Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

MH. KIKWETE AND 50-CENT US


[ Read More ]

JOKE OF THE DAY..



 A tourist asked a boat Guy do u know biology,physiology,geology,psychology and criminology?The boat guy said No........The tourist then said damn, what the hell do u know on the face of this earth you will die illiteracy!!

After a while a boat started sinking' then a boat guy asked the tourist Do you know swimology and escapology from crocodology? The tourist answer No........the boat guy said well you will drownology and crocodilogy will eat your assology and you will dieology because of your badmouthlogy!

                have a nice weekend
[ Read More ]

Fuso laua watu watano Moro

WANUNUZI watano wa mahindi  wamekufa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya tairi la gari walilokuwa wakisafiria, kupasuka na kusababisha gari hilo kupinduka,  katika eneo la Magubike katika Barabara ya Dodoma- Morogoro.Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Adolphina Chialo, aliwataja waliokufa katika ajali hiyo juzi usiku kuwa ni Mwarami Abdallah, mkazi wa Mzense jijini Dar es Salaam, Selemani Ngula (30), Kasimu Mwitago (30).

Kwa mujibu wa kamanda huyo, maiti mwingine ametambuliwa kwa jina moja la Kiejo (30) wakati mwingine hajatambuliwa. Chialo pia aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni, Timoth Paul,  Elisafi Mkumbwa na Hamisi Selemani, wote wakazi wa Kibaigwa  na kwamba majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu.

Alisema gari hilo lilikuwa linatokea katika Kijiji cha Kibaigwa, wilayani Kilosa kwenda jijini Dar es Salaam na kwamba chanzo cha ajali ni mwendo mkali.Alisema watu hao walikuwa wanasafiri kwa kutumia gari aina ya Mistubish Fuso iliyokuwa ikiendeshwa na Jackson Bezaleli Senyegwa (27) mkazi wa Kibaigwa ambaye alitoroka mara baada ya ajali hiyo.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi katika wodi namba moja,mmoja wa majeruhi Hamisi Selemani, alisema gari hilo lilikuwa limebeba gunia 100 za mahindi, jambo lililosababisha  moja ya matairi kuelemewa na kupasuka.

Alisema abiria wote waliokuwa nyuma ya gari hilo walifariki papo hapo baada ajali na kwamba walifunikwa na mahindi.Kamanda huyo alisema miili ya watu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, na kuomba wananchi kujitokeza ili kutambua miili ambayo haujatambuliwa.
[ Read More ]

Vijana wa Zanzibar kupata mafunzo ya kujiajiri kutoka India





VIJANA wanaomaliza vyuo vikuu vya Zanzibar wataanza kunufaika na utaratibu wa kupatiwa mafunzo maalumu ya biashara pamoja ufundi yatakayowawezesha kufungua miradi kujiajiri na kuwaajiri vijana wengine na kukuza hali zao za maisha.

Utaratibu huo unatarajiwa kutekelezwa kufuatia mazungumzo yaliyofanyika kati ya ujumbe wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar unaoongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (IT&C) ya Andhara Pradesh yaliyofanyika Hoteli ya Grand Kakatiya mjini Hyderabad.

Mbali na hatua hiyo Serikali ya Andhra Pradesh imemwomba Balozi wa Tanzania nchini India, John Kijazi kuandaa utaratibu utakaowezesha Zanzibar kunufaika na makubaliano yaliyofikiwa katika ziara ya Makamu wa Kwanza wa Rais kukuza mashirikiano katika nyanja za kiuchumi, biashara, kilimo na elimu kwa faida ya nchi mbili hizo.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Serikali ya Andhra Pradesh, Pannola Lakshmaiah alisema utaratibu huo unapaswa kuandaliwa mikakati ya ya utekelezaji mapema ili Serikali mbili hizo hasa Zanzibar iweze kunufaika mapema na kuchangia harakati zake za kuinua hali yake ya kiuchumi.

Alisema Jimbo la Andhra Pradesh limepata heshima kubwa duniani kote kwa Teknolojia ya Mawasiliano na Habari (IT), ambapo pia katika eneo hilo kunapatikana mji maalum wa Teknolojia ya Mawasiliano (Hyderabad Technology City) unaotoa mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa eneo hilo na India kwa ujumla.

“Jambo muhimu tutiliane saini makubaliano ya mashirikiano leo hii jioni (jana) na kitakachofuata Balozi aandae utaratibu wa utekelezaji kwa vile hakuna muda wa kusubiri, teknolojia ya habari na mawasiliano hivi sasa ni ajira ni uchumi ni kila kitu”, alisema Waziri wa IT& C.

Katika mazungumzo hayo, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Ramadhan Abdallah Shaaban alisema bado Zanzibar iko nyuma katika elimu ya IT&C, licha ya juhudi kubwa zinazoendelea kuchukulia kuinua elimu hiyo, ukiwamo mpango mahsusi ulioanzishwa na Serikali ya Zanzibar uitwao E -government.

Waziri Shaaban alisema kuna haja Serikali ya Andhra Pradesh ambapo inafanana kiutawala na Zanzibar ndani ya Jamhuri ya Muungano kushirikiana kuandaa utaratibu wa masomo kwa vijana wa Zanzibar.

Alisema kazi hiyo inaweza kufanikishwa chini ya utaratibu wa kupeleka wataalamu Zanzibar kutoa mafunzo hayo au vijana wa Zanzibar kwenda India kujifunza na baadaye kurudi nyumbani kutumia ujuzi huo kwa maslahi yao na nchi.    

Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed  Mazrui alisema Zanzibar kuna vijana wengi wanaomaliza vyuo vikuu na kukaa muda mrefu bila ya kupata ajira na utaratibu huo utawasaidia kupunguza tatizo la uhaba wa ajira na kuwapa mafunzo ya kazi maalumu za amali zitakazosaidia kuimarisha maendeleo.

Waziri Mazrui alisema maeneo mengine ambayo Zanzibar inaweza kunufaika katika mashirikiano na Andhra Pradesh ni usindikaji wa bidhaa kama vile za matunda, viungo pamoja na mazao ya baharini.

Waziri Mazrui alisema Zanzibar imejaaliwa kuna rasilimali za viungo kama vile karafuu zao ambao linasafirishwa kwa wingi kwenda India na kama kutakuwa na utaratibu wa kufanyiwa ‘branding’ na baadaye kusafirishwa litaweza kupata soko kubwa zaidi ya sasa katika soko la dunia.
[ Read More ]

Bomu Lililofichwa Kwenye Kilemba Lamuua Rais Mstaafu wa Afghanistan





Aliyekuwa rais wa Afghanistan Burhanuddin Rabbani ameuliwa baada ya mtu aliyelificha bomu kwenye kilemba chake kulilipua bomu hilo wakati wakisalimiana.
Rais Burhanuddin Rabbani ambaye pia alikuwa ndiye mkuu wa baraza kuu la kutafuta amani nchini Afghanistan, alifariki dunia baada ya mtu aliyekuwa akimuamini kumgeuka na kujilipua kwa bomu alilolificha kwenye kilemba chake.

Wasaidizi wanne wa Rabbani nao walifariki dunia baada ya bomu hilo kulipuka wakati Rabanni aliposimama kumsalimia kwa kumkumbatia mwakilishi wa Talibani baada ya kumalizika kwa mazungumzo marefu baina yao ya kutafuta suluhisho la amani nchini Afghanistan.

Fazel Karim Aymaq ambaye ni mjumbe wa baraza la amani la Afghanistan alisema kuwa watu wawili wanaoaminika sana walifika nyumbani kwa Rabbani mjini Kabul ili kuleta ujumbe wa amani toka kwa Talibani.

"Mmoja wao alisalimiana na Rabbani kwa kuweka kichwa chake kwenye mabega ya Rabbani na kulilipua bomu alilokuwa amelificha kwenye kilemba chake", alisema Aymaq.

Taarifa zaidi zilisema kuwa mjumbe huyo wa Talibani alikuwa akijulikana kama Mohammad Masoom na alikuwa akifahamiana vizuri sana na Rabbani akiaminika kuwa anatafuta suluhisho la amani.

Masoom aliluwa akienda mara kwa mara nyumbani kwa Rabbani na aliwahi kumkaribisha Rabbani nyumbani kwake na alimpa ulinzi wa kutosha hali iliyomjengea uaminifu wa kutosha kwa rais huyo wa zamani.

Masoom aliteuliwa na Talibani kuwa mwakilishi wa Talibani katika mazungumzo ya kutafuta suluhisho la amani kati ya Talibani na serikali ya Afghanistan.

Kuuliwa kwa Rabbani ni pigo kubwa sana kwa rais wa Afghanistan, Hamid Karzai ambaye aliamua kukatisha ziara yake nchini Marekani na kurudi Afghanistan.

Mamia ya watu waliandamana leo kwenye mitaa ya mjini Kage.bul kulaani kuuliwa kwa rais huyo mstaafu aliyekuwa akiheshimika kwa jitihada zake za kuleta amani kwenye nchi hiyo ambayo imeharibiwa kwa vita.

"Alitaka amani nchini Afghanistan na alijitolea maisha yake kupigania njia ya kuleta amani", alisema mmoja wa waandamanaji hao.

source nifahamis
[ Read More ]

Kim Kardashian & Kris Humphries Wedding Photos!

[ Read More ]

Kesi ya ajali ya Meli Zanzibar yasitishwa





KESI ya ajali ya meli ya MV Spice Islanders iliyofunguliwa dhidi ya manahodha wa meli hiyo na mmiliki wake, imesitishwa.Kesi hiyo ambayo jana ilitajwa kwa mara ya pili katika Mahakama Kuu ya Zanzibar, imesitishwa kupisha uchunguzi wa kamati iliyoundwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein.

Hatua hiyo imefikiwa na Mrajisi wa Mahakama hiyo, George Kazi baada ya wakili wa utetezi, Hamidi Mbwezeleni, kuiomba Mahakama iiahirishe kwa sababu Katiba ya Zanzibar inapinga kesi moja kusikilizwa na vyombo viwili vinavyofanya kazi kwa mujibu wa katiba hiyo.

“Kama kuna haja ya watu hawa kushtakiwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, basi tume hiyo ikae pembeni mpaka Mahakama itakapomaliza kazi yake na kama kuna haja ya tume hiyo kufanya kazi yake, basi Mahakama inabidi ikae pembeni mpaka tume hiyo itakapomaliza kazi yake,” alisema.

Bila kufanya hivyo alisema: "Hukumu ya watu hawa itakuwa na utata kwa sababu endapo Mahakama ikisema kuwa wana makosa na wanastahili adhabu halafu tume hiyo ikasema kuwa hawana makosa na hawastahili adhabu, Wazanzibari hawatatuelewa,” alisema Mbwezeleni na kusisitiza:

“Upande mwingine ni kwamba kama Mahakama ikisema kuwa watu hawa hawana makosa na wanastahili kuwa huru halafu tume hiyo ikasema kuwa watu hawa wana makosa na wanastahili kuchukuliwa hatua za kisheria, hali itakuwa tete kwa wananchi dhidi ya Serikali yao na Mahakama kwa ujumla.”

Awali, maelezo hayo ya upande wa utetezi yalipingwa na Wakili wa mashtaka, Ramadhan Nasibu ambaye alisema kama Serikali, haina shaka yoyote juu ya kamati hiyo kwa sababu inafahamu kwamba uamuzi wake hauwezi kuingilia wala kuharibu uamuzi wa Mahakama, kwa kuwa Mahakama ni chombo huru kinachosimamia haki.

“Upande wa mashtaka unajizuia kuhoji uhalali wa tume hiyo kwa sababu ushahidi wao hauwezi kuizuia Mahakama isifanye kazi yake wala haitakuwa mwisho wa mashtaka ya watu hao. Tume hiyo haina meno kwa sababu ushahidi wao utakaopatikana hauwezi kuwatia watuhumiwa hao hatiani,” alisema.

Baada ya malumbano hayo, Mrajisi wa Mahakama alikubaliana na hoja za upande wa utetezi na kuahirisha kesi hiyo.

Akisoma uamuzi huo Mrajisi Kazi alisema: “Siko tayari kusema kuwa tume hiyo ni halali ama si halali, ila kwa pointi iliyotolewa na upande wa utetezi, nami ninaona kwamba ni ya msingi, hivyo ninalazimika kuiahirisha kesi hii mpaka tume hiyo itakapomaliza kazi yake na kutoa mapendekezo.”

“Siwezi kuwa katika mtizamo tofauti na upande wa utetezi kuhusu suala hilo, kwa sababu kuna hatari ya uamuzi wa tume na mahakama, kupingana. Hivyo ninaahirisha kesi hii mpaka tume hiyo itakapomaliza kazi yake.”
Mrajisi Kazi pia alisema kuwa dhamana ya watuhumiwa hao iko wazi hivyo wanatakiwa kudhaminiwa kwa hati ya Sh1milioni kila mmoja na watahitajika Mahakamani hapo mara tu baada ya tume hiyo kukamilisha kazi yake na kutoa uamuzi.”

Septemba 10, mwaka huu meli ya MV Spice Islanders iliyokuwa ikitokea Unguja kwenda Pemba ilizama katika Kisiwa cha Nungwi, kilometa 20 kutoka Unguja na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 200 na majeruhi zaidi ya 600, huku ikiaminika kwamba mamia ya abiria wengine hawakuolewa baharini.

Siku tatu baada ya ajali hiyo, watu wanne akiwamo
Nahodha wa meli hiyo, Saidi Abdala Kinyanyite (58), mkazi wa Mbagala, Dar es Salaam na Nahodha Msaidizi, Abdallah Mohamed Ali (30), mkazi wa Bububu, Zanzibar walifikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa uzembe na kusababisha vifo vya watu.

Watuhumiwa wengine katika kesi hiyo ni Simai Nyange Simai (27), Mkazi wa Mkele, Zanzibar ambaye ni Ofisa Usalama wa Bandarini na vyombo vyote vya usafiri wa majini na Yussuf Suleiman Jussa (47), Mkazi wa Kikwajuni Zanzibar ambaye ni Ofisa wa meli hiyo na mwanahisa.
[ Read More ]

Watu 36 Wauliwa Kwa Kupigwa Risasi Baa

Zaidi ya watu 36 wamefariki dunia nchini Burundi baada ya watu waliokuwa na silaha kuvamia baa na kuwapiga risasi watu wote waliokuwemo kwenye baa hiyo Watu 36 wameiaga dunia huku wengine wakiwa wamelazwa hospitali hali zao zikiwa mbaya baada ya watu waliokuwa na silaha kuvamia baada moja iliyopo nje kidogo ya mji mkuu wa Burundi, Bunjumbura na kuwamiminia risasi watu wote waliokuwemo kwenye baa hiyo.

Tukio hilo lilitokea jana wakati kundi la watu wanaoaminika kuwa ni waasi wa Burundi wanaoishi nchini Kongo kuvuka mpaka na kuivamia baa hiyo iliyopo kwenye mji wa Gatumba.

Gavana wa Bunjumbura, Jacques Minani alisema kuwa watu waliofanya shambulio hilo waliingia Gatumba baada ya kuvuka mto wakitokea nchini Jamhuri ya Kongo.

Mmoja wa watu waliojeruhiwa kwenye shambulio ambaye alipigwa risasi ya tumbo, alisema kuwa watu waliofanya shambulio hilo walikuwa wamevaa nguo za kijeshi.

"Mmoja wao alisema Waue wote waue wote hakikisha hakuna atakayenusurika", alisema majeruhi huyo aliyejulikana kwa jina la Jackson Kabura.

Kundi kubwa la watu waliokuwa na silaha nzito za kivita waliivamia baa inayojulikana kwa jina la 'Chez les Amis' na kuwalazimisha watu wote walale chini.

Mwanaume mmoja ambaye alinusurika maisha yake ingawa ndugu zake wawili waliuawa kwenye shambulio hilo alisema kuwa "Walimwambia kila mtu alale chini na ndipo walipoanza kupiga risasi."

Miili ya watu iliachwa kwenye maegesho ya magari katika hospitali moja mjini Gatumba huku taarifa zaidi zikisema kuwa idadi ya majeruhi imekuwa kubwa kuliko uwezo wa hospitali.

Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi aliahirisha safari yake ya kwenda New York, Marekani na kutembelea eneo lilipofanyika shambulio hilo na kuahidi kuwachukulia hatua kali watu wote waliohusika.

na nifahamishe.
[ Read More ]

JELA MIAKA 30 KWA KUMLAWITI MKEWE!


  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Wilaya ya Mpanda, imemhukumu Haruna Ndayage (54), mkazi wa mtaa wa Kashaulili, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuingilia mkewe kinyume na maumbile.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi, Desdel Magezi, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashtaka.
Alisema shahidi wa tano ambaye ni daktari aliithibitishia mahakama kuwa mlalamikaji baada ya kufanyiwa uchunguzi iligundulika kuwa aliingiliwa kinyume na maumbile yake.
Aidha, alisema ushahidi uliotolewa na watoto wao ulionyesha kuwa Haruna alimfayia kitendo hicho mkewe, kwani watoto wote walimtaja baba yao ndiye mhusika wa kitendo hicho.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mshtakiwa aliiomba mahakama impunguzie adhabu, kwani wakati akifanya kosa hilo hakuwa na akili timamu.
Alidai kwa miaka 24 waliyoishi na mkewe hakuwa na ugomvi wowote naye isipokuwa miezi sita kabla ya tukio hili waalikuwa na ugomvi ugomvi ambao hakuweza kuueleza mahakamani hapo.
Hata hivyo, Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Finias Mjula, alipinga utetezi huo na kuiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa ili awe mfano kwa watu wengine wenye tabia ya kuwadhalilisha wake zao.
Awali katika kesi hiyo, ilidaiwa kuwa Oktoba 28, mwaka jana, majira ya saa 12 alfajiri, mshtakiwa alimwingilia kinyume cha maumbile mkewe.

[ Read More ]

Moto Wateketeza Soko Jingine Jijini Mbeya

Jiji la Mbeya liko kwenye taharuki hivi sasa kufuatia ajali ya moto unaoendelea kuwaka katika soko la Sido, ambako wafanyibiashara wa lililokuwa soko la Mwanjelwa walihamia baada ya soko hilo la awali kuungua.






[ Read More ]

MV Spice Islanders ilibeba abiria 3,000


Meli ya MV Spice Islanders ikielewa katika bahari eneo la Nungwi Zanzibar nchini Tanzania, inasadikiwa kuwa kabla ya kupata ajali meli hiyo ilikuwa imebeba abiria 3,000, huku uwezo wake ukiwa abiria 600

MELI ya MV Spice Islanders iliyopata ajali mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha vifo vya takriban watu 200 na majeruhi 619 ambao waliokopolewa, ilibeba abiria 3,000 wakati uwezo wake ni kubeba abiria 600 tu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa idadi hiyo kubwa ya abiria, haijumuishi mizigo ambayo kiasi chake bado hakijajulikana.

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dadi Fakhi Dadi alisema jana kuwa mkoa huo umepoteza watu 1,600 katika ajali hiyo, huku Wilaya ya Wete pekee ikiwa imepoteza watu 1,141.Dadi alisema hayo alipokuwa akizungumza mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.

“Wilaya ya Micheweni imepoteza watu 367, huku Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba ikipoteza watu 27 na Wilaya ya Chakechake imepoteza watu 148,” alisema Dadi na kuongeza:

“Kwa idadi hiyo ikijumlishwa na idadi ya watu 619 waliosalimika katika ajali hiyo na wengine 204 waliotambuliwa na kuzikwa na wengine watano waliookotwa Mombasa, huenda meli ile ilikuwa na watu 3, 000,” alisema Dadi.

Kutokana na takwimu zinazoendelea kukusanywa, hadi sasa zaidi ya watu 2,000 hawajulikani walipo, mbali ya wale 198 walioopolewa na kuzikwa na wengine 619 walionusurika.

Wabunge wa CUF wajiandaa kuishtaki Serikali
Wakati Serikali ikiendelea kukusanya takwimu za waliokufa au kupotea kwenye ajali hiyo, baadhi ya wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), wamekuwa wakizunguka majimboni mwao kufanya tathmini kwa lengo la kuishtaki Serikali.

Mbunge wa Jimbo la Ziwani, Ahmed Juma Ngwali alisema anatafuta idadi kamili ya wananchi wake walioathirika kwa ajali hiyo ili afanye utaratibu wa kuishtaki Serikali kutokana na uzembe uliosababisha ajali hiyo.

“Tukishapata orodha kamili ya wananchi, nakwenda kutafuta orodha ya abiria waliokuwa kwenye meli, nalinganisha. Kwa wale waliokuwa na tiketi, nitasimamia walipwe bima zao na mmiliki wa meli. Wale waliozidi nitaishtaki Serikali kwa kuzembea,” alisema Ngwali.

Ngwali aliyekuwa akizunguka nyumba hadi nyumba kuorodhesha watu hao, alisema kwa kiasi kikubwa, Serikali ndiyo iliyofanya uzembe katika tukio hilo.

“Huu ni uzembe na ni lazima twende mahakamani. Ikiwa samaki wa Magufuli (Waziri wa Ujenzi), hadi leo wanasotesha watu mahakamani, itakuja kuwa watu?” alisema.

Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk alisema anakusudia kupeleka hoja binafsi bungeni ili kumwajibisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa tukio hilo.

“Inaonyesha Serikali haina takwimu sahihi, ndiyo maana sisi tumeamua kufanya tathmini ya kina,” alisema na kuongeza kuwa tathmini hiyo itamsaidia kuratibu misaada anayopata kutoka kwa mashirika mbalimbali kwa ajili ya watu walioathirika katika tukio hilo.

“Kwa mfano sasa Benki ya Watu wa Kenya (KCB) imetoa ahadi ya kusomesha watoto yatima waliofiwa na wazazi katika ajali hiyo. Lazima niwe na takwimu sahihi za kuwapa benki hiyo,” alisema Mbarouk.

Akizungumzia suala la Waziri Mkuu mbunge huyo alisema: “Sisi ni wasemaji wa wananchi siyo Serikali. Nina mpango wa kupeleka hoja binafsi Bungeni ili Waziri Mkuu awajibike.”

Alieleza sababu za kutaka Waziri Mkuu awajibike kuwa ni pamoja na Serikali kupuuza swali lake alilouliza bungeni kuhusu usalama wa vyombo vya majini hadi sasa.

Kazi ya kuwaokoa walizama bado nguvu
Kazi ya uokoaji wa miili ya watu wanaosadikiwa kunasa ndani ya meli hiyo inaonekana kuwa ngumu baada ya wataalamu wa uokoaji kutoka Afrika Kusini kushindwa kuendelea na kazi kutokana na kina kirefu cha maji katika eneo hilo.

Tetesi za kushindikana kwa kazi hiyo zilianza kusikika jana kutoka kwa wavuvi ambao wamekuwa wakifanya kazi zao katika eneo hilo kwa kipindi kirefu huku. Wavuvi hao wanasema eneo hilo lina urefu wa zaidi ya mita 300 kutoka usawa wa bahari.

Mzamiaji kutoka eneo la Nungwi, Karim Abdallah alisema: “Hili eneo tunalifahamu lina kina kirefu sana unaweza kubeba kamba zinazojaza boti na ukifika eneo hilo na kutupa nanga haifiki chini, tulifahamu kwamba wataalamu hao hawawezi kufanya lolote katika eneo hilo.”

Kauli ya wavuvi hao ilionekana kuthibitishwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ambayo iliamua kuondoa mahema yaliyokuwa yamewekwa katika fukwe za Nungwi kwa ajili ya kuhifadhi miili ilinayopatikana.

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Pembe Juma alisema wameamua kuanua mahema hayo kwa sababu uwezekano wa kupata miili iliyobaki ni mdogo.

“Tumelazimika kuondoa mahema hayo kwa sababu hali inavyoonekana ni wazi kuwa wataalamu hao wanaweza wakashindwa kupata miili ya watu wanaokisiwa kubaki katika eneo hilo” alisema Juma.

Hata hivyo, alipoulizwa juu ya hali ya waokoaji hao ambao bado wako katika eneo la tukio wakiongozwa na Kikosi cha Maji cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) alisema: “Sina mamlaka ya kuzungumzia mazingira ya wataalamu hao isipokuwa taarifa nilizonazo kwa sasa ndizo hizo nilizowapa.”

Wataalamu hao walitakiwa kuanza kazi hiyo juzi lakini wakashindwa kuendelea na kazi hiyo kwa sababu ya hali ya bahari kuwa mbaya. Hata hivyo, walianza tena kazi hiyo leo ingawa si kwa kuingia baharini kutafuta waliokwama chini ya maji, bali kutafuta maiti zinazoelea katika maeneo mbalimbali ya Tanga, Mombasa, Unguja na Pemba.

Katika hatua nyingine mtu mmoja alinusurika jana baada ya kuwadhihaki hadharani watu waliokumbwa na mkasa huo wa ajali ya meli kwa kudai kwamba walistahili.

Mashuhuda waliokuwapo katika eneo hilo walidai kuwa sekunde chache baada ya kutamka maneno hayo, alivamiwa na watu waliokuwa eneo hilo lakini akafanikiwa kukimbilia katika duka la vitabu la Masomo na hatimaye kuokolewa na Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiongozwa na Mkuu wa Polisi Kituo cha Malindi, Haji Mgoro.

Mkurugenzi wa duka hilo, Farouk Karim Karim alisema hatua ya mtu huyo kukimbilia dukani kwake ilihatarisha maisha yake baada ya umati watu kufunga mitaa yote inayozunguka Soko Kuu la Darajani ukimlazimisha kumtoa mtu huyo vinginevyo waingie kumtoa wenyewe.

“Kwa kweli mimi sikufahamu hata walipoanzia. Nilikuwa hapa dukani ghafla nikashtuka mtu anaingia ndani huku akisema nakufa, kabla hata sijamuuliza kilichomsibu umati watu ukawa umeshajazana dukani kwangu ndipo nilipolazimika kufunga mlango na kuwaita polisi,” alisema Karim.

Seif atoa mkono wa pole
Maalim Seif, jana aliongoza ujumbe wa viongozi wa Serikali kutoa pole kwa wafiwa waliopoteza ndugu na jamaa zao. Katika ziara hiyo, alifuatana Mawaziri wasiokuwa na Wizara Maalumu; Haji Faki Shaali na Machano Othman Said, Waziri wa Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto, Zainab Omar na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Said Ali Mbarouk.

Akizungumza na ndugu na jamaa wa marehemu hao katika Ukumbi wa Umoja ni Nguvu, Mkoani na baadaye Uwanja wa Gombani katika Mkoa wa Kusini Pemba, Maalim Seif aliwataka wakazi wa Zanzibar, kuvuta subira kwa kuwa msiba huo ni wa taifa zima na ni mipango ya Mungu.

Alisema Serikali inaamini kuwa kulikuwa na uzembe katika tukio hilo ndiyo maana imeamua kuunda tume huru ambayo itafanya uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo.Alisema Serikali haitasita kumchukulia hatua mtendaji yeyote atakayebainika kuhusika katika uzembe uliosababisha ajali hiyo.Akiwa Mkoa wa kusini Pemba, Maalim Seif ametoa mkono wa pole na ubani kwa familia zaidi ya 112.lias Msuya na Jackson Odoyo, Zanzibar
MELI ya MV Spice Islanders iliyopata ajali mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha vifo vya takriban watu 200 na majeruhi 619 ambao waliokopolewa, ilibeba abiria 3,000 wakati uwezo wake ni kubeba abiria 600 tu.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa idadi hiyo kubwa ya abiria, haijumuishi mizigo ambayo kiasi chake bado hakijajulikana.

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dadi Fakhi Dadi alisema jana kuwa mkoa huo umepoteza watu 1,600 katika ajali hiyo, huku Wilaya ya Wete pekee ikiwa imepoteza watu 1,141.Dadi alisema hayo alipokuwa akizungumza mbele ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad.

“Wilaya ya Micheweni imepoteza watu 367, huku Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba ikipoteza watu 27 na Wilaya ya Chakechake imepoteza watu 148,” alisema Dadi na kuongeza:

“Kwa idadi hiyo ikijumlishwa na idadi ya watu 619 waliosalimika katika ajali hiyo na wengine 204 waliotambuliwa na kuzikwa na wengine watano waliookotwa Mombasa, huenda meli ile ilikuwa na watu 3, 000,” alisema Dadi.

Kutokana na takwimu zinazoendelea kukusanywa, hadi sasa zaidi ya watu 2,000 hawajulikani walipo, mbali ya wale 198 walioopolewa na kuzikwa na wengine 619 walionusurika.

Wabunge wa CUF wajiandaa kuishtaki Serikali
Wakati Serikali ikiendelea kukusanya takwimu za waliokufa au kupotea kwenye ajali hiyo, baadhi ya wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), wamekuwa wakizunguka majimboni mwao kufanya tathmini kwa lengo la kuishtaki Serikali.

Mbunge wa Jimbo la Ziwani, Ahmed Juma Ngwali alisema anatafuta idadi kamili ya wananchi wake walioathirika kwa ajali hiyo ili afanye utaratibu wa kuishtaki Serikali kutokana na uzembe uliosababisha ajali hiyo.

“Tukishapata orodha kamili ya wananchi, nakwenda kutafuta orodha ya abiria waliokuwa kwenye meli, nalinganisha. Kwa wale waliokuwa na tiketi, nitasimamia walipwe bima zao na mmiliki wa meli. Wale waliozidi nitaishtaki Serikali kwa kuzembea,” alisema Ngwali.

Ngwali aliyekuwa akizunguka nyumba hadi nyumba kuorodhesha watu hao, alisema kwa kiasi kikubwa, Serikali ndiyo iliyofanya uzembe katika tukio hilo.

“Huu ni uzembe na ni lazima twende mahakamani. Ikiwa samaki wa Magufuli (Waziri wa Ujenzi), hadi leo wanasotesha watu mahakamani, itakuja kuwa watu?” alisema.

Mbunge wa Ole, Rajab Mbarouk alisema anakusudia kupeleka hoja binafsi bungeni ili kumwajibisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa tukio hilo.

“Inaonyesha Serikali haina takwimu sahihi, ndiyo maana sisi tumeamua kufanya tathmini ya kina,” alisema na kuongeza kuwa tathmini hiyo itamsaidia kuratibu misaada anayopata kutoka kwa mashirika mbalimbali kwa ajili ya watu walioathirika katika tukio hilo.

“Kwa mfano sasa Benki ya Watu wa Kenya (KCB) imetoa ahadi ya kusomesha watoto yatima waliofiwa na wazazi katika ajali hiyo. Lazima niwe na takwimu sahihi za kuwapa benki hiyo,” alisema Mbarouk.

Akizungumzia suala la Waziri Mkuu mbunge huyo alisema: “Sisi ni wasemaji wa wananchi siyo Serikali. Nina mpango wa kupeleka hoja binafsi Bungeni ili Waziri Mkuu awajibike.”

Alieleza sababu za kutaka Waziri Mkuu awajibike kuwa ni pamoja na Serikali kupuuza swali lake alilouliza bungeni kuhusu usalama wa vyombo vya majini hadi sasa.

Kazi ya kuwaokoa walizama bado nguvu
Kazi ya uokoaji wa miili ya watu wanaosadikiwa kunasa ndani ya meli hiyo inaonekana kuwa ngumu baada ya wataalamu wa uokoaji kutoka Afrika Kusini kushindwa kuendelea na kazi kutokana na kina kirefu cha maji katika eneo hilo.

Tetesi za kushindikana kwa kazi hiyo zilianza kusikika jana kutoka kwa wavuvi ambao wamekuwa wakifanya kazi zao katika eneo hilo kwa kipindi kirefu huku. Wavuvi hao wanasema eneo hilo lina urefu wa zaidi ya mita 300 kutoka usawa wa bahari.

Mzamiaji kutoka eneo la Nungwi, Karim Abdallah alisema: “Hili eneo tunalifahamu lina kina kirefu sana unaweza kubeba kamba zinazojaza boti na ukifika eneo hilo na kutupa nanga haifiki chini, tulifahamu kwamba wataalamu hao hawawezi kufanya lolote katika eneo hilo.”

Kauli ya wavuvi hao ilionekana kuthibitishwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ambayo iliamua kuondoa mahema yaliyokuwa yamewekwa katika fukwe za Nungwi kwa ajili ya kuhifadhi miili ilinayopatikana.

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Pembe Juma alisema wameamua kuanua mahema hayo kwa sababu uwezekano wa kupata miili iliyobaki ni mdogo.

“Tumelazimika kuondoa mahema hayo kwa sababu hali inavyoonekana ni wazi kuwa wataalamu hao wanaweza wakashindwa kupata miili ya watu wanaokisiwa kubaki katika eneo hilo” alisema Juma.

Hata hivyo, alipoulizwa juu ya hali ya waokoaji hao ambao bado wako katika eneo la tukio wakiongozwa na Kikosi cha Maji cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) alisema: “Sina mamlaka ya kuzungumzia mazingira ya wataalamu hao isipokuwa taarifa nilizonazo kwa sasa ndizo hizo nilizowapa.”

Wataalamu hao walitakiwa kuanza kazi hiyo juzi lakini wakashindwa kuendelea na kazi hiyo kwa sababu ya hali ya bahari kuwa mbaya. Hata hivyo, walianza tena kazi hiyo leo ingawa si kwa kuingia baharini kutafuta waliokwama chini ya maji, bali kutafuta maiti zinazoelea katika maeneo mbalimbali ya Tanga, Mombasa, Unguja na Pemba.

Katika hatua nyingine mtu mmoja alinusurika jana baada ya kuwadhihaki hadharani watu waliokumbwa na mkasa huo wa ajali ya meli kwa kudai kwamba walistahili.

Mashuhuda waliokuwapo katika eneo hilo walidai kuwa sekunde chache baada ya kutamka maneno hayo, alivamiwa na watu waliokuwa eneo hilo lakini akafanikiwa kukimbilia katika duka la vitabu la Masomo na hatimaye kuokolewa na Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiongozwa na Mkuu wa Polisi Kituo cha Malindi, Haji Mgoro.

Mkurugenzi wa duka hilo, Farouk Karim Karim alisema hatua ya mtu huyo kukimbilia dukani kwake ilihatarisha maisha yake baada ya umati watu kufunga mitaa yote inayozunguka Soko Kuu la Darajani ukimlazimisha kumtoa mtu huyo vinginevyo waingie kumtoa wenyewe.

“Kwa kweli mimi sikufahamu hata walipoanzia. Nilikuwa hapa dukani ghafla nikashtuka mtu anaingia ndani huku akisema nakufa, kabla hata sijamuuliza kilichomsibu umati watu ukawa umeshajazana dukani kwangu ndipo nilipolazimika kufunga mlango na kuwaita polisi,” alisema Karim.

Seif atoa mkono wa pole
Maalim Seif, jana aliongoza ujumbe wa viongozi wa Serikali kutoa pole kwa wafiwa waliopoteza ndugu na jamaa zao. Katika ziara hiyo, alifuatana Mawaziri wasiokuwa na Wizara Maalumu; Haji Faki Shaali na Machano Othman Said, Waziri wa Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto, Zainab Omar na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Said Ali Mbarouk.

Akizungumza na ndugu na jamaa wa marehemu hao katika Ukumbi wa Umoja ni Nguvu, Mkoani na baadaye Uwanja wa Gombani katika Mkoa wa Kusini Pemba, Maalim Seif aliwataka wakazi wa Zanzibar, kuvuta subira kwa kuwa msiba huo ni wa taifa zima na ni mipango ya Mungu.

Alisema Serikali inaamini kuwa kulikuwa na uzembe katika tukio hilo ndiyo maana imeamua kuunda tume huru ambayo itafanya uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo.Alisema Serikali haitasita kumchukulia hatua mtendaji yeyote atakayebainika kuhusika katika uzembe uliosababisha ajali hiyo.Akiwa Mkoa wa kusini Pemba, Maalim Seif ametoa mkono wa pole na ubani kwa familia zaidi ya 112.

habari na glp

[ Read More ]

SAIDIA ZANZIBAR.


[ Read More ]

Mtoto miezi 4 aelea bila boya





Hata hivyo, taarifa ya kutozama kwa mtoto huyo iliibua mjadala mzito ambapo kwa mujibu wa wanamaji, inawezekana alikuwa amevalishwa nepi na ‘pempasi’ yenye nailoni ndiyo maana hakuzama.

Kundi lingine lilidai kuwa, hata kama angekuwa amefungwa pempasi, angezama eneo la kichwa na kubakiza sehemu iliyofungwa pempasi ikiwa juu hivyo wao waliamini ni Mungu tu!

 Hata hivyo, habari za uhakika zilidai kuwa mtoto huyo anaendelea vizuri.
Hadi gazeti hili linatinga mitamboni, zaidi ya watu 240 waliripotiwa kupoteza maisha na zaidi ya 600 kuokolewa katika ajali hiyo mbaya.


na glp.

[ Read More ]

Zanzibar ferry accident day 2

[ Read More ]

VIDEO AJALI YA MELI ZNZ

[ Read More ]

KATIKA VIWANJA VYA MAISARA KUTAMBUA MIILI YA NDUGU ZAO.









DK. SHEIN AKIWA KATIKA ENEO LA TUKIO NUNGWI AKIJUMUIKA NA WANANCHI KUPOKEA MAJERUHI NA MAITI

































MMOJA wa Abiria aliyekuwa katika ajali hiyo Khamis Jabu Faki (62) akizungumza na Mwandishi wa Redio Zenj Fm Hafidh Kassim baada ya kufikishwa katika ufukwe wa pwani ya Nunwi akielezea jinsi ya ajali ilivyotokea.

WANANCHI wa Kijiji cha Nungwi wakiwa ufukweni mwa Bandari ya Nungwi wakiwasiliana na waokoaji wakiwa baharini.
MAJERUHI wa ajili ya Meli ya Spice wakipata huduma ya kwanza baada ya kuwasal katika bandari ya Nungwi baada ya kunusurika.


WANANCHI wakiwa katika Ufukwe wa Bandari ya Nungwi kuwatambua watu wao
MOJA ya boti inayoopowa maiti na majeruhi ikiwa na miili ya watu waliokufa katika ajali ya meli ikiwa katika bandari ya Nungwi.
HALI ya uokoaji ikiendelea katika pwani ya Nungwi.
WANANCHI na Askari wa Vikosi vya Ulinzi wakiwa na miili ya marehemu wakiitowa katika boti za uokoaji bandari ya Nungwi.
ASKALI wa Jeshi la Wananchi wakitowa msaada wa katika zoezi hilo la uokoaji wakiwa katika bandari ya Nungwi.
WATALII kutoka Nchi Ufaransa wakitowa huduma ya kwanza kwa majeruhi wa Meli ya Spice iliozama katika Mkondo wa bahari ya Nungwi.
MSAADA hutolewa popote ndivyo inavyoonekana Watalii kutoka Ufaransa wakitowa huduma ya kwanza kwa majeruhi

MTALII kutoka Ufaransa Jullie akitowa huduma ya kwanza kwa mmoja wa mtoto aliyenusurika katika ajali ya Meli ya Spice baada ya kuokolewa wakiwa katika bandari ya Nungwi.
MWANDISHI wa habari gazeti laZanzibar Leo Ramadha Makame akimuhoji mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo katika ufukwe wa bahari ya Nungwi
[ Read More ]