Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

AJALI....

-
Rehema Mwinyi.




Mtoto Mwanaidi Ibrahim (4) (kulia), ambaye wazazi wake wote wawili walifariki dunia katika ajali ya gari, Kibamba juzi, akiwa amebebwa na Mama yake mdogo, Sharifa Ally wakati wa maombolezo ya msiba wa wazazi wake hao, Kibamba, Dar es Salaam jana. Kushoto ni ndugu yake Salha Jaffar (3). Mtoto huyo kwa sasa amebaki yatima.

Ajali ya gari iliyochukua nafasi juzi alfajiri eneo la Kibamba, Dar ndani yake kuna zaidi ya tukio, baada ya kuibuka kwa taarifa mpya kwamba kulikuwa na wanandoa watarajiwa ambao roho zao zilizimika papo papo...

ndani ya daladala lililoangukiwa na lori la mafuta, kulikuwa na wanandoa watarajiwa ambao walikuwa safarini kwenda Morogoro kwa ajili ya kukusanya michango ya harusi.

Kwa mujibu wa mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Chaudama Emanuel, wanandoa watarajiwa waliopoteza maisha ni Justin na Helen.

Akifafanua kila kitu, Chaudama alisema kuwa Justin na Helen walipata ajali hiyo walipokuwa wanakwenda kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi yanayokwenda mikoni na nchi jirani, Ubungo ambako walikuwa wapande basi la Hood kwenda Moro.

“Kwanza kulikuwa na ubishi wa wao wenyewe, masikini mdogo wangu (Justin) alitaka wasubiri basi hapa hapa Kibamba, lakini wifi akataka wakapandie Ubungo, kwahiyo Justin akamsikiliza mchumba wake kumbe walikuwa wanafuata wito wa Mungu,” alisema Chaudama.

Aliongeza: “Walikuwa wanakwenda Morogoro kufuata michango ya harusi, walitakiwa kurudi leo leo (juzi) jioni au kesho (jana) asubuhi na ndoa yao ingefungwa Jumamosi (leo) kanisani kwa sababu sisi ni Wakatoliki.”

MKOSI
Wakati hali ikiwa hivyo kwa Justin na Helen ambao pumzi yao ilikatika siku mbili kabla ya kutimiza tukio muhimu katika historia ya binadamu, yaani ndoa, ‘ishu’ nyingine ya kusikitisha ni kuwa, mwanamke aliyekuwa amesotea mtoto kwa muda mrefu, akiwa njiani kwenda kujifungua kwenye hospitali ya Mwananyamala, Dar ni mmoja wa abiria waliopoteza maisha hali inayotafsiriwa na wakazi wa Kibamba kuwa ni mkosi wa mji huo.

Katika ushuhuda wa gazeti hili baada ya ajali hiyo, mtoto mchanga akiwa amepoteza maisha, alitokeza kwenye tumbo la mama huyo, tukio ambalo liliwaliza wengi walioshuhudia.

Shuhuda mmoja aliyezungumza na gazeti hili eneo la tukio na kueleza kwamba anamfahamu mwanamke huyo aliyekuwa mjamzito, alisema kwamba alikuwa na mumewe wakienda hospitali ya Mwananyamala baada ya kushikwa na uchungu.

“Walikuwa wanakwenda hospitali Mwananyamala, sasa Mungu ana yake ndiyo maana wamepata ajali kabla ya kufika hospitali. Inasikitisha sana,” alisema mtoa habari wetu huku akijifuta machozi.

Katika ajali hiyo, Lori la kubeba mafuta lenye namba za usajili T192 ABP, lililiangukia daladala aina Hiace na kuua abiria wote waliokuwemo.


Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba, katika idadi hiyo, waliopoteza maisha ni wanaume wanane na wanawake watatu.

Kutokana na ajali hiyo, waandishi wetu walizunguka mitaa mbalimbali ya eneo la Kibamba ambako ndiko inasemekana watu wengi waliopoteza maisha wanaishi, na kushuhudia nyumba nyingi zikiwa katika hali ya utulivu.

Picha iliyoshuhudiwa na Risasi Jumamosi ni kuwa japo si kila nyumba iliyokutwa na msiba lakini uzito wa tukio hilo, ulivuta hisia za watu wengi ambao waliungana na wafiwa kuomboleza.

chanzo cha habari hii:GLOBAL PUBLISHER.





Leave a Reply