Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Mwili wa Marehemu Haji Mohammed wapokelewa kwa Simanzi Zanzibar na Wapenzi wake na Wananchi katika Bandari ya Zanzibar.

-
Rehema Mwinyi.



Marehemu Haji Mohammed Kirembwe cha Siti Bint Saad, wakati wa uhai wake akiimba na kikundi cha gusagusa .

 Mtoto wa Kwanza wa Marehemu Haji Mohammed, akishindikizwa na nduga na jamaa waliofika katika bandari ya Zanzibar kupokea mwili huo leo jioni ukitokea Jijini  Dar-es- Salaam, 
Marehemu Haji Mohammed anatarajiwa kuzikwa kesho saa 4.00 asubuhi na sala ya maiti itafanyika Mskiti Nambari Muembetanga. 

Marehemu alikuwa Msanii kwa muda mrefu na Kikundi chake cha kwanza kujiunga kilikuwa Kikundi cha Taraab cha Malindi, akiwa ni mpiga kinanda na mtunzi na muimbaji katika kikundi hicho.Na hatimae kuanzisha kikundi  kilichojulikana kwa Jina la  East African Melody.

Akiwa Mkurugenzi wa Kikundi hicho na alikihamishia makazi ya Kikundi hicho katika Jiji la Dar-es-Salaam na kutoa burudani kwa Wapenzi wao.
Pia alianzisha Kikundi cha Gusagusa ambacho kilikuwa kikipiga nyimbo za zamani katika ukumbi wa DDC Kariakoo siku za week end hutowa burudani hiyo.
 Wananchi wakipokea jeneza la Marehemu Haji Mohammed katika bandari ya Zanzibar leo jioni.

Leave a Reply