Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

BREAKING NEWS:Inna lillahi wa inna ilaihi raji'un...

-
Rehema Mwinyi.



Habari tulizozipata sasa hivi kuwa bwana Shabani Hilika Ametutoka, Inalilah.
Mnikulu Zanzibar afariki dunia
MNIKULU katika Ikulu ya Zanzibar, Shaaban Ahmada Hilika, amefariki dunia leo katika hospitali ya Mnazimmoja alikokuwa amelazwa kwa matibabu.
Hilika anatarajiwa kuzikwa kesho katika kijiji cha Mfenesini  baada ya Sala ya Adhuhuri, na mwili wa marehemu utaondokea Amani  nyumbani kwao, baada ya kuagwa na kusaliwa..
Hilika amekuwa Mnikulu katika Ikulu ya Zanzibar tokea uongozi wa Aawamu ya Sita ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya Dk.Amani Abeid Karume na kuteuliwa tena kushika nafasi hiyo na Rais wa Awamu ya Saba wa Zanzibar, Dk.Ali Mohamed Shein.
Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu, Amin.

One Response so far.

  1. Anonymous says:

    Ameen, inna lillah wainna ilayh rajiun.

Leave a Reply