
"Wanawake wote wanapenda kulia bila sababu za msingi," ndicho baba yake alichoweza kusema.
Kijana huyo mdogo alikua akawa mtu mzima, na bado akawa anashangaa kwa nini wanawake huwa wanalia. Mwisho, Akaamua kumuuliza Mungu. "Mungu, kwa nini wanawake huangua kilio kwa urahisi?"

"Wakati namuumba mwanamke nilitaka awe ni wakipekee, maalum.
Nilitengeneza mabega yake kuwa na nguvu ya kutosha kubeba uzito wa dunia, lakini mpole kutosha kutoa faraja.Nilimpa nguvu ambayo inamuwezesha kuendelea wakati kila mtu mwingine anapokata tamaa, na uwezo wa kuitunza familia yake hata kama akikutana na kikwazo cha ugonjwa na uchovu bila kulalamika.



Nikampa hekima ya kujua kwamba mume mzuri kamwe hawezi kutambua machungu ya mke wake, lakini wakati mwingine ni vipimo vya nguvu yake na imani yake vitamwezeshe kutatua na kuendelea kusimama karibu naye.

"Nahizo ndizo zababu zenyewe mwanangu," alisema Mungu, "uzuri wa mwanamke si katika nguo alizovaa, ama haiba aliyoibeba, au jinsi anavyo tengeneza nywele zake.
Uzuri wa mwanamke ni upo katika macho yake, kwa sababu ni mlango wa moyo wake -. Mahali ambapo upendo anaishi "
Iende kwa wanawake wote ambao hawachoki kupambana na hali zote zinazojitokeza katika maisha yao.Usiogope kulia pale inapobidi liaaaaaa dada baada ya hapo endelea kusimama!
source Dina marios