Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

UN yalaani hatua ya Korea Kaskazini

-
Rehema Mwinyi.


Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya kukutana kwa dharura, hatimaye limeshutumu vikali hatua ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la kinyuklia.

Baraza hilo lilikutana kwa dharura saa chache tu baada ya jaribio hilo kufanywa na limeonya hatua kali zitachukuliwa dhidi ya Korea Kaskazini.

Kauli ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa imetolewa muda mfupi tu baada ya serikali ya Korea Kaskazini kutangaza imefanya jaribio lililofanikiwa la Kombora la nyuklia lililo kubwa zaidi ya lile iliyolipua mnamo mwaka wa 2006.

Mataifa wanachama sasa wanataka hatua kali zichukuliwe dhidi ya Korea Kaskazini ambayo tayari iko chini ya vikwazo vya baraza hilo la usalama la Umoja wa Mataifa. Lakini serikali ya Korea Kaskazini imepuuza kauli hiyo na kusema iko tayari kukabiliana vilivyo na wapinzani wake wote.

Wataalamu wa makombora wa Urusi wanasema kombora lililolipuliwa lina uwezo sawa na yale yaliyoangushwa na Marekani katika miji ya Hiroshima na Nagasaki nchini Japan wakati wa vita vya pili vya dunia.

Hata China ambayo imekuwa ikiunga mkono Korea Kaskazini chinichini sasa imesema itakubaliana na azimio lolote la Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa.

Ili kuelewa wasiwasi huu ambao umekumba jamii ya kimataifa ni muhimu kuelewa uwezo wa zana za Kinyuklia.

Kulingana na shirika moja la utaalamu wa kivita la Marekani, Center for Defense Information, makombora matano au sita ya aina iliyofanyiwa majaribio siku ya Jumatatu, yakilipuliwa mara moja yana uwezo wa kuharibifu duniani kote na kuwaacha manusura wachache sana.

Ikiwa na silaha kama hizi, si ajabu Korea kaskazini sasa imeionya Marekani itakabiliana nayo kivita iwapo serikali ya Rais Obama itajaribu kuishambulia

Leave a Reply