Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

KIBAKA AHARIBIWA SURA KATIKA NYUMBA YA BONDIA.

-
Rehema Mwinyi.


Gregory McCalium kabla na baada ya kupewa kichapo na babu ambaye ni bondia mstaafu

Kibaka aliyezamia kwenye nyumba ya babu mmoja nchini Uingereza mwenye umri wa miaka 72 na kuanza kumtishia kwa kisu bila kujua kwamba babu huyo alikuwa ni bondia mstaafu, aliambulia kipigo kilichoichakaza sura yake.
Kibaka huyo Gregory McCalium mwenye umri wa miaka 24 mkazi wa wa Oxford nchini Uingereza, alivamia kwenye nyumba ya jirani yake ambayo babu huyo alikuwa akiishi na mke na kujaribu kuwapora mali zao bila kujua kwamba babu huyo alikuwa bondia mstaafu.

Babu Frank Corti mwenye umri wa miaka 72 alikuwa ni bondia maarufu enzi za ujana wake akiwa amejikusanyia vikombe kadhaa katika mashindano mbali mbali ya ndondi nchini Uingereza.

Picha iliyotolewa na polisi wa Uingereza ilionyesha jinsi sura ya kibaka huyo aliyekuwa na kisu ilivyoharibiwa vibaya na ngumi nzito za babu huyo.

Babu Corti baada ya kumwangushia kipondo McCalium alimlaza chini na kumlalia mpaka polisi walioitwa na mkewe walipokuja kumchukua.

Jumanne wiki hii McCalium alihukumiwa kwenda jela miaka minne na nusu kwa kosa hilo la jinai.

"Mwanzo nilishtuka aliporusha kisu chake, lakini kama watu wengine jinsi ambavyo wangejihami na mimi niliamua kufanya hivyo" alisema Corti.

"Umepata ulichostahili" alisema mwendesha mashtaka Angela Morris akimwambia McCalium wakati akisomewa mashtaka yake mahakamani hapo.

Tukio hilo lililotokea mida ya asubuhi lilimwacha kibaka McCallium akiwa amepasuliwa chini ya jicho lake na amechanika mdomo wake.

source:nifahamishe.com

Leave a Reply