Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

KWA NINI MWANAMKE HULIA?




Kijana mdogo alimuuliza mama yake, "Kwa nini unalia?" mama yake alimjibu "Kwa sababu mimi ni mwanamke,". kijana kwa mshangao akamwambia mama yake "Sielewi,". Mama yake akamkumbatia akamwambia, "Na kamwe, hautaweza kuelewa."
"Wanawake wote wanapenda kulia bila sababu za msingi," ndicho baba yake alichoweza kusema.
Kijana huyo mdogo alikua akawa mtu mzima, na bado akawa anashangaa kwa nini wanawake huwa wanalia. Mwisho, Akaamua kumuuliza Mungu. "Mungu, kwa nini wanawake huangua kilio kwa urahisi?" 


Mungu akasema:
"Wakati namuumba mwanamke nilitaka awe ni wakipekee, maalum.
Nilitengeneza mabega yake kuwa na nguvu ya kutosha kubeba uzito wa dunia, lakini mpole kutosha kutoa faraja.Nilimpa nguvu ambayo inamuwezesha kuendelea wakati kila mtu mwingine anapokata tamaa, na uwezo wa kuitunza familia yake hata kama akikutana na kikwazo cha ugonjwa na uchovu bila kulalamika. 

Nikampa nguvu ya kuvumilia kuzaa na uvumilivu wa kuudhiwa mara kwa mara na watoto wake. 
Nikampa usikivu na upendo kwa watoto wake chini ya yoyote na hali zote, hata wakati mtoto wake ana maudhi kwake vibaya sana. 

Nikampa nguvu na uvumilivu wa kubeba karaha ya mume wake na roho ya kusamehe makosa yake na kuwa kinga ya ubavu wake wa kulinda moyo wake.
Nikampa hekima ya kujua kwamba mume mzuri kamwe hawezi kutambua machungu ya mke wake, lakini wakati mwingine ni vipimo vya nguvu yake na imani yake vitamwezeshe kutatua na kuendelea kusimama karibu naye. 


Na hatimaye, nikampa uwezo wa kumwaga machozi. Hii ni ya kipekee kutumika wakati inahitajika. "
"Nahizo ndizo zababu zenyewe mwanangu," alisema Mungu, "uzuri wa mwanamke si katika nguo alizovaa, ama haiba aliyoibeba, au jinsi anavyo tengeneza nywele zake.
Uzuri wa mwanamke ni upo katika macho yake, kwa sababu ni mlango wa moyo wake -. Mahali ambapo upendo anaishi "


Iende kwa wanawake wote ambao hawachoki kupambana na hali zote zinazojitokeza katika maisha yao.Usiogope kulia pale inapobidi liaaaaaa dada baada ya hapo endelea kusimama!


source Dina marios

[ Read More ]