Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Tamasha la 12 la kimataifa la filamu laanza Zanzibar

-
Rehema Mwinyi.

TAMASHA la 12 la filamu la kimataifa la Zanzibar (ZIFF), 2009 limezinduliwa rasmi jana mjini hapa katika eneo la Mji Mkongwe, viwanja vya Ngome Kongwe kuhudhuriwa na umati mkubwa wa watu.

Burudani kutoka kwa mshairi Mrisho Mpoto 'Mjomba', Beni na Siti zilipamba uzinduzi wa tamasha hilo ambalo litaendelea hadi Julai 12.

Baada ya uzinduzi huo, filamu ya Izulu Lami (My Secret Sky) ya dakika 93 ilionyeshwa.

Kwa mujibu wa Mkurugenzu wa ZIFF, Profesa Muhando, Watanzania wameingiza filamu 13 katika tamasha hilo na mgeni wake rasmi anatazamiwa kuwa muigizaji maarufu wa Hollywood, Danny Glover.

Danny Glover anatarajiwa kwasili nchini Jumatatu tayari kwa ratiba ndefu ikiwa ni pamoja na mwaliko wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (Unicef) na kuwatembelea watoto walioathirika na ugonjwa wa ukimwi.

Leave a Reply