuhumiwa alitiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo hicho.

Katika kosa la kwanza la kumzuia polisi kufanya kazi yake na la kumjeruhi askari huyo, alihukumiwa kifungo cha miaka mitano huku kwa la kumchania nguo, kuharibu simu na kofia alihukumiwa miaka miwili.

[ Read More ]

Mwanamke Amuua Mpenzi Wake Kwa Kumkalia


Mwanamke mmoja nchini Marekani mwenye uzito wa kilo 136 amepandishwa kizimbani kwa kosa la kumuua mpenzi wake aliyezaa naye watoto watatu kwa kumkalia hadi alipofariki.

Taarifa ya polisi wa Cleveland nchini Marekani ilisema kuwa mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Mia Landigham na mpenzi wake Mikal Middleston-Bey walikuwa kwenye mzozo wa ndani ya nyumba mnamo mwezi wa nane mwaka jana.

Taarifa zaidi zilisema kuwa mzozo huo ulikuwa mkubwa sana na kupelekea Mia aliyekuwa na uzito wa kilo 136 wakati huo kurushiana makonde na Mikal.

Mia alifanikiwa kumwangusha chini Mikal ambaye alikuwa mwembamba sana mwenye mwenye uzito wa kilo 54.4 tu. Mia alimkalia Mikal kwa dakika kadhaa aliponyanyuka Mikal alikuwa hapumui tena na alifariki dakika chache baadae.

Kufuatia tukio Mia alipandishwa mahakamani juzi jumatano na kuhukumiwa kwenda jela miaka mitatu na kufanya kazi za kuitumikia jamii kwa masaa 100.

Mia alikiri kosa lake la kumuua bila kukusudia mpenzi wake huyo ambaye amezaa naye watoto watatu. Mia pia aliiomba radhi familia ya marehemu kwa kusababisha kifo chake.

Wakili wa Mia aliiambia mahakama kuwa uhusiano wa Mia na Mikal ulikuwa na historia ya migogoro mingi na alimuomba jaji ampunguzie adhabu Mia kwa kuwa hana historia ya makosa ya jinai.

"Napenda kusema kuwa naomba radhi na nimehuzishwa na yaliyotokea natamani ningekuwa na uwezo wa kuurudisha uhai wake", alisema Mia.

source nifahamishe.com
[ Read More ]