Banner 468

1234453_10201664080105694_1716282793_n
Facebook

Fuso laua watu watano Moro

-
Rehema Mwinyi.

WANUNUZI watano wa mahindi  wamekufa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya tairi la gari walilokuwa wakisafiria, kupasuka na kusababisha gari hilo kupinduka,  katika eneo la Magubike katika Barabara ya Dodoma- Morogoro.Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Adolphina Chialo, aliwataja waliokufa katika ajali hiyo juzi usiku kuwa ni Mwarami Abdallah, mkazi wa Mzense jijini Dar es Salaam, Selemani Ngula (30), Kasimu Mwitago (30).

Kwa mujibu wa kamanda huyo, maiti mwingine ametambuliwa kwa jina moja la Kiejo (30) wakati mwingine hajatambuliwa. Chialo pia aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni, Timoth Paul,  Elisafi Mkumbwa na Hamisi Selemani, wote wakazi wa Kibaigwa  na kwamba majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu.

Alisema gari hilo lilikuwa linatokea katika Kijiji cha Kibaigwa, wilayani Kilosa kwenda jijini Dar es Salaam na kwamba chanzo cha ajali ni mwendo mkali.Alisema watu hao walikuwa wanasafiri kwa kutumia gari aina ya Mistubish Fuso iliyokuwa ikiendeshwa na Jackson Bezaleli Senyegwa (27) mkazi wa Kibaigwa ambaye alitoroka mara baada ya ajali hiyo.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi katika wodi namba moja,mmoja wa majeruhi Hamisi Selemani, alisema gari hilo lilikuwa limebeba gunia 100 za mahindi, jambo lililosababisha  moja ya matairi kuelemewa na kupasuka.

Alisema abiria wote waliokuwa nyuma ya gari hilo walifariki papo hapo baada ajali na kwamba walifunikwa na mahindi.Kamanda huyo alisema miili ya watu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, na kuomba wananchi kujitokeza ili kutambua miili ambayo haujatambuliwa.

Leave a Reply