Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Aliyemzushia Mumewe Amembaka Atupwa Jela

-
Rehema Mwinyi.

Mwanamke mmoja wa nchini Uingereza ambaye alimshtaki mumewe akidai mumewe amembaka ili aweze kuvunja uhusiano wao na kisha ajirushe na mwanaume mwingine amehukumiwa kwenda jela miezi minne.
Michaela Lodge, alifanya mapenzi na mumewe Martin katika nyumba waliyokuwa wakikaa pamoja mwezi novemba mwaka jana halafu baadae aliwapigia simu polisi akidai mumewe amemshambulia na amembaka.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la Uingereza, polisi walimhoji mwanamke huyo kwa masaa 62 wakati mumewe alitupwa selo kwa masaa 12 na baadae kuachiwa kwa dhamana baada ya kusisitiza kuwa alifanya mapenzi na mkewe kwa hiari yake bila kumlazimisha.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 45 na mkazi wa mji wa Essex alitengeneza barua ya ushahidi miezi miwili baadae akisisitiza kuwa amebakwa na mumewe lakini hataki mumewe ashtakiwe.

Mwezi februari mwaka huu mwanamke huyo alimwandikia barua mumewe akikiri kuwa aliongopa madai ya kubaka.

"Siwezi kuendelea na kesi hii tena, wakati tulipopanda kitandani sote tulikuwa na hamu ya kufanya mapenzi, niliwaongopea polisi kuwa umenibaka" ilisema barua hiyo.

Bwana Lodge aliwaonyesha polisi barua hiyo ya mkewe na haukupita muda polisi walimkamata mkewe.

Akitoa hukumu, jaji Rodger Hayward Smith alisema "Yalikuwa ni madai ya kutisha uliyokuwa umeyapangilia mapema ili kumtoa maishani mwako".

Michaela, mama wa watoto watatu alihukumiwa jana kwenda jela miezi minne pamoja na maombi ya mumewe kuwa asamehewe adhabu ya kifungo jela.

source:nifahamishe.com

Leave a Reply