habari na dina marios
zawadi ya ua Mwanamitindo,
Jamila Swai ambaye ni mmoja kati ya
waliofanikisha shughuli hiyo
waliofanikisha shughuli hiyo
usiku huu katika hoteli ya Double Tree Hilton,
Masaki jijini Dar.
MC Taji Liundi akiwajibika.
















Mwanamitindo Jamila Swai akipita jukwaani.
wadau.
Ankal akiwa amejiachia na wadau waliohudhuria hafla hiyo pamoja
Masaki jijini Dar.




















na wanamitindo.
Wadau wa Vodacom pia walikuwepo.


Biashara ikiendelea mara baada ya show kumalizika.


Wageni waalikwa toka sehemu mbali mbali
walijitokeza kuona Style Motomoto








walijitokeza kuona Style Motomoto
Fashion Show usiku huu ndani ya hoteli ya Double Tree Hilton,
Masaki jiji Dar.
Masaki jiji Dar.

Mtoto Deus Juma(7)akiwa wadi namba moja katika Hospitali ya Wilaya ya Geita akiuguza majeraha kwenye mikono yake baada ya kuchomwa moto na mama yake mzazi.Picha na David Azaria
----
POLISI wilayani Geita katika mkoa wa Mwanza wamemkamata mwanamke kwa tuhuma za kumuunguza mwanawe kwa maji ya moto mikono yote miwili na kisha kumfungia ndani kwa siku tatu. Mary Dominick anadaiwa kufanya kitendo hicho wiki iliyopita nyumbani kwake katika Mtaa wa Msalala, mjini Geita baada ya kumtuhumu mtoto huyo kuiba Sh 6,000 zilizokuwa ndani ya nyumba. Mtoto huyo, Deus Juma (7) anayesoma darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Kivukoni amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Geita. Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk Abdallah Dihenga alisema walimpokea mtoto huyo juzi akiwa na majeraha mikononi. Akiwa katika wodi namba moja hospitalini hapo chini ya uangalizi wa majirani waliodai ni wanakikundi cha kusaidiana ambacho mama yake ni mwanachama, mtoto huyo alisema siku ya tukio baada ya mama yake kurejea nyumbani akitokea kwenye shughuli zake, alimuita na kuanza kumpiga huku akimtuhumu kuiba fedha licha ya yeye kujitetea. Juma ambaye alikuwa akijieleza huku akilia, alisema, “pamoja na kujitetea kwa muda mrefu lakini mama hakunielewa hata kidogo na kuendelea kuning’ang’aniza kwamba mimi ndiye mwizi niliyemuibia fedha zake,” alisema na kuongeza: “Aliniingiza ndani na kisha kunifunga mikono yote miwili pamoja na miguu kwa mpira wa kufungia mizigo kwenye baiskeli na kuanza kunipiga” . Alidai baada ya kipigo hicho, mama yake hakumfungulia mpira aliokuwa amemfunga miguuni na mikononi hali iliyomlazimu kulala sakafuni kwa siku tatu kabla ya kufunguliwa na kukutwa mikono imevimba.Kwa mujibu wa mtoto huyo, mama yake alipokuta mikono imevimba alichemsha maji ya moto na kumkanda na alipoona uvimbe haupungui, aliamua kuchukua barafu na kumuwekea kwenye mikono. Inaelezwa kwamba jana asubuhi ndipo mtoto huyo alifunguliwa na baada ya kutoka nje, alikimbilia barabarani alipokutana na wasamaria wakampeleka kwa Mwenyekiti wa Kitongoji, Sosthenes Mahushi.Kiongozi huyo wa kitongoji alithibitisha kumpokea mtoto huyo na kisha kumpeleka polisi kabla ya kumfikisha hospitalini hapo. Mtoto huyo alishuhudiwa akiwa na majeraha usoni na kichwani anayodai yalitokana na kupigwa na kipande cha ubao.Vile vile mikono imevimba huku akiwa na vidonda vikubwa katika viganja kiasi cha kushindwa kukunja vidole. Polisi wilayani hapa imethibitisha tukio hilo na kusema mwanamke huyo anashikiliwa na kwamba atafikishwa mahakamani wakati wowote uchunguzi utakapokamilika.Wakati huohuo, wanawake waliokutwa hospitalini hapo wakimhudumia mtoto huyo hawakuwa tayari kuzungumza na kuandikwa majina yao gazetini. Pia hapakuwa na ndugu wala jamaa waliopatikana mara moja kuzungumzia undani wa maisha ya mtoto huyo. Mama yake pia hakupatikana kuthibitisha tuhuma kutokana na kushikiliwa na polisi.

From Kitchen Cabinet Cures
That innocent-looking can of soda pop-no matter what it’s sweetened with-may be taking a toll on your immunity. Here’s why:
1. People who drink sodas instead of healthy beverages (think low-fat milk and pure fruit juice) are less likely to get adequate vitamin A, calcium, and magnesium. What’s more, soda contains phosphoric acid that depletes calcium and magnesium. These two nutrients help keep your immunity operating at peak efficiency.
2. Sodas containing high-fructose corn syrup also contain high levels of free radicals linked to tissue damage, the development of diabetes, and diabetic complications.
3. Plastic soda (and water) bottles contain a toxic chemical called bisphenol A (BPA) that can leach from bottles into soda…into you. Emerging evidence links BPA to a myriad of maladies, including immune system depression. Public health experts recommend that we protect children from exposure to products containing BPA-especially those they consume or use every day.
4. Diet soda actually contributes to weight gain. A study of 1,550 people concluded that people who drink diet soda have a 41 percent increased risk of being overweight or obese-for every can or bottle they drink per day! Turns out, any sweet taste signals body cells to store fat and carbohydrates, which makes you hungrier. Sweet tastes also promote insulin release, which blocks your body’s ability to burn fat. The hard truth: No published study has ever proven that drinking diet soda will help you lose weight.
Study: Diet Soda May Increase the Risk of Stroke.
WATU kutoka zaidi ya familia 10 katika Shehia ya Mikunguni, wamekumbwa na maradhi ya kuharisha baada ya kutumia maji yasiyo salama yanayosadikiwa kuchanganyika na kinyesi cha binadamu.
Tatizo hilo limewakumba zaidi watoto baada ya kutumia maji hayo yaliyokuwa na ladha ya uchungu pamoja na rangi ya udongo.
Katika taarifa yake kwa Zanzibar Leo, Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), imesema hali hiyo imesababishwa na mwananchi mmoja katika eneo hilo kujenga shimo la karo na kusababisha kinyesi kuchanganyika na maji safi baada ya bomba la maji la chini ya ardhi kupasuka kwa kemikali za kinyesi.
Afisa Uhusiano wa ZAWA, Zahor Suleiman alisema katika kukabiliana na tatizo hilo, Mamlaka lichukua hatua ya kufunga laini ya maji katika eneo hilo na kubadilisha mfumo mzima wa usambazaji maji ili yasipite kwenye karo hilo.
Mabadiliko hayo, yamesababisha wananchi wa shehia hiyo kukosa huduma za maji na kusababisha usumbufu mkubwa, hata hivyo hatua hiyo imechukuliwa ili kunusuru maisha ya wananchi na kuhakikisha wanapata huduma ya maji safi na salama kwa wote.
Shehia ya Mikunguni kwa muda mrefu imekuwa ikikosa huduma za maji safi kutokana na uchakavu wa miundombinu, lakini wakati ZAWA ikiweka laini mpya baada ya siku tatu tu hali ya maji ilibadilika na kuwa na ladha ya uchungu
MTOTO mwenye ulemavu wa ngozi (albino), Juma Kapela (3) aliyekuwa ameibwa tangu Jumatano iliyopita wilayani Mpanda mkoani Rukwa, amepatikana akiwa hai, lakini akiwa amechanjwa chale mwili mzima na ametelekezwa msituni. Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Daniel ole Njoolay, jana alithibitisha kupatikana kwa mtoto huyo na kumpokea ofisini kwake, lakini akiwa amechanjwa chale mwili mzima, kutokana na kile kinachoaminika kuwa ni imani za kishirikina na jitihada za kumdhuru kushindikana. Njoolay alisema alimpokea Juma na dada yake ambaye pia ni albino, Wande Kapela (5), ambao walikuwa wamefuatana na bibi yao ambaye pia ni mlezi wao, Maria Elias (60) na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda, Naomi Nnko. Juma na dada yake, Wande, wamekuwa wakilelewa na bibi yao kijijini Itunya kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika wilayani Mpanda, na Juma aliliripotiwa kuibwa Jumatano iliyopita na mtu asiyefahamika kwa kile kinachodaiwa ni imani za kishirikina. Mkuu wa Mkoa alisema awali mkoa ulipendekeza kuwa watoto hao wapelekwe kuishi kwenye Shule ya Msingi ya Malangali mjini hapa pamoja na wenzao ambao ni albino, lakini baada ya kubaini kuwa bado ni wadogo haikufanyika hivyo lakini sasa wamekubaliwa na wataishi kwenye nyumba ya watoto yatima mjini hapa ya Mt Martin de Pores iliyopo Katandala. “Hii ni faraja kubwa, hata Waziri Mkuu Pinda nilipomfahamisha kuhusu kupatikana kwa Juma akiwa hai, alisema tu ‘Mungu ni Mkubwa’. Nimekuwa nikimjulisha kuibwa kwa mtoto huyu tangu Jumatano iliyopita. Pia nimeendelea kufanya hivyo hadi alipopatikana akiwa hai juzi, na leo muda mfupi ujao nitamtaarifu kuwa watoto hawa sasa wataishi na kutunzwa kwenye nyumba hiyo ya watoto yatima,” alisema Njoolay. Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, kupatikana kwa Juma kunatokana na msako mkali uliofanywa siku nne mfululizo ukijumuisha Jeshi la Polisi , Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na wananchi wa maeneo ya vijiji vilivyopo si tu mwambao wa Ziwa Tanganyika bali pia wilayani Mbozi, Mbeya. Akizungumza kwa Kiswahili kidogo huku akichanganya na Kisukuma, bibi wa watoto hao, Maria, alidai kuwa amekuwa akiishi na kuwatunza watoto hao tangu miaka miwili baada ya baba mzazi wa watoto hao aitwaye Kwangulija Kapela kumtelekeza mama wa watoto hao na kwenda kuishi Urambo, Tabora. Alisema baba huyo ambaye ni mwanawe, alimtelekeza mkewe, Mbaru Busagija, akimtuhumu kumzalia mfululizo watoto albino ambapo alidai kuwa uzazi wa watoto hao umetia nuksi familia yao. Mama yao huyo ameolewa na anaishi pia Urambo . Akielezea mkasa huo, bibi alisema siku ya tukio, Juma alikuwa na dada yake Wande karibu na nyumba yao wakati yeye amekwenda kutafuta mboga ndipo alipotokea mtu wasiyemfahamu na kuwafukuza na kumkamata Juma na kutoweka naye. “Nilipojulishwa kuibwa kwa mjukuu wangu nililia sana ndipo majirani walipokuja na kwenda kutoa taarifa kwa viongozi wa kijiji ambao waliitaarifu Polisi na msako ukaanza,” alisema bibi huyo. Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Isuto Mantage, alisema hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusika na tukio hilo na kwamba msako wa kumtafuta mtuhumiwa unaendelea. |
Vodacom Foundation kusaidia wahanga wa Gongolamboto
Mkurugenzi wa Mahusiano na Vodacom Foundation Bi Mwamvita Makamba ameviambia vyombo vya habari kwamba
Kampuni yake kupitia mfuko wa kusaidia jamii wa Vodacom Foundation umeguswa na janga la milipuko ya mabomu yaliyotokea katika kambi ya Jeshi Gongolamboto Jijini Dares Salaam:Na hivyo kumfanya kuamua maamuzi ya haraka kama yafuatayo.
1. Kufungua tena namba yao ya maafa ili kuruhusu watanzania ambao wangependa kuchangia wenzao kufanya hivyo kwa kutuma ujumbe mfupi kwenda namba 15599 kupitia mitandao yote.
Ujumbe huu utatozwa shilingi 1000 na pesa zote zitaenda kwenye tume ya maafa ya serikali ili kuweza kununua vitu vya dharura vya wahanga. Red alert itawasha rasmi kesho ijumaa tarehe 18.
2. Vodacom Foundation itatoa chakula na vinywaji kwa siku nzima ya ijumaa kwa wahanga zaidi ya 1000 waliopo Uwanja wa taifa ambao wengi wao ni watoto
3. Pia Vodacom foundation imetoa namba za simu kwa timu ya clouds ilioanzisha kituo cha habari na matukio huko shule ya mzambarauni ukonga. Namba hizi zinatumika kupiga bure na kutoa taarifa ya kupotelewa Ndugu au jamaa na pia kutoa taarifa ya maafa zaidi ambayo hayajulikani ili taarifa ziende kwa wahusika. Namba hizi ni 0767 111401 , 0767111402 na 0767111403
4. Pamoja na kuwawezesha watanzania kutuma mchango wao kupitia ujumbe mfupi, Vodacom Foundation pia unakusanya misaada ya chakula na maji na vifaa mbalimbali katika Ofisi zao zilizopo Mlimani city kwa watu ambao hawajui waipeleke wapi. Misaada hiyo itakabidhiwa kwa red Cross ambao wanahudumia wahanga waliopo Uwanja wa taifa na sehemu mbalimbali
Waziri wa Ulinzi akizungumza na mkuu wa JWTZ na mnadhimu wa jeshi hilo
Waathirika wakikimbia miji yaoo
Hii ni nyumba moja wapo iliyo sambaratika kutokana na mabomu hayo
Majeruhi wakipata huduma hospitali ya Temeke
Majeruhi akifikishwa hospitalini hapo Temeke huku akisaidiwa na wasamaria wema!!!
Mungu ibariki Tanzania na watu wake.
KASHFA ya kukithiri kwa noti mpya bandia inazidi kuongezeka na sasa imebainika kuwa hata baadhi ya benki nchini zinashindwa kuzibaini na hivyo kujikuta zinaziingiza kwenye mzunguko.
Hali hiyo inatokana na Karani wa Fedha wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Februari 14 kuchukua fedha benki ya CRDB tawi la Lumumba na bila kutambua hatimaye akagundua amepewa noti nyingi za Sh 10,000 zikiwa bandia.
Hata pale mmoja wa wafanyakazi wa TSN aliyepewa noti hizo alipokwenda kuweka baadhi ya noti hizo kwenye moja ya benki bila kujua kuwa ni bandia, karani wa benki hiyo alizipokea na kuzipitisha kwenye mashine na kuridhika kuwa ni halali.
Kitendo hicho kinaonesha kuwa mashine za benki hazizitambui noti hizo na hata wafanyakazi wenyewe wa benki yawezekana hawana utaalamu wa kutosha wa kutofautisha noti bandia na halali hasa za Sh 10,000.
Noti hizo ziligunduliwa na wafanyakazi waliopewa fedha hizo baada ya kuanza kuzitumia na kukataliwa mitaani ambapo jana baadhi yao walijikuta wakiwa na noti hizo.
Meneja wa Fedha wa TSN, Diana Lyatuu, alithibitisha kuchukuliwa fedha hizo kutoka benki ya CRDB tawi la Lumumba kwa kubadilishwa na hundi.
Noti nyingi ambazo zimezagaa ni zinazoishia na namba 366 na 362 ambazo ndizo wafanyakazi wengi wa TSN walikabidhiwa.
Mmoja wa wafanyakazi wa TSN, Nelly Mtema, alikamatwa na Polisi baada ya kuzitumia fedha hizo alizopewa ofisini kwa ajili ya kwenda kulipia bili ya maji katika ofisi za Kampuni ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO).
Akielezea tukio hilo, Mtema alisema Februari 15 asubuhi alikwenda Dawasco kulipia maji lakini akashangaa kuwekwa chini ya ulinzi kwa maelezo kuwa ana fedha bandia.
“Niliwakatalia kuwa si bandia kwani nililipwa ofisini, lakini nikapelekwa Polisi kituo cha Kimara,” alisema Mtema ambaye baada ya kuzichunguza noti hizo aligundua bandia zikiwa tatu za Sh 10,000.
Aliongeza kuwa baada ya sakata hilo, alilazimika kupiga simu ofisini, kufahamisha kuwa fedha alizopewa ni bandia na amekamatwa na polisi baada ya kuzitumia kulipia huduma ya maji.
“Ofisini walizungumza na polisi juu ya kuwapo tatizo hilo ndipo nikaachiwa,” alisema Mtema.
Mkurugenzi wa Masoko wa CRDB, Tully Mwambapa, alipoulizwa juu ya tatizo hilo, alisema ana uhakika asilimia 100 ya fedha hizo hazikutolewa na benki yake.
“Sisi tuna sheria inayomtaka mteja ahesabu na ahakiki fedha zake kabla ya kuondoka dirishani, itakuwaje keshia aondoke ndipo tupokee malalamiko ya kuwapo fedha bandia?” Alihoji Mwambapa.
Keshia wa TSN alipoulizwa alisema hakuona haja ya kuhakiki fedha hizo kwa vile anaiamini benki hiyo kwani amefanya nayo kazi kwa siku nyingi. Hata hivyo, Mwambapa alisema: “Benki yangu ina sera ya kutoaminiana katika mambo ya fedha.”
Alijitetea kuwa kila dirisha lina kamera inayochukua mwenendo wa matukio ya kuanzia asubuhi hadi jioni yanayofanywa na karani aliyepo kwenye dirisha husika. “Ndiyo maana nasema fedha hizo hazikutoka kwetu,” alisema
Hali hiyo inatokana na Karani wa Fedha wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Februari 14 kuchukua fedha benki ya CRDB tawi la Lumumba na bila kutambua hatimaye akagundua amepewa noti nyingi za Sh 10,000 zikiwa bandia.
Hata pale mmoja wa wafanyakazi wa TSN aliyepewa noti hizo alipokwenda kuweka baadhi ya noti hizo kwenye moja ya benki bila kujua kuwa ni bandia, karani wa benki hiyo alizipokea na kuzipitisha kwenye mashine na kuridhika kuwa ni halali.
Kitendo hicho kinaonesha kuwa mashine za benki hazizitambui noti hizo na hata wafanyakazi wenyewe wa benki yawezekana hawana utaalamu wa kutosha wa kutofautisha noti bandia na halali hasa za Sh 10,000.
Noti hizo ziligunduliwa na wafanyakazi waliopewa fedha hizo baada ya kuanza kuzitumia na kukataliwa mitaani ambapo jana baadhi yao walijikuta wakiwa na noti hizo.
Meneja wa Fedha wa TSN, Diana Lyatuu, alithibitisha kuchukuliwa fedha hizo kutoka benki ya CRDB tawi la Lumumba kwa kubadilishwa na hundi.
Noti nyingi ambazo zimezagaa ni zinazoishia na namba 366 na 362 ambazo ndizo wafanyakazi wengi wa TSN walikabidhiwa.
Mmoja wa wafanyakazi wa TSN, Nelly Mtema, alikamatwa na Polisi baada ya kuzitumia fedha hizo alizopewa ofisini kwa ajili ya kwenda kulipia bili ya maji katika ofisi za Kampuni ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO).
Akielezea tukio hilo, Mtema alisema Februari 15 asubuhi alikwenda Dawasco kulipia maji lakini akashangaa kuwekwa chini ya ulinzi kwa maelezo kuwa ana fedha bandia.
“Niliwakatalia kuwa si bandia kwani nililipwa ofisini, lakini nikapelekwa Polisi kituo cha Kimara,” alisema Mtema ambaye baada ya kuzichunguza noti hizo aligundua bandia zikiwa tatu za Sh 10,000.
Aliongeza kuwa baada ya sakata hilo, alilazimika kupiga simu ofisini, kufahamisha kuwa fedha alizopewa ni bandia na amekamatwa na polisi baada ya kuzitumia kulipia huduma ya maji.
“Ofisini walizungumza na polisi juu ya kuwapo tatizo hilo ndipo nikaachiwa,” alisema Mtema.
Mkurugenzi wa Masoko wa CRDB, Tully Mwambapa, alipoulizwa juu ya tatizo hilo, alisema ana uhakika asilimia 100 ya fedha hizo hazikutolewa na benki yake.
“Sisi tuna sheria inayomtaka mteja ahesabu na ahakiki fedha zake kabla ya kuondoka dirishani, itakuwaje keshia aondoke ndipo tupokee malalamiko ya kuwapo fedha bandia?” Alihoji Mwambapa.
Keshia wa TSN alipoulizwa alisema hakuona haja ya kuhakiki fedha hizo kwa vile anaiamini benki hiyo kwani amefanya nayo kazi kwa siku nyingi. Hata hivyo, Mwambapa alisema: “Benki yangu ina sera ya kutoaminiana katika mambo ya fedha.”
Alijitetea kuwa kila dirisha lina kamera inayochukua mwenendo wa matukio ya kuanzia asubuhi hadi jioni yanayofanywa na karani aliyepo kwenye dirisha husika. “Ndiyo maana nasema fedha hizo hazikutoka kwetu,” alisema