Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

SIMU ZA VIGANJANI ZANYE TELEVISHENI KUATHIRIWA NA UZIMAJI WA MITAMBO YA ANALOJIA LEO



BAADHI ya watumiaji wa simu za viganjani zenye televisheni ni miongoni mwa watu watakaoathirika na uzimaji wa mitambo ya utangazaji wa televisheni ya mfumo wa analojia.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasialiano nchini  (TCRA), akitoa taarifa kuhusu uzimaji wa mitambo hiyo ya analoji kwenda dijitali, kwa mkoa wa Dar es Salaam, Injinia Endrew Kisaka alisema hali hiyo inatokana na simu hizo kuunganishwa na mfumo huo.
Alisema  simu hizo zitakosa huduma hiyo ya matangazo hadi pale kampuni hizo za simu kwa shirikiana  na malaka hiyo kuzindua mfumo utakaokwenda sambamba na dijitali hivi karibuni.
Injinia Kisaka, alisema uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika haraka ili kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza kwa watumiaji wa simu hizo.
Akifafanua zaidi kuhusu changamoto kuhusu ving’amuzi, alisema endapo utatokea usumbufu wananchi wasisite kurudi sehemu waliko nunua king’muzi hicho kwa maelezo zaidi.
“Unajua kuna baadhi ya maeneo kama vile yenye majengo marefu na mabonde ambapo maeneo hayo hukosekana ‘signal’ sasa mkiona hivyo rudini kwa wauzaji wenu wawape ushauri wa kitaalamu utakaosaidia kupata matangazo hayo kwa ubora”alisema Kisaka.
Naye  Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka hiyo, Prof. John Nkoma alisema serikali imejitahidi kuondoa kodi katika kuingiza ving’amuzi ambapo imesaidia kupunguza bei na kuwa sh 39,000 ambayo anaamini kila Mtanzania atamudu kukipata.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekuwa ikitoa elimu kwaumma kwa kiwango  chakuridhisha,hivyo uhamaji hautakuwa na usumbufu kwa watumiaji wa huduma za utangazaji.
 
Pamoja na hayo, alieleza mabadiliko hayo hayatahusu
utangazaji kwa satelaiti, waya (cable) na redio.
NA  FULLSHANGWEBLOG.COM DAR ES SALAAM
[ Read More ]

Rest in Peace.


She was a student, 23 years old, Her fault some people say because she boarded the wrong bus, And oh yeah
SHE WAS A GIRL, Six men raped her one by one and then used an iron rod to tear her vagina-Small intestine and large intestine came out They left her to die on the road Naked! Wounded! Exposed! Devastated What’s more is that no one even turned to look at her No one even bothered to throw a shawl on the ill-clad ill-fated girl
She can never live a normal, married life again She Went into coma five times since 16th December She was unconscious Critical and hasn't been able to stop crying But don’t worry She wasn't your sister She wasn't your daughter But she could be. The brutality has to stop right here guys These people deserve capital punishment for
their cruel, Perverted act She died yesterday Saturday 29th December 2012 Rest in Peace♥ and I pray that her killers get the WORST punishment possible This doesn't only happen in India. But in every country around the
world, Is this how we treat our women? It Makes me ashamed to even live on this planet today.May your Soul Rest in Peace. Amin.
[ Read More ]

Mwili wa mhanga wa ubakaji wachomwa


A girl lights candles during a candlelight vigil for a gang rape victim who was assaulted in New Delhi, in Kolkata December 29, 2012. A woman whose gang rape provoked protests and a rare national debate about violence against women in India died from her injuries on Saturday, prompting promises of action from government that has struggled to respond to public outrage. REUTERS/Rupak De Chowdhuri (INDIA - Tags: CIVIL UNREST CRIME LAW TPX IMAGES OF THE DAY)
Mhanga wa ubakaji na mauaji yaliyozusha maombolezo makali pamoja na hasira nchini India amefanyiwa taratibu za mazishi kwa kaida za Kihindi, kwa kuchomwa tukio lililofanyika kwa faragha leo Jumapili30.12.2012).
Tukio hilo lilifanyika saa kadhaa baada ya mwili wa marehemu kurejeshwa nchini humo kutoka Singapore.
Mwanamke huyo ambaye hakutajwa jina lake mwenye umri wa miaka 23, ambaye alisababisha maandamano makubwa nchi nzima tangu aliposhambuliwa kinyama katika basi mjini New Delhi wiki mbili zilizopita, alichomwa moto bila kuwapo watu ambao wangeshuhudia tukio hilo kwa ombi la wazazi wake waliokuwa na fadhaa kubwa.
Undertaker Roland Tay (L) and his crew carry the coffin of an Indian rape victim into a van as they leave a funeral parlour for the airport in Singapore December 29, 2012. A woman whose gang rape sparked protests and a national debate about violence against women in India died of her injuries on Saturday, prompting a security lockdown in New Delhi and an acknowledgement from India's prime minister that social change is needed. REUTERS/Edgar Su (SINGAPORE - Tags: OBITUARY CRIME LAW TPX IMAGES OF THE DAY) // eingestellt von se 
Mwili wa marehemu ukichukuliwa katika jeneza
Taratibu za mazishi
Taratibu hizo za mazishi za kuchoma moto , zilifanyika baada ya ndugu na marafiki kufanya taratibu za mwisho za maombi kwa muda mfupi katika wilaya ya kusini magharibi ya Dwarka mjini Delhi, kwa mujibu wa waombolezaji ambao wamemweleza msichana huyo ambaye alikuwa mwanafunzi wa taaluma ya udaktari kuwa alikuwa mtu anayetambulika na wengi na mwenye kipaji.
"Nimekuja kwa sababu nilikuwa nampenda kwa dhati msichana huyu. Alikuwa mtu mwenye uwezo mkubwa kuliko wasichana wengine wote katika eneo tunakoishi," amesema Meena Rai, ambaye alikuwa rafiki wa karibu na jirani.
Waziri mkuu awataka Wahindi kuwa watulivu
Waziri mkuu Manmohan Singh na Sonia Gandhi, kiongozi wa chama kikuu tawala cha Congress, walikuwa katika uwanja wa ndege mjini New Delhi kuwapa pole wazazi wa msichana huyo wakati mwili wake ulipokuwa ukiwasili nyumbani kwa ndege ya kukodi ikiwa na mwili wa mtoto wao.
India's high commissioner to Singapore T.C.A Raghavan (2ndL) walks along the corridor to speak to journalists at the Mount Elizabeth hospital after the announcement of the death of the Indian gang-rape victim, in Singapore on December 29, 2012. The victim, 23, died Saturday in Singapore after suffering severe organ failure, the hospital treating her said, in a case that sparked widespread street protests over violence against women. AFP PHOTO/ROSLAN RAHMAN (Photo credit should read ROSLAN RAHMAN/AFP/Getty Images)Balozi wa India nchini Singapore T.C.A Raghavan katika hospitali ya Mount Elizabeth
Baada ya matibabu ya awali katika hospitali mjini Delhi , alipelekwa nchini Singapore siku ya Jumatano usiku. Lakini madaktari wameshindwa kuzuwia viungo vyake kadha vilivyoshindwa kufanyakazi na alitangazwa kuwa amefariki katika saa za alfajiri siku ya Jumamosi(29.12.2012).
Kifo chake kilisababisha serikali kuahidi ulinzi bora zaidi kwa wanawake, na tathmini ya kina kwa taifa hilo ambapo matukio ya ubakaji hutokea kila siku na udhalilishaji huo wa kingono hupuuziwa kila mara, kama mchezo wa mzaha tu.
An Indian girl participates in a protest to mourn the death of a gang rape victim, in Bangalore, India , Saturday, Dec. 29, 2012. Shocked Indians on Saturday were mourning the death of the woman who was gang-raped and beaten on a bus in New Delhi nearly two weeks ago in an ordeal that galvanized people to demand greater protection for women from sexual violence. (Foto:Aijaz Rahi/AP/dapd). // eingestellt von se Msichana akishiriki katika maandamano India
Wimbi la maandamano lilizuka nchini India tangu shambulio hilo usiku wa Desemba16 wakati mwanamke huyo alipofanyiwa unyama huo pamoja na kushambuliwa kwa kupigwa kwa chuma, na kusababisha kupata majeraha mabaya tumboni.
Mishumaa yawashwa kumuenzi marehemu
Maelfu ya watu walishiriki katika tukio la kuwasha mishumaa usiku siku ya jumamosi (29.12.2012) baada ya waziri mkuu Singh kuongoza miito ya kuwataka watu kuwa watulivu na kuepusha kurejewa kwa maandamano yaliyokuwa na ghasia.
Indian students and activists carry placards at India Gate during a protest following the gang-rape of a student in New Delhi on December 19, 2012. Indian police December 17 arrested the driver of a bus a day after a student was gang-raped and thrown out of the vehicle, reports said, in an attack that has sparked fresh concern for women's safety in New Delhi. The attack sparked new calls for greater security for women in New Delhi, which registered 568 rapes in 2011 compared with 218 in India's financial capital Mumbai the same year. AFP PHOTO/ SAJJAD HUSSAIN (Photo credit should read SAJJAD HUSSAIN/AFP/Getty Images)Wanafunzi na wanaharakati wakishiriki maandamano nchini India
Msichana huyo alitarajia kuolewa na mpenzi wake ambaye nae alijeruhiwa katika shambulio hilo, amesema hayo Meena Rai , ambaye amekuwa akifanya ununuzi kwa ajili ya maandalizi ya haurusi hiyo na marehemu. Harusi ilikuwa inatarajiwa kufanyika mwezi Februari mwaka ujao.


source:dw
[ Read More ]

Muhanga wa ubakaji India afariki dunia


rape case
Mwili wa mwanamke wa India ambaye amefariki hospitalini nchini Singapore baada ya kubakwa kinyama mjini New Delhi ulitarajiwa kurejeshwa nyumbani siku ya Jumamosi (29 Disemba). Balozi  wa India  nchini  Singapore, T. C. A Raghavan  amewaambia waandishi  habari kwamba mwanamke huyo alifariki kutokana na viungo vyake kushindwa kufanya kazi akiwa anapatiwa matibabu. Endelea…
[ Read More ]

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu Mstaafu wa Hesabu za Serikali afariki Dunia


Waumini wa Dini ya kiislamu wakiwa pamoja kwa ajili ya kumsalia maiti
Vingozi mbali mbali wa serikali waliohudhuria katika sala ya kumsalia maiti

Waumini hao wakiwa kwenye hatuwa ya mwishi ya kumsindikiza ndugu yao katika makaburi ya kisutu
Waumini wa dini ya kiislamu  wakiwa kwenye hatuwa ya mwishi ya kumsindikiza ndugu yao katika makaburi ya kisutu
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu Mstaafu wa Hesabu za Serikali wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa  Tanzania Bwana Mohd Aboud Mohd aliyefariki Dunia Nchini India  amezikwa katika makaburi ya Wangazija yaliyopo Kisutu Mjini Dar es salaam.
Mamia ya waislamu, familia, wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za  Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania walihudhuria mazishi hayo wakati wa jioni.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wake Dr. Mohd Gharib Bilal, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mwenyekiti wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere Dr. Salim Ahmed Salim na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa SMT walikuwa miongoni mwa watu waliohudhuria mazishi hayo.
Marehemu Mohd Aboud Mohd maarufu Mfaransa  alizaliwa Zanzibar Tarehe 25/1/1927 na kupata elimu zake za Dini na Dunia na alipomaliza masomo yake ya sekondari aliajiriwa serikalini mnamo tarehe 1/1/1944.
Marehemu Mohd Mfaransa kwa umahiri wake wa utumishi serikalini alipata fursa ya kupandishwa daraja hadi kufikia kuwa msaidizi Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  hadi mwanzoni mwa mwaka 1967.
Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume alimpendekeza Mzee Mohd Mfaransa  kushika wadhifa wa Msaidizi Mkaguzi Mkuu wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 1/3/1967.
Tarehe 16/10/1967 Marehemu Mohd Mfaransa  aliteuliwa rasmi Mtanzania na Mwafika wa kwanza  baada ya Uhuru wa kuwa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wadhifa aliokuwa nao hadi kustaafu kwake tarehe 25/12/1987.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Matehemu mzee Mohd Aoud Mohd    {Mfaransa }  mahala pema peponi amin.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
30/12/2012
[ Read More ]

Tume ya Uchaguzi yakabidhi ripoti ya miaka mitano ya tume kwa Rais



 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar,Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar,(ZEC) Khatib Mwinyichande,akiongoza ujumbe wa Tume hiyo walipofika Ikulu Mjini Zanzibar,Kumuaga Rais kwa kumaliza muda wa kazi wa Tume hiyo jana
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar,Dk.Ali Mohamed Shein,akipokea Ripoti ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar,(ZEC) kutoka kwa Mwenyekiti wake Khatib Mwinyichande, alipoongoza ujumbe wa Tume hiyo walipofika Ikulu Mjini Zanzibar,Kumuaga Rais kwa kumaliza muda wa kazi wa Tume hiyo jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Na Rajab Mkasaba, Ikulu
 
WAJUMBE wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar wanaomaliza muda wao wa utumishi, leo wamemkabidhi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein Ripoti ya miaka mitano ya Tume ya Uchaguzi katika kipindi cha utumishi wao.
Akikabidhi ripoti hiyo, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mhe. Khatib Mwinyichande alitoa pongezi kwa mashirikiano makubwa iliyoyapata Tume hiyo katika kipindi chote cha utumishi wao ndani ya miaka mitano.
Wajumbe hao ambao wamefika Ikulu mjini Zanzibar kwa ajili ya kukabidhi ripoti hiyo pamoja na kumuaga rasmi Rais baada ya kumaliza muda wao wa kazi, walieleza kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya utumishi wao, Tume ilipata ushirikiano mkubwa kutoka kwa wadau wa uchaguzi kwa kuhakikisha kuwa amani inapatikana katika kipindi cha uchaguzi.
Aidha, Tume hiyo ilieleza kuwa ilipata ushirikiano mkubwa kutoka kwa Taasisi/Mashirika ya uchaguzi ya Kimataifa na Kikanda pamoja na kuweza kuwajengea uwezo wa kielemu watendaji wake kadhaa kwa kujiunga na vyuo mbali mbali vya ndani na nje ya Zanzibar.
Katika maelezo yao wajumbe hao walieleza kuwa katika utekelezaji wa majukumu yake, Tume iliendesha kwa mafanikio makubwa uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 na chaguzi ndogo nne, pamoja na kusimamia na kuendesha Kura ya Maoni ya mwanzo katika historia ya Zanzibar kufuatia maridhiano ya kisiasa ya terehe 5 Novemba mwaka 2009.
Mbali ya majukumu mbali mbali yaliotekelezwa na Tume hiyo katika kipindi cha utumishi wake ilikuwa ni pamoja na kuendeleza mashirikiano na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushauriana juu ya utekelezaji bora wa majukumu ya Tume hizo.
Kwa mujibu wa maelezo ya Mwenyekiti wa Tume hiyo, alieleza kuwa ripoti hiyo waliyomkabidhi Rais inatoa muhtasari wa kazi zote zilizofanywa na Tume katika kipindi cha utumishi wake.
Sambamba na hayo, Tume hiyo inayomaliza muda wake ilieleza imani yake kuwa Ripoti hiyo mbali ya kutoa maelezo juu ya kazi zilizofanywa na Tume katika kipindi hicho, lakini pia, itakuwa ni mwongozo kwa Wajumbe wengine wa Tume watakaoteuliwa kushika nafasi zao.
“Ni matumaini ya Tume hii, kwamba Serikali itayafanyia kazi mapendekezo yalioainishwa katika ripoti hii”,alisema Mwinyichande.
Nae Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein alitoa pongezi kwa Tume hiyo inayomaliza kazi zake kwa kazi nzuri iliyoifanya katika kipindi chake chote cha utumishi.
Dk. Shein alisema kuwa chaguzi zote zilizofanywa chini cha Tume hiyo zimefanywa kwa mafanikio makubwa licha ya kuwepo baadhi ya changamoto ndogo ndogo.
Alisema kuwa Tume hiyo imefanya kazi kubwa na nzuri ambapo yeye mwenyewe binafsi pamoja na wenziwe waliomo Serikalini wanathamini sana juhudi za Tume hiyo ilizozichukua katika utumishi wake wote wa miaka mitano.
Katika maelezo yake Dk. Shein alisema kuwa Tume hiyo imehfanya kazi ya kupongezwa ambayo imewajengea sifa kubwa ndani na nje ya Zanzibar sanjari na kuijengea sifa kubwa Zanzibar.
Aidha, Dk. Shein aliwaeleza Wajumbe wa Tume hiyo kuwa, kutokana na uzoefu wa kazi yao hiyo nzuri watarajie kutoa mchango wao wa uzoefu kwa wale wote watakaohitaji mchango huo.
“Hongereni kwa kazi nzuri mliyoifanya katika kipindi hichi cha miaka mitano cha utumishi wenu katika Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, kwani kazi yenyewe ni ngumu na hasa joto huzidi wakati wa uchaguzi unapofika”alisisitiza Dk. Shein.
Pamoja na hayo, Dk. Shein alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwathamini Wajumbe hao huku akiwapongeza kwa juhudi zao za kuwawezesha kielimu watendaji wa tume hiyo kwa elimu ya juu ikiwa ni pamoja na Shahada ya Kwanza,Uzamili na nyenginezo.
Kwa maelezo ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mhe. Khatib Mwinyichande kwa Dk. Shein, Tume hiyo inamaliza siku tatu kuanzia leo kwani Wajumbe hao waliteuliwa tarehe 02/01/2008 na kufanya kazi kwa kipindi cha miaka mitano na utumishi wao unamaliza tarehe 01/01/2013
Wajumbe hao wanaomaliza muda wao, waliteuliwa na Rais Mstaafu wa awamu ya sita Mhe. Dk. Amani Abeid Karume.
[ Read More ]

MAKACHERO KUTOKA DAR WATUA ZANZIBAR KUCHUNGUZA SHAMBULIO LA PAROKO


Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi Zanzibar

Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dar es Salaam, imetuma timu ya Makachero kuja Zanzibar kuungana na wenzao wengine wa Polisi Zanzibar katika Upelelezi wa tukio la kushambuliwa kwa Paroko wa Parokia ya Mpendae Amrose Nkenda.

Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa makosa ya Jinai Zanzibar ACP Yusuf Ilembo, amesema kuwa timu hiyo ambayo inaongozwa na Afisa mmoja wa ngazi ya juu (hakumtaja jina) ina jumla ya Makachero watano waliobobea katika masuala ya upelelezi hapa nchini.

Amesema kuwa nia ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Saidi Mwema, kuituma timu hiyo kuja hapa Zanzibar, ni kutaka kuengeza nguvu katika tukio hili ambalo linatazamwa kwa aina tofauti hasa ikizingatiwa kuwa aliyeshambuliwa ni Kiongozi mkubwa wa dini na limetokea katika kipindi cha siku kuu ya Krismas.

Amesema Jeshi la Polisi limeamua tukio hili kupelelezwa kwa pamoja kati ya wenzao wa makao makuu ya Polisi Dar es salaam na wa hapa Zanzibar ili kuhakikisha kuwa wale wote waliohusika katika kumshambulia Paroko huyo wanakamatwa.

Hata hivyo kamanda Ilembo amesema kuwabado Polisi wanaendelea na Upelelezi wa kubaini sababu za kushambuliwa kwa Paroko huyo bila ya kuibwa kwa kitu chochote kutoka kwa mshambuliwa.

Amesema kuna uwezekana kuwa watuhumiwa wameshindwa kuchukua kitu chochote baada ya kubaini kuwa eneo la tukio lisingekuwa salama kwao kwa vile kulikuwa na walinzi na ni eneo ambalo ni karibu kabisa na makazi ya viongozi wengine wa dhehebu hilo.

Akizungumzia siku kuu ya mwisho wa mwaka 2012 na mwanzoni mwa mwaka 2013, Kamanda Ilembo amewahimiza wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa pale wanapobaini kuwepo kwa wahalifu ili wachukuliwe hatua.

Naye Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar ACP Aziz Juma Mohammed, amewatahadharisha wazazi na walezi kutowaruhusu watoto wadogo kuranda barabarani ama kwenda katika fukwe za bahari kuogelea pasipo uangalizi wa watu wazima.

Kamanda Aziz amesema kuwa uzoefu unaonyesha kuwa watoto wengi wamekuwa wakigongwa na magari ama kuzama na kufa maji katika siku hizi za siku kuu za mwisho wa mwaka kwa kukosa uwangalizi wa watu wazima.

Aidha amewataka wananchi kutoziacha nyumba zao wazi ama bila ya kuwa na uwangalizi wa kutosha ili kutowapa nafasi kwa wahalifu kupata fursa ya kuwaiba.
[ Read More ]

Chuo Kikuu Cha Taifa Cha Zanzibar SUZA chamtunukia Muheshimiwa Haroun Ali Suleiman Cheti cha Shukurani


Bwana Hassan Simba Hassan SUZA Public Relation Officer.

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo -Taaluma Dr. Haji Mwevura akimkabidhi WAZIRI wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Muheshimiwa Haroun Ali Suleiman  cheti maalumu cha shukurani kwa mchango wake mkubwa alioutoa wakati alipokua waziri wa elimu .

WAZIRI wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Muheshimiwa Haroun Ali Suleiman.
                  Naibu Makamu Mkuu wa Chuo -Taaluma Dr. Haji Mwevura 



WAZIRI wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Muheshimiwa Haroun Ali Suleiman akimshukuru
                  Naibu Makamu Mkuu wa Chuo -Taaluma Dr. Haji Mwevura 



                  




Kutoka kushoto ni    Naibu Makamu Mkuu wa Chuo -Taaluma Dr. Haji Mwevura, Bwana Hassan Simba Hassan  SUZA Public Relation Officer, Waziri wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Muheshimiwa Haroun Ali Suleiman
               





[ Read More ]

MAKAMU WA RAIS DKT GHARIB BILAL AFUNGUA RASMI KITUO CHA POLISI CHA KIBOJE ZANZIBAR JANA


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Kamishina wa Polisi wa Zanzibar, Mussa Ali Mussa, wakifunua kwa pamoja kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Kituo cha Polisi cha Kiboje, baada ya kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho ulioanza Februari 14, 2012 na kuzinduliwa jana Desemba 26, wakati wa hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika Kiboje Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe  kuashiria ufunguzi rasmi wa Kituo cha Polisi cha Kiboje, baada ya kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho ulioanza Februari 14, 2012 na kuzinduliwa jana Desemba 26, 2012, wakati wa hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika Kiboje Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaliminana na maofisa wa Usalama wa Wilaya ya Kati, wakati alipowasili eneo hilo kwa ajili ya kufungua rasmi Kituo cha Polisi cha Kiboje, kilichpo Mkoa wa Kusini Unguja jana.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Cheti, Saleh Ahmed Said, kutoka Migoz Supermarket, ambaye ni mmoja kati ya watu waliochangia ujenzi  wa Kituo hicho cha Polisi cha Kiboje, wakati wa hafla za ufunguzi wa kituo hicho zilizofanyika jana Desemba 26, 2012 Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Kamishina wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, wakati akitembelea kukagua jengo la Kituo cha Polisi cha Kiboje, baada ya kufungua rasmi jengo hilo lililoanza kujengwa Februari 14, 2012 na kuzinduliwa jana Desemba 26, 2012, wakati wa hafla ya ufunguzi huo iliyofanyika Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Kamishina wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa, wakati akitembelea kukagua jengo la Kituo cha Polisi cha Kiboje, katika Chumba cha Mawasiliano baada ya kufungua rasmi jengo hilo lililoanza kujengwa Februari 14, 2012 na kuzinduliwa jana Desemba 26, 2012, wakati wa hafla ya ufunguzi huo iliyofanyika Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Kamishina wa Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa (kulia) wakati akitembelea kukagua jengo la Kituo cha Polisi cha Kiboje katika Chumba cha Ofisi ya Polisi Jamii, baada ya kufungua rasmi jengo hilo lililoanza kujengwa Februari 14, 2012 na kuzinduliwa jana Desemba 26, 2012, wakati wa hafla ya ufunguzi huo iliyofanyika Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja.
Kikundi cha ngoma cha Tukulanga kikitoa burudani wakati wa hafla hiyo.

 Kikundi cha Sanaa cha Polisi kikitoa burudani ya maigizo.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)
[ Read More ]

Letters to my Children by Benn Haidari


When Benn Haidari was separated from his children by domestic turbulence and physical distance, he refused to become just another absent father. With only the simplest medium and purest will, he set out to maintain contact the only way he knew how: a series of letters to his children. In them, he carefully identifies the lessons he thinks they ought to learn about life and, through these ideas, teaches them about himself. Rich in its detailing of life's peculiarities, passionate about simple pleasures and compelling in its poignancy, Letters to my Children serves as a reminder of the love and hope to be found in every day and every envelope.

get your copy now http://www.amazon.com/dp/B00846Y4PE/ref=tsm_1_fb_lk


[ Read More ]

Father Ambros Mkenda wa Kanisa la Katoliki la Mpendae amepigwa risasi



Photo: Father Ambros Mkenda wa Kanisa la Katoliki la Mpendae amepigwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake majira ya saa 12 jioni leo wakati akitokea kanisani. Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Azizi Juma amethibisha kutokea kwa tukio hilo na amesema hakuna mtu anayeshikiliwa kuhusika na tukio hilo lakini uchunguzi unaendelea. Father Mkenda hivi sasa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Mnazi Mmoja, ambapo Askofu wa Anglikan Michael Hafidh amesema bado ni mapema mno kuelezea kama ataendelea kuwepo hospitalini hapo au atasafirishwa huku akilaani vitendo ambavyo hivi vinavyoendelea vya kuwahujumu viongozi wa dini.
Father Ambros Mkenda wa Kanisa la Katoliki la Mpendae amepigwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake majira ya saa 12 jioni jana wakati akitokea kanisani. Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Azizi Juma amethibisha kutokea kwa tukio hilo na amesema hakuna mtu anayeshikiliwa kuhusika na tukio hilo lakini uchunguzi unaendelea. Father Mkenda hivi sasa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Mnazi Mmoja, ambapo Askofu wa Anglikan Michael Hafidh amesema bado ni mapema mno kuelezea kama ataendelea kuwepo hospitalini hapo au atasafirishwa huku akilaani vitendo ambavyo hivi vinavyoendelea vya kuwahujumu viongozi wa dini.

[ Read More ]

Oman kuendeleza mashirikiano na Zanzibar



  Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiagana na balozi mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Sheikh Mansoor Al-Busaid baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika ofisini kwake Migombani.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na Balozi mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Sheikh Mansoor Al-Busaid ofisini kwake Migombani.
 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akimshindikiza balozi mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Sheikh Mansoor Al-Busaid baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika ofisini kwake Migombani
(Picha na Salmin Said, OMKR)

Na Hassan Hamad OMKR
 
Oman imeahidi kuendeleza mashirikiano yake na Zanzibar katika sekta mbali mbali zikiwemo elimu, habari, utunzaji wa kumbukumbu na majengo ya asili.
 
Balozi mdogo wa Oman aliyepo Zanzibar Sheikh Mansoor Al-Busaid ameeleza hayo wakati akizungumza na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad ofisini kwake Migombani.
 
Balozi Al-Busaid ambaye alionana na Makamu wa Kwanza wa Rais kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa utumishi hapa nchini, amesema mashirikiano hayo yataendelezwa kwa maslahi ya pande zote mbili.

“Hivi sasa waandishi wawili wa gazeti la Zanzibar Leo wako nchini Oman, tumewapeleka kwa ajili ya kuripoti uchaguzi wa mabaraza ya miji ‘municipality election’ na pia tunatarajia kuchukua waandishi wengine wawili wa magazeti kwenda Oman”,alieleza balozi Al-Busaid.
 
Ameishukuru Serikali pamoja na wananchi wa Zanzibar kwa kumpa ushirikiano mzuri katika kipindi chote cha utumishi wake, na kuahidi kuwa balozi mzuri wa kuzidi kuitangaza Zanzibar nje ya nchi.
 
Amefahamisha kuwa Zanzibar ni nchi ya amani na pahala pazuri pa kuwekeza, na kuelezea umuhimu wa kuwaalika wawekezaji wengi zaidi kuja kuwekeza.
 
Nae Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad ameishukuru Serikali ya Oman kutokana na misaada yake kwa Zanzibar ambayo inasaidia harakati za serikali za kukuza uchumi
wake.
 
Ameelezea kufarajika kwake kutokana na uamuzi wa Sultan Qaboos wa Oman kuanzisha Mfuko wa Elimu Zanzibar ambao utawasaidia wanataaluma wa Zanzibar kukuza ujuzi wao na kuinua kiwango cha elimu nchini.
 
“Nimepata moyo sana kwa Sultan Qaboos kuanzisha mfuko wa elimu Zanzibar ambao naamini utawasaidia sana wanataaluma wetu, na hii inathibitisha kuwa Sultan Qaboos anaipenda na kuithamini sana Zanzibar”, alifahamisha Maalim Seif.
 
Maeneo mengine ambayo Oman iko mstari wa mbele katika kushirikiana na Zanzibar ni pamoja na masuala ya utamaduni, afya na utunzaji wa kumbukumbu.
 
Kwa mujibu wa maelezo ya viongozi hao tayari Sultan Qaboos amekialika kikundi cha taarab cha wanawake cha Zanzibar kwenda nchini Oman kwa ajili ya kuonyesha umahiri wao wa kuimba na kucharaza ala za muziki wa Taarab.
 
Wamefahamisha kuwa Oman na Zanzibar zina uhusiano wa muda mrefu wa kindugu, na kwamba hata tamaduni zake zinashabihiyana kwa kiasi kikubwa.
[ Read More ]

Nafasi ya Masomo/kusomesha Marekani


Opportunity in Swahili at The University of Mississippi

The Department of Modern Languages has funding to support someone to do a 2-year master's degree in Modern Languages with a specialization in Teaching English as a Second Language (TESL), Spanish, French or German while teaching two basic Swahili courses each semester for two years. We can offer a stipend of $5,250 per semester ($10,500 per year), which will be split between the Departments of Modern Languages and African-American Studies. This assistantship will waive both resident and non-resident tuition and will be offered for four semesters with successful academic progression toward the master’s degree. We anticipate courses with about ten students in them per semester in both Swahili 1 and 2.
This is a great opportunity to do a master's degree at UM and to get additional teaching experience in Swahili, while being completely funded to do so. For more information, please contact Dr. Donald L. Dyer, Chair, Department of Modern Languages, The University of Mississippi, University, MS 38677 [mldyer@olemiss.edu].
Dr. Donald L. Dyer
Chair of Modern Languages
Professor of Russian and Linguistics
Co-Director of the UM Chinese Language Flagship Program
The University of Mississippi
University, MS 38677
Editor of Balkanistica
Editor of Romance Monographs
[ Read More ]