TAMASHA la 12 la filamu la kimataifa la Zanzibar (ZIFF), 2009 limezinduliwa rasmi jana mjini hapa katika eneo la Mji Mkongwe, viwanja vya Ngome Kongwe kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu. Burudani kutoka kwa mshairi Mrisho Mpoto 'Mjomba', Beni na Siti zilipamba uzinduzi wa tamasha hilo ambalo litaendelea hadi Julai 12. Baada ya uzinduzi huo, filamu ya Izulu Lami (My Secret Sky) ya dakika 93 ilionyeshwa.

KAIMU Mufti wa Tanzania, Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea kwenye Kijiji cha Mnolela Wilaya ya Lindi Vijijini baada ya tairi ya mbele ya gari alilokuwa akisafiria kutoka Mtwara kupasuka na kupinduka. Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Lindi, Sifuel Shirima zinaeleza kuwa tukio hilo lilitokea jana saa 8:09 katika barabara

Madaktari waliochunguza kifo cha mwanamuziki maarufu wa mtindo wa Pop, Michael Jackson, aliyefariki dunia Alhamisi, wamesema matokeo ya awali hayajaonyesha hila yoyote. Lakini vipimo vingine vikiwemo vya sumu vimechukuliwa ambapo uchunguzi wake unaweza kuchukua majuma kadhaa, ofisi ya mchunguzi wa vifo vya Los Angeles ilieleza.