Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

MISS PROGRESS INTERNATIONAL ATEMBELEA WALEMAVU WA NGOZI SHINYANGA LEO

-
Rehema Mwinyi.


Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solutions, Peter Mwendapole akiwa na watoto wa wenye ulemavu wa ngozi wanaosoma na kulelewa katika shule ya Buhangija mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solutions Bw. Peter Mwendapole na Miss Progress International Julieth William Lugemba na wenyeji wao wenye ulemavu wa ngozi wanaosoma na kulelewa katika shule ya Buhangija mkoani Shinyanga.
Miss Progress International, Julieth William Lugembe akiwa na watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Buhangija kilichopo mkoani Shinyanga wakati alipofanya ziara mkoani humu kuangalia matatizo mbalimbali yanayowakabili albino.

MSHINDI wa dunia taji la Miss Progress International Julieth William, leo ametembelea watu wenye ulemavu wa ngozi Mkoani Shinyanga.
Julieth alitembelea watu hao na watoto wenye ulemavu huo wa ngozi kwa lengo la kutaka kufahamu mahitaji yao kabla ya kuweza kuwasaidia.
Ziara hiyo iliyoandaliwa na kampuni ya One Touch Solutions inayoandaa shindano la Miss Progress Tanzania ilimedhaminiwa na Precision Air na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel
Mlimbwende huyo aliyetwaa taji hilo mwaka jana nchini Italia alianza kwa kutembelea shule ya Buhangija, ambayo inatunza watoto wenye ulemavu huo.
Akiwa katika shule hiyo alipata fursa ya kutanzama mazingira ya shule hiyo pamoja na kuzungumza na watoto hao kwa muda wa dakika 30.
Katika moja ya mahitaji waliyotaka watoto hao ni kumaliziwa kwa moja ya bweni lao ambalo halijamalizika ili kuweza kupata nafasi nzuri ya kulala kutokana na lile wanalotumia kuwa dogo, jambo linalowafanya walale kitanda kimoja watu watatu.
Baadaye alitembelea ofisi za mkoa za Chama cha Maalbino (TAS) na kuweza kuzungumza na watu wazima ili nao kutaja mahitaji yao.
Katika kikao hicho watu hao wenye ulemavu walitaja mahitaji yao ikiwaa ni pamoja na kutaka kupewa elimu ya ujasiliamali ili waweze kuendesha maisha yao na kuondokana na utegemezi.
Pia alikutana na Ofisa Elimu wa mkoa wa Shinyanga, Eva Lopa, Ofisa Ustawi wa Jamii, Jesca Kagunila. Leo Julieth atakuwa mkoani Mwanza kabla kuelekea Arusha.

Leave a Reply